Dar es Salaam: Machinga wa Karume waandamana kuelekea ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Wasema hawana imani na Viongozi. Mabomu ya machozi yarindima

Dar es Salaam: Machinga wa Karume waandamana kuelekea ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Wasema hawana imani na Viongozi. Mabomu ya machozi yarindima

Sasa naamini kuna uwezekano mkubwa serikali ikawa inahusika na haya matukio ya moto unaounguza masoko ya nchi hii usiku tu, hawa hawawezi kujichunguza ndio maana huwa hawatoi majibu ya ripoti za tume wanazounda, hawa ni corrupt.
Hivi zile shule zikizokuwa zinaungua kila wiki kipindi kile
Inaweza kuwa na yenyewe ni hujuma?
Eeh
 
Je historia ya eneo la Karume ni ipi? Kama walivamia wahesabu maumivi. Kama halipo kwenye master plan ya jiji kama eneo la biashara ndio imekwisha hivyo.
 
Moto umekuwa unafuatana sana na Makala. Kote alikopita masoko yaliwaka moto. Waanze na Makala kwanza ana weza kuwa na kiberiti chake maalum kuumiza wahangaikaji kwa lengo la kuwahamisha 😔😔😔😔
 
Sasa usiwe kigeugeu wa kisiasa.

Wamachinga wametoka wapi hapa nchini, kila mtu akkimbila Dar es salaam ili awe mchinga Jiji hili litakuwaje.

Halafu badala ya kusema siasa zetu zikirie kuendeleza kilimo ili kila mtu ajiajiri kwenye kilimo, wewe unataka wasidiwe watu mia moja u mia mbili watu ambao ni wachache mn kufikiriw kisera.

Viongozi waanzishe sera jumla jumla za kuwaendeleza Watanzania kue walo, kijijini.
Katambi amekusikia!
 
Bora mkolon arudi kwnye hii nchi kulko mkolon ccm
Hayo yote ni kuonesh jinsi gani serikali inashindwa kuwapa kipaumbele watu wake nakutatua matatizo on time. Haina haja yakuja mkoloni bali nyinyi wenyewe wananchi mnaweza sema ndio hivyo wakianzisha wenzenu nyinyi mnajifungia ndani mnasema kaandamaneni wenyewe. Kwa style hiyo wacha CCM iendelee kuwanyoosha.
 
Sasa usiwe kigeugeu wa kisiasa.

Wamachinga wametoka wapi hapa nchini, kila mtu akkimbila Dar es salaam ili awe mchinga Jiji hili litakuwaje.

Halafu badala ya kusema siasa zetu zikirie kuendeleza kilimo ili kila mtu ajiajiri kwenye kilimo, wewe unataka wasidiwe watu mia moja u mia mbili watu ambao ni wachache mn kufikiriw kisera.

Viongozi waanzishe sera jumla jumla za kuwaendeleza Watanzania kue walo, kijijini.
Umekariri kila machinga katoka mkoani!? Machinga kibao wa hapa hapa Dar na hawakujui huko mikoani. Hao watu kwani serikali ndio huwa inawalisha kabla ya hili tukio!? Waachwe wajitafutie wenyewe wala haeaendi ikulu magogoni kuomba.
 
Wamachinga wa nchi hii tunapata tabu sana. Nafikiri wanataka kuweka STAND ya DALADALA pale maana mpaka sasa hivi stendi za daladala zimekuwa adimu sana.
Hadi mtakapojitambua ndiyo hamtapata tabu, vinginevyo acheni mpigwe tu.
 
Hivi hilo eneo liko chini ya nani?

Ova
Screenshot_20220117-150137.jpg
 
Wafanyabiashara ndogondogo maarufu machinga wa soko la Karume (Mchikichini) wameandamana hadi kwenye Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla kushinikiza kiongozi huyo atoe tamko la kuwaruhusu waendelee kufanya shughuli zao kwenye soko hilo.

Wafanyabiashara hao wameandamana leo Jumatatu Januari 17, 2022 ambapo walikuwa wanaimba "Tunataka Soko letu" wakiwa wamezingira geti la ofisi hiyo, ikiwa ni siku moja imepita tangu soko hilo kuteketea kwa moto usiku wa kuamkia jana.

Wakizungumza katika tukio hilo, baadhi ya wafanyabishara hao wamesema wanafanya hivyo baada ya kukosa imani na maamuzi yaliyochukuliwa na viongozi hao huku wakionyesha kusikitishwa kwao na kitendo cha wenzao kuvunjiwa mabanda yao waliyojenga usiku wa kuamkia leo na jeshi la polisi.

Silvanus Mwakipesile amesema Mkuu wa Mkoa aliwaahidi leo saa 2:00 asubuhi angefika kwenye soko hilo kuwaona na kuwapa muongozo lakini wanashangaa kabla ya kiongozi huyo kwenda kuna watu wamevunjiwa mabanda yao na sehemu hiyo kuwekwa chini ya ulinzi mkali ukisimamiwa na Jeshi la Polisi.

"Tumekosa imani na viongozi jana alisema anakuja lakini hadi sasa hatujamuona na chakushangaza waliojenga vibanda vyao wamebomolewa, sisi hatuwezi kuwasubiri wao maisha yetu magumu watuache tujenge wenyewe ili tuendelee kufanya kazi zetu," amesema

"Siku zilizotolewa kwa ajili ya kufanya uchunguzi ni nyingi tunataka tuachwe tujenge mabanda wakati uchunguzi ukiendelea na si kubaki hivihivi tutakula Nini na tunawatoto wanatakiwa kwenda shule,"amesema Saida Mohamed


Hata hivyo Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Ng'wilabuzu Ludigija amewaomba wafanyabishara hao kuwa wavumilivu na kufuata utaratibu uliotangazwa na Serikali kwamba waiachie kamati ifanye kazi kwa siku saba na kutoa ripoti badala ya kuandamana kutaka kushindana na Serikali.

"Mnatakiwa kujiongeza pamoja na kwamba mnadai haki lakini lazima mfuate utaratibu Jana Waziri tuiachie Kamati ifanye kazi na walete ripoti tunaomba kuweni na subira,"amesema.

Jana baada ya soko hilo kuungua Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam (RC), Amos Makalla aliwataka wafanyabiasha wa soko hilo kuwa watulivu huku akiahidi kuundwa kamati ambayo itachunguza chanzo cha moto huo kwa siku 14 akipiga marufuku shughuli zozote kuendelea wakati wa uchunguzi huo.

Muda mfupi baada ya RC Makalla kutoa tamko hilo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Innocent Bashungwa aliagiza kamati hiyo kufanya uchunguzi kwa siku saba badala ya 14.

UPDATES
POLISI WATUMIA MABOMU YA MACHOZI KUWATAWANYA MACHINGA WALIOANDAMANA
Polisi wametumia mabomu ya machozi kuwatawanya Wafanyabiashara wa soko la Karume (Mchikichini) ambao wameandamana na kufunga barabara karibu na ofisi ya Mkuu wa Mkoa wakishinikiza kuruhusiwa kuendelea na biashara katika soko hilo lililoungua

Wafanyabiashara hao maarufu walifunga Barabara kwa kutumia mawe na magogo katika makutano ya Uhuru na Kawawa, Ilala Boma wakimtaka RC Amos Makalla atoe tamko la kuwaruhusu waendelee kufanya shughuli zao kwenye soko hilo

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Innocent Bashungwa ameagiza Kamati iliyoundwa kufanya uchunguzi wa Moto uliotokea kwa siku saba.

Chanzo;- Mwananchi
mammmamae waliependa wenyewe chaguo lao wenyewe, wacha waisome namba ccm mbele kwa mbele.
 
Pamoja na yooote tukubaliane kurudisha tena mabanda pale ni upunguani, pale ni kati kati ya mji pajengwe soko lenye hadhi ya eneo husika
 
Back
Top Bottom