DP World tayari imejenga "Bandari Kavu" Rwanda yenye uwezo wa kontena elfu 50, wakati bandari yetu ni ya kontena elfu 19 tu

DP World tayari imejenga "Bandari Kavu" Rwanda yenye uwezo wa kontena elfu 50, wakati bandari yetu ni ya kontena elfu 19 tu

Nobunaga

JF-Expert Member
Joined
Mar 22, 2019
Posts
1,205
Reaction score
5,121
Katika hili wala hauhitaji kujua aliye nyuma ya hawa DP World ni nani, haijatokea kwa bahati mbaya, hakuna coincidence hapa, ni mipango iliyopangwa ikapangika na sasa tunaenda kupigwa mchana kweupeee.

==========================

TAARIFA KUHUSU UWEKEZAJI UNAOPENDEKEZWA NA DP WORLD TANZANIA

DP World imejenga kituo cha hadhi ya kimataifa cha bandari kavu na kitovu cha usafirishaji katika Rwanda, ambayo ni ndogo kijiografia na isiyo na bahari yenye uwezo wa kuhifadhi makontena 50,000 kwa wakati mmoja. Kinyume chake, bandari ya Dar es Salaam katika Tanzania kubwa kijiografia ina uwezo wa kuhifadhi kontena 19,000 TU kwa wakati mmoja.

Hii ina maana kwamba kama meli kubwa ya kontena yenye uwezo wa kubeba takriban TEU 20,000 au zaidi ingetia nanga Dar es Salaam, kituo kidogo cha kontena cha bandarini hakingeweza kuhifadhi shehena ya meli moja tu.

Wakati mjadala wa kitaifa wenye SIASA NYINGI ukiendelea kuhusu masharti ya uwekezaji ujao wa DP World nchini Tanzania, bandari ya Dar es Salaam bado ina uhitaji mkubwa wa uwekezaji wa miundombinu. Wakati huo huo, Rwanda tayari imejenga bandari kavu ya hadhi ya kimataifa, na nchi jirani ya Kenya inatafuta wawekezaji wa kibinafsi kuendesha sehemu muhimu za bandari zake za Lamu na Mombasa.

Ingawa hoja halali kuhusu masharti ya uwekezaji inapaswa kushughulikiwa, ni wakati sasa kwa Tanzania kujadiliana na DP World kwa kina kwani bandari ya Dar es Salaam itakuwa kama njia tuu ya kupeleka shehena Rwanda. Hii ina maana Rwanda itakuwa inapata faida kubwa kupitia bandari yetu kulinganisha na sisi.
20230614_095424.jpg

48936667281_53f2eb2f38_o-1-scaled.jpg


hand.jpg


hand.jpg


DSC_5067-1-scaled.jpg
 
Katika hili wala hauhitaji kujua aliye nyuma ya hawa DP World ni nani, haijatokea kwa bahati mbaya, hakuna coincidence hapa, ni mipango iliyopangwa ikapangika na sasa tunaenda kupigwa mchana kweupeee.

==========================
Na ndio kile kipengele cha kutovunja mkataba hata kitokee nini kinapopigiwa kelele. Ila naomba kuuliza, kwamba uchukue kontena Dar hadi Rwanda halafu ndio upeleke Zambia? Au kontena litike Dar linende kukaa Reanda halafu ndio ulipakie tena kwa mara ya pili kwenda Kongo?
 
binafsi nafurahi Rwanda ikipiga hatua kimaendeleo kuziona fursa kuzing'amua na kuzichangamkia.

lengo langu labda uwenda majirani wazembe,wala rushwa na wavivu watajifunza kwa huyu jirani yao Rwanda,nchi changa iliyotoka kwenye machafuko lakini kwa muda mchache wanatengeneza nchi yao.
 
Mleta mada ahsante sana,mkataba wa DP World na Rwanda hamna tofauti kubwa na huu wa bandari sana labeda katika kuendeleza ndiyo kuna utofauti. Hivi kweli leo hii watanzania tunafikia sehem kukataa uwekezaji ambao unafaida kubwa kwa Taifa letu eti tunakimbia kudanganywa kua bandari inauzwa. Hivi angalia kutoka kontena elfu 19 mpaka kontena elfu 50 mnaona jambo la kawaida. Watu wengi awajui kua mbali na kodi kwa serikali lakini pia bei ya vitu kutoka nje itashuka lakini pia itasaidia ata kusafirisha malighafi na bidhaa nyingine kua rahisi na haraka kwetu.
 
Mleta mada ahsante sana,mkataba wa DP World na Rwanda hamna tofauti kubwa na huu wa bandari sana labeda katika kuendeleza ndiyo kuna utofauti. Hivi kweli leo hii watanzania tunafikia sehem kukataa uwekezaji ambao unafaida kubwa kwa Taifa letu eti tunakimbia kudanganywa kua bandari inauzwa. Hivi angalia kutoka kontena elfu 19 mpaka kontena elfu 50 mnaona jambo la kawaida. Watu wengi awajui kua mbali na kodi kwa serikali lakini pia bei ya vitu kutoka nje itashuka lakini pia itasaidia ata kusafirisha malighafi na bidhaa nyingine kua rahisi na haraka kwetu.
Mnalipwa kiasi gani kutetea huu uozo wa huu mkataba? Hebu kama mmeamua kujitoa ufahamu nyinyi kwa vipande 30 vya feza basi waoneeni huruma watoto wa watoto zenu.Hatupendi wajukuu zetu waje watuone kama sote tulikuwa hamnazo,lazima watu wahoji na wapatiwe majibu ya kueleweka pale panapohijika.
 
Mnalipwa kiasi gani kutetea huu uozo wa huu mkataba? Hebu kama mmeamua kujitoa ufahamu nyinyi kwa vipande 30 vya feza basi waoneeni huruma watoto wa watoto zenu.Hatupendi wajukuu zetu waje watuone kama sote tulikuwa hamnazo,lazima watu wahoji na wapatiwe majibu ya kueleweka pale panapohijika.
Kukimbilia kusema kua watu wanao kubali kua tuingie ubia wa kuendesha na kuboresha bandariz etu mnawaona kua wasaliti na wamepewa pesa...huu si ukweli bali ni kukosa tu hekima za kuyajua mema na malengo ya Taifa ili. Vipi,wale mnaopinga mkiambiwa mmeongwa na wafanyabiashara wanao tumia hiyo bandari kutupiga pesa na kuuza vitu kwa bei ya juu sijui utasemaje. Ifike sehem watanzania tukubali kua tunabidi kupiga hatua kwa kufanya maamuzi sahihi. Itakuaje vizazi vyetu vya mbeleni wakute tuna bandari lakini bado maisha ya watanzania ni duni? Si watatuona mazezeta kwa kushindwa kutumia bandari kuinua uchumi wa mtu mmoja na nchi kwa ujumla?
 
Katika hili wala hauhitaji kujua aliye nyuma ya hawa DP World ni nani, haijatokea kwa bahati mbaya, hakuna coincidence hapa, ni mipango iliyopangwa ikapangika na sasa tunaenda kupigwa mchana kweupeee.

==========================

TAARIFA KUHUSU UWEKEZAJI UNAOPENDEKEZWA NA DP WORLD TANZANIA

DP World imejenga kituo cha hadhi ya kimataifa cha bandari kavu na kitovu cha usafirishaji katika Rwanda, ambayo ni ndogo kijiografia na isiyo na bahari yenye uwezo wa kuhifadhi makontena 50,000 kwa wakati mmoja. Kinyume chake, bandari ya Dar es Salaam katika Tanzania kubwa kijiografia ina uwezo wa kuhifadhi kontena 19,000 TU kwa wakati mmoja.

Hii ina maana kwamba kama meli kubwa ya kontena yenye uwezo wa kubeba takriban TEU 20,000 au zaidi ingetia nanga Dar es Salaam, kituo kidogo cha kontena cha bandarini hakingeweza kuhifadhi shehena ya meli moja tu.

Wakati mjadala wa kitaifa wenye SIASA NYINGI ukiendelea kuhusu masharti ya uwekezaji ujao wa DP World nchini Tanzania, bandari ya Dar es Salaam bado ina uhitaji mkubwa wa uwekezaji wa miundombinu. Wakati huo huo, Rwanda tayari imejenga bandari kavu ya hadhi ya kimataifa, na nchi jirani ya Kenya inatafuta wawekezaji wa kibinafsi kuendesha sehemu muhimu za bandari zake za Lamu na Mombasa.

Ingawa hoja halali kuhusu masharti ya uwekezaji inapaswa kushughulikiwa, ni wakati sasa kwa Tanzania kujadiliana na DP World kwa kina kwani bandari ya Dar es Salaam itakuwa kama njia tuu ya kupeleka shehena Rwanda. Hii ina maana Rwanda itakuwa inapata faida kubwa kupitia bandari yetu kulinganisha na sisi.
View attachment 2656852

View attachment 2656853

View attachment 2656854

View attachment 2656854

View attachment 2656855
Hayatuhusu sisi. Wakajenge na Burundi
 
Hivi mnataka kusema Kagame kawatumia waarabu wa Dubai kumdanganya huyu msaliti wetu wakaingia yale makubaliano ya hovyo namna ile?

Nakumbuka juzi tu Kagame alikuja Tanzania, ile ziara inawezekana ilikuwa ni kuweka sawa hii mipango ya kukamilisha kuichukua bandari yetu?

Inawezekana waarabu wa Dubai nao walitumia akili ya kumtongoza msaliti wetu ili wamnufaishe Kagame?
 
Back
Top Bottom