DP World inatisha 2: Tazama bandari inazozihudumia Uingereza


Waache washangilie, asante kwa kuchambua vizuri sana na wewe ulisoma ukaelewa hawa washangiliaji wengi walienda shule kucheza na kutembea tu ndio maana akili za wehu kama akina musukuma nazo wanazotegemea
 
Pande moja inapo kiuka wajibu wake ndio kigezo kikuu cha mkataba kuvunjika. Hata wewe hapo ulipo kama umeolewa, Je mme wako akianza kuleta malaya wenye uti hapo kwenu, yeye akikataa kupokea talaka yako utabaki kwenye ndoa na kushiriki tendo kisa yeye ni lazima akubali kwa hiari yake ndio uondoke ?

Kuwa muelewa, huo ni mkataba wa milele, Hakuna kifungu chochote ambacho kimeweka muda wa mkataba kukoma
 
Naona hoja za bandari zimekushinda umeanza kuhororoja, kubwabwaja na kubweka bila mpango.


Kwa kutumia lugha yako, Uingereza siyo jirani yetu. Jirani zetu ni wanaotuzunguka. Ususahau hilo.


Tunaisikfia DP World kwa kuwa tumepeleka posa tuoane nao. Sasa Wajomba lazima tuwasifie sifie msiipingepinge ndoa ingawa wajomba wenyewe ndiyo mpo vile. Kina Deus Soka.

Waarabu wanasema "mjomba ni mzazi hata kama ni kiazi cha orojo".

Utajaza.mwenyewe mjomba.


Mama anaupiga mwingi Kimataifa.
 

Dubai sio nchi, ilitakiwa iwe UAE, dubai ni state ndani ya UAE hivo serikali inaingia mkataba na state ajabu sana
 
Hakuna tatizo bado hatujasaini HGA.


Mama anaupiga mwingi Kimataifa.
 
Hakuna tatizo bado hatujasaini HGA.


Mama anaupiga mwingi Kimataifa.

Tatizo lipo kubwa maana waliojipeleka kujiuza kwenye state ya Dubai wanasema dubai ni nchi shame on them yanaongea tu wakati yameingizwa chaka
 
Fanya kazi tafuta pesa lea familia yako vizuri somesha watoto na uwatengenezee mazingira ya kujiajiri na kujitegemea ayo mambo mengne yanaumiza kichwa tuuu CCM na viongozi wake wameshaamua na ata tukipiga kelele dude litaenda tuu
Cha msingi tafta pesa ata nchi ikiuzwa utahamia msumbiji, rwanda,comoro,ata visiwa vya Caribbean island uko
 
Waarabu wa Dubai wanatisha.


Mama Samia hujakosea kabisa kuamuwa kuwaleta DP World Tanzania.

Tupo na wewe 100%.
Sasa naanza kuamini wewe ni mama samia

Unakuja na thread za kusifu na kuabudu na mapambio mengi kwa mama
 
Hakuna tatizo bado hatujasaini HGA.


Mama anaupiga mwingi Kimataifa.
Don't you know that IGA creates obligations among party members ???
Which cave have you crawled from with this bismal understanding ???

Wewe shuleni ulikuwa unafauluje kwa aina hiii ya uelewa ? Vitu vidogo kama hivi vinapitaje juu ya kichwa chako bila kuvielewa! Moja ya kanuni muhimu za INTERNATIONAL COMMERCIAL AGREEMENTS ni BREACH OF LEGITIMATE EXPECTATION. Ikimaanisha kwamba nchi itashitakiwa na wawekezaji, hata kwa hasara ambazo zinategemewa kutokea kwenye uwekezaji (LIKELIHOOD)...

Nakupa mfano hai, ACACIA GOLD MINE walienda kufungua kesi kule London Uingereza, dhidi ya serikali ya Tanzania hata kabla haijakamata makinikia. Wao walienda kufungua kesi kuizua serikali ya Tanzania isiendelee na mikakati yake ambayo ingewaletea hasara. Kule London walisema kile kitendo kimewachafua na kufanya hisa zao zishuke kule LONDON STOCK EXCHANGE. Hivyo kama mwaka huu wa fedha 2023/2024 mwekezaji alitegemea kupata faidi bilioni 100, ila serikali ikaingilia utendaji wake, sheria inaruhusu mwekezaji kufanya makadirio ya faida ambayo angeyapata kutokana na mwelekeo wa masoko ya dunia mwaka huo.

IGA inasema kwamba Tanzania ikishasaini huu mkataba na kupitishwa na bunge la Tanzania (Ratified by the Parliament), Tanzania haitakuwa na nguvu ya kuzuia tena vibali vya utekelezaji wa miradi mbali-mbali kupitia HGA au PROJECT AGREEMENT. Hili limewekwa wazi kwenye Ibara ya 1 (2), Ibara ya 6 na Ibara ya 7. Sasa ukizingatia kwamba tayari huu mkataba umeshakuwa ni sehemu ya sheria za Tanzania, serikali haiwezi kabisa kujitoa. Lakini baya zaidi tukikataa kusaini HGA basi wataenda kutuburuza kwenye mahakama za kimataifa......

Hivi wewe mambo marahisi kama haya unashindwaje kuyaelewa ????

Karl Marx once said "Religion is an opium of the masses"
 
Dubai sio nchi, ilitakiwa iwe UAE, dubai ni state ndani ya UAE hivo serikali inaingia mkataba na state ajabu sana
UAE tunayo mikataba mpaka ya Kidiplomasia. Tuna balozi yetu Abu Dhabi na wanabalozi yao Dar.


Dubai ni nchi iliyopo kwenye muungano wa UAE, (nchi saba) mfano wake ni kama Zanzibar na Tanganyika (nchi mbili) Kuna mambo ya Muungano na kuna mambo hayapo kwenye muubgano. Ushahidi 👇🏾

 

Pale kwenye saini uliona saini wa kiongozi yeyote wa nchi ya Dubai na cheo chake?
 
Sasa naanza kuamini wewe ni mama samia

Unakuja na thread za kusifu na kuabudu na mapambio mengi kwa mama
Koma. Waislaam hatuabudu binadam wala sanamu.


1. Sema: Yeye Mwenyezi Mungu ni wa pekee. 1
2. Mwenyezi Mungu Mkusudiwa. 2
3. Hakuzaa wala hakuzaliwa 3
4. Wala hana anaye fanana naye hata mmoja. 4



Mama anaupiga mwingi Kimataifa.
 

Dhamana ya Dubai ni UAE , sasa dhamana ya Tanganyika ni URT, sasa umeona mandate ya UAE kwenye mkataba huo? Jibu hakuna yaani nchi inaingia mkataba na kampuni binafsi, ndio maana kwa kuwafichia aibu tunaona tuwashauri kua iundwe kampuni iwe na share 50/50 na DP world na kampuni hiyo iwe inamikiwa na serikali direct au taasis za serikali ili baadae sasa uwezo ukiongezeka tutamaliza share zote 50 ziwe zetu maana tunakua na uzoefu na hapo tumewashauri hivo baada ya kuona mmechemka sasa kuwafichia aibu kiutu uzima mfanye hivo, sisi sio wajinga, tumesoma na duniani tumekaa na kuzunguka na exposure tunayo ya kutosha haswaa,
 
Kwani serikali ya UAE peke yao wanaweza kuuvunja?
 
Pale kwenye saini uliona saini wa kiongozi yeyote wa nchi ya Dubai na cheo chake?

Tazama na viambatanishi utaona hao waluisaini walipewa idhini na nani.

Hivi unawafanya wanasherua wetu qajinga sana? Wewe ndiye mwenye kuijuwa sheria? Una kipi jwenye elimu ya sheria cha kuwashinda wanasheria wetu?


Mama anaupiga mwingi Kimataifa.
 
Wapelekwe Zanziba Sisi Watanganyika hatutakii

Hata kama wanahudumia Dunia nzima.

Sisi watangayika tuachwe hivyo na Bandari yetuuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…