Dodoma: RC Antony Mtaka amchana Waziri wa Elimu kuhusu mwisho wa Watoto kusoma kuwa ni saa tisa
Nchi hii inayumba sana kwa sababu ya kuoneana aibu. Anthony has made it. Development is integrated with difference in opinions. Na hakuna kuambiana huko ofisini. Tell it in broad day light. Joyce amemkera sana Anthony I hope. Hata mimi ningemjibu hivyo hivyo zaidi ya Anthony. Watoto wakifeli RC ndiye anasakamwa. Remember, waziri ni policy tu lakini utendaji uko TAMISEMI kwa akina Anthony. Niliwahi kusema kuwa wakuu wa mikoa watakaofanikiwa ni Anthony, Kafulila, and Queen.
Kwa nini wasiitane wakajadiliana na siyo kudhalirishana?

Tamko la Mtaka, linaondoa heshima ya waziri kwa wanafunzi na wazazi, huoni kwamba kuna siku waziri anaweza kuzomewa kwa tamko la kidhalirishaji la mkuu wa mkoa?

Mkuu wa mkoa, aache dharau, angelikuwa yeye ndio waziri angependa kudhalirishwa kiasi hiko?

Kwani kulikuwa na ulazima wa yeye kutaja jina la waziri kwenye mpango na mikakati yake ya kuboresha Elimu mkoani kwakee?
 
Swala la Elimu yetu kufanywa kama mpira wa danadana na kila mmoja kuwa anachezea, ni makosa makubwa sana, mwongozo wa pamoja uko wapi?

Napingana na huyo mkuu wa mkoa wenu pendwa, Inakuweje awe na mpango wa kivyake vyake?

Mkuu wa mkoa wa Songea naye awe na matakwa yake, na wa mikoa mingine, tutakuwa taifa la aina gani?
Sasa kama mpango huo huo aliutumia mkoa wa SIMIYU, na ukaleta matokeo mazuri sana, kwanini asiutumie tena?nenda SIMIYU, ukaona mapinduzi ya elimu aliyoyaacha huko kutokana na mfumo huo.
 
kwa mara ya kwanza nasikia maagizo ya waziri niliona kama hakutumia akili sawasawa. muda wa ziada ilikuwa advantage kwa wanafunzi hasa wasio na uwezo wa tuisheni,pia kuendelea kuwaweka pamoja wanafunzi badala ya michezo. shule ziliweka mkazo zaidi madarasa yenye mitihani ya taifa. Waziri ni hovyo kabisa
Ni kweli mkuu.

Nadhani waziri alibugi kwa namna flani
 
Mtaka Hana adabu kabisa. Nigelikuwa Samia I would have fired him immediately. Angelitafuta forum ya staha kusema aliyoyasema na si kubwatuka mbele za wazazi kumdhalilisha mteule mwenzake. Mtu anaweza kugeneralise kuwa the gov is disunited in it's dealings Amesema màneno ya kishenzi akiwa part of the government machinery.
Hafai kukalia ofisi ya umma.
Mkuu afunguliwe uzi huyu mfuasi wa Chatorism hawa ndo Mataga wanao vuruga....
 
Ni kweli Ndalichako ni wa hovyo sana, lakini Tony naye angetumia lugha ya kidiplomasia kidogo kwakuwa watz wa siku hizi wanaelewa kwa haraka.
Hapana mkuu. Sometimes ukitumia lugha ya kidiplomasia ujumbe haufiki.

Ukiwa kwenye administration unaelewa zaidi alilofanya Mtaka. Sometimes you have got to blast someone in front of everybody ili mambo yaende.

Believe me
 
Sasa kama mpango huo huo aliutumia mkoa wa SIMIYU, na ukaleta matokeo mazuri sana, kwanini asiutumie tena?nenda SIMIYU, ukaona mapinduzi ya elimu aliyoyaacha huko kutokana na mfumo huo.
Kwani yeye Mtaka anaugomvi na waziri?

Je, kulikuwa na ulazima wa kutaja jina waziri kwenye mikakati yake ya kuinua elimu katika mkoa wake?

Haoni kwamba, tayari amemhasimisha waziri kwa wanafunzi na kwa wazazi kwamba yeye hafai kusikilizwa, na siku ya siku anaweza kuzomewa...?

Hao wote ni wateule wa Rais, kwa nini wasinge fanya chemba kwanza?

Mtaka aache udhalirishaji
 
Mtaka Hana adabu kabisa. Nigelikuwa Samia I would have fired him immediately. Angelitafuta forum ya staha kusema aliyoyasema na si kubwatuka mbele za wazazi kumdhalilisha mteule mwenzake. Mtu anaweza kugeneralise kuwa the gov is disunited in it's dealings Amesema màneno ya kishenzi akiwa part of the government machinery.
Hafai kukalia ofisi ya umma.
Mkuu afunguliwe uzi huyu mfuasi wa Chatorism hawa ndo Mataga wanao vuruga
Kwamba yeye hashindi kwenye kiyoyozi? Kwamba yeye haindeshwi kwenye gari ya kiyoyozi? Kwamba watoto wake hawasomi "international schools"??

CCM wanafiki sana sana, wacha wararuane
Baaambieee hao Mataga...
 
Hiyo sio mara ya kwanza kuja na kauli za ovyo ovyo ambazo hazina logic yoyote.

View attachment 1851226

Watu wanaamua kufanya special day siku watoto zao wanapotoka hatua moja ya elimu kwenda nyingine.

Wanawavisha tu vijoho siku ya graduation kwenye harakati za kuwatunzia kumbukumbu zao ukubwani kuifanya hiyo siku special zaidi.

Guess what? Ndalichako hataki eti majoho ni kwa sherehe za undergraduates na kuendelea; how shallow is this woman.

Huwa anatoa kauli kutokana na mtazamo wake tu (moral views of things) not weighing the pros and cons on practical side of her decision/statement.

Mkuu wa mkoa hayuko pekee mpaka kamtolea uvivu in maana kuna watu wengi washachoka kusikiliza kauli zake za kipuuzi.
Haya tuma salamu kwa watu watatu.
 
Kwa nini wasiitane wakajadiliana na siyo kudhalirishana?

Tamko la Mtaka, linaondoa heshima ya waziri kwa wanafunzi na wazazi, huoni kwamba kuna siku waziri anaweza kuzomewa kwa tamko la kidhalirishaji la mkuu wa mkoa?

Mkuu wa mkoa, aache dharau, angelikuwa yeye ndio waziri angependa kudhalirishwa kiasi hiko?

Kwani kulikuwa na ulazima wa yeye kutaja jina la waziri kwenye mpango na mikakati yake ya kuboresha Elimu mkoani kwakee?
Unajuaje kama hajamtafuta ili wakae na waziri akaishia kumpiga RC danadana??

RC anataka strategies sasa atamsubiri waziri mpaka lini huku waziri anampiga danadana tu??
 
Unajuaje kama hajamtafuta ili wakae na waziri akaishia kumpiga RC danadana??

RC anataka strategies sasa atamsubiri waziri mpaka lini huku waziri anampiga danadana tu??
Ukikaa vizuri ukatulia ukafikirii...! nakuhakikishia mkuu, utakubaliana kwamba, Mtaka, kafanya kosa, kamchonganisha waziri kwa watoto woote wa shule zote hadi vyuoni na kwa wazazi kwamba, hastahili kusikilizwa, kitu ambacho hakikuwa cha lazama mkuu wa mkoa kutamka vile Mbele ya kikao cha wazazi na watoto! Kafanya udhalilishaji

Mtaka mpaka hapa, hafai atimmliwe, ama amwombe radhi waziri peupe kama alivyokuwa akijinadi kwa wazazi
 
Mataka awaasa wananchi wampuuze Waziri wa Elimu kuhusu mambo ya elimu Kwenye mkoa wa Dodoma.

Mataka amesema wampuuze Waziri ambaye watoto wake wanasoma international school.

Sikiliza audio hapo.
Mama Ndali umezoea kuwaonea wakuu wa taasisi za elimu halafu system inakuangalia tu.

View attachment 1851200


Ndalichako ni Waziri wa kawaida sana. Tokea aingie Wizarani ni kufitinisha tu wenzake.

Wakuu wa taasisi wanamkoma huyu Mama. Wakuu wa idara Wizarani wanaipata habari yake.

Ndalichako badilika Mama Samia yupo tofauti na mwendazake.

Hakuna thamani uliyoongeza hapo Wizarani zaidi ya kufitinisha wakurugenzi na mamlaka za uteuzi.

Tabia ya kuwafitinisha wenzako waondolewe kwenye uteuzi acha mara 1.
Ndalichako alishindwa Baraza la Mitihani kwa ubishi wake ilikuwaje apewe Wizara.
Mama Samia tuondolee huyu Ndali
LAkini pia si kweli kuwa watoto wanabaki shule kwa sababu masaa waliyopewa tangu asubuhi hayatoshi.
Mara nyingi unakuta mtoto anakuambia wanabaki kufanya masomo ya ziada wakati tangu asubuhi mpaka saa tisa waalimu walioingia kufundisha ni wawili tu na wamefundisha masaa yasiyozidi mawili. alafu unaambiwa saa tisa watoto wabaki kwa masomo ya ziada. Matokeo yake ni kuwashindisha njaa watoto tu.
Anachotetea Mtaka kinakuwa na maana tu iwapo ni kweli waalimu wanawajibika kikamilifu katika muda wao halali wa kufundisha. Otherwise hii kitu inaitwa masomo ya ziada si ya ziada.
 
Mtu mwenye Phd ukimsikiliza ata masters tu provided kweli kaisotea na transcript zake zimejaza B’s kwenda juu kuanzia sekondari anapoongea kuna reasonability ya intelligence unaiona.

Siku zote nimekuwa nasema Ndalichako doesn’t add up kama Phd; she is just too shallow ukimsikiliza mara nyingi.

Mtu mwenye Phd ukimsikiliza ata masters tu provided kweli kaisotea na transcript zake zimejaza B’s kwenda juu kuanzia sekondari anapoongea kuna reasonability ya intelligence unaiona.

Siku zote nimekuwa nasema Ndalichako doesn’t add up kama Phd; she is just too shallow ukimsikiliza mara nyingi.
Erratum: it is "reasonableness" not "reasonability"!
 
Ntinje, mimi ni form four failure, nipo mtaani nafanya umachinga. Ila nikipata nafasi naperuzi kidogo kuhusu wanafalsafa wa kale eg. Karl Marx
 
Huyu jamaaa anakosea Sana kusema maneno kama hayo hata kama ana point, kumsema waziri anayeaminiwa na rais ni utovu wa nidhamu, haya wangetakiwa wayamalize ndani ya serikali
 
Mtaka ukae ukijua ipo siku ya kwako yatajulikana, wale influencers unaowalipa mtandaoni kukusifia utawalipa hadi lini?
Mtaka ni kiongozi wa hovyo sana ambae anatumia kuchangia na kulipa watu wenye ushawishi mtandaoni ili wamsifie huku yeye akiendelea kupiga madili. Ipo siku mama Samia atakumulika, muda utasema
Hio ni jungu.
Kama unafahau, au unawafahamu wanaompamba Mtaka mitndanoini kwa nini usiseme wazi.
Mtaka ni kijana safi, kwa kuli na vitendo.
Hata wakati wa Mwendazake , yeye ingalau akii zilikuwa zimetulia.
Hakuwahi kumweka mtu ndani kwa kadri ya kumbukumbu zangu, kama fashioni za kina Makonda na wenziwe.
 
Back
Top Bottom