Dkt. Kigwangalla: Mashine ya nyungu iliyo Muhimbili ivunjwe, viongozi wavae barakoa

Dkt. Kigwangalla: Mashine ya nyungu iliyo Muhimbili ivunjwe, viongozi wavae barakoa

Huyu akili anazo hajasikia watu wamedanja sababu ya chanjo fala kweli hili
Wachache acha kupotosha mfano marekani walipowe ni Zaid ya million 150+ waliokufa kutoka na adverse drug reaction hawafiki 1000 kwa hiyo huwez sema chanjo ni mbaya

kila dawa Ina adverse reaction kwa baadhi ya watu kinachoangaliwa ni wangapi iko ndo wanachoangalia
 
Siku nikisukumiziwa kwenye uraisi hivi viumbe jamii ya kigwangala nitavianzishia mahakama ya unafiki na nitajenga ZOO (si jela) kubwa ya kuwaweka wakishahukumiwa maana unafiki wao ni kero kwa maendeleo ya binadamu[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]
Hahhahhahaaha
 
Ukisikia unafiki ndio huu sasa.alishindwa nini kuonesha msimamo wake kabla magufuli hajafa?
 
Huyu Kigwangalla mbona alishaingia kwenye hiyo mashine ya nyungu?

Sijui huyu Kigwangalla ni dini gani maana siyo kwa unafiki huu!!!

Utawala wa Magu umetusaidia kujua unafiki wa viongozi na wasomi wa nchi hii. Anachokiongea Kigwangalla ni ushahidi kuwa wanaccm wengi walikuwa kifungoni, na wote ilibidi wafuate ujinga wake ili wabaki kwenye mlo. Naendelea kuamini kuwa ccm sio chama imara kabisa, bali hutegemea tabia binafsi za rais aliye madarakani ambaye huwa ni mwenyekiti wao.
 
Ukisikia unafiki ndio huu sasa.alishindwa nini kuonesha msimamo wake kabla magufuli hajafa?
Magufuli alikuwa Simba wa vita ,asingethubutu kuongea huu upuuzi mbele yake.
 
Dah Magu amka uone waganga njaa hawa walivyo wanafiki. Huu unafiki wa kiwango cha juu sana sana.
Hivi Magu angekuwa hai ungethubutu hata kuacha mdomo wako wazi?

Hawa ndio viongozi wanaongoza watanzania.
Hivi mnajua hayo manyungu na unafiki wenu umeuza watu wangapi hadi sasa?
Aamke aje wapi mkuu?acha tupumue
 
Kwahiyo alikuwa anasubiri magufuli afe ndio aseme? Wachawi wengi nchi hii
 
Kwa siku kadhaa nnaendelea kushuhudia waliokua Wandamizi ktk Serikali ya Magufuli wakitoa statement za kukosoa baadhi ya mamabo aliyoyaamini. Moja wa hao ni Kigwangala lkn enzi hizo aliunga mkono kila kitu, inamaana walikua wakilinda ugali na matumbo yao na sio utumishi. Ilikua kwamba kama hawakubaliani na msimamo wa mzee wajiuzulu lkn balaa waliendelea kuunga mkono na sasa wameonyesha how stupid they are
Screenshot_20210404-140431_Instagram.jpeg
Screenshot_20210404-141739_Instagram.jpeg
 
Marehemu hajaoza washaanza kumkataa kama sio wao waliokua wanamsifu
 
Kama ni kweli kasema hivyo duuh, hawa Viongozi wetu hata siwaelewi, na wa Fedha nae kaanza kuongea.

Mimi najiuliza hivi kama waliona yasiyo sawa wakati Mwendazake bado akiwepo kwa nini hawakuthubutu kuhoji?

Hii inaonesha kuwa kwao madaraka ni bora kuliko Wananchi...kwa hiyo wao tukiumizwa sisi huwa wanatuchungulia tu kwa jicho pembe kulinda ugali wao.

Nape alijaribu kupaza sauti kuhusu Kodi wakati bado Mzee akiwepo lakini nadhani naye ni kwa vile alishaona hana cha kupoteza tena.
Ndivyo ilivyo mkuu, Mwanasiasa wa Bongo muogope km Ukoma,hawafai hao ndio maana Mimi huwa siwapendi kabisa.
 
Back
Top Bottom