DP World tayari imejenga "Bandari Kavu" Rwanda yenye uwezo wa kontena elfu 50, wakati bandari yetu ni ya kontena elfu 19 tu

DP World tayari imejenga "Bandari Kavu" Rwanda yenye uwezo wa kontena elfu 50, wakati bandari yetu ni ya kontena elfu 19 tu

Wacha DP World waje tupate maendeleo ya haraka.

Na hapa vijana tujiunge tutafute Train letu Dar-Dom fursa imewekwa jana wazi kabisa.
 
Mleta mada ahsante sana,mkataba wa DP World na Rwanda hamna tofauti kubwa na huu wa bandari sana labeda katika kuendeleza ndiyo kuna utofauti. Hivi kweli leo hii watanzania tunafikia sehem kukataa uwekezaji ambao unafaida kubwa kwa Taifa letu eti tunakimbia kudanganywa kua bandari inauzwa. Hivi angalia kutoka kontena elfu 19 mpaka kontena elfu 50 mnaona jambo la kawaida. Watu wengi awajui kua mbali na kodi kwa serikali lakini pia bei ya vitu kutoka nje itashuka lakini pia itasaidia ata kusafirisha malighafi na bidhaa nyingine kua rahisi na haraka kwetu.
Ninachoshangaa Waafrila mtu akiwa na kamgao Yuko tayari kupambana kufa alimradi yeye na familia yake wananufaika. Kama watz wamesema hapana kwanini msisitishe , nguvu kubwa inayotumika ni ya Nini?
 
Shida yetu kubwa ni mkataba wa milele, na vipengele vingine lukuki ambavyo havina maslahi Kwa watanganyika
 
Ninachoshangaa Waafrila mtu akiwa na kamgao Yuko tayari kupambana kufa alimradi yeye na familia yake wananufaika. Kama watz wamesema hapana kwanini msisitishe , nguvu kubwa inayotumika ni ya Nini?
Kwani wanao sema kua serikali iendelee na utaratibu huo wao sio watanzania? Wanaweza wakawa watanzania wengi wanasema hapana kwasababu wamekaririshwa uongo au awajui umuhimu wake. REF. referendum ya 1992 kuhusu vyama vingi,wengi walisema hapana lakini mwisho wa siku wachache wakaibuka washindi
 
DP World - Rwanda ni kituo kama kama unavyoona ICD zetu hapa Dar... Wanafungua kontena zenye mzigo, wanatoa mzigo wanaweka ndani wanamsubiri mwenyewe aje kuchukua... Wanachowafanyia waagizaji wa Rwanda, mtu akiagiza mzigo , hana haja ya kuja Dar , ataweza kupokea mzigo wako hapo hapo.. Hapa anahudumia end customers ( waagizaji)

Hivyo ni dhana tofauti na uendeshaji wa bandari... Bandari unahudumia kwanza meli zinazotia nanga kwenye bandari husika ( shipping line) na pia halafu unaongeza wigo wa kuhudumia wateja wa nchi nyingine kwa jinsi ambavyo serikali itakubaliana na nchi hizo.. Ambao wanachukua kontena zao , pamoja na meli nyingine kama za nafaka, magari , abiria , mafuta nk.

Kulinganisha bandari ya kavu - DP World Kigali na uendeshaji wa bandari Dar ni vitu tofauti , vyenye operation tofauti kabisa ..

Nilivyosikia waziri , anasema anataka bandari yetu iwe end to end port.. Nilicheka nikaona hata waziri mwenyewe hajui anachosema... Bandari duniani haziwezi kuwa end to end ports - zenyewe ni conduits, ni sehemu ya kupitishia mzigo..

Singapore ambayo ni ya pili duniani kwa shughuli za kontena .... Wao siyo end to end port , wanatumika zaidi kama transhipment port..mizigo au meli zinapitia hapo kwenda Asia , Ulaya, au kuja Africa nk.... Wanapitisha mzigo, hawafungui mzigo..
Sasa Dar port kupitia uwekezaji inaweza kuongeza uwezo wa kuhudumia nchi za jirani, DR Congo, Zambia, Rwanda na Wengine.. Katika hilo hatutakuwa na maajabu sana , kwa vile tutakuwa tunanyang'anyana mizigo na bandari za jirani , katika kuwahudumia nchi ambazo hawana bandari ... Beira, Mombasa, Nacala, Walvis Bay, Durban na wengine na wao watawekeza na kufanya hiki hiki tunachofanya... Hivyo tunaweza kuongeza tija ya bandari ya Dar es Salaam, lakini tusiweke malengo ambayo yatatekelezeki, kwa sababu ya strategic position yetu inatupa wigo mpaka mahali fulani na siyo zaidi.... Bandari za maeneo jirani zitafanana kwa potential market na hata matokeo yake na bandari ya Dar es salaam zinafanya kazi katika soko linalofanana, kwani zinategemea wateja wale wale ..Zitazidiana vitu vidogo vidogo hapa na pale ...
 
Na ndio kile kipengele cha kutovunja mkataba hata kitokee nini kinapopigiwa kelele. Ila naomba kuuliza, kwamba uchukue kontena Dar hadi Rwanda halafu ndio upeleke Zambia? Au kontena litike Dar linende kukaa Reanda halafu ndio ulipakie tena kwa mara ya pili kwenda Kongo?
Naona hii itakuwa mahususi kwa ajili ya upande wa DRC Congo na Uganda ambao na wao wanatumia bandari ya Dsm.
 
Na ndio kile kipengele cha kutovunja mkataba hata kitokee nini kinapopigiwa kelele. Ila naomba kuuliza, kwamba uchukue kontena Dar hadi Rwanda halafu ndio upeleke Zambia? Au kontena litike Dar linende kukaa Reanda halafu ndio ulipakie tena kwa mara ya pili kwenda Kongo?
Hushangai hata mashati, viatu na mitumba tunachukua Kampala ambapo hawana bandari ya bahari?....


Ukimaliza kushangaa hilo, shangaa nguzo za umeme za kule Njombe na Mufindi zikitolewa Tz kwenda Bandari ya Beira Msumbiji na kuoakiwa kisha kushushwa bandari ya Db Dubai pale mzizima?!


Ha!....hii ni ndoto tu. Haina uhalisia!
 
Huyu tahira mleta uzi anafananisha bandari na bandari kavu na hawa ndio wanateuliwa wakurugenzi uku bara kutoka Zanzibar
 
Katika hili wala hauhitaji kujua aliye nyuma ya hawa DP World ni nani, haijatokea kwa bahati mbaya, hakuna coincidence hapa, ni mipango iliyopangwa ikapangika na sasa tunaenda kupigwa mchana kweupeee.

==========================

TAARIFA KUHUSU UWEKEZAJI UNAOPENDEKEZWA NA DP WORLD TANZANIA

DP World imejenga kituo cha hadhi ya kimataifa cha bandari kavu na kitovu cha usafirishaji katika Rwanda, ambayo ni ndogo kijiografia na isiyo na bahari yenye uwezo wa kuhifadhi makontena 50,000 kwa wakati mmoja. Kinyume chake, bandari ya Dar es Salaam katika Tanzania kubwa kijiografia ina uwezo wa kuhifadhi kontena 19,000 TU kwa wakati mmoja.

Hii ina maana kwamba kama meli kubwa ya kontena yenye uwezo wa kubeba takriban TEU 20,000 au zaidi ingetia nanga Dar es Salaam, kituo kidogo cha kontena cha bandarini hakingeweza kuhifadhi shehena ya meli moja tu.

Wakati mjadala wa kitaifa wenye SIASA NYINGI ukiendelea kuhusu masharti ya uwekezaji ujao wa DP World nchini Tanzania, bandari ya Dar es Salaam bado ina uhitaji mkubwa wa uwekezaji wa miundombinu. Wakati huo huo, Rwanda tayari imejenga bandari kavu ya hadhi ya kimataifa, na nchi jirani ya Kenya inatafuta wawekezaji wa kibinafsi kuendesha sehemu muhimu za bandari zake za Lamu na Mombasa.

Ingawa hoja halali kuhusu masharti ya uwekezaji inapaswa kushughulikiwa, ni wakati sasa kwa Tanzania kujadiliana na DP World kwa kina kwani bandari ya Dar es Salaam itakuwa kama njia tuu ya kupeleka shehena Rwanda. Hii ina maana Rwanda itakuwa inapata faida kubwa kupitia bandari yetu kulinganisha na sisi.
View attachment 2656852

View attachment 2656853

View attachment 2656854

View attachment 2656854

View attachment 2656855
Tatizo si ubinafsishaji, DP World, Dubai au ufanisi wa DP World. Tatizo ni jinsi mkataba ulivyo.
Kumbuka, Tanzania tumekuwa wabovu sana katika mikataba ya kimataifa. Nature ya mikataba tunayoingia ndio chanzo cha matatizo.
Ukiusoma huo mkataba unaojadiliwa wa DP World ni tofauti kabisa na ule mkataba walioingia na Uingereza (southamptom), Marekani, Ujerumani na Singapore. Hili ndilo suala la Kujadili na sio ufanisi wa DP world.
Ndugu zanguni, msitutoe nje ya mstari.
 
Back
Top Bottom