Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Wezi gani wapumbavu hivi?
Yani walishindwa hata kwenda Malawi.
Unaiba 2bil unaenda Mbeya?
Pumbavu.
[/QUO
Huo ndiyo ulikuwa uwezo wao wa kufikiri, kwa hiyo tusiwalaumu. Mtu hajawishika hata milioni 2 lazima apate kiwewe cha kushika fedha nyingi kama hizo.
Wale waliokuwa wanakata paa wangekamata hizo billions 2 wasingechukua nusu 😆hawa na wale wa NBC wote sawa tu akili zao. kuna mwenzao yule aliyejaribu kukata paa aingie
Mshahara wao elf 80 halafu wanapaewa 2bill kweli? Sio sawa kabisa.Hao watu wanaopewa jukumu la kusafirisha billion 2 kutoka point A kwenda Point B wanalipwa mshahara bei gani?
Tuanzie hapo kwanza.
[emoji23][emoji23] umasikini kitu kibaya sanaKuna usemi unasema "hatua zote tisa"
Umeamua kutenda kitu hiyo ni hatua ya kwanza, kwanini usimalizie tisa?
Ushaamua kuiba kiasi kama hicho, unachotakiwa umalizie hatua za kukata mawasiliano na ndugu, kupotea nchini, kuacha ujinga, kuacha kuwaza nini kitatokea usipowaona ndugu zako...
Sasa umefanya hatua ya kwanza, zinazofuata ni kununua power tiller, sanlg na flat screen ya Sunda? Upo sawa kweli?
Yaani kama ni mme unamwambia kabla ya kufungwa andika kabisa talaka maana hapo hakuna kitu kabisaEti wamenunua tv moja ya sunda..[emoji23][emoji23]ovyo sana hawa jamaa
Wezi gani wapumbavu hivi?
Yani walishindwa hata kwenda Malawi.
Unaiba 2bil unaenda Mbeya?
Pumbavu.
Huo ni umasikini wa akili[emoji23][emoji23] umasikini kitu kibaya sana
Umesahau godoro na kitandaHapo mtu kanunua TV yake flat akatupa chogo... Akawa anafuatilia taarifa za habari kwa makini huku pawatila ina pumua nje ikingoja msimu wa kilimo uanze... Hahaaaaa
Yaani walichanganyikiwa kuona mabundaUmesahau godoro na kitanda
Unalimpa mtu 200,000 mshahara alafu huyo Huyo unambebesha fedha mabilion asafirishe, kama mtu una tamaa utaingia kingiAisee hizi kampuni za ulinzi now zinapoteza Credibility kabisa
Labda kumbukumbu zangu haziko sawa... Ni lini kumekuwa na maandamo halali yanayo mwambia ukweli YESU!!!JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIAJeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam linawashikilia watu 32 kwa tuhuma za wizi wa fedha kiasi cha Tsh Tsh Bil 2.082.00
WIZARA YA MAMBO YA NDANI
JESHI LA POLISI TANZANIA
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
KUKAMATWA KWA WATU 32 KWA TUHUMA ZA MABILIONI YA BENKI YA NMB JIJINI DSM.
Mnamo tarehe 08/06/2020 majira ya saa tisa mchana huko katika Benki ya NMB tawi la Mbezi
Beach wafanyakazi watano wa kampuni ya ulinzi ya SECURITY GROUP OF AFRICA @ SGASecurity Tanzania Limited wakiwa na gari namba T 853 DPX MITSUBISH CANTER walikabidhiwa kiasi cha fedha Tsh Tsh 2 /= kwa maelekezo ya kuzisafirisha kutoka NMB tawi la Mbezi Beach ili wazipeleke tawi la NMB Benki House - CASH CENTRE iliyopo maeneo ya Posta Mpya.
Mara baada ya kukabidhiwa fedha hizo wafanyakazi hao badala ya kuzipeleka walipoelekezwa, walitoweka na fedha hizo.
Jeshi la Polisi Kanda Maalum DSM siku hiyo ya tarehe 08/06/2020 majira ya saa 12 jioni lilibaini kutelekezwa kwa gari hilo maeneo ya Mbagala rangi tatu jirani na Shule ya SAINT MARY.
Jeshi la Polisi Kanda Maalum kupitia kikosi kazi chake cha kupambana na ujambazi lilianza ufuatiliaji mara moja ikiwa ni pamoja na kufika eneo lilipoonekana gari hilo na kubaini kuwa wafanyakazi hao watano wamekula njama na kuiba kiasi cha fedha Tsh kutoka kwenye sanduku moja la chuma kati ya masanduku manne waliyokabidhiwa.
Aidha, masanduku matatu yaliyokutwa katika gari hilo yalifunguliwa na kukutwa na kiasi cha fedha Tsh 1,302,000,000 /= pia katika gari hilo zilikutwa silaha mbili aina ya Short gun Pump Action yenye risasi 12 na Short gun Protector yenye risasi 05, pamoja na sare za kampuni hiyo.
Watuhumiwa hao walikamatwa Mkoa wa Mbeya na Kigoma wakiwa wamenunua vitu vifuatavyo:-
(i).Trckta Power Tiller aina ya TRA-Change Model 7C/15 lenye thamani ya Tsh 20,000,000/=
(ii),Pikipiki moja aina ya SANLG
(iii).TV flat screen moja aina SUNDA na vitu mbalimbali vya matumizi ya ndani kama kitanda, godoro,jiko la gesi,rnakochi n.k
Mpaka sasa katika shauri hili Jumla ya Tsh 1,497,680,000/= zimeokolewa, mbali na thamani ya vitu vilixyonunuliwa kutoka sehemu ya fedha zilizoibiwa.
Jumla ya "'atillnuniwa 32 wamekamatwa na kuendelea kuhojiwa juu ya ushiriki wao kuhusiana na tukio hili
Aidha Jeshi la Polisi linaendelea na msako mkali ili kuwakamata watuhumiwa wote waliohusika na tukio hili.
ONYO KUHUSU MAANDAMANO YANAYOHAMASISHWA KUPITIA MITANDAO YA KIJAMII
Jeshi la Polisi kanda Maalum Dar es salaam linatoa onyo kali kwa kikundi au mtu yeyote atakayeshiriki maandamano hayo batili tarehe 07/07/2020 kwa madai ya kudai Tume huru ya uchaguzi waaache mara moja vinginevyo watashughulikiwa kwa mujibu wa sheria.
LAZARO B. MAMBOSASA- SACP KAMANDA WA POLISI KANDA MAALUM DAR ES SALAM.
06/07/2020
View attachment 1498964View attachment 1498965
View attachment 1498948View attachment 1498950View attachment 1498951