Dededege inamtesa sana mwanangu, wakuu nisaidieni dawa

Dededege inamtesa sana mwanangu, wakuu nisaidieni dawa

Samahani mkuu, inawezekana wengine tulipitwa na huo uzi.

Kama haitachukua muda wako, kwa ufupi kabisa, kijana wetu ana shida gani?
1. Ilianza lini?
2. Maendeleo ya ukuaji wake yapoje?
3. Ulishawahi kufanya EEG?
4. Dawa gani anatumia?
Shida ni degedege, anakuwa vizuri.. uzito unaongezeka.. muonekano mzuri, dawa anatumia kwa sasa sodium valproate na hio EEG sijui ni kipimo gani??
 
Poleni sana. Mimi nakushauri usichoke kuzunguka hospital. Kuna ugonjwa mwingine unaweza kuzunguka hospital hata nne kabla hujapata dr atakayetambua tatizo. Jingine uwe mwangalifu kwani binadamu siku hizi wamekuwa wanyama. Kuna mtu anaweza kuwa na ujasiri wa kutumia shida yako na akakupiga fedha nyingi kwa kisingizio cha kuwa anakupa dawa. Nakushauri usitoe fedha kwa hizi dawa za kienyeji kwani wengi ni matapeli. Mwenye nia nzuri atakusaidia kwanza mtoto akipona ndiyo utajua cha kufanya.
HUU NDIO USHAURI NILIOUBEBA, KWA WALE MLIONIPIGIA SIMU..TAFADHALI NAZINGATIA HILI..UBARIKIWE MKUU
 
Habari ya mudaa huu wakuu, nilishawa kuja kuomba ushauri kuhusiana na tatizo la mwanangu, baadhi ya watu walipa ushauri tukafanya CT SCAN pale benjamini lakini hakuwa na tatizo lolote kwenye kichwa.

Nimerudi tena wakuu, naombeni msaada maendeleo ya ukuaji hayasongi mbele, mtoto anamiezi 16 lakini hata kusimamia hasimami, na daktari wa viungo anasema hatuwezi kumfanyisha mazoezi mpaka hii degedege ifike kikomo.

Naombe msaada wakuu, 😭😭😭
Kuna dogo alizaliwa na hii kitu alifanyiwa dawa za kienyeji, alikuwa anapigwa vifagio mguuni. Ukimuona sasahivi huamini kama ndie yeye ila sijui dawa kaipata wapi. Tafuta njia hii kama utaipata
 
Hili swala la kusimama jitahid ikitokea kasimama Kwa bahati mbaya au ukamsimamisha akasimam Kwa sec kadhaa/Dak inakubid umpitishie mwichi / mtwangio ktikati ya miguu yake kutoka nyuma! Njia ya pili inakupasa unyoe mavz yako hrf yakaange kwenye chungu yakisha ungua upate unga wake hrf unamchanja pande 4 za kiunoni yaaan mbele chini ya kitov,nyum,kulia na kushoto, hrf unammalizia na kwenye miguu usawa wa magoti kulia na kushoto Kila ukichanja unampaka hiyo kitu! Hii imesaidia wengi sana jaribu dawa unayo mwenyewe
Eh... My God!!🤯🤯
 
Habari ya mudaa huu wakuu, nilishawa kuja kuomba ushauri kuhusiana na tatizo la mwanangu, baadhi ya watu walipa ushauri tukafanya CT SCAN pale benjamini lakini hakuwa na tatizo lolote kwenye kichwa.

Nimerudi tena wakuu, naombeni msaada maendeleo ya ukuaji hayasongi mbele, mtoto anamiezi 16 lakini hata kusimamia hasimami, na daktari wa viungo anasema hatuwezi kumfanyisha mazoezi mpaka hii degedege ifike kikomo.

Naombe msaada wakuu, 😭😭😭
Habari!
Pole na kuuguza.
Utaratibu wa kuuguza na kupata jibu kwenye tiba utategemea pia na njia utakayo izingatia.

Kwa ulinganifu wa historia fupi uliyoitoa ya tiba, bado kuna mapengo yasiyoelezeka.

Mfano:
1: Tiba ya mtoto huyu inahitaji kumhusisha daktari bingwa wa watoto pamoja na daktari bingwa wa mishipa ya fahamu.
Sina hakika kama hiki ndicho kilichofanyika.

2: Kwa msaada wa wazazi, historia ya mtoto inatakiwa ichukuliwe tangu mimba, jinsi alivyozaliwa, uchanga wake na ukuaji na mambo mengine muhimu yaliyojitokeza hapo kati.

Pia, ni nini hasa hutokea wakati wa degedege vs huambatana na nini?

Lengo ni kujaribu kujua tatizo lilianzia wapi na ni kiasi gani.

3: Kulingana na hatua ya historia, kumwangalia mtoto, vipimo vitaagizwa kulingana na yaliyong'amuliwa. Si kila degedege kipimo ni kimoja. Hii hutegemea na tatizo husika.

Mfano: mapendekezo hutegemea na aina ya degedege na chanzo. Kuna aina nyingi sana za vyanzo vya degedege vya muda mfupi na vya muda mrefu au kudumu. Kuanzia maumbile, urithi mpaka physiologia ya mwili.

4: Si kila dawa hufaa kwa kila degedege. Uchaguzi wa dawa hutegemea na aina ya degedege. Unaweza usifanikiwe na dawa hii au ile kutokana na uchaguzi wa aina ya dawa au kiasi cha dozi husika.

5: Kuna vitu pia utahitaji kutokumfanyia au kufanya ili kutokuwa chanzo cha degedege kutokea.

Hivyo, degedege si jambo la kuchukua kwa tiba ya mwelekeo mmoja. Ni suala pana, linahitaji ufuatiliaji wa karibu, uvumilivu, uelewa na uzingatifu.

Nakutakia matibabu mema.
Wape nafasi wataalamu husika hapo juu.
 
HUU NDIO USHAURI NILIOUBEBA, KWA WALE MLIONIPIGIA SIMU..TAFADHALI NAZINGATIA HILI..UBARIKIWE MKUU
Umefanya la maana, degedege inasabishwa na vitu vingi mno Kuna mdau hapo kakuuliza kama umeshawahi kufamnyisha EEG umemjibu hukujui hiko kipimo so hii inaonyesha dogo anahitaji vipimo vingi kujua chanzo Cha hilo tatizo ni nini endelea kuhudhuria hospitali hasa zenye ma Dr bingwa wa watoto Nina Imani dogo atapona tu.
 
Habari ya mudaa huu wakuu, nilishawa kuja kuomba ushauri kuhusiana na tatizo la mwanangu, baadhi ya watu walipa ushauri tukafanya CT SCAN pale benjamini lakini hakuwa na tatizo lolote kwenye kichwa.

Nimerudi tena wakuu, naombeni msaada maendeleo ya ukuaji hayasongi mbele, mtoto anamiezi 16 lakini hata kusimamia hasimami, na daktari wa viungo anasema hatuwezi kumfanyisha mazoezi mpaka hii degedege ifike kikomo.

Naombe msaada wakuu, 😭😭😭
Mshana Jr msahada wako juu ya hili swala tafadhali.
 
Umefanya la maana, degedege inasabishwa na vitu vingi mno Kuna mdau hapo kakuuliza kama umeshawahi kufamnyisha EEG umemjibu hukujui hiko kipimo so hii inaonyesha dogo anahitaji vipimo vingi kujua chanzo Cha hilo tatizo ni nini endelea kuhudhuria hospitali hasa zenye ma Dr bingwa wa watoto Nina Imani dogo atapona tu.
Shukrani mkuu
 
Habari!
Pole na kuuguza.
Utaratibu wa kuuguza na kupata jibu kwenye tiba utategemea pia na njia utakayo izingatia.

Kwa ulinganifu wa historia fupi uliyoitoa ya tiba, bado kuna mapengo yasiyoelezeka.

Mfano:
1: Tiba ya mtoto huyu inahitaji kumhusisha daktari bingwa wa watoto pamoja na daktari bingwa wa mishipa ya fahamu.
Sina hakika kama hiki ndicho kilichofanyika.

2: Kwa msaada wa wazazi, historia ya mtoto inatakiwa ichukuliwe tangu mimba, jinsi alivyozaliwa, uchanga wake na ukuaji na mambo mengine muhimu yaliyojitokeza hapo kati.

Pia, ni nini hasa hutokea wakati wa degedege vs huambatana na nini?

Lengo ni kujaribu kujua tatizo lilianzia wapi na ni kiasi gani.

3: Kulingana na hatua ya historia, kumwangalia mtoto, vipimo vitaagizwa kulingana na yaliyong'amuliwa. Si kila degedege kipimo ni kimoja. Hii hutegemea na tatizo husika.

Mfano: mapendekezo hutegemea na aina ya degedege na chanzo. Kuna aina nyingi sana za vyanzo vya degedege vya muda mfupi na vya muda mrefu au kudumu. Kuanzia maumbile, urithi mpaka physiologia ya mwili.

4: Si kila dawa hufaa kwa kila degedege. Uchaguzi wa dawa hutegemea na aina ya degedege. Unaweza usifanikiwe na dawa hii au ile kutokana na uchaguzi wa aina ya dawa au kiasi cha dozi husika.

5: Kuna vitu pia utahitaji kutokumfanyia au kufanya ili kutokuwa chanzo cha degedege kutokea.

Hivyo, degedege si jambo la kuchukua kwa tiba ya mwelekeo mmoja. Ni suala pana, linahitaji ufuatiliaji wa karibu, uvumilivu, uelewa na uzingatifu.

Nakutakia matibabu mema.
Wape nafasi wataalamu husika hapo juu.
Shukran mkuu
 
Habari!
Pole na kuuguza.
Utaratibu wa kuuguza na kupata jibu kwenye tiba utategemea pia na njia utakayo izingatia.

Kwa ulinganifu wa historia fupi uliyoitoa ya tiba, bado kuna mapengo yasiyoelezeka.

Mfano:
1: Tiba ya mtoto huyu inahitaji kumhusisha daktari bingwa wa watoto pamoja na daktari bingwa wa mishipa ya fahamu.
Sina hakika kama hiki ndicho kilichofanyika.

2: Kwa msaada wa wazazi, historia ya mtoto inatakiwa ichukuliwe tangu mimba, jinsi alivyozaliwa, uchanga wake na ukuaji na mambo mengine muhimu yaliyojitokeza hapo kati.

Pia, ni nini hasa hutokea wakati wa degedege vs huambatana na nini?

Lengo ni kujaribu kujua tatizo lilianzia wapi na ni kiasi gani.

3: Kulingana na hatua ya historia, kumwangalia mtoto, vipimo vitaagizwa kulingana na yaliyong'amuliwa. Si kila degedege kipimo ni kimoja. Hii hutegemea na tatizo husika.

Mfano: mapendekezo hutegemea na aina ya degedege na chanzo. Kuna aina nyingi sana za vyanzo vya degedege vya muda mfupi na vya muda mrefu au kudumu. Kuanzia maumbile, urithi mpaka physiologia ya mwili.

4: Si kila dawa hufaa kwa kila degedege. Uchaguzi wa dawa hutegemea na aina ya degedege. Unaweza usifanikiwe na dawa hii au ile kutokana na uchaguzi wa aina ya dawa au kiasi cha dozi husika.

5: Kuna vitu pia utahitaji kutokumfanyia au kufanya ili kutokuwa chanzo cha degedege kutokea.

Hivyo, degedege si jambo la kuchukua kwa tiba ya mwelekeo mmoja. Ni suala pana, linahitaji ufuatiliaji wa karibu, uvumilivu, uelewa na uzingatifu.

Nakutakia matibabu mema.
Wape nafasi wataalamu husika hapo juu.
Shu
Mshana Jr msahada wako juu ya hili swala tafadhali.
Ushauri wako mkuu Mshana Jr
 
Shida ni degedege, anakuwa vizuri.. uzito unaongezeka.. muonekano mzuri, dawa anatumia kwa sasa sodium valproate na hio EEG sijui ni kipimo gani??
kama mmefanya CT scan na haijaonyesha tatizo....

Binafsi nashauri ufanye EEG kama mdau alivyokuuliza hapo juu...I am confident enough EEG itakuwa na majibu yote...

Nina swali kwako...Je wakati wa kujifungua mtoto alilia ama alichelewa kulia?..

Ushauri wa mwisho usijisumbue kumpeleka kwa waganga wa jadi utapoteza pesa na muda wako..
 
Hili swala la kusimama jitahid ikitokea kasimama Kwa bahati mbaya au ukamsimamisha akasimam Kwa sec kadhaa/Dak inakubid umpitishie mwichi / mtwangio ktikati ya miguu yake kutoka nyuma! Njia ya pili inakupasa unyoe mavz yako hrf yakaange kwenye chungu yakisha ungua upate unga wake hrf unamchanja pande 4 za kiunoni yaaan mbele chini ya kitov,nyum,kulia na kushoto, hrf unammalizia na kwenye miguu usawa wa magoti kulia na kushoto Kila ukichanja unampaka hiyo kitu! Hii imesaidia wengi sana jaribu dawa unayo mwenyewe
Mmmh
 
kama mmefanya CT scan na haijaonyesha tatizo....

Binafsi nashauri ufanye EEG kama mdau alivyokuuliza hapo juu...I am confident enough EEG itakuwa na majibu yote...

Nina swali kwako...Je wakati wa kujifungua mtoto alilia ama alichelewa kulia?..

Ushauri wa mwisho usijisumbue kumpeleka kwa waganga wa jadi utapoteza pesa na muda wako..
MTOTO ALICHELEWA KULIA MKUU
 
kama mmefanya CT scan na haijaonyesha tatizo....

Binafsi nashauri ufanye EEG kama mdau alivyokuuliza hapo juu...I am confident enough EEG itakuwa na majibu yote...

Nina swali kwako...Je wakati wa kujifungua mtoto alilia ama alichelewa kulia?..

Ushauri wa mwisho usijisumbue kumpeleka kwa waganga wa jadi utapoteza pesa na muda wako..
Alichelewa kulia mkuu, ushauri wako mkuu
 
Back
Top Bottom