Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Ulilolisema ni sahihi kabisa, 80% ya marafiki zangu, majirani zangu I mean age mates wangu wanaishi majumbani kwao. Home Kijitonyama washkaji wengi wanafanya kazi lakini hawajatoka kwenye nyumba za wazazi. Ila nilichogundua ni pamoja na kuwepo kwa space, na wengine wanaambiwa na wazazi wao wenyewe kwanini unataka kupanga wakati vyumba nyumbani vipo?Habari zenu,
Mjanja M1 nimeona maeneo mengi Dar vijana wenye umri mkubwa miaka 30 na kuendelea wakiishi kwa wazazi wao na wengine kuzalia makwao.
Kautafiti kangu kamegundua zaidi kuwa kuna wanaume waliooa pia ambao wanaishi na wake zao kwenye nyumba za wazazi wao.
Vijana wengi wa Dar wameshakata tamaa ya kujenga makazi yao binafsi, wengi wanategemea cha wazazi eg. Nyumba, Magari n.k
Utafiti wangu pia umegundua kuwa kuna vijana wanaojitegemea lakini maisha yao hayapo vizuri kwani kesho yao imekuwa ngumu kueleweka, na mara nyingi utakuta kijana anaishi kwenye nyumba za kupanga na bado kodi ya pango inamsumbua kulipia.
Vijana hawa wenye umri mkubwa hawana future iliyobora maana kuna uwezekano kwenye uzee wao wakawa wanaishi maisha ya tabu kwa kukosa makazi yao binafsi.
USHAURI - NAOMBA SERIKALI IONGEZE NAFASI ZA AJIRA KWA VIJANA, NA PIA IONDOE VIKWAZO VINGI KWA WANAOFANYA BIASHARA.
NB. HUU NI UTAFITI WANGU KAMA MJANJA M1, KAMA UTAUPINGA BASI UTAKUWA SAHIHI PIA.
Written by Mjanja M1.
Kama Bado Sina familia niendelee kurelax au siyoUpo sahihi, lakini kama una familia au mtoto inakupasa uwe na kwako.
Ikiwa wao wenyew wamejiriwa na wananchi... Hii nchi n huzuni😔Wazo zuri ila serikali hio hio haina hela ya kuwalipa ikiwaajira inatumia kisingizio kwamba vijana mjiajiri
Wewe kaa tu,Mo na utajiri wake wote lakini mpaka leo anaishi kwa wazazi wake.Kwani mwisho wa kukaa kwa wazazi ni miaka mingapi? Usikute napitiliza bila kujua.
😂 sawa umeelewekaKila mmoja akae kwa wazazi wake, wazazi nao waende kwao🤒.
Half american
Wewe kaa tu,Mo na utajiri wake wote lakini mpaka leo anaishi kwa wazazi wake.
Yesu mwenyewe yupo kwa baba yake
Hakuna muda maalumu, kaa uwezavyo mpaka utakapochumbiwa😄😄Kwani mwisho wa kukaa kwa wazazi ni miaka mingapi? Usikute napitiliza bila kujua.
Ushauri mzuri.Hakuna muda maalumu, kaa uwezavyo mpaka utakapochumbiwa😄😄