ChoiceVariable
JF-Expert Member
- May 23, 2017
- 66,537
- 75,687
Aliharibu kuchukua hatua ndio wakamsinitch,hivi unaijua serikali au Watzn walivyo wewe?Alikuwa na kila madaraka kabla ya kutumbuliwa, alifanyaje kudhibiti hayo yote??
Huu waraka wake japo alihisi utasaidia kumfanya aonekane kiuhalisia umezidi kumuharibia na kudhihirisha kuwa hakuwa sahihi kwa nafasi aliyopewa maana alishindwa kuzuia ujinga wote huo.
Aandike wakati ni wajibu wake kuchukua hatua? Amesema alikuwa anakwamishwa na Kuna watu wanawalinda Hawa wapigahi..Alitakiwa kuandika akiwa kwenye nafasi yake sio saiv anaonekana kulilia tonge lilipokonywa ktk mdomo wake
Kelele tuAandike wakati ni wajibu wake kuchukua hatua? Amesema alikuwa anakwamishwa na Kuna watu wanawalinda Hawa wapigahi..
Iko.hivi wakurugenzi na wakuu wa idara Huwa ni mawakala wa wapigahi wa wizarani na Iko hivyo kwenye ngazi na taasisi zote..
Mchengerwa aliwaondoa maafisa manunuzi wote pale Tarura kilichofuatia ni yeye kuundiwa zengwe na kuondoshwa utumishi,Bashungwa hivyo hivyo nk..
Yaani Hadi Wakandarasi wanaotumiwa na wakubwa huku Juu wewe Meneja wa chini au mtumishi ukisimamia utaratibu unaondoka hapo ndio Utajua hujui..
Hakuna Cha mfupa, sababu kubwa ni 2.Halmashsuri ni mfupa uliomshinda fisi.
Kinondoni karibu barabara zote ni za lami, mpaka zinazoishia majumbani mwa watu zimewekwa lami, au kule ndio kuna makao makuu ya TARURA Tanzania? Ukipita makumbusho, Sinza, Mwananyamala, Mwenge, Tandale kote ni lami tu..Sio swala la mbunge Wala nini hapo ni serikali iongeze Bajeti Tarura.
Tarura Nchi nzima Wana mtandao wa Barabara zaidi ya km 180,000 na zinazaliwa Kila siku kadiri mijininavyokua harafu Bajeti yake ni Bil.800 tuu ikiwemo Mishahara na uendeshaji Sasa unategemea nini hapo?
Halafu wakazi wa Dar ukiwasikia humu JF wanavyojisifia maisha mazuri utadhani wanaishi Marekani kumbe hovyo tu.Kutoka malamba mwisho kwenda king'azi ile barabara ni muhimu sana lakini sijui kama mbunge na diwani wanaifikiria,kwenye suala la maji safi na salama huko king'azi mpaka leo wananchi wanatumia maji ya tope,za chini ya kapeti zinadai huyo mtemvu ana canter za kuuza maji na ndio anatia ugumu wa maji ili yeye na macartel wenzake wa maji waendelee kuuza maji kwa raia,huduma ya afya wananchi ndio awaelewi kabisa!
Huyu nae ni kinyaa ndo maana mama alimtumbua
Na kama DC amekumbana na upinzani basi Hali ni mbaya Sana.Watanzania wanapenda mizaha sana, Mtu alikuwa DC anajua uchafu wote unaofanyika kwenye halmashauri badala tuungane kupinga uozo huo tunamlaumu tena aliyetufumbua macho.. ukumbuke hilo eneo la Korogwe lina wabunge 2 lakini hujawahi kuwasikia wakipaza sauti juu ya matatizo hayo hadi akabaki DC peke yake na RC Mgumba ambao wote wametumbuliwa
Kinondoni ni kama CBD huko lazima kuwe na lami,Miji yote mjini Kati na wanakoishi viongozi au taasisi za serikali Kuna lami.Kinondoni karibu barabara zote ni za lami, mpaka zinazoishia majumbani mwa watu zimewekwa lami, au kule ndio kuna makao makuu ya TARURA Tanzania? Ukipita makumbusho, Sinza, Mwananyamala, Mwenge, Tandale kote ni lami tu..
Ila kama vipi Barabara zingerudishwa Halmashauri hawa madiwani wangetumwa kuzifuatilia kwa nguvu kwa kuwa zipo kwenye mamlaka yao. TARURA ni upigaji mwingine tu, maofisi mengi kwa kazi ambayo ingeweza kufanywa na DED. Yaani TARURA ni kama cheo cha DC kisivyo na ulazima kuwepo.
Hii ni kwa jamii ya watu wasiojitambua. Kodi mnalipa wote ila maendeleo yafanyike kwenye makazi ya viongozi. Ndio maana nasema ni vyema barabara zingerudi Halmashauri, hapo zingetengenezwa kwa uwiano. Kila halmashauri ingejitengenezea barabara zake itakavyo, hizo pesa za ruzuku wanazopewa TARURA zingepelekwa moja kwa moja kwa kila halmashauriKinondoni ni kama CBD huko lazima kuwe na lami,Miji yote mjini Kati na wanakoishi viongozi au taasisi za serikali Kuna lami.
Kwa hiyo elewa kwamba kidogo kinachopatikana kitapelekwa kwanza kwenye maeneo yenye sifa hizo
Hakuna uwiano uliowahi kufanyika Toka zama hizo za Halmashauri,diwani yupi anaweza Pinga uamzi wa ded na DC?Hii ni kwa jamii ya watu wasiojitambua. Kodi mnalipa wote ila maendeleo yafanyike kwenye makazi ya viongozi. Ndio maana nasema ni vyema barabara zingerudi Halmashauri, hapo zingetengenezwa kwa uwiano. Kila halmashauri ingejitengenezea barabara zake itakavyo, hizo pesa za ruzuku wanazopewa TARURA zingepelekwa moja kwa moja kwa kila halmashauri
Mkuu.Kwanza tatizo anafunguka kinafki.
Alipokua na cheo kwenye Wilaya hiyo hiyo hakufanya chochote, ametoka kwenye cheo ndio anaongea hapo tumueleweje kama sio alikua na ugomvi na mkurugenzi.
Diwani ndiye muwakilishi wa wananchi, DED au DC hana mamlaka yoyote kwa fedha ya Halmashauri, DED yeye ndiye anaelekezwa nini cha kufanya na madiwani.Hakuna uwiano uliowahi kufanyika Toka zama hizo za Halmashauri,diwani yupi anaweza Pinga uamzi wa ded na DC?
Hujui kitu wewe endelea kuhadithiwa hivyo hivyoDiwani ndiye muwakilishi wa wananchi, DED au DC hana mamlaka yoyote kwa fedha ya Halmashauri, DED yeye ndiye anaelekezwa nini cha kufanya na madiwani.
Bahati mbaya tulikuwa au mpaka sasa tuna madiwani wasiojua mamlaka yao iko wapi, hata hivyo wananchi tumeanza kuwasanua madiwani kuhusu mamlaka yao ndio maana unaona halmashauri kadhaa sasa zinaomba CAG aingie kati kufanya ukaguzi maalum, madiwani wameanza kujitambua. Kwa kuwa tunakwenda mbele, haturudi nyuma naamini hata barabara wangekomaa zijengwe kupitia vyanzo vyao vya ndani pamoja na ruzuku (miradi ya maendeleo).
Binafsi nashangaa viongozi kutumia Halmashauri kama punching bag mngejua pesa zinazopotea mawazarani mngechoka kabisa kule bajeti ya seminar na viburudisho tu zaidi bilioni moja,Bado posho za safari na mengineyoHakuna Cha mfupa, sababu kubwa ni 2.
Mosi mfumo mbaya wa Usimamizi ngazi ya Halmashauri yaani serikali kuu kuweka mkono wake inafanya Halmashauri kuwa wakala wa Serikali kuu.
Pili ni kutokuwa na Mamlaka kamili Kwa ngazi hiyo kunasababisha madiwani hawana Cha kumfanya Mkurugenzi Wala DC
Mwisho kazi ya Halmashauri ni kuratibu upigaji wa wakubwa kama unavyoona Polisi wanafanya.
Apumzike kwa amani, aache kiherehereKinyaa chake ni nini ? Wewe mhurumie tuu maana anauwawa sio muda mrefu!!
Kama wewe unaamini madiwani hawawezi kumbishia DC au DED basi wewe ndio hujui kitu. Tumia hata kanuni ya mwendazake ya kusema anataka apate koneksheni, maana yake ni kuwa DC angepata upinzani sana ikiwa madiwani si wa chama chake. Sijakuambia kwa makusudi usome sheria ya Serikali za MitaaHujui kitu wewe endelea kuhadithiwa hivyo hivyo
Huna akili