Dereva wa Basi la Saratoga apigwa na Askari wa JWTZ

Dereva wa Basi la Saratoga apigwa na Askari wa JWTZ

Jeshi la polisi bhana,sio kwamba wamemkamata mtuhumiwa hapana Bali wamemhoji ilikuwaje.wakati mtu yupo hoi.

Dah,nacheka Sana.

Ila inawezekana dereva kaovertake harafu hatua kidogo kaenda kusimama mbele kumchukua abilia.

Saa Kamanda kajiuliza huyu amenipita mshale na fujo juu kumbe anakuja kusimama hapa tu.mamamae ngoja
Kwa hiyo suluhisho ni kipigo?!!
 
Sihalalishi alichofanyiwa dreva Basi

Ila Madreva mabasi sometimes wanakera Sana, wanajifanya wana haraka sn kuliko watumiaji wengn wote wa barabara.

Sometimes Wanachomekea kwa fujo na overtaking zao za kipuuzi sn zisizochukua tahadhali za usalama barabarani.

Ukikaa kizembe kwny usukani, ukawakadiria kwa macho, unastuka mtu huyu Hapa, wanachezesha Basi ghafla, unamkwepa unahama Njia, wanakusababishia ajali afu wao wanalala zao mbele na matusi juu wanatukana.





Sent using JamiiForums mobile app
Nikiwa na safari za kibaha, najitahidi niende mapema kabla muda wa mabasi, au nitoke baada ya mabasi kupita, jamaa wana fujo.
 
Sasa Gari ya jeshi haitakiwi ku overtake? Mbna km hii habari sijaelewa, au kuna linginee??
over take vs take over wenye hiyo tabia ni mabus au malori yanayochukua muda mrefu kuwa barabarani. Kufanya take over kwa magari ya hospital & ulinzi wa mipaka ya nchi unastahili kichapo kwani unakuwa unahatarisha usalama wa wananchi.
 
Dereva wa basi la Saratoga linalofanya safari kutoka Dar es Salaam kwenda Kigoma, Yasini Shabani (45), ameshambuliwa kwa kupigwa maeneo mbalimbali ya mwilini na Askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), anayejulikana kwa jina la Emmanuel Peleka baada ya basi hilo kulipita gari la JWTZ katika eneo la Picha ya Ndege Kibaha mkoani Pwani.


1. Huyo dereva wa basi atakuwa alizingua (kusababisha ajali).
2. Kwanini iwe dereva wa Saratoga na sio wengine?
3. Wana fujo sana barabarani madereva wa mabasi.
4. Kuna mtu asiyejua fujo za madereva wa mabasi barabarani.
5. Kwanini tutetee hao wapuzi kupata mkong'oto toka kwa wanajeshi kwa rafu zao barabarani?

My take:
Sitetei wajeda kwa walilolifanya, ila mara nyingine tuwapongeze kuwa-discipline wapuzi kama hao madereva.

Wanakera sana hao na mipuuzi sana hao ndugu zetu madereva. Tutii sheria bila shuruti na hao wajeda hawatapiga mtu.
 
Dereva wa basi la Saratoga linalofanya safari kutoka Dar es Salaam kwenda Kigoma, Yasini Shabani (45), ameshambuliwa kwa kupigwa maeneo mbalimbali ya mwilini na Askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), anayejulikana kwa jina la Emmanuel Peleka baada ya basi hilo kulipita gari la JWTZ katika eneo la Picha ya Ndege Kibaha mkoani Pwani.



Barabarani huwa tunaheshimianaga sana, na hawa watu wanaobeba abiria ni wa kuheshimu sana. Hata kama wanaweza kuwa na mauzi hapa na pale
 
Kwa maana unataka kusema askari hatakiwi kufuata sheria za kiraia? Anatakiwa kufuata sheria zote za jeshi na za kiraia.
Akiwa kwenye operation za kijeshi hatakiwi kukupa copy anaenda wapi hapo anatakiwa kuzingatia za kijeshi tu

Ni vyema kupisha gari za jeshi lolote ziwe JWTZ, polisi,magereza nk hujui kulikoni hata magereza waweza kuwa wanakimbiza gaini kulipekleka mahakamani au lupango wapishe bila wanajeshi huwezi ishi kwa amani wakati wewe uwe mwanaume au mwanamke mnafanyana na mke au mume kitandani kwa raha zenu wao hawalali kuhakikisha mko salana mnaendelea kufanyana kwa raha zenui bika adui kuvamia nchi au eneo

Mnapofanyana kwa raha zenu wako lindo. Hivyo wape heshima zao ukiona wako mbele au nyuma na magari yao wapishe

Visheria vyako vya barabarani wakiwa kwenye magari official ya jeshi shika adabu yako usilete ujuaji watakuua mchana kweupe na huna kwa kuwapekeka
 
Tusikie na Upande wa pili ,si rahisi upigwe vibao kisa ku overtake ingekuwa hivyo Route ya Lugalo watu wangekuwa wanakula vibao daily.
Niliwahi kuzingua pale, nikaambiwa nizime gari, nianze kusuma..

Kilicho nitokea nakijua mwenyewe.. ila tuliwezena maana tulipita kidogo huko, tuli ongea lugha moja
 
Madereva wa mabasi makubwa baadhi ni washenzi Sana,wanaendesha Kama vile Barabara ni ya kwao peke yao,tungesikia na upande wa pili ilikuaje
Mkuu hao wanajeshi wa Nyumbu huwajui, kuna mda wanapita upande wa kulia wa barabara na usipowapisha kazi unayo ma hamna wanachowahi cha maana zaidi unakuta anapeleka watu kazin . Infact kimewahi kutumia huo usafiri humo ndani unaweza ukaambiwa usikae na siti zipo wazi kisa tu kuna mwanamke anakuzoea afu kuna mtu mnene amekataliwa na huyo huyo mwanamke.
 
Back
Top Bottom