Dkt. Tulia Ackson: Mshahara wa Mbunge ni Tsh milioni 4.6 na sio vinginevyo

Dkt. Tulia Ackson: Mshahara wa Mbunge ni Tsh milioni 4.6 na sio vinginevyo

Kwanini alipwe pesa za mfuko wa jimbo (za umma) ziwekwe kwenye akaunti ya mtu binafsi (mbunge mwenyewe). Kwanini mbunge amlipe katibu wake kwa kwa kutumia pesa za umma huku hiyo nafasi upatikanaji wake hauwi wa ushindani? na huyo dereva wa mbunge huwa anapatikana kwa mchakato upi wa ajira?
Maswali yako ni mazuri sana atakayeweza kuyajibu nitaamini kwamba dunia imetundikwa na kuning'inia kwenye kamba nyembamba hewani
 
Nimemsikiliza akiongea anaonekana kuwaaminisha watu wabunge hawapati kingi kama wakurugenzi wengine kwenye mashirika ya umma.

Lakini anasahau kwa idadi ya wabunge mara hizo posho na mishahara bado hesabu inakuwa kubwa, amesema wabunge pamoja na waziri mkuu wanafika 395 ukipiga mara hizo figure utaona wanavyolifanya taifa kuzidi kuwa masikini.

Kigezo kingine alichotumia ku-justify hizo posho zao amesema hata wafanyakazi wengine wa umma wakisafiri hulipwa pesa za usafiri na gharama nyingine.

Lakini tunaona hawa wafanyakazi huwa wanacheleweshewa posho zao wakati mwingine hawapati mpaka wanafika vituo vyao vya kazi, na hata mishahara huchelewa, hili kwa wabunge haliwezi tokea.

Issue nyingine aliyozungumzia kuhusu wabunge 19 waliokuwa wa Chadema, anasema Chadema ndio wanatakiwa kumaliza taratibu zao ndani ya chama ndio bunge liwaondoe au lah.

Hapa Tulia anajua fika mtu akishaadhibiwa adhabu yake huanza kutekelezwa pale inapotolewa, sio mpaka atakapokata rufaa either akishinda ndio asiadhibiwe, au akishinda ndio aadhibiwe, na KM wa Chadema alishawaandikia barua kuwajulisha kuhusu hilo, lakini nashangaa bado wanakuwa wagumu kuelewa.
HILI LAKO JIPYA- LILETE KIKAO KINGINE- LEO TUNAJADILI KAMA WANAKATWA KODI AU HAWAKATWI?
 
Angalau CCM ina track records za kuaminika kwakua imeiweka nchi hii intact na kubafilisha viongozi kutoka makabila na makundi mbalimbali ya jamii...Hivyo vingine nipe records zake kwenye governance na democracy!
Nchini kwetu kuna utulivu kwa sababu ya UOGA. Lakini hakuna amani
 
Mh.Naibu Spika Dr.Tulia yuko sahihi mno.....

Namshangaa mh.Silaa anapotaka POSHO ikatwe KODI.....
 
Angalau CCM ina track records za kuaminika kwakua imeiweka nchi hii intact na kubafilisha viongozi kutoka makabila na makundi mbalimbali ya jamii...Hivyo vingine nipe records zake kwenye governance na democracy!
Ccm ni mafundi wa ufisadi wa kura na kula
 
Kwanini alipwe pesa za mfuko wa jimbo (za umma) ziwekwe kwenye akaunti ya mtu binafsi (mbunge mwenyewe). Kwanini mbunge amlipe katibu wake kwa kwa kutumia pesa za umma huku hiyo nafasi upatikanaji wake hauwi wa ushindani? na huyo dereva wa mbunge huwa anapatikana kwa mchakato upi wa ajira?
Na vipi kama Mbunge hana dereva, anajiendesha mwenyewe au anapanda bodaboda, hiyo posho ya dereva anairudisha?
Au ndio kusema kila Mbunge ana dereva?
 
Ktk kipidi cha ITV Dk 45, mambo yabwagwa hadharani.

Hivi punde akihojiwa ktk kipidi hicho, Naibu spika wa Bunge la Jamhuri ya Muunganao wa Tanzania Mheshimiwa Dr Tulia Ackson, amedai mshahara wa Mbunge ni milioni 4.6 tu. Anakatwa Kodi Tsh 1500,000 na kubakiwa na Tsh 3100,000.

Ameendelea kudai posho ya kikao ni Tsh 120,000. Pia Kuna posho ya kumlipa Dereva na Katibu wa Mbunge na posho ya mafuta. Pia Kuna mfuko wa Jimbo.

Watu wa nje ya Bunge wakipiga hesabu wanadai ni Tsh 11,0000,000 jambo ambalo sio kweli. Hizo hela zinapita kwa Mbunge japo zote sio zake.

Kwa kauli hii ya Naibu spika wa Bunge ni dhahiri kuwa wabunge wanakatwa Kodi tofauti na uvumi uliopo mtaani.
Kwanini katibu wa mbunge na dereva wasilipwe na bunge direct kama watumishi wengine? hapa kuna maswali mengi sn ya kujiuliza, basi na katibu wa RC na dereva nao walipwe na RC badala ya serikali
 
Kipindi cha dak 45 ITV hakina watangazaji wazuri wa kuuliza maswali nadhani wanafukuzia uteuzi tofauti kabisa na Aloyce Nyanda wa Star TV anajitahidi kuuliza maswali magumu na ya ukweli.
 
Kazi ya Mbunge inayomfanya alipwe 4m ni ipi hadi kumfanya alipwe tena 120k kama posho ya kikao? Juzi juzi Waziri Mkuu kaenda Wizara ya fedha na kuwasimamisha watu kwa sababu wamejilipa posho kwa kukaa kikao ambacho wanatekeleza sehemu ya majukumu yao, Wabunge wao ni special case ama!

Kuna kuijua dini na kumjua Mungu, ukimjua Mungu utamwogopa na kuhakikisha unajitahidi kutenda haki ila ukiijua dini tu ni shida.!
 
Sijamsikiliza kwa hiyo huo mshahara haustahili kodi??
Ila huu wa laki ndiyo ukatwe kodi siyo??
Kwanini yeye mbunge kwa mshahara huo huo asiwalipe watumishi, dereva na katibu wake??

Waache kuupiga mwingi, WALIPE KODI, huo ndiyo uzalendo, na wao waonyeshe mfano, siyo kutupia wananchi tozo, ilihali wao ndiyo wanufaika.
Ni unyonyaji na ubwanyenye.

Everyday is Saturday............................... 😎
 
Ni kichaa pekee ataamini kuwa kuna mtu anaweza kukatwa kodi 1.5 million kwenye milioni 4.6.
 
Rais mstaafu Alhaji Mwinyi aliwahi kusema madaraka matamu sana inahitajika hofu ya Mungu kuyaishi madaraka.
 
Tulia ni muongo mkubwa.

Ktk kipidi cha ITV Dk 45, mambo yabwagwa hadharani.


Hivi punde akihojiwa ktk kipidi hicho, Naibu spika wa Bunge la Jamhuri ya Muunganao wa Tanzania Mheshimiwa Dr Tulia Ackson, amedai mshahara wa Mbunge ni milioni 4.6 tu. Anakatwa Kodi Tsh 1500,000 na kubakiwa na Tsh 3100,000.

Ameendelea kudai posho ya kikao ni Tsh 120,000. Pia Kuna posho ya kumlipa Dereva na Katibu wa Mbunge na posho ya mafuta. Pia Kuna mfuko wa Jimbo.

Watu wa nje ya Bunge wakipiga hesabu wanadai ni Tsh 11,0000,000 jambo ambalo sio kweli. Hizo hela zinapita kwa Mbunge japo zote sio zake.

Kwa kauli hii ya Naibu spika wa Bunge ni dhahiri kuwa wabunge wanakatwa Kodi tofauti na uvumi uliopo mtaani.
 
Naibu spika wa JMT amesema mbunge anakatwa kodi.
Na kwa figure ya mshahara wa mbunge alioutaja ambao ni 4.6 minions na kodi ikuwa ni 1.5 milions kwa hesabu ya haraka tu unakuja kuona kuwa kodi anayokatwa mbunge ni zaidi ya 30% au tufupishe tuseme tu ni 30%.
Hivi tuna wabunge wazalendo kiasi hiki?
Miaka yote wainyamazie tu kodi kubwa inayogusa mfupa wao kiasi hiki?
Note: Mkitaka kuwadanganya wananchi basi tafuteni uongo mtakatifu.
Aweke salary slips za wabunge wazalendo tuzione
 
Tulia ni muongo.
Ktk kipidi cha ITV Dk 45, mambo yabwagwa hadharani.

Hivi punde akihojiwa ktk kipidi hicho, Naibu spika wa Bunge la Jamhuri ya Muunganao wa Tanzania Mheshimiwa Dr Tulia Ackson, amedai mshahara wa Mbunge ni milioni 4.6 tu. Anakatwa Kodi Tsh 1500,000 na kubakiwa na Tsh 3100,000.

Ameendelea kudai posho ya kikao ni Tsh 120,000. Pia Kuna posho ya kumlipa Dereva na Katibu wa Mbunge na posho ya mafuta. Pia Kuna mfuko wa Jimbo.

Watu wa nje ya Bunge wakipiga hesabu wanadai ni Tsh 11,0000,000 jambo ambalo sio kweli. Hizo hela zinapita kwa Mbunge japo zote sio zake.

Kwa kauli hii ya Naibu spika wa Bunge ni dhahiri kuwa wabunge wanakatwa Kodi tofauti na uvumi uliopo mtaani.
 
Back
Top Bottom