DAR: Licha ya RC Makonda kusema atakayenunua Makontena yake atapata laana kali, Waziri Mpango aagiza yapigwe mnada

JPM hupenda kufanya kazi kwa kujitegemea kimawazo. Ukimpelekesha tu basi ujue umeshaharibu.

Alipomkingia kifua wakati wa ile vita ya wauza sembe, haikumaanisha kwamba dogo ni msafi bali hakutaka kuvunja morali iliyokuwa imeshajengeka.

JPM ana msimamo mkali kwenye mambo yake.
 
Wasiwasi wangu vilivyokuja vilishachukuliwa vilivyopo nivingine, hili ninaliamini 78%.
Haiwezekani muda wote wawe wanasubiri kusamehewa kitu kisichosameheka na wasitafute plan b.
Yes
 
Sure
 
Makonda sio Nikolas Biwott wa Kenya enzi za Rais Moi.
Lakini kuna wakati Makonda anaonekana kama mtu asietishwa na yeyote tokea amzabe makofi Jaji Warioba licha ya kuwa waziri mkuu mstaafu pale Ubungo Plaza,akazawadiwa na raisi Kikwete kuwa DC Kinondoni.
Japo Magu ni mtu wa misimamo mikali lakini kuna wakati damu ni nzito kuliko maji.
 
Taifa lisilo na mashauri upelekea anguko kuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
yaani wewe unajifanya kipofu wakati masikio makubwaaaa !! pale SIZONJE aliposema yeye haangali vyeti anaangalia uchapakazi inamaana hukumuelewa... ''MAKONDA WE CHAPA KAZI TU'' na kazi ndo hii sasa ya makontena
haya ndio matunda ya mbeleko kwa BASHITE aka PAULO
 
Kuna watu wapo duniani kama bendera hawajahi tumia japo punje ya ubongo wao kwasababu ya mahaba.

1. Yale makontena yamebeba viti vya ofisini wala si madawati, Niambieni ni shule gani wanakalia viti vya kuzunguka?
2. Uagizwaji Wa makontena haukuzingatia taratibu, niambieni tangu lini msamaha umeanza kutolewa kwa huruma ya walengwa?
3. Kwanini mwenye Makontena aliyakana pale mwanzo?
4. Yakiachwa yapite Bure Tutakuwa tumewafundisha nini Wasimamizi Wa forodha na ushuru kwa vitu visivyo zingatia utaratibu?
5. Kwanini yaliandikwa jina la Makonda (Personal)?
===============
NOTE; Mtoto hata ukimkalisha kiti cha mwalimu Mkuu haina maana ndiyo atajua kusoma na kuandika
 
Wanakera sana mkuu, tumekuwa taifa la udaku udaku tu na mambo yasiyo na msingi kuanzia viongoz wakuu mpaka kwetu huku. Wenzetu Kenya wanapiga hatua za maana aisee sijui nani katuletea hiki kituko.
Kilichofikiriwa ni kuokoa chama kwanza dhidi ya white man with pure heart, kwanza hata kama mengine yataangamia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanakera sana mkuu, tumekuwa taifa la udaku udaku tu na mambo yasiyo na msingi kuanzia viongoz wakuu mpaka kwetu huku. Wenzetu Kenya wanapiga hatua za maana aisee sijui nani katuletea hiki kituko.
Kenya wamepiga hatua ya wapi, unaishi kenya mkuu, au unasikiliza kupitia BBC Swahili

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tanzania cjui nani katuroga, huko vijijini watoto wanakaa chini si angalau wameletewa viti hivi wasome
 
Majibu yako ni kama ifuatavyo;

1: YALE NI MSAADA so yapite BURE, na atakayenunua atalaaniwa na Mungu wake yeye binafsi.
2: Ametumia utaratibu wa sheria mpya ambayo haijaundwa bado, ya kuagiza mizigo kwa jina lako binafsi na kuomba msamaha wa KODI
3; Aliyakana kwasababu hakusikia vizuri jina lake km limetamkwa, si unajua mara Daudi Bashite, mara Boy from Koromije, mara Paulo Makonda, yani majina mengi so yanachanganya sometime.
4: Watatunga na kutumia sheria mpya ambayo itaondoa vuguvugu lote hili, sheria mpya itaruhusu mtu binafsi kuingiza mizigo ya misaada na kuitoa free.
5: Waliandika makonda kwasababu Diaspora wanamfaham kama Makonda, wangeandika bashite yasingefika,

Subiri ujio wa sheria mpya,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
asante kwa majibu asanteeh.... IN MAKINDA'S VOICE
 
Lakini kibaya zaidi ambacho watu hawakioni ni kwamba, hizi laana na lawama anazozirusha kwa serikali inaleta picha kwamba haifuati wala kuheshimu taratibu.

Ni kandamizi na ya kibabe. Hivi kweli wahusika wa Forodha, TPA na mawaziri wameshindwa kabisa kuelewa kwamba hivyo vitu vinaenda kusaidia watoto? Hiyo ndio picha tunayoipata kwamba anaonewa, lakini Je, ni kweli anaonewa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…