Diamond kaangushwa na mameneja wake sio Wanaharakati

Hivi Diamond Platnumz ana tuzo ngapi kulinganisha na huyo Burna Boy? Nadhani Diamond is way too far from Burna Boy when it comes to number of awards winning...pia alikuwa na mameneja hao hao unaowaponda
Acha ujinga aisee..ishu ni idadi ya tuzo au ukubwa wake?.

Burnaboy ana hadi Grammy..na hii BET anaichukua for three times in a row tokea 2019.

Mziki wa Burnaboy ni mkubwa na mzuri consistently na jina lake limekuwa kubwa pia.
 
Kwa madufu ya eyoo Laizaa ataendelea kutikisa tandale na Kenya na Uganda tu! Music yenye taste kama ya Burnaboy iko level zingine [emoji23][emoji23][emoji23]
[emoji23][emoji23][emoji23] producer wake mwingine ni S2kizzy ambaye anadaiwa kodi ya nyumba laki nne sijui..utulivu wa kupika mziki mzuri utatoka wapi?.
 
Eeeeh Bwana wewe ni mwenye vision sana mm nahisi hata huyo bwamdogo akikupa weye umeneja utafika mbali sana sababu unaijua hasa ile cream ilioko ndani umeeleza maneno mafupi matamu na ya kueleweka @ Diranghe 100% nimekukubali bro .Unajua tatitizo la wasinii wa bongo wanajidanganyana sana wanachulia mambo rahisi rahisi tu.
 
[emoji23][emoji23][emoji23] producer wake mwingine ni S2kizzy ambaye anadaiwa kodi ya nyumba laki nne sijui..utulivu wa kupika mziki mzuri utatoka wapi?.
Hahahah sasa Producer hana hela ya kodi kubabae kuna kazi tena hapo😂?
 
Una point yenye mashiko sana
 
Nani atakruhusu uingie ndani na siraha,..
 
Binafsi naona hata kutopata tuzo, kwake ni mafanikio makubwa sana kuwa nominee wa hizo tuzo.........na naona sisi watz tunawivu na roho mbaya sana kwa mtu aliyefanikiwa.....kifupi hatupendi maendeleo ya mtu. Unachokiona mitandaoni wakati wengi wakiomba ashindwe, ndiyo maisha halisi ya Mtz..........ktk jamii zetu wengi huwa hawapendi mafanikio ya mtu mwingine
 
Asante kwa elimu hii
 
Tupe wasifu wa mama Dangote kwanza kabla hatujaanza kutoa maoni
Huyu amewahi kuolewa na wanaume 4.
Amewahi kutukanana na mumewe wa zamani mara kadhaa
Na kikubwa zaidi hajawahi kuingia darasani.
Mwisho kabisa ana kipaji cha kumpigia mtu umbea mpk akafa.
 
Lol[emoji23][emoji23][emoji23]
Geuza haya Manene kwa kiingereza,..

Bunyero bunyero nataka msambwanda wa buku jero,.. Inama nipachike rungu..

Weny Lugha yao watamkataa asubui tu
 
NAKAZIA Pia kuna mahala nilisoma kwamba Media za Marekani kuna waafrica wachache walioajiriwa kutoka SA na Kidogo Nigeria sijui kwa Tanzania na Kenya kama kuna mtangazaji yeyote kwenye media za kimataifa kama BET na MTV anayeiwakilisha East Africa Uwepo wao ungesaidia sana kutoa kipaumbele hususani kwa nyimbo za wanamuziki wa EA sasa hivi hata kama zinapigwa hazipigwi inavyostahili ,ukilinganisha na mtu wa nyumbani ambavyo angetumia fursa kuzitangaza hii ingesaidia sana nyimbo zetu kujulikana kwenye Platform za Kimataifa.

Vijana wengi wenye vipaji nao wanaiendea siasa sababu kwa Tz inalipa sana, naskia kuna mmoja alishawahi kufuzu kutangaza
Channel O ila ndo hivyo tena sasa ni DC .
 
Nilitaka kupita kimya pasipo kuchangia ila mtifuano uliopo umenishawishi nami kutoa maoni yangu, japo napenda ieleweke kuwa maoni yangu sio sheria, ila natoa maoni kama mdau wa muziki ambaye nina maarifa pia ya muziki( napiga chombo na ninajua kanuni za muziki). Naanza kuchangia kwa kusema kuwa, tukijadili uharari wa ushindi wa tuzo kwa kuegemea kwenye ushabiki hatutaweka kuona na kupata ufumbuzi wowote. Nawapongeza wote waliochaguliwa kuwania tuzo hiyo kwani kuna kitu kilionekana ndani ya kazi zo, ikumbukwe kwenye mashindano yupo atakaye washinda wengine. Mtu akishindwa hatakiwi kuleta visingizio ila kuangalia namna ya kujipanga zaidi wakati mwingine.

Kwa mtazamo wangu na kwa ujuzi kidogo nilionao wa muziki kama nilivyosema hapo mwanzo, naamini kijana kutoka Nigeria yaaani Burner Boy, ameshinda kihalali kabisa na sio kwa sababu za visingizio wavavyotumia mashabiki wa upande mwingine, japo sikatai kuwa management inaweza mpeleka msanii mbali, lakini hakuna ubunifu katika kazi ya msanii huyo, siku zote ataishia kulalama tu bila mashiko, management sio kigezo kilichomuangusha msanii wetu Diamond, kilichomwangusha ni ubunifu finyu, ndugu zangu hata ukijunze vipi kuogelea hauwezi kumshinda samaki kuogelea.

Wakati Wanigeria wanatengeneza muziki wao kwa kuingiza zaidi utamaduni wao, sisi tumekuwa tukiokoteza midundo na mitindo kutoka kwao, halafu tunategemea kushinda nao, angalia asilimia ya nyimbo za wasanii wetu, hapa simtaji Diamond tu, ila na wasanii wengine wengi wa kitanzania, mara nyingi ukisikiliza nyimbo zao hazina misingi ya muziki naweza kuziita ni kelele tu ambazo watu wameamua kuzikubali, na wasanii wengine wanaofanikiwa kusikika zaidi wengi hawana ubunifu ukocopy aina za muziki za watu wengine ambazo nazo hawazijui vizuri yaani ni kama kusema, ukocopy nyimbo ya salsa kutoka Latin America halafu uende ukashinda nao jibu nadhani unalo.

Najua wengine watasema mbona Wizkid naye kashindwa kwani naye anakocopy, jibu ni kuwa pamoja kwamba Wizkid na wasanii wengineo kuwa na management nzuri na kufuata misingi ya muziki wao, wameshindwa na Burner Boy kwa sababu moja tu msimu huu jamaa amewazidi ubunifu, ukitaka kujua hilo sikiliza album zao. Uhusiano wa Burner Boy na P.didy au kuwa management nzuri sio kitu pekeee kilichochagiza yeye kupata tuzo hio bali ni ubunifu narudia tena ni ubunifu wa hali ya juu, ubunifu huo umeonekana kuanzia kwenye uandishi, midundo ya nyimbo zake na namna anavyotumia sauti yake.

Ushauri wangu, wasanii wa hapa nyumbani yaani Tanzania wanatakiwa kuacha kucopy kwani kunarudisha nyuma ubunifu wao, pia wanapoandika nyimbo wanatakiwa wajua watu wanaowalenga, hizi nyimbo zao za matusi zinawafubaza akili zao, wanapoona zimepata muitikio hususani kutoka katika kundi la vijana wasiojua kitu kuhusu muziki bali wenye kiu ya kusikia maneno ya ngono na viungo vya uzazi vikitajwa, wajiona wamekuwa wakubwa sana, lakini ukitaka kujua kinachowafanya wasikilize nyimbo hizo ni upuuzi unaosapoti upuzi wao, ni muda ambazo hizo nyimbo zinabaki vichwani mwa watu, mara nyingi nyimbo hizo hazidumu kwanini jibu ni kuwa kilichopendwa ni maneno ya hovyo na sio muziki wenyewe. wasanii kutunga tungo zitakazodumu na kukonga watu nyonyo bila kujali lugha zao, kumbuka muziki ni lugha inayoeleweka na watu husasani pale unapotungwa na kupangwa kwa ueledi.​
 
Wanaharakati wenyewe movement zao kwenye vyama vyao hazieleweki na watu hawa waelewi, Burna kastahili sababu ya album yake ya mwaka jana na tuzo aliyoipata Grammy plus umoja waliokuwa nao wanaijeria ktk kupush na kusapoti wasanii wao.

Halafu yule mzungu sio wabongo tuliojaa chuki na roho mbaya, mpaka katoa kajilizisha na kumbuka zile kura za jopo la majaji zina nguvu kuliko kelele za hao wanaharakati wenu mitandaoni.

So cha msingi hasikate tamaa kesho inaweza kuwa yake,aendelee kujituma.

Mameneja hao hao ndio waliokuwa naye kipindi media zimemtupa na kumtenga na hakutokea hata mwanaharaka mmoja kumtetea,mameneja hao ndio walio mfanya ashinde tuzo nne za channel 0,mbili MTV Europe, Moja MTV MAMA na mameneja hao hao ndio walio mfanya leo hii awe ashapiga show zaidi ya 90% ya nchi zilizo kusini mwa jangwa la Sahara.
 
Huyu amewahi kuolewa na wanaume 4.
Amewahi kutukanana na mumewe wa zamani mara kadhaa
Na kikubwa zaidi hajawahi kuingia darasani.
Mwisho kabisa ana kipaji cha kumpigia mtu umbea mpk akafa.
Duuuuuh hiyo ni CV ya mama wa mwanamuziki mkubwa toka Africa mashariki na kati halafu ndo aweze kutoboa kimataifa kweli acheni ushamba, meneja wake ni mganga mzuia mvua mwingine muuza drugs na maisha ya ujanja ujanja unategemea nini hapo tena bora wameshindwa maana angerudi na tuzo huyo kwa tunayemjua na ushamba wake angeamuru WASAFI TV na WASAFI FM wamtangaze yeye tu kwa siku 7 mfululizo.

Pia inawezekana kweli dogo alizuiwa kuingia ndani na mavazi yake hayo ya kike maana nnavyowajua wapambe wake wangeshatuonyesha mapicha picha mengi alivyokuwa ndani kiufupi dogo kariabisha taifa kmmk.
 
Mbona babu Tale ana Masters ya uhusiano wa kimataifa!
Ikiwa darasa la saba la mihogo ya sokoni inanukia kisokosoko, linaweza kumfikisha Babu Tale kupata Masters ya uhusiano wa kimataifa, basi tupe ushahidi!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…