David Kafulila: 35% tu ya kipato Cha mwanaume kinafika nyumbani tofauti na 90% ya Mwanamke

David Kafulila: 35% tu ya kipato Cha mwanaume kinafika nyumbani tofauti na 90% ya Mwanamke

Jabali la Siasa

JF-Expert Member
Joined
Jul 10, 2020
Posts
2,823
Reaction score
2,466
IMG-20250308-WA0287.jpg


Katika salama zake za siku ya Wanawake Dunia Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Ubia nchini PPPC Bwana David Kafulila kwanza amewapongeza wanawake wote kwa kuzaliwa wanawake.

Pili, David Kafulila amerejelea Utafiti uliofanywa na UNAC ya nchi Marekani uliokuwa na majibu kwamba Wanaume sio watu wanaozijali sana familia ukilinganisha na wanawake Kwa ni 35% tu ya kipato Cha mwanaume ndio kinafika nyumbani wakati ni 90% ya kipato cha mwanamke ndio kinafika nyumbani.

Tatu, Mkurugenzi huyo amezishauri familia ziachane na imani potofu badala yake zipeleke watoto wa kike shuleni kwani wakisoma wanafaida zaidi kwenye familia zao pengine kuliko hata wanaume.



===
 
Inawezekana ni huko USA ila kwa hapa, 99% ya kipato cha mwanaume mwenye familia inaishia kwenye familia!

Wachache wanaotumia kilevi, pengine ndo hiyo 1% anaitumia kwake binafsi kwenye kilevi na vitobo kama ni mtumiaji wa mara kwa mara.

Aache uchawa wa kike...inasikitisha kuona wanaume wamegeuka kuwa wanawake ili kutetea ugali wao.
 
Inawezekana ni huko USA ila kwa hapa, 99% ya kipato cha mwanaume mwenye familia inaishia kwenye familia!

Wachache wanaotumia kilevi, pengine ndo hiyo 1% anaitumia kwake binafsi kwenye kilevi na vitobo kama ni mtumiaji wa mara kwa mara.

Aache uchawa wa kike...inasikitisha kuona wanaume wamegeuka kuwa wanawake ili kutetea ugali wao.
Wanaume wanajitahidi sana kuhudumia familia Mimi naona ni 100% tunapeleka home
 
Aache kutuharibia,analeta takwimu za wanaume wachache ambao hawako responsible na familia zao ili kutafuta umaarufu kwenye majukwaa...
 
Hapo anapoongelea familia ni ile familia aliyozaliwa mwanamke, yaani kwa lugha nyingine ukioa mwanamke atahakikisha 90% ya kipato chake kinaenda upande aliotokea, halafu mkija kuachana inabidi agawane 50% ya mali za mwanaume
 
Hapo anapoongelea familia ni ile familia aliyozaliwa mwanamke, yaani kwa lugha nyingine ukioa mwanamke atahakikisha 90% ya kipato chake kinaenda upande aliotokea, halafu mkija kuachana inabidi agawane 50% ya mali za mwanaume
Hii ni kweli wanapeleka makwao walikozaliwa sio home
 
Huyu naye anataka kuzeeka vibaya tupeleke pesa zote nyumban ili iweje?
 
Huyu naye anataka kuzeeka vibaya tupeleke pesa zote nyumban ili iweje?

Inawezekana ni huko USA ila kwa hapa, 99% ya kipato cha mwanaume mwenye familia inaishia kwenye familia!

Wachache wanaotumia kilevi, pengine ndo hiyo 1% anaitumia kwake binafsi kwenye kilevi na vitobo kama ni mtumiaji wa mara kwa mara.

Aache uchawa wa kike...inasikitisha kuona wanaume wamegeuka kuwa wanawake ili kutetea ugali wao.
Utafiti hauwezi kuwa tofauti
 
Haya mambo ya kujipendekeza kisa Mkubwa ni mwanamke yanatia kinyaaa.

Hawa hawa wanawake hela zao ambazo zinaliwa na Manabii na Waganga?
Hawa hawa wanawake hela zao ni kwajili ya mama zao na familia zao?

Mtu una ishi na mwanamke ambae ana kazi ila atakuomba hadi hela ya saluni.

Ada, kodi, vyakula , usafiri zote zina muhusu baba.

Ni wanawake wachache sana wanatumikia familia kwenye hela yake .
 
Haya mambo ya kujipendekeza kisa Mkubwa ni mwanamke yanatia kinyaaa.
Huyo aambiwe ukweli, kuwa hayo ni kwa viumbe kama tumbili huko mwituni siyo huku kwetu
 
Back
Top Bottom