DP World inatisha 2: Tazama bandari inazozihudumia Uingereza

Huyu Bi kizee kakomaa kuwapigia debe hao wahuni sijui kaahidiwa nini?
 
Hao ni Uingereza, mifumo yao ina utitiri wa watu smart huku sheria zikifanyakazi.

tuambie maisha ya mfanyakazi wa ndani hapo UAE, Tanzanian vs Uingereza.

Shida yetu ni kutokuwa na watu smart wakuwaamini kusign hizo international contracts pamoja na kusimamia mradi wenyewe kiujumla.
 
Naunga mkono waarabu waje.

Wanaopinga ni wanafiki maana hawakuonekana kwenye maandamano
Hakuna aIpingaye DP kinachopingwa ni mashariti ya mkataba. Sote twataka mabadiliko ila sio ya style ya Richmond with their capacity charges
 
Hivi wewe ni Mtanzania kweli?Kwamba maslahi ya nchi yetu na vizazi vyetu si kitu mbele ya dini yako?
Mimi nakushauri friendly,kama.unaupenda kwa dhati huo uislam wako basi tafuta loudspeakers ukahubiri mitaani usilimishe watu kuliko usilimishaji wa nchi unaoutafuta.Baada ya mwaka 2025 utakuwa frustrated hao waarabu wako watakapofurushwa na regime mpya
 
Wewe maslahi gani ya nchi unayoyajuwa wewe zaidi ya Mama Samia Suluhu Hassan?

Wacha upoyoyo wewe.
 

Peeling back the DP World's mask.
 
Ndugu zanguni

Naomba niwakumbushe tu kua huduma za Uwanja wa ndege wa Dar zinaendeshwa na Swissport ambayo ni kampuni ya Switzerland toka mwaka 1985 ambapo wengi mnaopiga mayowe mlikua bado hata haijuilikani kama mtakuaja Duniani. Lakini kwa kua utendaji wao ni wa kiwango cha juu ndio maana wako mpaka leo pale

Haya tusitokwe mapovu. Swissport wanahudumia viwanja zaidi ya 200 duniani. Kwa wale mliowahi safiri lazima umeona mabango yao

TICTS wako bandarini miaka 33 sasa na hawajawahi nunua hata crane moja na utendaji wao umekutuumiza sana Wafanya biashara. Yaani mara kwa mara tumezoea kumuona Mh Waziri Mkuu akienda pale kuwahimiza wafanye kazi kwa bidii makontena yatoke. Hata hii ya masaa 24 ni baada ya Mh Waziri Mkuu kuwaambia wafanye kazi masaa 24 kuondoa msongamano port

Ndugu zanguni , sijawahi sikia mtu akilalamika kuhusu Swissport sababu utendaji wao ni wa kiwango cha juu sana.

Tumechoka hii aibu ya meli kukwepa bandari ya Dar sababu ya miundombinu mibovu.

NB: Natoa kauli hii nikiwa mmoja wa watumiaji wakubwa wa bandari na sio chawa asiejua hata meli ina magurudumu mangapi.

Niko tayari kukaa meza moja na Rafiki yangu wa Zamani Lema tulijadili hili ili wazi na kwa Data. Juzi nimemsikia akiongea kwa data za kupotosha. Ili mwananchi wa kawaida aelewe ninaomba niwekwe uwanja mmoja nae tujadiliane kwa hoja. Naamini hata yeye atanielewa na atakubaliana nami
 
Wapewe mara ngap;? s tulishawapa au wamerudisha! Au Hamkuelewa!? sahz tunafanya nao mpango tuwape na mbuga zote then tutamalzia na miradi kana standard gauge na rufiji dame
Ala msiki na log off
 
Hakuna mtu anaweza fanya biashara Kwa kuweka pesa zake harafu Bandari zingine wawepo wakwamishaji au waswahili wengine wasiojua maana ya baishara,hoja ya kwanza.

Pili Haina maana kuwa na Bandari ambayo watu wachache wanajifanya shamba la bibi huku nyie wengine mkiumia..

Serikali kodisha haraka hatuwezi kuendelea ku bear inefficiency,wizi na kulindana,ujinga huo ndio umeua posta ,ttcl na mashirika mengine kama uda.

Imagine eti Dart pamoja na kuwa na njia yake Wana post hasara wakati daladala ya kawaida zinaingiza pesa,kodisha Dart Kwa private sector ni upumbavu kuchukua Kodi kwenda kulipia walioshindwa.
 
Sema apewe serikali nzima tujue tunatawaliwa na mkoloni mwarabu toka falme za kiarabu. Bandari tu? Apewe nchi yote tujue moja
 
Mind kuwa mkoloni anapokuja huja na mila na desturi zake kuwalisha atakaowatawala. Kwa upande wa dini tayari mababu zao walishapandikiza dini yao ipo wataikuta inaabudiwa hawatapata ugumu wa kuineza.

Kuhusu siasa tayari wamepata wazawa wa kuwafanyia siasa ili wapate uwekezaji zaidi hata sehemu zingine wakizitaka watazipata kiulaini bila upinzani. Wachukue vyote hata mabwawa na madibwi wapewe tu tujue hatuna kitu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…