Dkt. Mwigulu: Kabla ya Samia kuingia madarakani mabenki yetu yaliishiwa pumzi

Dkt. Mwigulu: Kabla ya Samia kuingia madarakani mabenki yetu yaliishiwa pumzi

"Ilikuwa haisemwi kwa sauti kubwa lakini ni ukweli usiofichika kwamba mabenki yetu mengi yalikuwa yameishiwa pumzi. Ulikuwa ukienda kwenye counter zao unahesabu wateja wawili watatu na wateja wengi walikuwa wanadefault," Waziri wa Fedha na Mipango Dk. Mwigulu Nchemba.

Ameyasema hayo leo 05/03/2022 wakati wa uzinduzi wa jengo jipya la makao makuu ya CRDB, jijini Dar es Salaam.
Kwahiyo akaamua kutukamua kwa tozo ili ma benki ya pone?
 
Wapunguze tozo za mihamala ya kwenye simu waone kama tutaenda tena kwenye mabenk yao.
Lengo ni hilo rafiki, na wala si lingine...Wameua financial inclusion huku wakienzi ma benki ambayo yamekaa kinyonyaji na yasiyotaka kutoa huduma kwa watu masikini na walio mbali na mijini
 
Kipindi hicho waziri husika hakuwa Boss wake Dr.Mpango kweli? Anyway pamoja na hayo Lakini Madelu anaongea ukweli🤔
 
Wanasiasa wa TZ wanaweza hii?

IMG_20220306_175910.jpg

Waziri amejiuzulu kwa kutokubaliana na uamuzi wa rais kuipiga Ukraine
 
Hatuna Waziri wa pesa hapo, amekaa kujineemesha na kufuata mzoga, utakaponuka ndipo atakapojua kwamba mambo sivyo.
 
"Ilikuwa haisemwi kwa sauti kubwa lakini ni ukweli usiofichika kwamba mabenki yetu mengi yalikuwa yameishiwa pumzi. Ulikuwa ukienda kwenye counter zao unahesabu wateja wawili watatu na wateja wengi walikuwa wanadefault," Waziri wa Fedha na Mipango Dk. Mwigulu Nchemba.

Ameyasema hayo leo 05/03/2022 wakati wa uzinduzi wa jengo jipya la makao makuu ya CRDB, jijini Dar es Salaam.
Huyo ndiye Mwigulu Lameck Madelu Nchemba. Na hizo ndizo siasa chafu sasa...
"Who gains what, why, when, how..."

NB: Namkumbuka kipindi anavaa kama Savimbi... Tulipigwa mabomu na risasi za moto pale Soweto Arusha kwa uratibu wake.
 
Hivi wewe Nchemba mbona ni mtu mzima kwanini Huna msimamo??? Ni unafiki?? Njaa au kitu gani???
 
Mimi sishangai Baraza la Maaskofu RC siku walipokutana na Mama Samia walisema kabisa hadhrani huduma zao za kijamii zilidumaa na kusinyaa ktk awamu ya 5.Nikakumbuka kumbe JK alikuwa anaupiga mwingi ila chuki tu.muda kitu muhimu sana!
 
Tena yeye alikuwa anawaponda live mbele ya kadamnasi, wakiwa hai
Eti kuna wastaafu wengine wanawashwa washwa naye akamtolea uvivu nitumeni popote DUNIANI nitakwenda kwani mimi sio mbwa ninaye bweka ndani tu
 
Back
Top Bottom