DAWASA Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na ushauri

DAWASA Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na ushauri

Naomba kujua mpango wa DAWASA kufikisha majisafi Chanika Mjini. Kumbukeni pale kuna idadi kubwa sana ya watu ambao nadhani ni advantage kwenu
 
Nmesafiri yapata miez 4 narud wiki hii kuchek bili ya maji tsh 78,780

Kazi iendelee....
 
Dawasa tunaomba mjibu maswali yetu humu,..inamaana gani kuwepo humu halafu hamjibu malalako ya watu?
 
Ndugu wana JamiiForums,

Tunashukuru kwa maoni yenu mliyoweka hapa juu ya huduma mnazo pata kwenye matawi yetu yaliyo Jijini Dar es salaam , miji ya Kibaha na Bagamoyo Mkoani pwani. DAWASCO inapokea maoni na malalamiko yenu na tuna wahakikishia kuwa tutachukua hatua stahiki kwa haraka zaidi.

Ndugu wana jukwaa, DAWASCO inajipambanua kwa kusimamia maadili ,kutoa huduma iliyotukuka pamoja na kuhakikisha huduma ya Maji inapatikana kwa kila mwananchi.

Kama kutatokea kuharibika kwa bomba, wizi wa Maji, umepata huduma isiyo ridhisha au ufanyaji kazi usiofuata maadili, uaminifu na uadilifu, tafadhali toa taarifa kupitia njia zifuatazo:

1. Kupitia tovuti: DAWASCO - Welcome to new site
2. Kupitia mitandao yetu ya kijamii ikiwa ni pamoja na Twitter|DawascoOfficial..Facebook|DawascoOfficial ...Instagram|DawascoOfficial
3. Kwa mwananchiposta ; Unaweza kutuma barua kwa Afisa Mtendaji kama ifuatavyo:

Afisa Mtendaji Mkuu
DAWASCO
P. O. Box 5340
Sokoine Drive
Dar es Salaam, Tanzania.

4. Au kwa kupiga simu huduma kwa wateja dawasco
0800110064 /022 2164800 ( Kupiga namba hizi ni Bure)

DAWASCO HUDUMA KWA WATEJA 0800110064
DAWASCO ILALA 0743 451879
DAWASCO KAWE 0743 451861
DAWASCO KIBAHA 0743 451875
DAWASCO KIMARA 0743 451865
DAWASCO KINONDONI 0743 451863
DAWASCO BAGAMOYO 0743 451877
DAWASCO MAGOMENI 0743 451862
DAWASCO TEGETA 0743 451881
DAWASCO TABATA 0743 451867
DAWASCO TEMEKE 0743 451866

Sioni namaba ya Kinyerezi, mana tuliomba maji watu wengi tu hapa Ukonga Sabasaba karibu na Ofisi za Serikali za mitaa karibu na reli ya kati, hadi leo kimya. Tunaomba tujulishwe kinachoendelea.
 
Hivi unit 1 ni sawa na lita ngapi za maji?

Naomba anayejua anisaidie maana nahisi wasoma meter wa dawasa ni waongo kabisa na ni wezi wakubwa.
 
Hilo sijui.
Poa mkuu Nitafatilia maana nimetumiwa bill eti nimetumia unit 70 ambayo ni = 119, 253.73 !?

Matumizi yangu ya maji huwa ni lita 3000 tu kwa mwezi ambapo mara ya mwisho kulipa nililipa 10k.

Sijawaelewa kabisa dawasa kwa hizo unit 70.
 
Dawasa mnachosha sana
mita yangu imeharibika miezi6 sasa ime stuck hamtengenezi mkiambiwa hamji, ila ikifik tarrehe 20 natumiwa bill unit za kutosha wakati mi mwenyewe kipindi inasoma kwa mwezi nilikua natumia unit9 sizi mnanitumia unit 15
nalalamika naambiwa inabidi nilipe ndo washugulikie la sivyo wanakata maji!! uyo msoma mita mwenyewe anakuja kunikatia maji bila maelezo yani sijalipa mwezi mmoja wa 2 natumiwa bill na kuja kukatiwa maji!!! Bongo [emoji114]
 
Back
Top Bottom