Uchaguzi 2020 Dar: Jeshi la Polisi lasitisha wito wake kwa Tundu Lissu, lamtaka aendelee na Kampeni zake

Uchaguzi 2020 Dar: Jeshi la Polisi lasitisha wito wake kwa Tundu Lissu, lamtaka aendelee na Kampeni zake

Mwamba kutoka kanda ya Kati,

Twende tumechelewa sana , muda ni mchache.

Huku NEC CCM, Huku Polisi CCM, Huku IGP Sirro,Huku Mambo leo ,Huku Nyahoza ,Kule Pole pole ili mradi ni matamko tu yasiyo na Kichwa wala Miguu.

Ngoma inogire,Twende Mwamba muda ni mchache.
 
Uko sahihi maana urais wa nchi hii sio lazima ushinde kwa kura. Iwapo ushindi ungekuwa ni wa kura hiki alichokisema hapa ungebaki nacho. Ila nakushauri endelea kuomba watanzania waendelee kuwa makondoo a.k.a watu wa amani, kinyume na hapo utashuhudia ambacho hukuwahi kuwaza.
Mkuu huwa naheshimu sana michango yako. Tatizo mnaegemea upande mmoja kuwalaumu watanzania kuwa ni waoga. Upande wa pili ni aina ya wagombea mnaowaleta. Kuna tatizo kubwa kwa Mgombea wa CHADEMA, kutokana na Lissu kupigwa risasi, zile hasira Kuna watu amewahusisha na wapo front kwenye kuusaka uraisi ambao ni tishio kwa ustawi wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania. Tatizo linaanzia njia alizojaribu kutumia Lissu kuusaka uraisi haziwezi kufanya kazi nchi hii(nakuhakikishia). Hii sio Malawi,Zambia au Mali hii ni Tanzania. Na wengi mna underestimate system ya Tanzania. Sio ya mchezo mchezo kiongozi.
 
Kuna kipindi watu tumeshauri hapa..kwa wema tu kwamba Tundu Antipasy Lissu..kabla hajasmama kumwita aidha kumhoji ama kumshitaki ama kumuuliza maswali lazma ukae chini utafakar. Huyu ni mgombea anaijua anachosmamia...Katika jambo ambalo Polisi wamekwepa mtego mkubwa wa kudharilika ni huu. Maana Wangepata tabu kumhoji...mana "system ya answer by Question "ingewatoa kwenye line...wangemwongezea umaarufu mkubwa mwishowe wangejikuta wanalaumiwa na HP mwenezi. Hongera polisi kwa kulitafakar hili . mjue tu wagombea wote wakishinda ni Tanzania itakua imeshinda..tendeni haki Bila upendeleo Tafadhar sana!!

Sent from my SM-G920F using JamiiForums mobile app
 
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]Usalama wamemwambia Magu acha kuhangaika tulia tulii! Huyu kibaraka hawezi kuwa rais
Wamwambie na hili.
FB_IMG_1601425432271.jpg
 
Hata kina mange walikuwa Hivi,,



Leo hii wako wapi?
 
Kama kweli ka withdraw, huyo ndiye Siro halisi wa Mwanza enzi hizo. Huwa anazo busara, basi tu CCM hubemenda raia wema.

lissu anapaswa ajue sio kila mtu ni wa kumuona mjinga.

lazima atumie watu humu humu ndani ya serikali kuwaonyesha ccm kwamba hana tatizo na watu ambao wanajitambua.

kitendo cha kuita askari wajinga halafu wako nyuma yako wengine na unadai ni watu miongoni mwa unao waomba kura,hii nayo ni bangi.
 
Mkuu
Nakumbuka Hosni Mubarak na Elbashir walikuwa na wapambe wao kama ww, ila sasa hivi wapambe wao wote wana vusukari maana hawaamini wanachokiona.
Mkuu hii sio Misri wala Tunisia, hii ni Tanzania. Bado siku 25 tu.
 
Hahahaha wanajitekenya na kucheka kwenyewe
 
Bado polisi inabidi wa angaliwe kwa macho 4 maana hawaja wahi kuwa waungwana ata siku moja
 
"Kanda Maalum Ya Polisi Dar Es Salaam" inahusika vipi na uhalifu wa mkoa mwingine, swala la kosa aliloitiwa (Japo halijatajwa) Mh Tundu Lissu ni mkoa wa Mara na akatakiwa ku report Kilimanjaro. Mambosasa yanamhusu nini maswala ya mikoa mingine?.

Nchi yetu jeshi la polisi limekosa weredi kabisa, viongozi wanakurupuka na kujiamulia tu anachojisikia, hawajui "TERRITORIAL JURISDICTION/MAMLAKA YA KIENEO" yanakwenda vipi na yana nguvu gani kisheria na mipaka ya mamlaka hayo.

Mambosasa anatakiwa afanye kazi kulingana na "TERRITORIAL JURISDICTION" ya eneo lake, eneo lake na mamlaka aliopewa kisheria ni ya Kanda Maalum Ya Dar Es Salaam, hana mamlaka kisheria ya kuingilia maswala ya kikazi ya mikoa mingine. Aache kukurupuka kwani atalinajisi jeshi la polisi kuonekana halifuati sheria na mamlaka. Anapaswa arudishwe darasani na apelekwe kusoma upya sheria.

Barua ingekua imetokea "MAKAO MAKUU YA POLISI" raia tusingekua na pingamizi, na tungeiheshimu, kwasababu makao makuu ya polisi wana mamlaka ya mikoa yote kisheria. Ila barua inatoka "KANDA MAALUM YA DAR ES SALAAM". Kwa hilo watuache.

Acha lissu awanyooshe hawa vibwengo wenye vyeo vikubwa bila ya kuwa na elimu ya kukidhi matakwa ya kazi yao. Nchi inaendeshwa na kikundi cha watu wachache wanaojiamulia mambo bila kufuata sheria, wanatumia mamlaka na mabavu, ila sio sheria wala haki.

Au lasivyo wakiachiwa, kesho tutasikia Mhalifu amefanya kosa la Kubaka Morogoro halafu Jeshi La Polisi Mkoa Wa Kigoma limetoa barua ya kuachiliwa mara moja mhalifu huyo.

#KUFICHA AIBU, kesho utasikia Mambosasa anaongea na vyombo vya habari na kusema barua hio inayozunguka mitandaoni imeandikwa na watu "WASIOJULIKANA", wananchi tunaombwa tuipuuze.[emoji38][emoji16]
Kajinyonge!
 
bro shetani akikusemesha"tumsifu yesu kristo"
kemea kwa ukali.

usishangilie kwamba sasa ameokoka.
Kwa mokorokoro niliyoyaona kwenye hii issue ya Lissu ni hatuna jeshi la polisi ambalo linaweza kumfanya kitu Lissu:

1.Lissu amefanya kosa Moshi akaandikiwa barua kuwa aripoti Dar.Hakuna sheria ya namna hiyo

2.Aliefanya kosa ni Lissu ila barua ikaandikwa kwa chadema

3.Barua ilikuwa na kiwango cha chekechea("chana cha democrasia")

Ni vyema jeshi la polisi likaguliwe vyeti kuanzia IGP
432098.jpg
432090.jpg
543098.jpg
 


Mambosasa: Polisi tumesitisha kumuita Tundu Lissu, tunamtaka aendelee na Kampeni zake

Baada ya mgombea wa urais kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Tundu Lissu, kukataa kuitikia wito uliotolewa na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro, uliotolewa jana ukimtaka aripoti kituo cha Polisi Kilimanjaro.

Lissu kupitia ukurasa wake wa Twitter ameandika kuwa ataendelea na ratiba zake ikiwemo kikao cha mabalozi kinachofanyika leo.

“Wito wa polisi sio barua ya kirafiki ni amri kisheria, wito huo unatakiwa kueleza kosa la mtuhumiwa barua hii haielezi kosa ninaloitiwa na imepelekwa kwa Mwenyekiti wa chama, huu sio wito wa polisi kwa mujibu wa sheria, nitaendelea na ratiba yangu ya kikao na mabalozi kesho” ameandika Lissu kupitia kaunti yake ya Twitter.

Kwa mujibu ya barua iliyotumwa kwa Mwenyekiti wake wa Chama, Freeman Mbowe, Lissu alitakiwa kuripoti polisi 02/10/2020 kwa ajili ya mahojiano kufuatia kauli na matamshi yake ambayo amekuwa akiyatoa kwenye mikutano yake ya kampeni dhidi ya maafisa wa polisi.
Uchaguzi 2020 - Tundu Lissu: Wito wa Polisi siyo barua ya kirafiki, Nitaendelea na ratiba yangu ya kikao na mabalozi

View attachment 1587836
Video ya maelezo ya kamanda wa kanda maalum Lazaro Mambosasa akithibitisha kusitisha wito wa kumtaka Tundu Lissu kuripoti kwa jeshi hilo kanda ya Dar es Salaam
View attachment 1587905

Wamekubali kuwa sisi ni juu
 
Back
Top Bottom