Dodoma: Nicodamus Maganga (Mbunge) adai Mishahara na Posho haiwatoshi Wabunge. Ashangiliwa...

Kwan wa South Africa wanalipwaje? tuanzie hapo kwanza.
Kama inshu ni kufananisha awatetee na walimu wa Tanzania wafanane malipo na walimu wa Nigeria.
 
Wapumbavu hao wabunge. Hawakatwi chochote kwenye malipo yao halafu wanataka zaidi?Hivi hao wahuni wanatuona sisi zombies sio?
 
Ana roho ya kifisadi huyo na hafai kuwa Bungeni. Kifupi ni mzigo 2025 asirudi mjengoni, Kench taip.
 
Mwakilishi wa wananchi anataka afanane na wabunge wa nchi zingine kwa kulipwa pesa ndefu,na maslahi manono kama wabunge wa nchi zingine,hicho ndio kipaumbele chake,
Mi ni nirifikiri Cha kwanza ni. Kutaka serikali ifsnye juhudi Ili tuwe na huduma bora za afya,Elimu,ajira,kipato kama wananchi wa nchi zingine,
Du hatari!na wabunge wengi,ubunge ni kama ajira,ukimtoa hapo anakufa kwa kihoro,
Wacha niendelee kupiga boda boda,
 
Sijamsikia. Ila kama ni kweli basi ni hamnazo kabisa na kaenda bungeni kujiwakilisha yeye na familia yake na si kutetea maslahi ya wapiga kura wake wala kuwatetea wapiga kura wake, ambao wapo taabani kwa changamoto mbalimbali za maisha.

Mawazo kama hayo ndiyo yanayonifikisha katika kuamini kuwa ili kupata wanasiasa kindakindaki wenye nia thabiti za kuwatumikia wananchi, Mapato ya kodi za wananchi yasitumike, aslani, kugharimia siasa na wanasiasa.

Serikali isitoe fedha za ruzuku kwa vyama vya siasa, bali ili kugharimia uendeshaji wake, kila chama kiwe kinafanya harambee za kusaka michango kwa wananchama wao ya kukiwezesha kukabiliana na gharama za uendeshaji wake na za kushiriki uchaguzi Mkuu, km ilivyo kwa Marekani.

Pia serikali ifute posho za vikao vya bunge kwa wabunge, kwani mishahara ya kila mwezi wanayolipwa kwa kazi ya ubunge ndiyo stahiki zao.

Aidha Serikali iunde Tume Huru ya Utumishi wa Umma ambayo, pamoja na mambo mengine, ipange viwango vya mishahara, na stahiki nyingine kwa kila kada ya utumishi wa umma(equitably), ikiwemo mishahara ya waheshimiwa wabunge, bila ya ubaguzi wala upendeleo na kwa kuzingatia hali ya uchumi wa nchi.

Si haki kwa mtumishi anayelitumika taifa hadi akistaafu kwa lazima akifikishapo miaka 60, aambulie malipo ya pensheni kiduchu, wakati mbunge, kwa kutumika kwa miaka kiduchu tu (mitano) apewe marupurupi ya kukufurisha baada ya kumaliza muhula wa miaka mitano tu ya ubunge, na akichaguliwa tena na tena anatunukiwa malipo 'kitonga' kama hayo!
 
Hili sio bunge, ni genge la wajumbe waliloteuliwa na Magufuli ili kubadilisha katiba atawale milele, kumsifia, kupitisha kila jambo la serikali yake. Sasa Magufuli amekufa, lipo pale linafanya nini?

Ushauri wangu.
Wananchi tuanze kupachimbisha, popote pale hawa wabunge watakapoonekana hadharani tuwazomee, tuwapige mawe nk.
 
Tulishasema na nasema tena

Wabunge ni wabinafsi,wanajali matumbo yao tu

Ova
 
Wenzetu South na Kenya wanalipwa kwa dola...
Your browser is not able to display this video.
 
Ugaidi na uasi unaanzaga hivihivi. Watu wakiona mmekuwa miungu watu wanawafata kwa vurugu mnaumizana
 
upinzani ulituchelewesha sana!
 
Labda tunamuonea. Kwa maana kwamba hicho ndo kiwango chao walioko Bungeni. Tukumbuke mawaziri wana uelewa zaidi ya waliobaki ukumbini lakini, si ndo akina Mwigulu?
 
Mi nadhani na laana pia wanayo ( mtoa hoja na wote waliomshangilia)
Hata mlipane mabilioni kamwe hamji kutoshekaa
 
Mibunge ya Tanzania ni miradi sana... Haipo hapo kwa ajili ya Wananchi bali mitumbo yao.
 
Heheheh siku akikosa ubunge atajua kuwa mshahara unatosha

Jambo la muda tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…