DODOMA: Tundu Lissu ajeruhiwa kwa risasi, akimbizwa Hospitali

DODOMA: Tundu Lissu ajeruhiwa kwa risasi, akimbizwa Hospitali

NAAMINI MUNGU ANAKWENDA KUMPONYA RAISI WA TLS MPAKA MTASHANGAA
 
Mwanasheria Mkuu wa Chadema Tundu Lissu ameruhusiwa kutoka chumba cha upasuaji akiwa na fahamu na sasa anapelekwa Nairobi nchini Kenya kwa matibabu zaidi.
======
Taarifa zote za uhakika tutakuwa tunazitoa kila baada ya muda mfupi...
Picha HELKOPITA iliyombeba Mwanasheria Mkuu wa Chadema Tundu Lissu ikiwa angani kuelekea Nairobi
View attachment 583481
Siku zote Shetani hajawahi kumshinda Mungu .
 
Wakuu,

Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA, rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) na Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu, ajeruhiwa kwa risasi.

Kwa sasa wapo hospitali ya Mkoa, mjini Dodoma.

Ameshambuliwa kwa risasi wakati akishuka nyumbani kwake Area D Mjini Dodoma, alikuwa akitokea Bungeni na alienda Nyumbani kula chakula cha mchana.

Lissu amepigwa risasi 5, miguuni na tumboni.

Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe amesema hali ya Mbunge huyo aliye hospitalini sasa ni mbaya!




56d494001b8e52eca1b71490ff9635e4.jpg


9f94cea0e0708e5fafb57915caf1dd27.jpg

abc21fedd617180297c6247f403b7362.jpg


Updates to follow

=======

UPDATES:

=======

UPDATE: Ndege imeshawasili Dodoma ili kumchukua Tundu Lissu kumpeleka Muhimbili kwa matibabu zaidi

DODOMA: RPC amesema watu waliomshambulia Tundu Lissu walikuwa wakitumia gari aina ya Nissan la rangi nyeupe

Freeman Mbowe: Ndugu Lissu kwa sasa yuko katika chumba cha upasuaji anajaribu kuokoa maisha yake, nitazungumza baadaye.
View attachment 583459
UPDATES: Miongoni mwa waliofika hospitali kumuona Lissu ni Spika Job Ndugai, Waziri Ummy Mwalimu na katibu mkuu wa bunge, Dkt. Thomas Kashilila

TAARIFA YA AWALI KUHUSU SHAMBULIO LA KUPIGWA RISASI MHE. TUNDU LISSU

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimepokea kwa mshtuko mkubwa taarifa ya kupigwa risasi Mwanasheria Mkuu wa Chama ambaye pia ni Mnadhimu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni na Mbunge wa Singida Mashariki, Mhe. Tundu Antipus Lissu baada ya kikao cha Bunge mchana wa leo.

Shambulio hilo limetokea majira ya mchana nyumbani kwake Area D Dodoma na kujeruhiwa vibaya na kukimbizwa katika Hosiptali ya Mkoa wa Dodoma.

CHADEMA tunalaani vikali kitendo hicho, na tunafuatilia kwa karibu hali yake.

Taarifa zaidi zitaendelea kutolewa.

Imetolewa na Kurugenzi ya Uenezi, Mawasiliano na Mahusiano ya Nje.

CHADEMA MAKAO MAKUU

DAR ES SALAAM.

=====

Preliminary Press Statement on the incidence of Hon. Tundu Lissu being shot

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) has received with great shock the report on the shooting of the Attorney General of the Party who is also the Chief Whip of the Official Opposition in Parliament and MP of Singida East, Hon. Tundu Antipus Lissu just after a Parliamentary session today.

The attack took place at his Dodoma residence at midday and was seriously wounded and had been rushed to the Dodoma Regional Hospital.

CHADEMA strongly condemns this act, and we are following up closely on his condition.

We will continue to update as we get more information.

Issued by the Directorate of Ideology, Publicity, Communications and Foreign Relations.

=======

Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini ameeleza jinsi Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu alivyopigwa risasi nyumbani kwake mjini Dodoma.

Selasini amesema kuwa maelezo aliyopata ni kuwa alikuwa akifuatiliwa na gari tangu anatoka bungeni na dereva wake alilishtukia. Amesema kuwa alivyoona wanamfutilia alipofika nyumbani, dereva alimsihi Lissu asishuke ndani ya gari.

"Hao watu walipoona hawashuki walijifanya kuna kitu wanaangalia walivyoona kuna utulivu walisogeza gari lao ambalo ni tinted na kuanza kurusha risasi upande wa Lissu." amesema.

Selasini amesema, “Risasi zilimpata mguuni, mkononi na tumboni lakini daktari anasema anaendelea vizuri."

Lissu amepigwa risasi leo Alhamisi na kupelekwa chumba cha upasuaji katika Hospitali ya Rufaa ya Dodoma.

Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah, Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe, wabunge na viongozi wengine wa ulinzi wa Bunge wamefika katika hospitali hiyo kujua kinachoendelea.

Baadhi ya ndugu na wagonjwa wamefurika katika chumba cha upasuaji cha hospitali ya mkoa wakitafakari huku wengine wakilia.

MORE UPDATES

Katibu wa Bunge amethibitisha kufika kwa ndege Dodoma kumchukua Tundu Lissu kumpeleka hospitali ya Muhimbili ili kuokoa maisha yake

View attachment 583477

Rais Magufuli ametoa pole na kutaka Vyombo vya Dola kuchukua hatua:

3b0c289593c46e591d17070adda48d11.jpg


CCM imetoa pole

31c0c74743877f774b093e84c0906232.jpg


Waziri wa zamani, Mark Mwandosya naye ametoa pole

12d9f3126c463d0b2305ab6ada291270.jpg


KWA HIYO CCM WALIJUA HUYU BWANA YATAMTOKEA YA KUMTOKEA TOKA MWEZI AUGUST?
Kweli mwenyezi anajua kuumbua.
 
Unyama huu ni ktendo klchopangwa na lengo n kutoa uhai wake akka mungu ndo anaejua uhai wa mtu, na hao wanafk wanaoanza kutoa salam za pole n unafk mtu hao ndo wapangaj wa shambulio hilo, na mungu hakka atawaumbua. Hakka uongozi wenu hautakubalka na jamii, mtalaaniwa na mwsho wenu n mbaya,nyie endeleen na utawala wenu wa kdkteta uchwara, jiulzen gadafi yuko wapi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umesoma nilichoandika au umekimbilia kujibu tu. Dereva amegundua anafuatiliwa akaamua kwenda nyumbani. Wewe unafuatiliwa nyuma na usiowajua utaenda nyumbani? Ukiingia ndani ndio dead end hio huna cha kujitetea. Kuna sehemu nyingi za kwenda zaidi ya nyumbani tena unaendesha one of the very powerful cars on the market.

Lissu amekuwa akifuatiliwa na vijana wa kazi muda mrefu na alijua hilo na hata kulisemea kwenye moja ya press conferences zake akitaja aina na namba za gari! Kwa leo halikuwa tukio la kipekee sana mpaka dereva aliposhangaa wafuatiliaji wamekomaa naye mpaka nyumbani na ndio akatoa tahadhari kwa boss wake asishuke kwanza ili waone wafuatiliaji wanatakaje! Kwamba wameamua kumfyatulia risasi akiwa bado kwenye gari ina maana dereva angejaribu kuwakimbia wangemfukuzia na kupiga gari risasi matairi likiwa kwenye mwendo kasi ili ale mzinga! Story ingetengenezwa nyingine kabisa! Bora limefanyika kweupe nyumbani kwake ili kila mmoja aone na ajue tulikofika
 
wauwaji hawawezi kupiga risasi 8 halafu wapige tumboni,miguuni na dereva asiguswe..au laa hawakuwa professionals
Lini wamewahi kuwa competent watz?Wanaweza kutupiga wanyonge tuu.Ila kila mahali watz ni very predictable and incompetent km maprof yao. Kwanza aliyepanga issue nzima sio competent.FINALLY MUNGU NDIE MKUBWA.
 
Hapa kuna ka mchezo kanaendelea,ili serikali ionekane haitendi haki,
Kama hawa waliompiga risasi,ndio wale waliolipua ofisi za IMMA,hawa watu ni professionals,gun for hire,
Idara za kiientelligencia wawe makini,hii kesi ichunguzwe na vijana wa ikulu,sio polisi tu,alipopigiwa risasi,area D,Dodoma,ni eneo lililo kimya,ni low density area,huwa hakuna pirika pirika nyingi,ni kama masaki kwa dar,sasa kama watu wanafanya uharifu,na kupotea,mpaka sasa HV,hakuna aliyekamatwa,kazi sio ndogo
 
Hiyo bili analipa nani? Tls lile jengo halitajengwa ngo! Hela yote itaishia kwenye matibabu
 
Back
Top Bottom