Dawa za Kulevya: Freeman Mbowe akamatwa na Polisi; ahojiwa na kuachiwa

Dawa za Kulevya: Freeman Mbowe akamatwa na Polisi; ahojiwa na kuachiwa

Huu nao ni upepo utapita kama yalivyopita mengine!
hata tundulissu huwa wanamkamata kwa mbwembwe mwisho wa siku wanaaibika
 
Mkuu tusaidie hizo njia za kukimbia na kujificha,
zimeshindikana kivipi?
maana hata Tundu lisu alikamatwa bungeni
Dodoma au naye alishindwa kukimbia na kujificha?
 
ukitaka uamini nenda kisongo aliko rais wa arusha cell anayolala na wengine yule anatunzwa guest utamkuta ananawili tu kamatwa wewe baada ya cku mbili chawa had miguuuni jifunze
 
Mbowe hana tuhuma zozote,chuki za matajiri zinawasumbua sana utawala wa awamu ya tano lakini mwisho wa siku matatamani Dunia iapsuke mwingie ndani yake??

Mmefanya haya sababu ya kesi ya kesho ili muikimbie,na hamtaikimbia.
angeenda wiki iliyopita angeokoa muda. Kama mwananchi wa kwaida anachukuliwa mtaani anakwenda kuisaidia polisi Huyu kiongozi wa wananchi anashindwaje kujitolea asaidie kuwa mfano kwa maelfu ya wananchi wanaoangamia na kuteketea kwa madawa. hayo mengine ni hisia zako tu mkuu
 
mashujaa na majasiri hawajipelekagi wenyewe polisi hata siku moja. ni kazi ya polisi kuwatafuta.
Ila ni hatari waweza askari kuja na mizinga na vifaru na mabomu wakapiga ulipojificha kwa kuwa hawajui una nini huko ndani ulikojificha.Ni hatari kubwa kuliko kujisalimisha
 
Mboww kaenda mwenyewe hajakamatwa
Lakini ndimi za watesi wake zitagandamana na kaka la vinywa vyao na ushahidi wao utaangukia kubaya. Atainuliwa miongoni mwao na kwa aibu yao
 
Umemjibu vyema. Kwa sababu unabwia unga usikamatwe kisa unaowahisi bila ushahidi hawajakamatwa?
akipimwa akakutwa anatumia madawa atolewe uenyekiti, Akiendelea maana yake ni kivutio kwa vijana wa chadema kufuata njia na taifa kuwa la wagonjwa. Haki itendeke tusijifiche kwenye huruma za wananchi
 
Asa anajificha nn? Mbowe nae wasela wawakimbie police na yeye! Kweli mamwera noma
 
Mjue anawaona lakini- anawajua na kuwafahamu-akiwataja majina yenu na wapi vitovu vyenu vilipofukiwa mtakua tayari kusimama.
 
Hakuhusishwa na dawa za kulevya Mandela usimlinganishe na Mbowe.Mandela alihesabiwa kama mhaini wa kisiasa sio wa madawa ya kulevya.
Hii nayo ni siasa tu! Unamsamon mtu kwa kutumia runinga wakati namba yake ya simu unayo, ofisini na nyumbani kwake unakujua? Hii nayo ni siasa tu.

Unapoona nguvu kubwa inatumika kuwatafuta wabwia unga tena kwa kutumia runinga wakati, wangeenda na malori 50 kwenye baadhi ya maeneo dar wangewapata wengi zaidi ya hao 340 plus.

Hii ni vita ya kisiasa. Yawezekana hujui au unajifanya hujui sasa lakini huo ndo ukweli, na uweli huwa hauna maficho ya kudumu.

Time will tell!
 
Back
Top Bottom