DPP Biswalo Maganga kuwa Jaji, Rais Samia umekosea sana

DPP Biswalo Maganga kuwa Jaji, Rais Samia umekosea sana

Ndio maana katiba mpya ni muhimu sana hii haiwezi kutupeleka mbele tena tukiwa taifa la uhuru, haki na maendeleo.
Sheria zimekuwa zikikanyagwa toka mwendazake lakini ulikuwa kimya sasa mama ameshika kijiti unaleta ujuaji., Nchi yenu haihitaji majaji kufanyiwa vetting, majaji wanahukumu kesi kwa maelekezo tu., No justice at all -
Mwacheni mama wa kizanzibari naye awaongoze mlifkiri mzanzibari haitawezekana tena kuongoza Ikulu ya magogoni
 
Miongoni mwa watu walioteuliwa leo na Rais Samia Suluhu kuwa majaji wa mahakama kuu, jina la DPP Biswalo Maganga lipo pia.

Hili jambo limetushtua sana wadau wa mambo ya sheria, kuna kitu tunakiona hakiko sawa na kinakwenda kutuharibia zaidi mhimili wetu wa sheria. Nitaweka sababu za msingi sana kwanini Biswalo Maganga hastahili kuwa jaji.
Huyu alikuwa akishirikiana na jambazi lililo fariki juzi juzi kubambikizia watu kesi na kupora pesa zao. Alikuwa mhimili wa sukumagang
 
DPP wa Kabla ya Biswalo nae aliteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama kuu kama sikisei
 
Mkuu unahakika uteuzi huo hajapitia huo mchakato? Umejuaje hilo? Ili hali nakumbuka Maneno ya JPM alishawahi seme alishawahi kupendekezwa kuwa jaji na Tume.
Ulikuwa unamwamini Magu wewe?
 
Miongoni mwa watu walioteuliwa leo na Rais Samia Suluhu kuwa majaji wa mahakama kuu, jina la DPP Biswalo Maganga lipo pia.

Hili jambo limetushtua sana wadau wa mambo ya sheria, kuna kitu tunakiona hakiko sawa na kinakwenda kutuharibia zaidi mhimili wetu wa sheria. Nitaweka sababu za msingi sana kwanini Biswalo Maganga hastahili kuwa jaji...
Hayo kwamba hajafanyiwa vetting we umejuaje?
 
Pendekezo la jana kuwa na sifa za kuwa jaji halina maana linaweza kutumika leo kuwa jaji. Kwanini? Sifa za mtu hubadilika kutokana na nafasi aliyonayo, nyakati tuliyopo na mwenendo wake.
Swali la pili, umejuaje kua hakupendekezwa na tume ya uteuzi?
 
Mambo mengine nadhani mnamuonea tu.

Hili ni moja ya janga alilolitengeneza Magu. Na hatukusaidia chochote...
Hizi Sheria ni za ajabu Sana na wanaotunga ni wabunge tunaowachagua Rais yy anafanya endorsement tu Sasa nadhani nguvu ya umma itumike kudai katiba
 
Biswalo Mganga, mzaliwa wa kijiji cha Igala Wilayani Ukerewe, msomi wa sheria na miongoni mwa Watanzania wenye bahati sana katika teuzi, aliteuliwa kuwa DPP na Rais wa awamu ya nne Jakaya Mrisho Kikwete mwaka 2014. Alimrithi Elieza Feleshi ambaye mara moja aliteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu.

Nafasi ya Mkurugenzi wa Mashtaka wa Taifa ni nafasi kubwa, nyeti na ambayo ikitumiwa vibaya inaweza kuathiri Uhuru wa mtu kimakosa, uchumi au hata maisha.

Tangu nafasi hii ianzishwe nchini, Biswalo Mganga anaweza kuwa DPP aliyefanya mabaya mengi kwa Watanzania wenzake kuliko mazuri waliyotarajia. "Biswalo" jina lenye asili ya Kikerewe likiwa na maana ya "Aibu" ni jina linalotumiwa na mtu aliye kinyume kabisa na maana halisi ya jina lake. Biswalo Mganga hana aibu, hana kabisa soni wala simile pale anapotekeleza kile alichoelekezwa na mkubwa wake kiwe kibaya au kizuri.

Ni katika uongozi wa Biswalo ulipoanzishwa utaratibu wa ovyo ambao awali haukuwepo kisheria lakini yeye bila AIBU aliuanzisha na alipoona anapigiwa kelele yeye na Mteuzi wake wakapeleka mswada wa dharura Bungeni. Huu ni utaratibu eti wa Ku Bargain kati ya mtuhumiwa wa uhujumu uchumi ambaye yuko Mahabusu na serikali kama mshitaki mkuu ikiwakilishwa na Biswalo Mganga. Wengi wameumia na kufilisika kwa utaratibu huu hasa pale ulipotumiwa vibaya.

Mtu anakamatwa anapewa kesi ya Uhujumu uchumi ambayo imewekewa sheria ya kutokuwa na dhamana kisha anapewa nafasi ya kuandika barua kuomba kuelewana na mshitaki wake na kwamba yuko tayari kulipa kiasi chochote cha fedha atakachotajiwa. Hivyo anatajiwa na akifikiria kuendelea kukaa Mahabusu na mateso yote yale anaona bora akubali.

NIJE KWENYE SABABU YENYEWE!
Baada ya utangulizi huo utaona jinsi ambavyo mtu huyu Biswalo asiye na Swalo (aibu) alivyojitengenezea maadui wasio na sababu ya kuwa maadui maana wengi hawakukosa kwa kiwango cha kutozwa kiasi kikubwa vile cha fedha. Wengine walioona fedha zao zinapotezwa bila kosa waliamua kubali mahabusu kuliko kuuza Uhuru wao kwa kukiri wasichotenda kama alivyofanya Rugemarila na Seth.

Ukichukua orodha ya waliofanyiwa hayo na wengine ambao bado wako ndani lakini ndugu zao wanahangaika bila mafanikio, utaona wigo wa maadui halali na wa bandia ulivyo mkubwa. Hivyo Mama Samia ambaye alikuwa anayaona madudu yote ya Biswalo na asingependa Serikali yake iendelee kuchafuliwa na kashifa za uonezi kama hii ya kuchukua fedha za watuhumiwa kwa kisingizio cha watuhumiwa kukiri kosa.

Hivyo ili kusafisha kashifa hiyo akaona ni muda sahihi kumweka pembeni, lakini kumweka pembeni mtu huyu na kumwacha akae bila kumwangalia huku akiwa na siri nyingi za serikali ya kikatili iliyopita ni kujivua nguo kwa serikali na chama chao. Hivyo amepelekwa kwenye nafasi ambayo ataendelea kulindwa muda wote ili kuhakikisha usalama wake na usalama wa siri za ukatili uliopita.
 
Awatoe aweke wakina faru John na genge lake au sio. Mwache mama afanye kazi yake.
Nani snamzuia kufanya kazi. Tatizo inaonekana kana kwamba ameanza kupiga hatua na mguu wa kushoto. Sisi ni commentetors tu....!!
 
Miongoni mwa watu walioteuliwa leo na Rais Samia Suluhu kuwa majaji wa mahakama kuu, jina la DPP Biswalo Maganga lipo pia.

Hili jambo limetushtua sana wadau wa mambo ya sheria, kuna kitu tunakiona hakiko sawa na kinakwenda kutuharibia zaidi mhimili wetu wa sheria. Nitaweka sababu za msingi sana kwanini Biswalo Maganga hastahili kuwa jaji...
Mama amesema yeye na Jiwe kitu kimoja! Wakati wa jiwe sheria alikuwa yeye kinachomtoka mdomoni tu na ndio kinachoendelea

Sent from my Nokia 8.1 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom