DCI Wambura: Uchunguzi umebaini Hamza alikuwa gaidi wa kujitoa mhanga
Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Camillius Wambura amedai kuwa uchunguzi uliyofanywa na Jeshi la Polisi umebaini kwamba Hamza Mohammed alikuwa gaidi wa kujitoa mhanga.

Hamza aliuawa na polisi Agosti 25, mwaka huu baada ya kuwaua kwa risasi askari wanne, watatu kati yao wa polisi na mmoja wa kampuni binafsi ya ulinzi jirani na ulipo ubalozi wa Ufaransa jijini Dar es Salaam.

Akizungumza leo Alhamisi Septemba 2, 2021 jijini Mwanza na waandishi wa habari Wambura amesema uchunguzi huo ulijikita katika mambo makuu matatu ambayo ni kutaka kutambua Hamza Mohammed ni nani, nini kilimsukuma Hamza kwenda kufanya tukio lile na kutaka kutambua mshiriki mwingine katika tukio hilo.

Wambura amesema katika uchunguzi huo polisi imebaini kwamba Hamza alikuwa akiishi kisiri huku akiwa amegubikwa na viashiria vyote vya ugaidi.

"Amekuwa akijifunza mambo mbalimbali kupitia mitandao ya kijamii ambayo kwa kipindi kirefu amekuwa akijifunza mambo ya kigaidi kwa kuangalia mitandao ambayo inaonyesha matendo ya Al-Shabab na makundi kama ISIS yanayoendelea na wagaidi wengi hujifunza kupitia mitandao hiyo," amesema Wambura.

Amesema kwamba kitendo alichokifanya Hamza kilikuwa ni cha ugaidi wa kujitoa mhanga.

"Tabia na matendo ya Hamza aliyapata kupitia mawasiliano aliyokuwa nayo na watu wanaoishi katika nchi zenye matendo ya kihalifu ikiwemo ugaidi hasa wa kupitia mtandao yanayojulikana kama "Radicalisation through social media)," amesema Wambura.

Kuhusu taarifa zinazodai kwamba Hamza aliwashambulia askari hao kwa sababu walimdhulumu madini yake, Wambura amekanusha na kusema katika uchunguzi huo wamebaini kwamba Hamza hakuwa na madini wala fedha katika mazingira yale.

"Hamza hakuwa na madini wala pesa na hakuwa katika nafasi yoyote ya kumiliki madini wala pesa mbali ya kwamba watu wengi wameongea kwamba alikuwa anamiliki migodi ya madini kule Chunya na maeneo ya Makongolosi uchunguzi wetu umebaini hali hiyo ya maisha ilikwisha simama muda mrefu," ameongeza Wambura.

Wambura ameongeza kuwa taarifa ya uchunguzi huo pia imebaini kwamba Hamza alikuwa kwenye kundi la magaidi wanaoamua kuifia dini.

Chanzo: Mwananchi
Kada gaidi
 
Huyu Kamanda ni muongo tena uongo wake ni wa kiwango cha Tozo za Tanzania, hivi jamani Gaidi gani ambae hataki kuuwa Raia anataka polisi tu??? Tutizame hao IS walvyo wanataka public ya watu ili wajitoe muhanga na kuwauwa watu wengi, Hamza anaonekana katika video hanaa time kabisa na Raia jambo ambalo magaidi hawalifanya hata siku 1, Polisi wasema ukweli kwanini hakuwabali kwamba baadhi yao wamekuwa si waaminifu na kumdhumu huyo hamza? Mazingira yote yanaonesha hamza alikuwa akilipa kisasi kwa polisi na si kwamba gaidi...tafsiri ya gaidi atupe kamanda kisha aseme upumbavu huu tena. Shame!
Ndio maana watu walipendekeza iundwe tume maalumu kuchunguza hili tukio na si Polisi pekee yao.
 
Ile intelijensia ya polisi ya fujo kwenye mikutano ya CHADEMA ilikuwa wapi mpaka Hamza akawa gaidi na huku ni mjumbe wa mkutano mkuu wa CCM wilaya?
Intelligence yao ya kipuuzi ati mbowe alitaka kulipua vituo vya mafuta mbona hawakusema alitaka kuwaua police. Taarifa hii ni ya uongo Cia, Scotland yard waingilie kati ukweli ujulikane
 
Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Camillius Wambura amedai kuwa uchunguzi uliyofanywa na Jeshi la Polisi umebaini kwamba Hamza Mohammed alikuwa gaidi wa kujitoa mhanga.

Hamza aliuawa na polisi Agosti 25, mwaka huu baada ya kuwaua kwa risasi askari wanne, watatu kati yao wa polisi na mmoja wa kampuni binafsi ya ulinzi jirani na ulipo ubalozi wa Ufaransa jijini Dar es Salaam.

Akizungumza leo Alhamisi Septemba 2, 2021 jijini Mwanza na waandishi wa habari Wambura amesema uchunguzi huo ulijikita katika mambo makuu matatu ambayo ni kutaka kutambua Hamza Mohammed ni nani, nini kilimsukuma Hamza kwenda kufanya tukio lile na kutaka kutambua mshiriki mwingine katika tukio hilo.

Wambura amesema katika uchunguzi huo polisi imebaini kwamba Hamza alikuwa akiishi kisiri huku akiwa amegubikwa na viashiria vyote vya ugaidi.

"Amekuwa akijifunza mambo mbalimbali kupitia mitandao ya kijamii ambayo kwa kipindi kirefu amekuwa akijifunza mambo ya kigaidi kwa kuangalia mitandao ambayo inaonyesha matendo ya Al-Shabab na makundi kama ISIS yanayoendelea na wagaidi wengi hujifunza kupitia mitandao hiyo," amesema Wambura.

Amesema kwamba kitendo alichokifanya Hamza kilikuwa ni cha ugaidi wa kujitoa mhanga.

"Tabia na matendo ya Hamza aliyapata kupitia mawasiliano aliyokuwa nayo na watu wanaoishi katika nchi zenye matendo ya kihalifu ikiwemo ugaidi hasa wa kupitia mtandao yanayojulikana kama "Radicalisation through social media)," amesema Wambura.

Kuhusu taarifa zinazodai kwamba Hamza aliwashambulia askari hao kwa sababu walimdhulumu madini yake, Wambura amekanusha na kusema katika uchunguzi huo wamebaini kwamba Hamza hakuwa na madini wala fedha katika mazingira yale.

"Hamza hakuwa na madini wala pesa na hakuwa katika nafasi yoyote ya kumiliki madini wala pesa mbali ya kwamba watu wengi wameongea kwamba alikuwa anamiliki migodi ya madini kule Chunya na maeneo ya Makongolosi uchunguzi wetu umebaini hali hiyo ya maisha ilikwisha simama muda mrefu," ameongeza Wambura.

Wambura ameongeza kuwa taarifa ya uchunguzi huo pia imebaini kwamba Hamza alikuwa kwenye kundi la magaidi wanaoamua kuifia dini.

Chanzo: Mwananchi
Bado Kuna uwalakini!
DCI hajafafanua maelezo kujibu yafuatayo;

*Kitu gani kilipelekea Hamza akawashambulia Askari TU??
Mbona DCI hoja hiyo ameikwepa?

Kama Ni ugaidi wa kujitoa muhanga, kwa Nini aliacha kujitoa muhanga sokoni, hospitalini, mashuleni au katika umati wa watu na badala yake akaamua kuwamiminia njugu askali police na akionekana mwenye jaziba kana kwamba kulikua na kisasi??

#utaelewa Ni kwa Nini Ndugai anawachukia wasomi, lengo Ni kufanywa wajinga na kuaminishwa Kila kitu!
 
Tunaliomba Jeshi la Polisi pia lifuatilie nyenendo za viongozi wa Chadema na baadhi ya wafuasi wake ambao kimsingi walifurahia sana kitendo cha Gaidi Hamza kuwauwa Askari wetu.
hii inathibitisha kuwa viongozi wa Chadema na baadhi ya wafuasi wao wana kila dalili za kujihusisha na vitendo vya Kigaidi ndio maana walifurahia vitendo vilivyo fanywa na Hamza.
ni muhimu sana wafuatiliwe popote pale walipo ktk kila kona ya nchi hii.

nasisitiza tena Jeshi la Polisi kamwe lisivumilie vitendo vya viongozi wa chadema na baadhi ya wafuasi.
 
Askari wetu kuna vitu wanaongea kwa maslahi yao yenyewe bila kujua wanaitumbukiza nchi pabaya zaidi
Hakuna mtu anaweza kuja kuwekeza kwenye nchi ambayo inaugaidi
 
Uchunguzi wa tukio la Tundu Lissu kushambuliwa haujakamilika mpaka leo zaidi ya miaka mitatu lakini tukio la Hamza ndani ya siku kumi uchunguzi umekamilika. Hili ndio Jeshi letu la polisi. 🤔
 
Taarifa hizi zifike kwa mabalozi wote kuwa Tanzania kwasasa ni sehemu hatarishi kwa Ugaidi.
Magaidi wa Tanzania wana sifa tofauti na wa nchi nyingine. Hizo taarifa ingekuwa vizuri wakashare na mataifa mengine kuisadia dunia njia mpya ya kuwa profile magaidi.... Yaani hapa tumewazidi FBI na Scotland Yard. Wambura inabidi kwa hili apewe tuzo la kimataifa. Magaidi wawili TZ wenye vigezo tofauti na magaidi wengine duniani.
 
Ivi kama taifa tupo concerned na Swala la ugaidi na impact zake kila anayetokea tuki portray kama Gaidi haitaleta Shida kitaifa?
 
Mjumbe wa mkutano mkuu wilaya ccm ni GAIDI..!
Naamini bado wengi sana ndani ya chama wamchunguze na ndu..guy ile video animcharaza mwanaccm mwezake bakora naona wazi kuna ugaidi mkubwa ataufanya badae.
Ccm ni chama cha kuzalisha magaidi 😬😬
 
Watanzania sio wajinga.

Watu wa Chunya huko Makongorosi walikuwa wanamkubali Hamza. Aliahidi kujenga shule, aliajiri watu kibao.

Leo Dci Wambura unadai Hamza alikuwa amepoteza Chanel. Hakuwa na mbele wala nyuma.

Bastola aliyotumia kufanya uhalifu alitoa wapi?

Kwa hiyo unataka kusema alikuwa vagabond?
 
Mkuu tuipumzishe familia yake..wanapitia kipindi kigumu

Case closed[emoji4][emoji4][emoji4]
 
Wao wameona wafiche aibu yao kwa kusingizia dini yake maana kwao wao mtu akiwa muislam ni gaidi,kama wao walijua alikuwa na viashiria vyote vya ugaidi kwa nini walishindwa kumkamata mapema? Wao warudishe tu dhahabu za marehemu.
 
Wao wameona wafiche aibu yao kwa kusingizia dini yake maana kwao wao mtu akiwa muislam ni gaidi,kama wao walijua alikuwa na viashiria vyote vya ugaidi kwa nini walishindwa kumkamata mapema? Wao warudishe tu dhahabu za marehemu.
Ukweli huwa haujifichi.
 
Back
Top Bottom