Dar inaongoza vijana watu wazima kuishi kwa wazazi wao

Dar inaongoza vijana watu wazima kuishi kwa wazazi wao

Habari zenu,

Mjanja M1 nimeona maeneo mengi Dar vijana wenye umri mkubwa miaka 30 na kuendelea wakiishi kwa wazazi wao na wengine kuzalia makwao.

Kautafiti kangu kamegundua zaidi kuwa kuna wanaume waliooa pia ambao wanaishi na wake zao kwenye nyumba za wazazi wao.

Vijana wengi wa Dar wameshakata tamaa ya kujenga makazi yao binafsi, wengi wanategemea cha wazazi eg. Nyumba, Magari n.k

Utafiti wangu pia umegundua kuwa kuna vijana wanaojitegemea lakini maisha yao hayapo vizuri kwani kesho yao imekuwa ngumu kueleweka, na mara nyingi utakuta kijana anaishi kwenye nyumba za kupanga na bado kodi ya pango inamsumbua kulipia.

Vijana hawa wenye umri mkubwa hawana future iliyobora maana kuna uwezekano kwenye uzee wao wakawa wanaishi maisha ya tabu kwa kukosa makazi yao binafsi.

USHAURI - NAOMBA SERIKALI IONGEZE NAFASI ZA AJIRA KWA VIJANA, NA PIA IONDOE VIKWAZO VINGI KWA WANAOFANYA BIASHARA.

NB. HUU NI UTAFITI WANGU KAMA MJANJA M1, KAMA UTAUPINGA BASI UTAKUWA SAHIHI PIA.

Written by Mjanja M1.
Ulilolisema ni sahihi kabisa, 80% ya marafiki zangu, majirani zangu I mean age mates wangu wanaishi majumbani kwao. Home Kijitonyama washkaji wengi wanafanya kazi lakini hawajatoka kwenye nyumba za wazazi. Ila nilichogundua ni pamoja na kuwepo kwa space, na wengine wanaambiwa na wazazi wao wenyewe kwanini unataka kupanga wakati vyumba nyumbani vipo?
Hii ilinitokea hata mimi kabla sijahamishiwa kikazi mkoani, mama haukutaka nikapange kabisa maana madogo wote wapo mikoani kikazi.
 
Hawa vijana muwaonee huruma wana stress sana wengi hawapendi kubaki kwao wanalazimika

Kuna vijana tangu wamalize vyuo hawana mishe za maana hivyo hata kwenda kupanga anaona kodi zitamtesa na akizingatia kwao kuna vyumba/chumba

Wengi unakuta walisoma seko mpaka chuo ila hawana ujuzi wowote wa VETA wanategemea magamba yao ya vyuo. Mitaji ya biashara hawana familia maisha ya kuungaunga.

Wengine wamejiongeza kuwa boda au winga K/koo, udalali n.k

Wanaumia sana wanapoona wenzao waliosoma nao wakiwa wana mishe. Wao wakiamka asuhuhi hawajui waende wapi

Tusiwaseme sana vijana wa Dar ila wanachopitia Mungu mwenyewe anajua
 
Back
Top Bottom