DP World yashusha meli nzima ya vifaa bandarini, TPA wasema walishakabidhiana tangu April 7

DP World yashusha meli nzima ya vifaa bandarini, TPA wasema walishakabidhiana tangu April 7

DP World anafanya kazi UK, Unamaanisha waingereza ni wajinga?, always tumia kiasi cha ubongo ulichojaliwa.
International business zina special criteria, hii siyo biashara ya vitumbua, anayeingia kazi anakuwa amejizatiti kutimiza malengo fulani.
Hii hoja ya kuwa anafanya kazi UK, ni wajinga kama wewe na huyo rais wako kiazi ndiyo mnaishikilia. Hivi unajua hata UK anafanya kazi gani na kwa mkataba gani? Kwa taarifa yako haya ni mambo nilinayojua na sifuati mkumbo kama wewe n huyo rais wako!
 
The means describes the end result. Kama tu njia walitumia Dp kupata hii tenda ilikuwa na ukakasi sidhani kama SHAUKU ya watz itatimia hapo Bandarini. Let's wait and see
 
Mnachoshindwa kukielewa ni dhana mpya ya biashara ya bandari duniani, kingine hamkielewi ni huyo DP World kuwa mpangaji tu sawa na ambavyo tunawapangisha wapangaji kwenye nyumba zetu.
Ni wakina nani wanaopangisha pango kwa muda wa miaka 30? Sawa basi, utasema wanataka kurudisha fedha zao $250 Millioni? Tanzania tumetumia takribani $800 millioni-kwanini tusingesubiri hiyo mika 30 turudishe Investmens zetu?
Hapo mwenye nyumba ni TPA mwenyewe DPW ni mpangaji sawa na yule mdosi anayeanza kazi mwaka huu.
Kwamba sasa na mhindi kapewa kipande basi kuna uhalali wa DPW nae kuendelea? 'Mdosi' ana mkataba kama wa IGA? 'Mdosi' nae anapangishwa kwa miaka 30?
Na hao ni wapangaji wawili tu wa bandari za Dar kuna wapangaji wengine wa bandari ya Tanga, Bagamoyo na kule Mtwara.
Na hiyo, ni kwasababu za makelele ya Wapenda Nchi. hatahivyo, Initially according to the agreement kati ya Serikali yetu na DPW, ambamo Serkali inapaswa kuwaeleza na kupata ridhaa kutoka DPW upo uwezekano mkubwa kwamba hawa ni ma sub contractors, na kwasababu mkatabu huu umebubujikwa na Usiri after the fact, hatuezi kujua nini kimefanyika-ama unataka kusema walibadilisha vipengele vya masharti?
Dhana kwamba Samia kauza bandari zetu eti kwa waarabu ambao ni wajomba zake ni upuuzi kama upuuzi mwingine wowote ule.
Wewe ndie unasema imeuzwa, mimi nasema, wamegawiwa. Justification ya kugawiwa bandari yetu ambayo ina changia 40% ya mapato ya Serikali yetu is Unfathomable, ni vigumu kuelewa. Je, kuna rushwa? au Upendeleo kwa wajomba?
DPW anaendesha bandari za India, Belgium na Uingereza, na huko wameuza pia bandari zao kwa mwarabu?.

Hizo nchi wana vyanzo vingi vya mapato, hizo bandari zao sidhani vinachangia 40% ya mapato ya Serikali kama ilivyo Tanzania, na itoshe wamo wabia wengi ndani ya DPW waliotoka kwenye hizo nchi-Tanzania tuna wabia wangapi?
 
Hiyo haiondoi ukweli kwamba ccm yote hakuna mwenye akili na ushahidi ni huo wa mfano mmoja tu wa bandari, kwa miaka zaidi ya 60 inashindwa kuendesha bandari kwa faida wanazidiwa akili na kikampuni kilichoanzishwa mwaka 2005 kipindi ambacho Kikwete anaanza ngwe yake ya kwanza ya urais Ccm muache kuhadaa wananchi, hamna mnaloweza zaidi ya kuiba na kujilimbikizia mali kifisadi. Inakuaje kampuni inakuwa na ufanisi kuliko serikali ambayo hata kodi hailipi?
Kwa mantiki hiyo yako kampuni hiyo hiyo inaendesha bandari ya Southampton Uingereza.Nao waingereza hawana akili watu waliotawala nusu ya dunia?Qatar ina vitega uchumi vya uhakika kwenye Jiji la London na waliowaruhusu hawana akili?Njaa na udini ni magonjwa mabaya kwa ustawi wa akili ya mtu.
 
Wale wazee wa tpa wa kuingia kazini saa mbili kupiga dili kwenda kula lunch kwa shilole sijui wanarudi saa tisa kazini
Kazi wanayo

Ova
Na ndio hao na wapambe wao ndio wanalalamika sana kwa kuwa wanajua free lunch is no more.Itabidi ufanye kazi ndio ule.
 
Safi sana...Toka habari ya Dp world kuanza Kazi mwanzoni mwa mwezi huu mizigo inawahi kutoka wiki mbili kabla tofauti na zamani ..sasa wakiweka hiyo mitambo wafanyabiashara kupata mzigo siku chache baada ya meli kutia nanga ni furaha kwa wafanyabiashara...Kazi kwenu vijana wakupinga ambao hata hajawahi agiza headphone kikuu..
 
MAMLAKA ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), imesema kampuni ya DP World ya Dubai katika Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) imeanza kushusha vifaa katika Bandari ya Dar es Salaam kuanza uwekezaji.

Aidha, TPA imebainisha kuwa makabidhiano ni tangu Aprili 7, mwaka huu bila kuathiri uendeshaji wa bandari hiyo. Mkurugenzi wa Bandari ya Dar es Salaam, Mrisho Mrisho alisema hayo Dodoma akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Plasduce Mbossa katika Mkutano wa 13 wa Mwaka wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF).

Mrisho alisema DP World ambao wataendesha gati namba moja hadi saba, wameshusha meli nzima yenye vifaa vya kisasa ikiwamo mashine nane za RTG, mashine nyingine 19 za kushusha kontena, jenereta kubwa za kuendesha mashine hizo na mashine nyingine nne ziko njiani.

Hivyo vifaa vinajulikana na tulikuwa na uwezo wa kuvileta, tatizo mafisadi wapo kazini
 
Wewe endelea kubwatuka.Bandari zipi unaongelea au unasumbuliwa na msongo wa mawazo.
Ni hivi. Wananchi hawajaridhishwa na mkataba huu kati ya DPW na Serikali.

Wacha ni bwatuke tu. Ad hominem. Huna hoja.

NB: Inachekesha unauliza Bandari zipi zinaongelewa, wakati taarifa iliyo mezani inasema hivyo. Nani anae bwatuka hapa?

Amani ikufikie.
 
Ni hivi. Wananchi hawajaridhishwa na mkataba huu kati ya DPW na Serikali.

Wacha ni bwatuke tu. Ad hominem. Huna hoja.

NB: Inachekesha unauliza Bandari zipi zinaongelewa, wakati taarifa iliyo mezani inasema hivyo. Nani anae bwatuka hapa?

Amani ikufikie.
Wananchi wangapi?Una interest na Bandari na mkate umemwagiwa mchanga?Kelele zako binafsi hazisaidii chochote na kama mkataba umekupa tabu sana nenda kwa Mangi nunua kamba cha kufanya unajua. Mimi nitalipia hiyo kamba.
Hiyo treni imeshaondoka stesheni ndio sababu nikakuuliza bandari gani?Endelea kupiga domo.
 
MAMLAKA ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), imesema kampuni ya DP World ya Dubai katika Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) imeanza kushusha vifaa katika Bandari ya Dar es Salaam kuanza uwekezaji.

Aidha, TPA imebainisha kuwa makabidhiano ni tangu Aprili 7, mwaka huu bila kuathiri uendeshaji wa bandari hiyo. Mkurugenzi wa Bandari ya Dar es Salaam, Mrisho Mrisho alisema hayo Dodoma akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Plasduce Mbossa katika Mkutano wa 13 wa Mwaka wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF).

Mrisho alisema DP World ambao wataendesha gati namba moja hadi saba, wameshusha meli nzima yenye vifaa vya kisasa ikiwamo mashine nane za RTG, mashine nyingine 19 za kushusha kontena, jenereta kubwa za kuendesha mashine hizo na mashine nyingine nne ziko njiani.

Tanzania ilishindwa kununua hizo mashine[emoji856][emoji855]......Anyway wakitangaza kazi nishtue ndugu mjumbe...!!
 
MAMLAKA ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), imesema kampuni ya DP World ya Dubai katika Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) imeanza kushusha vifaa katika Bandari ya Dar es Salaam kuanza uwekezaji.

Aidha, TPA imebainisha kuwa makabidhiano ni tangu Aprili 7, mwaka huu bila kuathiri uendeshaji wa bandari hiyo. Mkurugenzi wa Bandari ya Dar es Salaam, Mrisho Mrisho alisema hayo Dodoma akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Plasduce Mbossa katika Mkutano wa 13 wa Mwaka wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF).

Mrisho alisema DP World ambao wataendesha gati namba moja hadi saba, wameshusha meli nzima yenye vifaa vya kisasa ikiwamo mashine nane za RTG, mashine nyingine 19 za kushusha kontena, jenereta kubwa za kuendesha mashine hizo na mashine nyingine nne ziko njiani.

Watanganyika wamekataa huu mpango ,mpeni hata mzawa itakua safi sana
 
Back
Top Bottom