Unalinganisha shule na jeshi? no wonder unaona maamuzi yanayoathiri ufaulu wa wanafunzi ni sahihi yafuate.

Mkuu wa mkoa anazijua changamoto za mkoa wake zaidi ya waziri, that should give him a chance to provide immediate solutions to immediate problems bila kusubiri mtu fulani huko juu ambae hajui hizo changamoto atoe tamko.

Kama mkuu wa mkoa hana nguvu ya kufanya maamuzi yeyote kutatua changamoto za mkoa wake basi hiyo ofisi ni pambo tu haina kazi.

Kila raia anawajibu wa kutii sheria pekee na si vinginevyo.
 

Huyu mtaka kwa namna alivyowasilisha ujumbe ni takataka kabisa, serikali gani ya kipumbavu hivi?, why?ngo'ombe anenepe siku ya mnada? Integrity iko wapi?kama anakero zake atumie vikao vya ndani, yuko chini ya Ummy na Waziri Mkuu kashindwa ushawishi au wamemtuma? Makonda mpya huyu pumbavu kabisa hana adabu, kuna hiari na lazima, kama mwalimu wa fizikia, hesabu na kemia hawapo umelisemea, uzoefu wako wa Shinyanga umewashirikisha wizara zote mbili? Sifieni huu utovu wa kinidhamu ila kaongea kichoko sana, hana heshima na kanuni, taratibu, sheria na miongozo.
 
vijana katika ubora wao wa buku 4
 
Fala sana huyu jamaa........yahn wao kuambiwa ukweli kwao kosa .

Mtaka kasema ukweli viongozi waache siasa na shule za kata wakati watoto wao wanasoma mashule ya kueleweka.
Tofauti inayoonekana kwa vijana wengi, na ndiyo maana hata ajira zimekuwa ngumu sana, inaonyesha mnaenda shule si kwa ajiri ya kuondoa ujinga

Jenga hoja, na usipende matusi kwani kutoa matusi bila kujenga hoja ni sehemu mojawapo ya kujiani jinsi ulivyo mweupe kichwani

Unadhani hayo anayosimamia mkuu wa mkoa ndio mwongozo kitaifa, na unadhani anachokifanya mkuu wa mkoa hamkivunjii heshima mwingine? Lakini je, kulikuwa na ulazima mkuu wa mkoa kumtaja waziri kwenye kikao hiko?
 
Kwa mtizamo wangu naona hata kama RC Mtaka alikuwa na nia nzuri ya anachokiwakilisha lakini njia aliyoitumia sio sahihi kabisa. Hata kama Mtaka anajiona bora kutokana na sifa anazopata toka akiwa RC Simiyu sidhani kama ndio iwe tiketi ya yeye kubwata kiasi kile halafu eti anamchambua waziri hadharani vile hata kama huyo waziri ana mapungufu kiasi gani. Wote ni wateule wa raisi sasa vipi yeye Mtaka amshushie heshima mwenzake mbele za watu kiasi kile. Tena badala ya kuishia kumpinga waziri kwa hoja tu na hoja yake ilikuwa na mashiko kiasi fulani yeye akahamia kwenye mambo binafsi sijui gari yenye bendera, kiyoyozi, mara International school, sijui kupeleka watoto kusoma Ulaya. Na mbaya zaidi kumchonganisha hadharani waziri na wanafunzi, walimu na wazazi.

Mtaka hakupaswa kutafuta sifa kwa kumdhalilisha mwenzake ambaye wanajenga nyumba moja. Alipaswa kuwasilisha mpango kazi wake ambao unapingana na sera wizarani kwa Ndalichako angepigwa dana dana angeenda nao kwa waziri mkuu moja kwa moja na waziri mkuu akishindwa angeenda nao kwa mamlaka ya uteuzi wake yaani raisi. Kwa mihemuko ile aliyoonyesha Mtaka kwa Ndalichako nadhani kuna jambo baya kati yao linaendelea inabidi mamlaka ya uteuzi wao iingilie kati ikiwezekana mmojawapo apigwe chini kama sio wote wawili. Siku zote ogopa sana mtu anayetaka aonekane yeye ni bora kwa kutumia njia ya kuwadhalilisha/kwashushia hadhi wenzake.

Kwa kifupi alichafonya Mtaka ni udhalilishaji kama udhalilishaji mwingine wowote. Aliposema mpuuzeni huyo waziri nisikilizeni mimi maana yake Mtaka alikuwa anamaanisha nini kwa huyo waziri ambaye anasema asisikilizwe?
 
In Africa it's dangerous to be right when your master is wrong RC Mtaka kasimama na wananchi na katupa jiwe gizani huu ndo ukweli ambao wananchi wengi wanapiga kelele viongozi pelekeni watoto wenu shule za kata
 
Anthony Mtaka amenena ukweli mtupu mtupu kweli na kweli kumuweka mtu guru. Viongozi kama hawa ni muhimu sana kwa wakati huu wa dunia ya kidigitali. Acha watoto wasome kwa sababu wapo na walimu wao na viongozi wa kijiji hadi mkoa.

Ushauri tu, ni viongozi kuwa na semina ya kunong'onezana changamoto na madhaifu yao katika maamuzi ili kuepuka kutoleana uvivu mbele ya kadamnazi.
 
Jiwe aliwaharibu sana vichwa vyenu... Mtaka yupo sahihi..
 
Hii ndio Aina ya Uongozi tunaouhitaji nchi hii.
Asante sana Anthony Mtaka.
 
Kama vile naisikia sauti nyingine ya upande wa Mtaka ikisema... "KATIBA MPYA NI MUHIMUUUU, ANAYESEMA KATIBA MPYA SIO MUHIMU MUMPUUZE.
MSIWASIKILIZE WANASIASA (bila kutaja jina au cheo).
Naongea hivi kwa sababu mimi ndio ninakaa na wananchi. Mnanielewa?"
 
Wewe kwa akili hizi ni Sifuri, Kuna mkoa unaitwa "Songea"

Wana ccm mna matatizo makubwa sana

Unatetea mambo wakati wewe una elimu ya kuunga unga na elimu ya shule za kata

Mkuu wa mkoa anataka kuboresha, wewe unataka watoto wawe Vilaza kama wewe
Wawe vilaza waendelee kuwa tawala
 
Wengine wameajiriwa na serikali lakini sisi raia tunaambiwa tujiajiri mana serikali haina nafasi.

Nasikia Mhe. Joyce Ndalichako ana mtoto mmoja na alifeli chuo, wajuzi ni kweli hayo.?
Kusoma Msolwa St. Gaspare na Canada sio mchezo.
 
Mtaka ana taka maamuzi ya chini yafanyike na kuamukiwa huko chini, Kama Ni katanibau wilayani maana mdio wanaojijua mazingira yao na sio maamuzi yafanywe na Serikali kuu. Loud and Clear. Yuko sawa. Ndio maana tunataka katiba mpya
 
Wewe ndio umesoma na kuona shule na jeshi tuu kwenye bandiko langu, kama Mimi nilivyoona Aya yako ya Mwisho.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…