DP World tayari imejenga "Bandari Kavu" Rwanda yenye uwezo wa kontena elfu 50, wakati bandari yetu ni ya kontena elfu 19 tu

DP World tayari imejenga "Bandari Kavu" Rwanda yenye uwezo wa kontena elfu 50, wakati bandari yetu ni ya kontena elfu 19 tu

Binafsi sioni cha ajabu kwa sababu ni rahisi kujenga bandari nchi kavu tofauti na kujenga baharini au pembeni ya bahari



Sent from my Infinix X612 using JamiiForums mobile app
 
Kama Samia ameshindwa kubuni vyanzo vya mapato aondoke ofisini waingie wenye uwezo

Asiuze nchi kwa waarabu kwa visingizio visivyokuwa maana
Unajieza kwa kp ebu toa orodha ya taasis inayojiendesha vizur ya serikali....
 
ila kagame mpambanaji sana, alishatutukana kwamba yeye angekuwa na bandari tu ingetosha, sasaivi ameamua kuleta uwekezaji kwenye bandari kabu sisi ya maji tu imeleta shida. angekuwa kwenye bahari huyo tusingemkuta.
 
Hakuna Sehemu ambayo DP world amewekeza ambayo hajawekeza kupanua Bandari, akipewa Bandari hata Hapa Tanzania anaweza kuweka zaidi ya hio 50k Teu.

Unaiongelea hii kampuni kama Vile ni kikampuni cha uchochoroni kinaweza kuwa controlled na Rwanda.
Read btn the lines acha kukurupuka....
 
Na ndio kile kipengele cha kutovunja mkataba hata kitokee nini kinapopigiwa kelele. Ila naomba kuuliza, kwamba uchukue kontena Dar hadi Rwanda halafu ndio upeleke Zambia? Au kontena litike Dar linende kukaa Reanda halafu ndio ulipakie tena kwa mara ya pili kwenda Kongo?
Ni mkataba wa hovyo sn
 
ila kagame mpambanaji sana, alishatutukana kwamba yeye angekuwa na bandari tu ingetosha, sasaivi ameamua kuleta uwekezaji kwenye bandari kabu sisi ya maji tu imeleta shida. angekuwa kwenye bahari huyo tusingemkuta.
Tatizo kwetu ni haya majangili ya CCM
 
Katika hili wala hauhitaji kujua aliye nyuma ya hawa DP World ni nani, haijatokea kwa bahati mbaya, hakuna coincidence hapa, ni mipango iliyopangwa ikapangika na sasa tunaenda kupigwa mchana kweupeee.

==========================

TAARIFA KUHUSU UWEKEZAJI UNAOPENDEKEZWA NA DP WORLD TANZANIA

DP World imejenga kituo cha hadhi ya kimataifa cha bandari kavu na kitovu cha usafirishaji katika Rwanda, ambayo ni ndogo kijiografia na isiyo na bahari yenye uwezo wa kuhifadhi makontena 50,000 kwa wakati mmoja. Kinyume chake, bandari ya Dar es Salaam katika Tanzania kubwa kijiografia ina uwezo wa kuhifadhi kontena 19,000 TU kwa wakati mmoja.

Hii ina maana kwamba kama meli kubwa ya kontena yenye uwezo wa kubeba takriban TEU 20,000 au zaidi ingetia nanga Dar es Salaam, kituo kidogo cha kontena cha bandarini hakingeweza kuhifadhi shehena ya meli moja tu.

Wakati mjadala wa kitaifa wenye SIASA NYINGI ukiendelea kuhusu masharti ya uwekezaji ujao wa DP World nchini Tanzania, bandari ya Dar es Salaam bado ina uhitaji mkubwa wa uwekezaji wa miundombinu. Wakati huo huo, Rwanda tayari imejenga bandari kavu ya hadhi ya kimataifa, na nchi jirani ya Kenya inatafuta wawekezaji wa kibinafsi kuendesha sehemu muhimu za bandari zake za Lamu na Mombasa.

Ingawa hoja halali kuhusu masharti ya uwekezaji inapaswa kushughulikiwa, ni wakati sasa kwa Tanzania kujadiliana na DP World kwa kina kwani bandari ya Dar es Salaam itakuwa kama njia tuu ya kupeleka shehena Rwanda. Hii ina maana Rwanda itakuwa inapata faida kubwa kupitia bandari yetu kulinganisha na sisi.
View attachment 2656852

View attachment 2656853

View attachment 2656854

View attachment 2656854

View attachment 2656855
Safi, kwa ukubwa wa soko la Rwanda hiyo mizigo itachukua muda gani kusambazwa nchi nzima au mingine itakuwa inaletwa bongo kwa kutumia Rwanda kama transit center.
 
naanza kuhusi hizi terms za kutaka tusijenge bandari ingine bongo alizileta kagame, ili tusijenge bandari nzuri ziwa Tanganyika kufika congo kirahisi, wala mpakani na burundi, ili dp word yake ya kigali iwe monopoly ya mizigo ya congo. na sisi tukaingia kichwa kichwa, na kagame alikuja hapa recently, alikuja kujadili nini?
 
Safi, kwa ukubwa wa soko la Rwanda hiyo mizigo itachukua muda gani kusambazwa nchi nzima au mingine itakuwa inaletwa bongo kwa kutumia Rwanda kama transit center.
yaani, itafika Dsm port, itasafirishwa moja kwa moja kwa reli tuliyojenga kwa kodi zetu au kwa barabara tulizojenga kwa kodi zetu, itafikia Rwanda. wacongo hawatahitaji kuja bongo kuchukua mizigo yao, watachukulia pale bandari ya kigali tu. unaona akili hiyo? kwahiyo anakuwa ameimiliki bandari ya dsm kwa mlango wa nyuma. hao watu wote walitakiwa waje bongo, watumie makampuni ya usafirishaji ya bongo, walete hela kwenye lodge/guest/hotel za bongo na walete mzunguko wa pesa. sasa watakatwa waishie kigali kwenye bandari ya dp word. bongolala.
 
kwa lugha nyingine, unaweza kuona kagame ameweka mazingira shindani, ikawa rahisi kununua mzigo Rwanda kuliko dsm, wafanyabiashara wote wa congo, uganda, kenya na kwengine wakakimbilia kufunga mzigo singapore ya africa (rwanda). very simple.
 
binafsi nafurahi Rwanda ikipiga hatua kimaendeleo kuziona fursa kuzing'amua na kuzichangamkia.

lengo langu labda uwenda majirani wazembe,wala rushwa na wavivu watajifunza kwa huyu jirani yao Rwanda,nchi changa iliyotoka kwenye machafuko lakini kwa muda mchache wanatengeneza nchi yao.
Huku tunapambania democratic ili wanasiasa nao waingia kula
 
Acha kupotosha watu, mteja let's say kutoka Congo DR amenunua mzigo wake China, yeye ndio ayaamua mzigo wake aupokelee wapi Final destination kutokana na freight aliyolipia. Kumbuka ukinunua mzigo kitu cha kwanza supplier atakuuliza final distinction ni wapi na mzigo wako utaupokelea wapi ( port of delivery ) acha kupotosha watu
Sijaelewa, kwamba final destinatin iwe DRC halafu mzigo ukashushwe Rwanda?
 
Mnalipwa kiasi gani kutetea huu uozo wa huu mkataba? Hebu kama mmeamua kujitoa ufahamu nyinyi kwa vipande 30 vya feza basi waoneeni huruma watoto wa watoto zenu.Hatupendi wajukuu zetu waje watuone kama sote tulikuwa hamnazo,lazima watu wahoji na wapatiwe majibu ya kueleweka pale panapohijika.
Na wewe umelipwa kiasi gani
 
Ninachoshangaa Waafrila mtu akiwa na kamgao Yuko tayari kupambana kufa alimradi yeye na familia yake wananufaika. Kama watz wamesema hapana kwanini msisitishe , nguvu kubwa inayotumika ni ya Nini?
Wewe peke yako ndio hutaki sie wengine tunamuhitaji Dpw
 
Back
Top Bottom