Dondosha mstari wowote wa Biblia unaoupenda leo ni Ijumaa

Dondosha mstari wowote wa Biblia unaoupenda leo ni Ijumaa

Unakumbuka kweli unachokisimamia

Kwa mujibu wa Isaya ulidai Yesu ndiye mwana, ndiye Roho na ndiye Baba yaani kwa maana yako Yesu anajibadilishabadilisha

Sasa hapa andiko linasema wapo watatu nafsi ambazo ni independent siyo mmoja kubadilikabadilika
Nimekujibu ila huenda hujaelewa. Umeshindwa kabisa kutoa maana ya hiyo Isaya 9, unahamisha tu goli. Sasa nitakuoa ufafanuzi wa 1 Yoh 5.

Kwanza ni vema kuelewa Yohana hapa anazungumza nini? Hoja ya msingi, HAKUNA KISA CHA UTATU HAPO!! Yohana anathibitisha kuwa YESU NI MWANA WA MUNGU na kwamba ndani yake mna uzima wa milele.

Tuanze na hao WATATU wanaoshuhudia mbinguni:
1. Baba - ukirejea ubatizo wa Yesu sauti ya Baba ilitoka katika wingu jeupe, huyu ni mwanangu mpendwa wangu...

Tena wakati Yesu anageuka sura bustanini Gethsemani sauti hiyo ilisikika, huyu ni mwanangu mpendwa...

2. Neno - rejea Yoh 1:1 Kristo ni Neno la Mungu, hakuna wakati hata mmoja Kristo aliongea ama kufanya kwa fikra zake mwenyewe isipokuwa alimsikia na kumwona Baba. Maana yake ni kwamba Kristo kama mwanadamu kamili hakutenda lolote kwa ufahamu wa kibinadamu bali kila alichofanya ni Baba ndiye alikuwa anatenda ndani yake, total surrender.

Yohana 5 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
¹⁹ Mwana hawezi kutenda neno mwenyewe ila lile ambalo amwona Baba analitenda; kwa maana yote ayatendayo yeye, ndiyo ayatendayo Mwana vile vile.

Kwa hiyo basi, yote aliyofundisha Kristo hapa duniani ni USHUHUDA wa Baba kwetu kupitia mwanaye wa pekee.

3. Roho Mtakatifu - wakati wa kubatizwa Yesu, Roho Mtakatifu alishuka na kukaa juu yake. Yohana Mbatizaji ndiye aliyeshuhudia hilo kwani alipewa ishara hiyo na Mungu jinsi ya kumtambua Mwana wa Mungu.

Siku ya Pentekoste Roho al8shuka na tazama Petro alivyo mshuhudia Kristo kuwa ni mwana wa Mungu akiwa amejaa Roho Mtakatifu.

Huo ni ushuhuda toka mbinguni, na hao wote washuhudiao wanakubaliana (hawatofautiani) katika huo ushuhuda.

Kristo alisema hapokei ushuhuda wake mwanadamu:

Yohana 5 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
³¹ Mimi nikijishuhudia mwenyewe, ushuhuda wangu si kweli.
³² Yuko mwingine anayenishuhudia; nami najua ya kuwa ushuhuda wake anaonishuhudia ni kweli.
³³ Ninyi mlituma watu kwa Yohana, naye akaishuhudia kweli.
³⁴ Lakini mimi siupokei ushuhuda kwa wanadamu; walakini ninasema haya ili ninyi mpate kuokoka.

Kumbe yuko MMOJA TU amshuhudiaye wala si wengi, naye ushuhuda wake ni wa kweli. Huyu ndiye aliyeshuhudia kwanza kama Baba, halafu kama Neno kisha kama Roho Mtakatifu. Ushuhuda qnaoutoa ni Roho kamili ndio maana hata Neno la Mungu li hai, ndio kusema WAKO WATATU. Muhimu ni kwamba hawa wote ni mmoja tu. Ndipo nalikuandikia kwamba Waebrania 1:1 inarejwa hapa, kwamba zamani Baba alinena na baba zetu kwa njia mbalimbali, lakini sasa ananena nasi kupitia Mwana (Neno). Hapo mwanzoaoinena kupitia kijiti cha moto, wingu, nk. Lakini sasa hatuhitaji kumsikia Mungu kupitia njia hizo kwani amelituma Neno lake kwa njia ya Kristo.

Hapa pia ni muhimu kutambua, Yohana alikuwa akijenga hoja yake kupitia kanuni ya kimaandiko kwamba jambo huthibitika kwa ushuhuda wa watu wawili ama watatu.

Hebu tuone wanaoshuhudia duniani:

1. Roho - huyu hata sasa yupi baada ya kuwa amevuviwa kwa waamini. Yeye anaendelea kumshuhudia Kristo ulimwenguni hata sasa. Ndio maana ukisoma Neno la Mungu bila Roho Mtakatifu hutoambulia kitu.

2. Maji - maji yanatupa uzima. Tukioshwa kwa damu ya Yesu tunapokea uzima kwa maji. Kumbuka alichomwa mkuki ubavuni yakatoka maji na damu? Maji ni ishara ya uzima katika Yesu.

3. Damu - tumekombolewa kwa damu ya Yesu Kristo, hata sasa damu iliyomwagika msalabani ni ushuhuda mkubwa wa Kristo kama mwana wa Mungu. Damu inatusafisha dhambi na kutuleta kwa Baba.

Nimeandika kwa haraka kwa sababu nimetingwa, lakini nadhani umrpata picha halisi. Sura hiyo haihusiani na habari ya Utatu Mtakatifu bali ukitaka kuielewa zaidi soma pia Yohana 5.
 
9Usimuonee mgeni,maana,ninyi mwajua moyo wa mgeni ulivyo,kwa kuwa ninyi mlikua wageni katika nchi ya Misri..
KUTOKA 23-9
 
Yohana 1:12
[12]Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake;
But as many as received him, to them gave he power to become the sons of God, even to them that believe on his name:
 
YOHANA 17

Maneno hayo aliyasema Yesu; akainua macho yake kuelekea mbinguni, akasema, Baba, saa imekwisha kufika. Mtukuze Mwanao, ili Mwana wako naye akutukuze wewe;
2 kama vile ulivyompa mamlaka juu ya wote wenye mwili, ili kwamba wote uliompa awape uzima wa milele.
3 Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma.
4 Mimi nimekutukuza duniani, hali nimeimaliza kazi ile uliyonipa niifanye.
5 Na sasa, Baba, unitukuze mimi pamoja nawe, kwa utukufu ule niliokuwa nao pamoja nawe kabla ya ulimwengu kuwako.
6 Jina lako nimewadhihirishia watu wale ulionipa katika ulimwengu; walikuwa wako, ukanipa mimi, na neno lako wamelishika.
7 Sasa wamejua ya kuwa yote uliyonipa yatoka kwako.
8 Kwa kuwa maneno uliyonipa nimewapa wao; nao wakayapokea, wakajua hakika ya kuwa nalitoka kwako, wakasadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma.
9 Mimi nawaombea hao; siuombei ulimwengu; bali hao ulionipa, kwa kuwa hao ni wako;
10 na wote walio wangu ni wako, na walio wako ni wangu; nami nimetukuzwa ndani yao.
11 Wala mimi simo tena ulimwenguni, lakini hawa wamo ulimwenguni, nami naja kwako. Baba mtakatifu, kwa jina lako ulilonipa uwalinde hawa, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo.
12 Nilipokuwapo pamoja nao, mimi naliwalinda kwa jina lako ulilonipa, nikawatunza; wala hapana mmojawapo wao aliyepotea, ila yule mwana wa upotevu, ili andiko litimie.
13 Na sasa naja kwako; na maneno haya nayasema ulimwenguni, ili wawe na furaha yangu imetimizwa ndani yao.
14 Mimi nimewapa neno lako; na ulimwengu umewachukia; kwa kuwa wao si wa ulimwengu, kama mimi nisivyo wa ulimwengu.
15 Mimi siombi kwamba uwatoe katika ulimwengu; bali uwalinde na yule mwovu.
16 Wao si wa ulimwengu, kama mimi nisivyo wa ulimwengu.
17 Uwatakase kwa ile kweli; neno lako ndiyo kweli.
18 Kama vile ulivyonituma mimi ulimwenguni, nami vivyo hivyo naliwatuma hao ulimwenguni.
19 Na kwa ajili yao najiweka wakfu mwenyewe, ili na hao watakaswe katika kweli.
20 Wala si hao tu ninaowaombea; lakini na wale watakaoniamini kwa sababu ya neno lao.
21 Wote wawe na umoja; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu; ili ulimwengu upate kusadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma.
22 Nami utukufu ule ulionipa nimewapa wao; ili wawe na umoja kama sisi tulivyo umoja.
23 Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ili ulimwengu ujue ya kuwa ndiwe uliyenituma, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi.
24 Baba, hao ulionipa nataka wawe pamoja nami po pote nilipo, wapate na kuutazama utukufu wangu ulionipa; kwa maana ulinipenda kabla ya kuwekwa msingi ulimwengu.
25 Baba mwenye haki, ulimwengu haukukujua; lakini mimi nalikujua, na hao wamejua ya kuwa ndiwe uliyenituma.
26 Nami naliwajulisha jina lako, tena nitawajulisha hilo; ili pendo lile ulilonipenda mimi liwe ndani yao, nami niwe ndani yao
Msisitizo yoh 17:3

Yohana 17:3
[3]Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma.
And this is life eternal, that they might know thee the only true God, and Jesus Christ, whom thou hast sent.
 
Back
Top Bottom