Dkt. Gwajima: Tukatae utapeli, Binti aliyedai anaishi na nyoka akiri haikuwa kweli

Dkt. Gwajima: Tukatae utapeli, Binti aliyedai anaishi na nyoka akiri haikuwa kweli

Na makanisani nako pia Wanawake wanaangamia kwa shuhuda za uongo zinazoambatana na imani za kidin
Mmmmm! Hapa pagumu, itabidi pasubiri kwanza mpaka uchaguzi (s/za mitaa na uchaguzi mkuu) upite. Labda na kama kutatokea mwamba mmoja aguse eneo hilo. Kimsingi huko hakugusiki mpaka watanzania wenyewe waamke.
 
Yaan ww ,

Unapewa nafasi tiririka unaleta mashart ya utaweka kwenye uzi[emoji2]
Hakuna Waziri wa kukuruhusu kumpa hoja kirahisi kama Waziri Dorothy...wale ni Miungu watu ...ukianza kusema kuna jambo..unakula block hapo hapo...I'm sorry for saying that it's true. Sio mawaziri wote' wako so open hivyo tiririka kama una jambo lenye Hoja ya maana utaisdika kashakupa nafasi Haiba haha kuanA kuandika uzi huko je na asiuone? Tiririka Hapa Hapa.
Nitamuandikia hata kwenye no yake, usiwazeee.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Tafadhali usije ukamfikishia habari zangu... hatukuachana kwa ubaya. Ni wewe tu ulinikataa mimi msukuma na kwenda kwa sharobaro mwenye crown.
Em sema kweli? [emoji23][emoji23][emoji23]
 
Hata kama jina sio imani kwann ajiite jina la jamii ya kiislam jaman hivi ile interview hamkutizama au ndio watu mnapenda kubishana okay mmeshinda jina sio imani
Si tunasoma vichwa vya habari tu
 
Sawa, lakini generally huwa kuna hii kasumba keamba kila Mariam ni mtu wa ijumaa na Maria ni mtu wa jumapili, sio muda wote hubaki hivyo watu wanabadili dini na kubaki majina yao wengine
Ndo maana nikasema jina sio imani
 
Sawa, lakini generally huwa kuna hii kasumba keamba kila Mariam ni mtu wa ijumaa na Maria ni mtu wa jumapili, sio muda wote hubaki hivyo watu wanabadili dini na kubaki majina yao wengine
Ndo maana nikasema jina sio imani
Baba yangu anaitwa mussa na ni mkristo na mimi sijawazungumzia hao na wala hawanihusu hapa nimemzungumzia veronica ambe kwenye interview yake ya kulalana na joka alisema anaitwa latifa aisee kama hujaelewa nilichokimaanisha usiniletee gaazeti la mazingzong saa hiz
 
Baba yangu anaitwa mussa na ni mkristo na mimi sijawazungumzia hao na wala hawanihusu hapa nimemzungumzia veronica ambe kwenye interview yake ya kulalana na joka alisema anaitwa latifa aisee kama hujaelewa nilichokimaanisha usiniletee gaazeti la mazingzong saa hiz
Natanguliza shukrani
 
Tatizo ni jamii isiyo na maadili. Hizi media zenyewe zimekaa kimagendomagemdo tu mtu analipwa juingea shit sjui kaliwa na msanii, sjui karogwa, sjui kafumaniwa ni ujinga ambao wabongo wanaupenda ndo maana zinapata views hata kama hazina tija
 
Ahsante Sana, naomba tu Kila anayeoona uongo uongo fulani kwenye Kila link basi tupeane ushirikiano. Maana naweza nikawa kuna link inaendelea mahali na mimi sijaiona na watu wanapotea.
Hongera kwa kazi nzuri Mhe. Waziri.

TCRA chini ya wizara yao ya mawasiliano katika hili wanatakiwa kukusaidia. Nasikitika kuwa wamelala usingizi wa pono kiasi kwamba unalazimika kuzitafuta mwenyewe mitandaoni habari zinazokuhusu wakati wao wapo, na wana bajeti na kila kitu. Waziri wao naye kazi yake kupigizana kelele na wapinzani tu wakati ana majukumu mengi ya kuyatekeleza katika kutunza maadili yanayoporomoka kwa speed ya mwanga, huku kitovu kikiwa ni mitandao ya kijamiii.

Nchi hii tusipojifunza kufanya kazi kwa teamwork na kuacha kila mtu ajipambanie kivyake hatutofika popote.
 
Wazirii Gwajima, kuna jambo nataka likufikie, haijalishi utalikubali au utalikataa, ila lazima nikufikishie.
Unataka kumwambia nini huyu mama?

Nakukumbusha tu kuwa upungazeze nchi hii hatuutaki, na juzi bungeni kaweka bayana msimamo wake katika hilo.

Labda umwambie mambo mengine.
 
BINTI ALIYEDAI ANAISHI NA NYOKA AJISALIMISHA KWA WAZIRI DKT. GWAJIMA

Aomba radhi, adai hajawahi kufanya hivyo alidanganya.

DAR ES SALAAM.

Itakumbukwa hivi karibuni ilienea video mitandaoni kupitia televisheni ya MBENGO TV ikionesha Binti mmoja aliyekuwa amebeba nyoka mkubwa huku akidai kwamba, hufanya naye mapenzi ili kupata fedha.

Kufuatia hali hiyo, Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia Wanawake na Makundi Maalumu Mhe. Dkt. Gwajima , alichukua hatua ya kukemea kitendo hicho na kumtaka ajitokeze kuomba radhi kwa Umma na kuondoa taarifa hiyo mtandaoni kutokana na kukiuka maadili.

Baada ya mmiliki wa Mbengo TV, Tarzan Mustapha aliyeambatana na mtangazaji Lenny kuomba radhi Mei 11, 2024, walielekezwa kumtafuta binti huyo waliyemrekodi vinginevyo wachukuliwe hatua za kisheria kwa kukiuka sheria ya usajili wao kwa kushirikiana kupotosha jamii kwa habari za utapeli.

Leo 20 Mei, 2024 Binti huyo aitwaye Veronica Bernad Anton aliyekuwa amebeba nyoka huyo naye amejisalimisha kwa Waziri Dkt. Gwajima na kuomba radhi kama video inavyoonesha.

Waziri Dkt. Gwajima ameelekeza kutafutwa kwa mmiliki wa nyoka au ajitokeze mwenyewe kabla hatua za Serikali kumtafuta hazijaanza ambapo, itaongeza makosa yake ya kutotoa ushirikiano kwa Serikali.

Waziri Dkt. Gwajima ameiasa jamii ya wanahabari na wasanii kuachana na utapeli na mambo yote yanayochochea mmonyoko wa maadili maana akiwa Waziri mwenye dhamana na Jamii yenye makundi maalum hatafumbia macho uongo, utapeli na uovu huo.

MWISHO

NB; nawasihi wanajamii wote kuheshimu Sheria kwa maendeleo na ustawi wa jamii na kutunza maadili.

Pia soma: Epuka kusambaza maudhui yasiyo na maadili. Anayedai kumiliki nyoka na kushiriki naye tendo, ajisalimishe
View attachment 2995537
View attachment 2995538
Huyo ni mshirika mwenzake wa hayo mambo anayajua vizuri.
 
Back
Top Bottom