Dkt. Slaa: CHADEMA walimteka mtu wao, wakamtesa, wakamtupa, mimi nikajua watekaji ni Usalama wa Taifa

Dkt. Slaa: CHADEMA walimteka mtu wao, wakamtesa, wakamtupa, mimi nikajua watekaji ni Usalama wa Taifa

Dr Salaa ni miongoni mwa watu waliokuwa na heshima sana nchini

Katika siku za karibuni Salaa amekuwa na 'project' ya kuharibu integrity and credibility yake

Kazi ya ubalozi ni kama asali, ameshailamba na sasa anataka kuchonga mzinga.

Dr ana uhuru wa kutoa maoni, kinachosikitisha ni maoni yaliyojengwa juu ya chuki
Chuki imeutawala moyo wake hata kufikia mahali ukweli anauona ni sumu kuliko chuki aliyobeba

Kuhusu TL , swali hilo anaulizwa mara nyingi na kila anapojibu wasomaji wanabaki ''WHAT?
''Waandishi'' humuuliza ku'push agenda bila kujua au kwakujua anafanya kile kilichokusudiwa

Anamsema TL kwa kuonyesha mfano wa 'Chadema walivyowahi kudhuriana'' .
Fact aliyo nayo ni kuambiwa na red brigade aliyekataa kumwambia kabla.

Dr Salaa anamaanisha tukio la TL kupigwa risasa lina utata ''hawezi'' kulizungumzia huku akiwa tayari kalizungumzia kwa tuhuma za red brigade. Nafsi inamsuta na anajificha ficha! anajua anachosema si kweli kina maumivu kwa Tundu Lissu na Rais wema duniani, anazunguka zunguka

Kila mtu anajua nani alifanya nini. CCM wanaomba maridhiano wasiyosema ni ya nini

Dr Slaa anajua masaa machache kabla ya TL kupigwa risasi JPM alisema nini

Mr Slaa anajua Camera zimeondolewa , Walinzi waliondolewa na hakuna uchunguzi
Hata waliojaribu kwenda kumsalimia TL baada ya risasi lukuki mwilini waliona cha mtema kuni.

Anajua matibabu ya TL yalizuiwa kwa makusudi

Badala ya kueleza mfano wa kipuuzi aliokutana nao Padr Slaa ange address controversies ambazo serikali haiwezi kuzieleza.

Tundu Lissu, Mhanga, anasema wazi waliopanga na waliotekeleza. Hakuna anayepinga hilo.

Dr Slaa anaweka doubt kwamba TL alishambuliwa kwa risasa.

Bwana Slaa amefikia kiwango cha chini sana kimaadili '' moral decay' kujidhalilisha

TL ni mlemavu , anaishi kwa maumivu ! Dr Salaa alitoroka kwasababu anawindwa.

TL hakuwindwa bali anaishi majeraha ya kuwindwa. TL ana makovu mwilini ana risasi imebaki

Dr Slaa anaamini kuna ufeki katika hilo, na kwamba, pengine ni wenzake! hatafuti fact tena

Dr Slaa unachokifanya kinakuondolea thamani ya utu., kwamba Uhai wa mwanadamu unautweza na kuuweka katika mizani na matamanio ya nafsi yako! upate mkate kwa kudhalilisha Utu.

Jaribu kuushinda ubinafsi ili uutukuze UTU! Uamini katika ubindamu si nafasi au teuzi!

Dr Slaa ukifungua mdomo jitathmini! sidhani kama umefikia kiwango hicho!


JokaKuu Pascal Mayalla Mag3
 
Siku hizi humu baada ya uzi ni matusi tu. Kwani mnaomtukana huyu mzee mnakosoa hoja ipi? Zamani watu wali quote sentensi na kupangua hoja! Mbona mambo mengi kaongea kwa ushahidi mzuri tu? Au mnataka kusikia yanayowasha masikio yenu tu!
Mnafiki ningeshangaa sana kama usingekuja kutetea huu utopolo wa Dr Mihogo kwa kigezo cha hoja,sasa hapo kuna hoja gani wewe mfuasi wa mungu mfu wa Chato?
 

Mwanasiasa Willbrod Peter Slaa amefanya mahojiano na kuzungumza mambo mengi kuhusu siasa, mahojiano haya ni mwendelezo ya interview aliyofanya wiki iliyopita.

TAARIFA YA CAG INAPOTOSHWA
“Kuna upotoshwaji kwenye taarifa ya CAG, nadhani Zito Kabwe angelisaidia sana taifa hili kama angekuwa mkweli, mimi na Zitto tulishiriki kutengeneza sheria ya ukaguzi wa fedha 2009, hata maneno yaliyopo kwenye sheria hiyo yametoka kwetu.

“Moja ya maelezo ya ile sheria inasema baada ya CAG kukabidhi ripoti yake kwa Rais kisha kuifikisha Bungeni siku saba baadaye, ripoti hiyo haitakiwi kuwa public discussion, kwa kuwa ni kama mhtasari tu wa ripoti.

“Inatakiwa Kamati ya Bunge ndiyo iifanyie kazi, mfano kuna sehemu unaweza kukuta risiti haikuonekana wakati wa ukaguzi lakini hiyo ikapitishwa na kuonekana ni wizi, tumepotosha maana ya ile taarifa ya CAG.

CAG AMESABABISHA TAHARUKI KWA RIPOTI YAKE
“Kwanza hata CAG mwenyewe amechangia kuleta hii taaruki kwa kuwa huwa ni ya awali tu na analijua hilo, inatakiwa irudi kwa akaunti ofisa wa Serikali ijadiliwe, pia CAG wakati anatoa taarifa zake hadharani hatakiwi kuingia ndani kutoa ufafanuzi zaidi kama anavyofanya.

“Unaweza kukuta ripoti hiyo ikifika kwenye Kamati ya Bunge vitu vingi vikawekwa sawa, mfano labda kulikuwa na upotevu fulani wa mambo madogomadogo ambayo kwa nje yanaonekana kama ni wizi lakini details zikiwekwa sawa kunakuwa hakuna tatizo.

UBUNGE WA KINA MDEE SPIKA HANA KOSA, NITAZUNGUMZA CHADEMA WAKISHAKAA KIKAO
“Nimeona kwenye vyombo vya habari kuwa watajadiliwa na chama chao katika rufaa yao, naona lawama zimepelekwa kwa mtu ambaye hausiki (Spika).

“Chama kilitakiwa kufungua kesi Mahakamani kuhoji Tume ya Uchaguzi kwa kupitisha majina hayo lakini sijaona kesi. Mimi nitazungumza baada ya rufaa yao kupitiwa na CHADEMA, nimesikia wanakaribia kuwajadili kwenye kikao chao.

HOJA YA KATIBA SIYO MAHITAJI MUHIMU YA WANANCHI
“Mabosi wa vyama vya siasa ni wananchi, wanatakiwa kujiuliza wanayoyafanya yanawagusa vipi wananchi, kwa sasa kuna mambo mengi ya muhimu lakini hivyo vyama vimekuwa bize kuzungumza habari za ajenda ya Katiba.

“Hawana ajenda ambazo mwananchi anaweza kujiuliza kama inaweza kuweka chakula mezani, hakuna katiba ambayo inaweza kuzungumzia kila kitu.

“Katiba yetu ina vipengele vingi vya muhimu lakini havitekelezwi, japo sijasema kuwa katiba siyo muhimu.

“Mimi ni kati ya watu waliozunguka Tanzania kukusanya maoni lakini tusipotoshe kuwa katiba ndiyo jibu la kila kitu, siyo kweli.

“Leo hii Marekani ina katiba tunayoisifu lakini Donald Trump si alishutumiwa anataka kufanya mageuzi.

KATIBA PENDEKEZWA NI MBOVU KULIKO KATIBA YA SASA
Sisi tuna maoni ya Jaji Warioba, licha ya kuwa kulikuwa kuna mambo yamekosekana lakini yapo mazuri ambayo tunaweza kuyatumia.

“Baada ya maoni hayo kupelekwa Bungeni ikachujwa ikatoka inayoitwa Katiba Pendekezwa, ni mbovu kuliko hata katiba tuliyonayo sasa hivi.

SIZUNGUMZII SUALA LA LISSU KUPIGWA RISASI SABABU UTEKAJI ULIKUWEPOA CHADEMA
“Kuna watu wananiuliza kuhusu Tundu Lissu kupigwa risasi, kuwa sipendi kulizungumzia hilo kwa kuwa sita taarifa zake za uhakika.

“Nitoe mfano iliwahi kutokea huko nyuma nikiwa Katibu Mkuu CHADEMA, nililetewa taarifa za mtu wangu anaitwa Joseph, huyu alikuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Wilaya ya Temeke, alitekwa saa sita usiku. Kesho yake saa sita mchana nikahitisha mkutano na waandishi wa habari nikaisema sana Serikali na Usalama wa Taifa.

“Saa nane mchana siku hiyohiyo Joseph akapatikana, alikutwa ametupwa maeneo ya Ununio ameumia sana usoni.

“Mwezi mmoja baadaye kijana wangu wa Red Brigade anakuja kwangu kuniambia yeye ndiye aliongoza kukosi cha kwenda kumteka nyara huyo mwenyekiti huyo.

“Nikauliza kwa nini hakuja kwangu akasema ‘wapo viongozi wanaojua’, nikaamua kunyamaza, ndiyo maana ninapoulizwa suala la Lissu ninasema hapana, CHADEMA kwanza wajiangalie wao ndani.

“Huyo kijana (Joseph) walivyomtupa ufukweni walijua amekufa, kumbe alikuwa hajafa labda upepo ulimpiga akaamka. Miaka kadhaa baadaye tukaanza kusikia watu wanaokotwa wamekufa ufukweni, unadhani inatoa pcha gani!

“Ukiwa kiongozi lazima uwe kunasema ukweli hata kama unaona watu wako wanakosea.

SINA TATIZO LA LOWASSA
“Mimi na Lowassa tulipishana kwenye principal siyo maisha, mimi niliwahi kufanya fund rising na Jakaya Kikwete siku moja baada ya kupanda jukwaani na kumsema tena kwa mambo mazito.

“Nimeishi Ulaya, nimeona mambo ya kwenye mabunge, kuna muda inafika hatua wabunge wanapigana ngumi lakini wakitoka wanaenda kunywa bia. Unatakiwa kutofautisha maisha binafsi na siasa. Hivyo sikuwa na tatizo binafsi na Lowassa.

AWAMU YA TANO HAIKUFELI DIPLOMASIA YA KIMATAIFA
“Watanzania tuwe wakweli, tumefeli wapi, mimi nimekutana na wafanyabiashara wengi, wapo walioniambia wamchoshwa na Tanzania yenye ufisadi.

“Wapo walioamua kuondoa biashara zao huko nyuma lakini katika awamu ya tano waliamua kurejesha biashara hapa nchini, kwa nini? Ni kwa sababu kulikuwa kuna mambo mengi yanaenda vizuri, nazungumza kwa kuwa najua zaidi kilichokuwa kinaendelea.”



Chanzo: Dar24
Hahaha kudadeki ni kama vile slaa karukwa na akili # sio kwa mipumba hiyo 😁
 
Mama Muangalie huyu mzee. Hata ubalozi wa Ukraine ni bora.

Wandugu kushindia Mihogo sio kazi ndogo
Dr Slaa hawezi kushindia mihogo wewe.
Ana hela nyingi tu hata kuwalisha wewe na ukoo wako wote miaka yenu yote.
 
Dr.Slaa Hajawahi kua mnafiki na siku zote anaongea maneno ambayo si lazima uyapende,yeye si muumini wa siasa maji taka za kina zito na lisu pamoja na wengine wa chama kijani.

Na ni mtu pekee aliyesema Mzee mamvi ni fisadi na hakurud nyuma KWA hilo kama wengine walivyo kuja kumsafisha KWA dodoki.

Tunapaswa kujifunza kwake,KWA misimamo na hata mtazamo wa siasa za kweli ndani yake
Dr. Slaa ni mkatoliki wa hovyo .
Ni Mdini sana.
kumpenda Kiongozi yeyote asiye mkatoliki. Na ndio ugomvi wake na Lowasa. Lowasa sio fisadi ni mtu aliyewekeza kutoka na fursa alizozipata kuanzia kwenye familia yake ,jeshini,kwenye Chama na serikali mpaka kufikia Waziri Mkuu. Ulitegemea awe maskini.

Slaa na Genge la wahuni wanaojificha nyuma ya Udini walimhofia sana Lowasa Mluteri kuwa huenda akaukwa uraisa mana jamii nzima ilikua inamkubali ndo waliotengeneza Mchongo na kumpaka matope.

Ndio maana awamu hii ya mama Samia Slaa anajitahidi kujitutumua ili aonyeshe kuwa serikali ya awamu ya SITA sio Bora kama ya awamu ya Tano. Tumemshtukia na kumpuuza. 2025 ni Mama Samia TU mpaka 2035 ,hivyo kama Slaa anaota urais anajidanganya kama kula chakula ndotoni.
 
Hizi ndio hoja za kumuuliza atoe maoni. Walau wewe umeibuka na hoja ya msingi. Dr Slaa kwa principles zake za kusimamia ukweli, hili la Lissu hajalisemea kwa viwango tunavyotegemea kwa levels zake.
Principles zipi anasimamia au zile za human rights sio kipaumbele cha Watanzania?
 
Hizi ndio hoja za kumuuliza atoe maoni. Walau wewe umeibuka na hoja ya msingi. Dr Slaa kwa principles zake za kusimamia ukweli, hili la Lissu hajalisemea kwa viwango tunavyotegemea kwa levels zake.
Alafu huyu alikuwa padre ila ndio hivyo muongo muongo.Ata sijui kama huwa anatubu dhambi zake
 
Ile kesi ya mwenyekiti ya Ugaidi jamaa hakuwa ameaingiziwa. Ilikua kweli. Ila hakukua tu na water tight evidence.

Hii ni kashfa kubwa kwa chadema kuwa kuna mambo wanayafanya kwa ajili ya kuichafua serikali.

Chama cha hatari sana hiki.
 
Siku hizi humu baada ya uzi ni matusi tu. Kwani mnaomtukana huyu mzee mnakosoa hoja ipi? Zamani watu wali quote sentensi na kupangua hoja! Mbona mambo mengi kaongea kwa ushahidi mzuri tu? Au mnataka kusikia yanayowasha masikio yenu tu!
Washamba,wajinga wamevamia jukwaa mkuu enzi za kina kibunango, mzee mwanakijiji, spiderman, na wengine akiwemo le mutuz field Marshal ungeona huu upuuzi?
 
Mdini sana huyu Mzee.
Kila akitokea Kiongozi Muislam Dr. Slaa anapanua mdomo Kama Chai Jaba.

Hivi haoni kuwa uhuru wa kisiasa ndio unampa fursa ya kuzungumza na kutetea Chama chake Cha UP.!!
Hatapata wanachama ndio atajua kuwa yeye SI chochote si lolote ndani ya CCM Wala Chadema.

Hawezi kupata wanachama hata laki Moja.
Kama anabisha 2025 achukue fomu agombee aone kuwa Watanzania sio wajinga.

Yani mpumbavu sana huyu Slaha mihogo ,amesahau watu walivyopoteza maisha Kwa maandamano aliyokua anayaratibu akiwa Katibu mkuu wa Chadema.? Amesahau kuwa Kuna watu walikua wanafungwa Kwa sababu ya kutaka haki hasa wakati wa uchaguzi ?

Hivi huyo Slaa haoni kuwa Afrika hakuna mtu anayetegemea serikali kula? Hata kabla ya hizi takataka za kikoloni zinazoitwa serikali na maendeleo kuja Afrika waafrika walikua wanatafuta chakula Chao wenyewe. Sasa kusema kuwa Katiba haimpi mtu chakula mezani ni kuwadharau watanzania. Yeye ndiye anayepewa chakula mezani lakini wanyonge wanajitafutia wenyewe hawahitaji serikali iwape chakula. Hata somalia pasipo na serikali watu wanaishi. Watu wanataka haki tuu. Watu wanataka wapate haki sawa mbele ya vyombo vya dola lakini haki ya kupanda na kufikia ndoto zao za kisiasa bila kuzuia na Dola Kwa sababu ya kulinda CCM pekee. Watu wanataka CCM iwekwe madarakani kihalali na waonyesha hayo waliyofanya sio Kwa kubebwa na Polisi na Tume.

Kama Dr. Slaa hajui ugumu wa kuendesha shughuli za kisiasa chini ya Katiba iliyopo basi Hana tofauti na mtoto wa kishetani anayemtoa baba yake kafara ili apate Mali.
Afrika Ina laana mbaya sana kuwa na wanasiasa wanafiki wanaojali matumbo yao.

Waafrika wanapigania mtu badala ya falsafa.
Kwa nchi yetu na Katiba iliyopo ni Bora TU Dr. Slaa akae kimya ale alichopewa na serikali ya CCM mana kama ana ndoto za Urais basi anajidanganya. Haiwezekani hii nchi akabidhiwe padri muasi. Mtu aliyemuasi Mungu hawezi kuwa mwaminifu Kwa wanadamu ndio maana hazungumzii haki. Kazi ya serikali ni kutenda haki.
Maendeleo ni Kodi za Wananchi wenyewe sio hisani. Haki ndiyo itakayowafanya Watanzania wapate mrejesho wa Kodi yao.

Leo Slaa amesahau kuwa wabunge na kamati zao wamekua wakihongwa ili watetee wezi ? Amesahau Sakata la Jairo. Leo anamfunga mdomo Zito wakati Kuna utata. Alikufa ni Magufuli Sasa Kuna dhambi Gani kuwajibishwa wasaidizi wake walioiba wakati wapo.? Hofu yao Nini kama sio kweli wezi wapo. ?
Magufuli alikua ni Rais lakini alikua na wasaidizi ambao ndio walioipaka matope serikali yake , wawajibishwe wao sio hayati. Aliwaamini wakamwangusha na kumpa ripoti za uongo.

Tunajua Slaa ni lile kundi lisilomkubali Mama Samia ndio maana anazunguka zunguka TU na vijembe vyake akidhani kuwa mama naye anaipenda hii katiba mbovu. Mama ni Mpenda haki na Demokrasia. Hakuna mpenda haki anayeamini katika katiba inayowafanya watawala kuwa miungu. Rais anakua na mamlaka makubwa kuliko Mungu kwenye nchi iliyoumbwa na Mungu . Haya maisha ni ya kupita TU hakuna haja ya kujisahau kama hao wazee wanavyojisahau wakidhani wataishi milele.
Wewe ndo mdini na si Dr.slaa
Ukiweka akili sawa na kuondoa mind set ya dini utamuelewa vizuri tu.
Nitarudi badae baada ya kula daku
 
..Dr.Slaa amesema nini kuhusu ubaguzi, utesaji, utekaji, na mauaji, ktk awamu ya 5 ?

..Umesahau kwamba Dr.Slaa aliwahi kusema kuwa akipata madaraka atamfunga Dr.John Magufuli?

..Dr alitakiwa kuanzisha chama au kujiunga na chama kingine cha upinzani lakini sio kujiegemeza Ccm.
Utekaji,mauaji,utesaji ulikuepo Tangu nchi hii inapata uhuru na hata Sasa.Labda wewe muhamiaji tu ndo unaona mpya.

Nakukumbusha tu,Dr Slaa anasimamia msimamo uleule.Hakuna kumung'unya maneno mbele ya fisadi na Sasa kasema wazi umerudi na CDM pia hupokea mafisadi.Mbona Yuko wazi sanaaa,Tatzo nchi hii mnaona KILA mtu ni mfia vyama
 
Dr. Slaa ni mkatoliki wa hovyo .
Ni Mdini sana.
kumpenda Kiongozi yeyote asiye mkatoliki. Na ndio ugomvi wake na Lowasa. Lowasa sio fisadi ni mtu aliyewekeza kutoka na fursa alizozipata kuanzia kwenye familia yake ,jeshini,kwenye Chama na serikali mpaka kufikia Waziri Mkuu. Ulitegemea awe maskini.

Slaa na Genge la wahuni wanaojificha nyuma ya Udini walimhofia sana Lowasa Mluteri kuwa huenda akaukwa uraisa mana jamii nzima ilikua inamkubali ndo waliotengeneza Mchongo na kumpaka matope.

Ndio maana awamu hii ya mama Samia Slaa anajitahidi kujitutumua ili aonyeshe kuwa serikali ya awamu ya SITA sio Bora kama ya awamu ya Tano. Tumemshtukia na kumpuuza. 2025 ni Mama Samia TU mpaka 2035 ,hivyo kama Slaa anaota urais anajidanganya kama kula chakula ndotoni.
Udini kusema ufisadi umerudi au?We ni mgeni nchii hii kushangaa Dr.Slaa kuongelea ufisadi?Wewe ndo mdini ulokosa hoja,unafikiri KWA kutumia mgongo wa dini
 
Utekaji,mauaji,utesaji ulikuepo Tangu nchi hii inapata uhuru na hata Sasa.Labda wewe muahamiajj tu ndo unaona mpya.

Nakukumbusha tu,Dr Slaa anasimamia msimamo uleule.Hakuna kumung'unya maneno mbele ya fisadi na Sasa kasema wazi umerudi na CDM pia hupokea mafisadi.Mbona Yuko wazi sanaaa,Tatzo nchi hii mnaona KILA mtu ni mfia vyama
..lakini huko nyuma walikuwa wakifanya kwa kujificha-ficha.

..awamu ya 5 ikawa ndio kama sera yao wakawa wanafanya kwa kutamba kwenye majukwaa.

..hivi ktk hizo awamu zilizopita uliwahi kumsikia kiongozi wa Ccm akibwatuka kauli za kikatili kama alivyokuwa akifanya Kheri James?
 
..lakini huko nyuma walikuwa wakifanya kwa kujificha-ficha.

..awamu ya 5 ikawa ndio kama sera yao wakawa wanafanya kwa kutamba kwenye majukwaa.

..hivi ktk hizo awamu zilizopita uliwahi kumsikia kiongozi wa Ccm akibwatuka kauli za kikatili kama alivyokuwa akifanya Kheri James?
Nakukumbusha tu maana umesahau hata juzi juzi tu mwangosi ulikuaje?Dr ulimboka unajua nani alimng'oa kucha?Abson kibanda?Mwakyembe?wafanya biashara wa madini?Mashekhe wa uamsho?,bomu la mkutano wa CDM Arusha?Unajua Ulemavu wa mkono wa Dr.Slaa ameupata wap?Na wengine wengi?Walikua wamejificha?

WaTZ wepesi kusahau sanaaa,Juzi mwezi wa12 tu hapa vijana wa4 hawajaonekana Hadi leo,na wengine wanazidi kupotea lakini Mnaleta hoja nyepesi tu.Nyinyi mmeimbishwa hoja na mafisadi na mmeipokea na kucheza Ngoma msiyo ijua,na Sasa mnaona aibu
 
Mimi kila nikiwaza kuwa ni Kwa Nini Tundu alipigwa risasi nakosa jibu kabisa , alikua na kosa Gani la kustahili kupigwa risasi nyingi vile ? Ni unyama wa Hali ya juu.

Dr. Slaa kumbe ni kati ya watu katili sana sana Duniani . Nimemchukia sana !
.
Kufurahia na kushabikia BINADAM Mwenzake kupigwa risasi na Majambazi( potelea mbali kama sio state mission ) Hata kama alipigwa na Wenzake wa Chadema hakustahili kupigwa na hakuwa na Madhara yoyote Kwa Chadema mpaka apigwe risasi.
Ni kweli kabisa kuwa kama uchaguzi 2020 ungefanyika Kwa uhuru kidogo kama ule wa 2010 alipogombea yeye basi Tundu angemgalagaza sana mgombea wa CCM.

Mihogo na PhD yake amesahau jinsi Lisu alivyokua ananyimea mpaka kutumia Helkopta kwenye kampeni na kutishiwa kuuawa wakati wa kampeni na kuchonwa sindano ya sumu huku akifungiwa asifanye kampeni . Lisu alimuacha mbali sana Slaa kwenye kampeni 2020. Hata Zanzibar alipokelewa Kwa shamrashamra kubwa ukilinganisha na mihogo 2010.

Ingetosha TU Kwa Slaa kusema kuwa suala la Lisu lilikua na utata hivyo uchunguzi huru ufanyike ili ukweli ubainike na wahusika wachukuliwe hatua
 

Mwanasiasa Willbrod Peter Slaa amefanya mahojiano na kuzungumza mambo mengi kuhusu siasa, mahojiano haya ni mwendelezo ya interview aliyofanya wiki iliyopita.

TAARIFA YA CAG INAPOTOSHWA
“Kuna upotoshwaji kwenye taarifa ya CAG, nadhani Zito Kabwe angelisaidia sana taifa hili kama angekuwa mkweli, mimi na Zitto tulishiriki kutengeneza sheria ya ukaguzi wa fedha 2009, hata maneno yaliyopo kwenye sheria hiyo yametoka kwetu.

“Moja ya maelezo ya ile sheria inasema baada ya CAG kukabidhi ripoti yake kwa Rais kisha kuifikisha Bungeni siku saba baadaye, ripoti hiyo haitakiwi kuwa public discussion, kwa kuwa ni kama mhtasari tu wa ripoti.

“Inatakiwa Kamati ya Bunge ndiyo iifanyie kazi, mfano kuna sehemu unaweza kukuta risiti haikuonekana wakati wa ukaguzi lakini hiyo ikapitishwa na kuonekana ni wizi, tumepotosha maana ya ile taarifa ya CAG.

CAG AMESABABISHA TAHARUKI KWA RIPOTI YAKE
“Kwanza hata CAG mwenyewe amechangia kuleta hii taaruki kwa kuwa huwa ni ya awali tu na analijua hilo, inatakiwa irudi kwa akaunti ofisa wa Serikali ijadiliwe, pia CAG wakati anatoa taarifa zake hadharani hatakiwi kuingia ndani kutoa ufafanuzi zaidi kama anavyofanya.

“Unaweza kukuta ripoti hiyo ikifika kwenye Kamati ya Bunge vitu vingi vikawekwa sawa, mfano labda kulikuwa na upotevu fulani wa mambo madogomadogo ambayo kwa nje yanaonekana kama ni wizi lakini details zikiwekwa sawa kunakuwa hakuna tatizo.

UBUNGE WA KINA MDEE SPIKA HANA KOSA, NITAZUNGUMZA CHADEMA WAKISHAKAA KIKAO
“Nimeona kwenye vyombo vya habari kuwa watajadiliwa na chama chao katika rufaa yao, naona lawama zimepelekwa kwa mtu ambaye hausiki (Spika).

“Chama kilitakiwa kufungua kesi Mahakamani kuhoji Tume ya Uchaguzi kwa kupitisha majina hayo lakini sijaona kesi. Mimi nitazungumza baada ya rufaa yao kupitiwa na CHADEMA, nimesikia wanakaribia kuwajadili kwenye kikao chao.

HOJA YA KATIBA SIYO MAHITAJI MUHIMU YA WANANCHI
“Mabosi wa vyama vya siasa ni wananchi, wanatakiwa kujiuliza wanayoyafanya yanawagusa vipi wananchi, kwa sasa kuna mambo mengi ya muhimu lakini hivyo vyama vimekuwa bize kuzungumza habari za ajenda ya Katiba.

“Hawana ajenda ambazo mwananchi anaweza kujiuliza kama inaweza kuweka chakula mezani, hakuna katiba ambayo inaweza kuzungumzia kila kitu.

“Katiba yetu ina vipengele vingi vya muhimu lakini havitekelezwi, japo sijasema kuwa katiba siyo muhimu.

“Mimi ni kati ya watu waliozunguka Tanzania kukusanya maoni lakini tusipotoshe kuwa katiba ndiyo jibu la kila kitu, siyo kweli.

“Leo hii Marekani ina katiba tunayoisifu lakini Donald Trump si alishutumiwa anataka kufanya mageuzi.

KATIBA PENDEKEZWA NI MBOVU KULIKO KATIBA YA SASA
Sisi tuna maoni ya Jaji Warioba, licha ya kuwa kulikuwa kuna mambo yamekosekana lakini yapo mazuri ambayo tunaweza kuyatumia.

“Baada ya maoni hayo kupelekwa Bungeni ikachujwa ikatoka inayoitwa Katiba Pendekezwa, ni mbovu kuliko hata katiba tuliyonayo sasa hivi.

SIZUNGUMZII SUALA LA LISSU KUPIGWA RISASI SABABU UTEKAJI ULIKUWEPOA CHADEMA
“Kuna watu wananiuliza kuhusu Tundu Lissu kupigwa risasi, kuwa sipendi kulizungumzia hilo kwa kuwa sita taarifa zake za uhakika.

“Nitoe mfano iliwahi kutokea huko nyuma nikiwa Katibu Mkuu CHADEMA, nililetewa taarifa za mtu wangu anaitwa Joseph, huyu alikuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Wilaya ya Temeke, alitekwa saa sita usiku. Kesho yake saa sita mchana nikahitisha mkutano na waandishi wa habari nikaisema sana Serikali na Usalama wa Taifa.

“Saa nane mchana siku hiyohiyo Joseph akapatikana, alikutwa ametupwa maeneo ya Ununio ameumia sana usoni.

“Mwezi mmoja baadaye kijana wangu wa Red Brigade anakuja kwangu kuniambia yeye ndiye aliongoza kukosi cha kwenda kumteka nyara huyo mwenyekiti huyo.

“Nikauliza kwa nini hakuja kwangu akasema ‘wapo viongozi wanaojua’, nikaamua kunyamaza, ndiyo maana ninapoulizwa suala la Lissu ninasema hapana, CHADEMA kwanza wajiangalie wao ndani.

“Huyo kijana (Joseph) walivyomtupa ufukweni walijua amekufa, kumbe alikuwa hajafa labda upepo ulimpiga akaamka. Miaka kadhaa baadaye tukaanza kusikia watu wanaokotwa wamekufa ufukweni, unadhani inatoa pcha gani!

“Ukiwa kiongozi lazima uwe kunasema ukweli hata kama unaona watu wako wanakosea.

SINA TATIZO LA LOWASSA
“Mimi na Lowassa tulipishana kwenye principal siyo maisha, mimi niliwahi kufanya fund rising na Jakaya Kikwete siku moja baada ya kupanda jukwaani na kumsema tena kwa mambo mazito.

“Nimeishi Ulaya, nimeona mambo ya kwenye mabunge, kuna muda inafika hatua wabunge wanapigana ngumi lakini wakitoka wanaenda kunywa bia. Unatakiwa kutofautisha maisha binafsi na siasa. Hivyo sikuwa na tatizo binafsi na Lowassa.

AWAMU YA TANO HAIKUFELI DIPLOMASIA YA KIMATAIFA
“Watanzania tuwe wakweli, tumefeli wapi, mimi nimekutana na wafanyabiashara wengi, wapo walioniambia wamchoshwa na Tanzania yenye ufisadi.

“Wapo walioamua kuondoa biashara zao huko nyuma lakini katika awamu ya tano waliamua kurejesha biashara hapa nchini, kwa nini? Ni kwa sababu kulikuwa kuna mambo mengi yanaenda vizuri, nazungumza kwa kuwa najua zaidi kilichokuwa kinaendelea.”



Chanzo: Dar24
Kwani ndiyo yule og,au wa baada ya kuungana na Wana chukua chako mapema.
 
Slaa ameongelea kuhusu CAG report na kusema kuwa sababu moja ya kutaka kuwa isiwe public mpaka itakapojadiliwa na Bunge ni kuepuka vitu kama risiti iliyohojiwa kupatikana baadae.
Huu ni upotoshaji mkubwa na unaweza kuzungumzwa tu na mtu asiyejua taratibu za pesa za umma. CAG anapokagua hesabu anawaambia wahusika dosari alizoziona katika kikao chake cha mwisho na aliowakagua. Baada ya hapo anaandika formal report ambapo anaainisha mapungufu yote alioyaona. Hizo zinaitwa Audit Queries. Audit queries zinajibiwa na accounting officer, ambae anamuandikia CAG. Kama ana risiti anaziambatanisha. Accounting Officer hata siku moja hajibu Bunge moja kwa moja. Bunge wanachoweza kufanya ni kumtaka Accounting Officer atoe majibu haraka kwa CAG.

Amandla...
 
Back
Top Bottom