Dodoma: RC Antony Mtaka amchana Waziri wa Elimu kuhusu mwisho wa Watoto kusoma kuwa ni saa tisa
Mtaka ukae ukijua ipo siku ya kwako yatajulikana, wale influencers unaowalipa mtandaoni kukusifia utawalipa hadi lini?
Mtaka ni kiongozi wa hovyo sana ambae anatumia kuchangia na kulipa watu wenye ushawishi mtandaoni ili wamsifie huku yeye akiendelea kupiga madili. Ipo siku mama Samia atakumulika, muda utasema
Ngoja na wewe tukuone hapo kisarawe utafanya Nini!
 
Mtaka yupo sahihi kuhusu Kambi zake. Lakini approach ya kumjibu waziri, yaani mteule wa rais hivi kuna mushkeli kidogo. Labda yupo undercover ili kumexpose waziri kurahisisha uamuzi wa mamlaka
Wote ni wateuzi wa rais
 
Naopongeza ujasiri wa mkuu wa Mkoa huu. Mtaka hongera sio Waziri anakurupuka tu bila kuwashirikisha wakumbuke hilo ni la Serikali za mtaa. Na huo ndio ukweli wototo wao wapo Canada sisi wapo shule za kata.
 
Waziri hajatoa agizo kwa feelings zake, ipo miongozo ya elimu. Badala ya kushambulia mtu angejikita kwenye mabadiliko kisera na nafasi hiyo anayo. Lakini pia anaweza kuwasiliana na waziri au hata Rais kwa marekebisho kama ana hoja.

Kwanini amdhalilishe waziri? Unajua matokeo ya kauli zake ikiachwa namna hii bila kuwajibika?

Nimesema wewe unajua vyema, Mbowe hata kama akiongea jambo hadharani akakosea kuna mtu pale ufipa anaweza kutoka hadharani kumkosoa akabaki salama? Uongozi una miiko yake lakini tukienda hivi mawaziri wataachia wakuu wa mikoa wafanye wanalotaka.

Mama Samia anapaswa kunyoosha rula. Huu ni utomvu wa nidhamu anapaswa kuchukua hatua ili viongozi waheshimiane otherwise tutasikia mengine na mwisho serikali kuwa dhaifu.
Usimdanganye Mama Samia achague kati ya watoto wa masikini, na watoto wa Viongozi kama Waziri Ndalichako.
Unamtaka Rais Samia aamue kuwa watoto wa wakubwa wasome mpaka saa 4 usiku lakini watoto wa wanyonge wasizidishe kusoma zaidi ya saa 9 jioni.
Waziri Ndalichako na miongozo ya Wizara wamekosea.
Wajirekebishe mapema iwezekanavyo.
Hali hii inanikumbusha miaka ya Baba wa Taifa wakati Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Kanali Nsa Kaisi, alipokaidi maagizo wa wakubwa akajichimbia Vijijini na kuhamasisha uchimbaji wa mtaro wa maji ulioleta ukombozi mkubwa kwa Vijiji kadhaa.
Msimsumbue Rais Samia na mawazo yenu ya kupinga Elimu ya watoto wa Shule za Kata
 
Kwani kipi kaongea kubaya hapo tatizo ccm mnataka watoto wa wenzenu waendelee kuwa mbumbu angalia mikoa ya watu walio pita pita shule huwezi kuta Wana ushabiki wa kijinga kwa ccm na hicho hicho ndicho hamkitaki ninyi
Mikoa gani mkuu? Nchi hii kuna shule kweli? Au kukariri makaratasi?
 
Kwa mtizamo wangu naona hata kama RC Mtaka alikuwa na nia nzuri ya anachokiwakilisha lakini njia aliyoitumia sio sahihi kabisa. Hata kama Mtaka anajiona bora kutokana na sifa anazopata toka akiwa RC Simiyu sidhani kama ndio iwe tiketi ya yeye kubwata kiasi kile halafu eti anamchambua waziri hadharani vile hata kama huyo waziri ana mapungufu kiasi gani. Wote ni wateule wa raisi sasa vipi yeye Mtaka amshushie heshima mwenzake mbele za watu kiasi kile. Tena badala ya kuishia kumpinga waziri kwa hoja tu na hoja yake ilikuwa na mashiko kiasi fulani yeye akahamia kwenye mambo binafsi sijui gari yenye bendera, kiyoyozi, mara International school, sijui kupeleka watoto kusoma Ulaya. Na mbaya zaidi kumchonganisha hadharani waziri na wanafunzi, walimu na wazazi.

Mtaka hakupaswa kutafuta sifa kwa kumdhalilisha mwenzake ambaye wanajenga nyumba moja. Alipaswa kuwasilisha mpango kazi wake ambao unapingana na sera wizarani kwa Ndalichako angepigwa dana dana angeenda nao kwa waziri mkuu moja kwa moja na waziri mkuu akishindwa angeenda nao kwa mamlaka ya uteuzi wake yaani raisi. Kwa mihemuko ile aliyoonyesha Mtaka kwa Ndalichako nadhani kuna jambo baya kati yao linaendelea inabidi mamlaka ya uteuzi wao iingilie kati ikiwezekana mmojawapo apigwe chini kama sio wote wawili. Siku zote ogopa sana mtu anayetaka aonekane yeye ni bora kwa kutumia njia ya kuwadhalilisha/kwashushia hadhi wenzake.

Kwa kifupi alichafonya Mtaka ni udhalilishaji kama udhalilishaji mwingine wowote. Aliposema mpuuzeni huyo waziri nisikilizeni mimi maana yake Mtaka alikuwa anamaanisha nini kwa huyo waziri ambaye anasema asisikilizwe?

Rais makini anapaswa kumtoa huyo Mtaka taka ndani ya masaa tu apishe kabisa, serikali imevuliwa nguo kwa kiasi hiki, no hapana kabisa
 
Utii hata kwa fyongo utii wa woga wewe hufai hata ukatibu kata huwezi kuhuji?
Una upepo mfu na infant wa kutupwa kabisa, think think. Poor Tanzania huna akili kabisa achana na ushabiki na mihemko
 
Waziri hajatoa agizo kwa feelings zake, ipo miongozo ya elimu. Badala ya kushambulia mtu angejikita kwenye mabadiliko kisera na nafasi hiyo anayo. Lakini pia anaweza kuwasiliana na waziri au hata Rais kwa marekebisho kama ana hoja.

Kwanini amdhalilishe waziri? Unajua matokeo ya kauli zake ikiachwa namna hii bila kuwajibika?

Nimesema wewe unajua vyema, Mbowe hata kama akiongea jambo hadharani akakosea kuna mtu pale ufipa anaweza kutoka hadharani kumkosoa akabaki salama? Uongozi una miiko yake lakini tukienda hivi mawaziri wataachia wakuu wa mikoa wafanye wanalotaka.

Mama Samia anapaswa kunyoosha rula. Huu ni utomvu wa nidhamu anapaswa kuchukua hatua ili viongozi waheshimiane otherwise tutasikia mengine na mwisho serikali kuwa dhaifu.
Miongozo ya Elimu?
Kwa Shule za Kata tu?
Mwambieni Waziri Ndalichako atekeleze hiyo miongozo kwenye Shule wanazosoma watoto wa Mawaziri, Wabunge, Wenyeviti wa Vyama vya Siasa, (Mbowe, Samia, Mbatia, Zitto, et al), uangalie moto utakavyomuwakia!
 
Kwa mtizamo wangu naona hata kama RC Mtaka alikuwa na nia nzuri ya anachokiwakilisha lakini njia aliyoitumia sio sahihi kabisa. Hata kama Mtaka anajiona bora kutokana na sifa anazopata toka akiwa RC Simiyu sidhani kama ndio iwe tiketi ya yeye kubwata kiasi kile halafu eti anamchambua waziri hadharani vile hata kama huyo waziri ana mapungufu kiasi gani. Wote ni wateule wa raisi sasa vipi yeye Mtaka amshushie heshima mwenzake mbele za watu kiasi kile. Tena badala ya kuishia kumpinga waziri kwa hoja tu na hoja yake ilikuwa na mashiko kiasi fulani yeye akahamia kwenye mambo binafsi sijui gari yenye bendera, kiyoyozi, mara International school, sijui kupeleka watoto kusoma Ulaya. Na mbaya zaidi kumchonganisha hadharani waziri na wanafunzi, walimu na wazazi.

Mtaka hakupaswa kutafuta sifa kwa kumdhalilisha mwenzake ambaye wanajenga nyumba moja. Alipaswa kuwasilisha mpango kazi wake ambao unapingana na sera wizarani kwa Ndalichako angepigwa dana dana angeenda nao kwa waziri mkuu moja kwa moja na waziri mkuu akishindwa angeenda nao kwa mamlaka ya uteuzi wake yaani raisi. Kwa mihemuko ile aliyoonyesha Mtaka kwa Ndalichako nadhani kuna jambo baya kati yao linaendelea inabidi mamlaka ya uteuzi wao iingilie kati ikiwezekana mmojawapo apigwe chini kama sio wote wawili. Siku zote ogopa sana mtu anayetaka aonekane yeye ni bora kwa kutumia njia ya kuwadhalilisha/kwashushia hadhi wenzake.

Kwa kifupi alichafonya Mtaka ni udhalilishaji kama udhalilishaji mwingine wowote. Aliposema mpuuzeni huyo waziri nisikilizeni mimi maana yake Mtaka alikuwa anamaanisha nini kwa huyo waziri ambaye anasema asisikilizwe?

Hongera sana Mkuu barikiwa mno
 
Yule mama ni zero nasemaga mara nyingi,sijui anatumiaga nini kufikiri huyu bibi,mtaka yuko sahihi,Mh rais tuondolee huyu bibi
 
Swala la Elimu yetu kufanywa kama mpira wa danadana na kila mmoja kuwa anachezea, ni makosa makubwa sana, mwongozo wa pamoja uko wapi?

Napingana na huyo mkuu wa mkoa wenu pendwa, Inakuweje awe na mpango wa kivyake vyake?

Mkuu wa mkoa wa Songea naye awe na matakwa yake, na wa mikoa mingine, tutakuwa taifa la aina gani?
Mkuu wa mkoa wa Songea hoyeee!!
 
mtaka yuko sahihi 100 percent kabsa waziri wa elimu ni hovyo. kama Yule fedha huu ni usawa wa ukweli n.a. uwazi.
 
Mtaka tumemsifia sana sasa kalewa sifa! Anajiona very exceptional

..Nakubaliana na wewe kwamba RC Mtaka hakutakiwa kumshambulia Waziri Ndalichako waziwazi kana kwamba hawatumikii serikali moja.

..Mtaka angeweza kuwaambia waalimu na wanafunzi waendelee na kambi zao za mafunzo ya ziada, na yeye kama RC wao atakwenda kuzungumza na Waziri wa Elimu ili kuweka mambo sawa.

..Mambo ya international school, sijui gari yenye kiyoyozi, etc etc hayakupaswa kuzungumzwa na RC mwenye heshima zake kama Mh.Mtaka.
 
Kisiasa huyo Mkuu wa mkoa kakosea sana. Alichofanya ni utovu wa nidhamu kwa serikali na Chama Cha Mapinduzi. Sema huyo RC ana nguvu kubwa sana ya umma nyuma yake... kumtumbua kizembe inaweza leta mtikisiko. Waziri angetulia zake na kufanya mambo yanayomhusu. Hii kuingilia hadi watoto wasomeje ni upumbavu kwa hadhi ya waziri.... waziri adili na mambo ya madawati, mitaala, maslahi ya walimu na mambo mengine ngazi ya kitaifa. Kambi za wanafunzi ni jambo dogo mno. Tusubiri uamuzi wa Mwenyekiti wa CCM (Rais wa JMT) katika hili.
 
Ni kweli kuna tatizo kidogo katika suala la elimu yetu, kutokana na kukosekana dira ya moja kwa moja ambayo kila waziri ataifuata kuendeleza pale alipoishia mwingine!
Hata hivyo pamoja na mapungufu ya waziri wetu wa elimu siungi mkono kitendo cha Mtaka kumtolea maneno aliyoyatoa kwani ni mbali ya kumdhalilisha pia amemkosea heshima kama kiongozi mwenye mamlaka zaidi yake! Wote ni wanaCCM kwanini wasiyaongee wawili wakamalizana? Angekuwa ni waziri wa CHADEMA ingekuwa sawa maana tumezoea kusikia wabunge wake wakizodolewa hadharani na hata kuitwa wezi lakini Mungu ni mwema anawavusha!
Hivyo busara itumike na ikibidi viongozi hao wakutanishwe!
 
Una upepo mfu na infant wa kutupwa kabisa, think think. Poor Tanzania huna akili kabisa achana na ushabiki na mihemko
Naona tunashabilikia udicteta type of rule. Wizara ingeconsult watu wa chini through their staffs in Councils and RC s office ili kupata uhalisia ulivyo chini. Sio kutoa tu amri bila kupata mambo yalivyo chini. Rc yeye na team yake walishajipanga kuondoa zero kwenye mkoa wao wewe unaleta amri ya kusitisha masomo saa tisa alasiri.
 
Back
Top Bottom