Dawa ya Umaskini, madeni, ukata, mifuko kutoboka, uhitaji, kufilisika hii hapa!

Mungu huyu huyu ambae kuhani wake mkuu wa Dunia anasema watu wa jinsia moja tuoane!!

Sawa tumekusikia mchungaji
 
Barikiwa sana,Uzi mzuri,umeinua kiwango Cha Imani yangu Kwa namna Fulani....hakika nitamjaribu Mungu
Mimi ndo kamekuwa kamchezo kangu kitambo sasa.

Nikitaka kuanza ujenzi, naanza na sadaka,

Naweza Anza ujenzi nikiwa na lak 5, nitajenga Hadi namaliza laki Tano Iko pale pale,

Natumia ktk ujenzi nalipa Kila kitu na haikauki, Kila nikienda kazini napata ya kijaziliza laki 5,

Majirani wasonifahamu hudhani labda mm ni Tajiri sana kumbe wap!!
 
Mungu huyu huyu ambae kuhani wake mkuu wa Dunia anasema watu wa jinsia moja tuoane!!

Sawa tumekusikia mchungaji
Huyo Si kuhani wake mkuu duniani ikiwa anasema machukizo hayo.

Jikite kwenye mada mjaribu Mungu kupitia matoleo na uje utupe ushuhuda.

Amen
 
Uwaambie pia sio watoe sadaka halafu waende wakawaf.ire watoto wawatu..watasema kila siku wamerogwa..watende pia matendo mema.
Huwezi pata pesa za Muujiza wa Mungu halafu upate ujasiri kutenda UOVU.

HAKIKA Imani Yako ikikua, utazama deep kumtafuta kumjua Mungu zaidi.

Ubarikiwe.
 
Sahihi na nimeshuhudia mkuu
Share nasi ushuhuda wako kama hutojali,

Watu humu tukiwaambia maandiko yasemavyo wanadhani ni hadithi, lakini tukishuhudia uhalisia wa applicability wa kulitumia NENO la Mungu kuleta matokeo chanya wataamini na kuepuka kwenda Kwa " WAPUMBAVU " Waganga na wapiga tunguli.
 
Ety kupata pesa za haraka!!

Wachungaji wa siku hizi mna shida sana.
Ndio, njia hii Mungu hujibu haraka sana.

Imagine una akiba pekee ya lak 2 Kwa Mfano,

Ukiichukua yote na kumjaribu Mungu Kwa kuwapa maskini chakula, au wenye uhitaji,

Mungu hawezi kuruhusu ulale njaa,

Atajibu haraka sana.

Nikuambiayo Si hadithi, ninatumia njia hii Mimi.

Amen
 
Mimi ndo kamekuwa kamchezo kangu kitambo sasa.
Kamchezo!!!?????

You can't be serious we mtoto, Mungu hajaribiwi kijinga namna hiyo like you do.

Huyo Mungu unayemchezea hako kamchezo utakuwa unamjua mwenyewe tu, Siyo huyu Mungu mkuu wa Ibrahim, isack na yacob.
 
Ubarikiwe.

Baraka za Mungu hazina majuto.

Mungu Mbinguni anatushangaa tunapolia ukata na wakati amekataza mwanadamu kumjaribu Mungu Kwa mengine isipokuwa katika matoleo, sadaka na ZAKA.

Amen
kuna jambo nimelipata kuna magumu napitia sana ni mwaka wa pili chungu sana kwangu ngoja nifanye na nishitakie baadhi ya mambo juu yake
 
Ungewashauri kwanza wachungaji wenzio watumie hiyo njia uchwara ili waache kulia lia shida kwa waumini.
 
Good,
Yatupasa tutambue kwamba chochote ambacho MUNGU ametubariki ndani yake ameweka mbegu.
Tusile mbegu bali tupande mbegu
 
Daaah hivi hapa wanaruhusiwa kutukana? Au niku dm kwa matusi makubwa sana
Usitukane,

Nenda kamjaribu Mungu Kwa kuwanunulia chakula yatima wanaorandaranda usiku huu Kwa akiba ndogo iliyo nayo ukimjaribu Mungu sawasawa na (Malachi 3:10-12).

Amini nakuambia, utajibiwa haraka sana, na utarudishiwa zaidi ya ulichotoa.

Amen
 
Good,
Yatupasa tutambue kwamba chochote ambacho MUNGU ametubariki ndani yake ameweka mbegu.
Tusile mbegu bali tupande mbegu
Amen,

Dunia ingejua kuwa kipato mtu akipatacho Si chake pekeake,

Mungu humpa mtu riziki na ndani ya riziki hiyo Huwa ameweka pesa Ili iende Kwa wengine kupitia sisi,

Ukila yote pekeako, unakula mbegu,

Ubarikiwe.
 
Kamchezo!!!?????

You can't be serious we mtoto, Mungu hajaribiwi kijinga namna hiyo like you do.

Huyo Mungu unayemchezea hako kamchezo utakuwa unamjua mwenyewe tu, Siyo huyu Mungu mkuu wa Ibrahim, isack na yacob.
Mungu ameruhusu kujaribiwa kupitia matoleo pekee.

So Mbingu zinatushangaa kuwa wahitaji ilhali IPO KANUNI ya kumjaribu Mungu na hatuitumii kupata pesa.
 
Sifanyi tena huu useenge labda Mungu anipe hayo maelekezo yeye mwenyewe
 
Amen, kuna siku kuna hela nilikua naiexpect muda mrefu na ikawa imekwama. Sasa hiyo siku, nilikua nasikiliza video ya mafundisho ya kiroho, mchana hivi. Katika kusikiliza prayer request, nikasikia mama mmoja akituma message namna ambavyo anapitia shida kali sana. Kumbuka na mm hapo nina shida na hela.

Sasa kwenye simu nilikua na 23000. Nilivyoingia kwenye yale maombi, nikasikia Roho Mtakatifu anasema omba namba ya huyo mama umtumie hiyo 20k. Nikataka kuobject kwamba mi mwenyewe apeche, Roho akanisisitiza sana. Basi nikasema sawa, hakuna shida. Baada ya prayer session, nikapiga simu redioni kurequest namba za huyo mama. Immediately nimekata ile simu, baada ya dkk moja, ikaingia ile hela niliyoisubiri kwa muda mrefu iliyokuwa imekwama.

Nilimshangaa sana Mungu. Sometimes ukiwa tayari kumtoa Isaka, Mungu huleta mwanakondoo na kukurejeshea tumaini mara moja. Hakika Bwana yu mwema.
 
Sifanyi tena huu useenge labda Mungu anipe hayo maelekezo yeye mwenyewe
Itakuwa ulienda kupeleka sadaka Yako Kwa manabii wa uongo, wakakufunga.

Nenda saizi mpe Jirani Yako maskini mhitaji, au kamlipie maskini aliye hospitali, mnunulie madawa na lipa bill zake utaniambia.

Ubarikiwe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…