Uchaguzi 2020 Dkt. Bashiru: CCM mwaka huu itavunja rekodi kwa kupata ushindi mkubwa wa kihistoria kwa sababu tunashindana na vyama dhaifu sana!

Uchaguzi 2020 Dkt. Bashiru: CCM mwaka huu itavunja rekodi kwa kupata ushindi mkubwa wa kihistoria kwa sababu tunashindana na vyama dhaifu sana!

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Katibu mkuu wa CCM Dkt. Bashiru amesema CCM itapata ushindi mkubwa na wa kihistoria ambao haijawahi kuupata tangu mfumo wa vyama vingi uanze.

Bashiru amesema mwaka huu CCM iliyoshikamana bila uwepo wa makundi inashindana na vyama dhaifu sana vya upinzani.

Chanzo: ITV habari

------
MWANDISHI: Baada ya kubaki siku 12 kuelekea uchaguzi mkuu, labda status ikoje kwa upande wa chama cha mapinduzi?

BASHIRU: Ni ushindi mkubwa sana, unajua mwaka huu tumeshindana na vyama dhaifu kuliko wakati wote. Sasa vyama dhaifu hata vingekuwa na wagombea wazuri lazima pia utendaji wao uendane na uwezo wa vyama vyao kwa hiyo mwaka huu ukilinganisha na mwaka 2015 tumeshindana na vyama dhaifu.

Kwa mfano ACT ni chama kipya, chama kilichokuwa na mbunge mmoja wa Kigoma mjini na halmashauri moja, hakikuwa na muwakilishi hata mmoja Zanzibar wala mbunge Zanzibar.

Kimesimamisha mgombea wa Muungano ambae sijui amepotelea wapi, namtafuta sijui yuko wapi? Ningekuwa ndie katibu wake mkuu ningeshaenda polisi, sasa hao ndio tunaoshindana nao.

Wengine ambao wanajikakamua vyama ni dhaifu, kulikuwa na chama ambacho kilikuwa kidogo kimejiimarisha cha CHADEMA lakini kilikuwa na washauri wazuri waliokipa ushindi, wakina mzee Lowassa, mzee Sumaye wako CCM, wako majukwaani wanakitafutia kura.

Kwa hiyo mwaka huu tutegemee matokeo na ushindi ni mkubwa kuliko ilivyowahi kutokea katika mfumo wa vyama vingi kwa hiyo tunashindana na vyama dhaifu, vyama vilivyogawanyika, vyama vipya.

Sisi ni chama kikongwe, chama imara, chama ambacho kina umoja zaidi na kinachotupa nguvu ni kwamba mwaka huu hatuna migogoro ndani ya chama, tumeshikamana na hiyo umeiona wakati tunateuana.

MWANDISHI: Kati ya wagombea kuna mgombea gani tishio?

BASHIRU: Hakuna tishio hata mmoja, nimeshakwambia kwamba vyama vyote ni vipya na vyama vyote ni dhaifu kwa hiyo hatuna mgombea tishio
 
Ahaaa ahaaa, hao ndio walimuingiza mjini Magufuli na CCM yao academia, kuwa kampeni hizi atakuwa anapita anapungia tu. Tuendelee kuomba ukondoo wa watanzania a.k.a amani itamalaki. Kinyume na hapo CCM watacheka kichina kwenye box la kura.
 
Sishangai kwa alichokisema.

Screenshot_2020-09-28-13-58-06-1.jpg
 
Nilidhani kuwa CCM kuwateua madokta na maprof wengi wangewanufaisha kwa kufanya kazi kitaalamu wakizingatia matokeo ya tafiti walizozifanya kisayansi kumbe wanazidiwa na kina kibajaji!

Na kwa upande mwingine Hawa wasomi wamesaidia Sana anguko la CCM na huenda ni mkakati wao wa muda mrefu! Magu ulibugi Sana hapa kwa kumkaribisha adui sebuleni kwako!
 
Ila CCM kama alishinda ule uchaguzi dhidi ya Lowassa Mnamo mwaka 2015.
Mungu anawaona.

1. Ule umati wa lowassa, jaman jaman Lowassa alikuwa anajaza mpaka sasa sijaona mgombea aliyefikia kujaza kule.

2. Alikuwa anaijua CCM. Na alitoa kauli kabisa anajua CCM wanapoweza shinda kwa bao la mkono..Yeye aka upgrage system zake.

Iwe huyu Mwanasheria aliyeshindwa kutafsiri Ibara ya 16 ya katiba yetu as amended from time to time.

Ingekuwa ni sheria kutangaza matokeo mapema. Naweza tangaza ushindi wa kishindo mapema kabisa kwa J.P.M
 
Bwashe kwani kuna vyama vingine vipya vilivyoundwa kushindana na CCM ukiacha kile kile chama kikuu cha upinzani cha TAL kinachoitoaga jasho CCM miaka yote?

Kwamba mwaka huu kuna vyama dhaifu kama vile ndo vimeundwa 2020? Bashiru asiishushie hadhi PhD kiasi hiki. Propaganda dhaifu kama hii akitamka Polepole (zero brain) ni sawa, lakini siyo huyu muuza ndizi mbobevu.
 
Nilidhani kuwa ccm kuwateua madokta na maprof wengi wangewanufaisha kwa kufanya kazi kitaalamu wakizingatia matokeo ya tafiti walizozifanya kisayansi kumbe wanazidiwa na kina kibajaji!

Na kwa upande mwingine Hawa wasomi wamesaidia Sana anguko la ccm na huenda ni mkakati wao wa muda mrefu! Magu ulibugi Sana hapa kwa kumkaribisha adui sebuleni kwako!
Mtu kama bashiru kuna uwezekano alifoji vyeti vya kitaaluma
 
Back
Top Bottom