Tetesi: Dr. Dau kufikishwa mahakamani. Yasemekana kahojiwa TAKUKURU

Tetesi: Dr. Dau kufikishwa mahakamani. Yasemekana kahojiwa TAKUKURU

Status
Not open for further replies.
Majipu mengi hapa ni yaliyoota miaka mitano mpaka saba nyuma, na sio ya kukuibia wewe au mimi bali mali za umma. Yeye hakuwa kwenye system kipindi hicho, sana sana 'kitanzi' chake ni richmond lakini hilo TL alishamtaja mwenyewe pale Morogoro wakati wa kampeini.
Falsafa ya JPM huenda ikawa imekaa vizuri maana kupanga ni kuchagua. Angelianza na maisha bora kwa wananchi alafu baadae akawakamata mafisadi au ndio hivi anaanza na mafisadi kwanza theni maisha bora yanafuatia.
Sasa hizo hela za maisha bora zipo wapi wakati watu wanaendelea kuzitumbua mfano kwa jinsi nchi yetu ilivyo kuna kama 3trilion hivi zinaibiwa hasa kwenye hii miradi ya PPF na NSSF
 
Kama ni kweli anastahili kunyongwa hadharani, haiwezekani kiwanja cha laki5 unajifanya kununua kwa 800Million?

Fisadi jasiri sana hilo.
 
Usemalo ni sawa mana hata 2015 walichukua pesa nyingi huku kwenye mifuko ya jamii....ngoja tuone huu mtinange dau hatakubali kwenda n maji atawataja wote

Hatoweza wataja mkuu, kwani atakuwa ana jihatarisha maisha yake na ya familia yake pia.
 
Sheria kali na hukumu za maana zitolewe kwa wahusika wote, sio viongozi wa NSSF tu bali hata wale azimio wauza viwanja na kampuni yao ifungwe mara moja ku operate Tanzania. Pia hawa watu inabidi mali zao na account zao zote zikamatwe,ziuzwe na kufidia pesa zote zilizopotea, kama sheria hizi hazipo basi ni wakati muafa wa serikali kupeleka pendekezo bungeni haraka lakini tayari wakiwa wameshakamata mali na account zote za ndani na nje za haya mafisadi. Kutowachukulia hatua kwa haraka na kuwapa dhamana na kuwafunga vifungo vya miaka mitano sijiu sita ndo kunawasabisha hawa watu waendelee kuwa wezi, tutoeni adhabu ili watu tuweze kujifunza na tuwe na hofu ya wizi. Serikali pia iangalie jinsi ya kuwapunguzia wakurugenzi wote mamlaka ya kuidhinisha pesa. Hii ni aibu sana, hata tukiangalia makampuni binafsi hakuna wakurugenzi,ceo,general managers walio na maamuzi ya pesa kwenye project ya 1.3 trioni, wekeni limitations ili kupunguza kasi ya wizi.
 
Hatoweza wataja mkuu, kwani atakuwa ana jihatarisha maisha yake na ya familia yake pia.
Atakua kilaza wa mwisho akifanya hivyo.....mambo yameshakua mabaya msiba wa wengi hunoga kuliko kufa peke yako
 
Sure! Lakini huo ni mtihani mkubwa kwake.

Mimi sizungumzii wale makada anaowaita wanafiki kwa kuwa walimpinga au wamepishana naye kwenye kauli/sera na mambo kama hayo.

Mimi nataka wale makada walio IFISADI nchi hii kwa kuifanya yao washitakiwe! Hao tu!!!
Ndiyo hao hao jamaa nijuavyo mimi hamuonei mtu aibu angalia ile hotuba ya ufunguzi wa bunge alimsema mkubwa wake moja kwa moja mpaka camera zilikua zinamwonyesha JK
 
Sawa, Serikali ya CCM awamu ya Tano haina undugu na yeyote, ubadhirifu wa fedha za uma ni makosa wacha sheria ifuate mkondo wake, na haki ionekane kwa pande zote.
Serikali ni ya Magufuli.
 
.....ANGEIGUSA "ESCROW" NINGEMKUBALI ZAIDI.
ESCROW NI YA JUZIJUZI TENA BADO MBICHI KABISA.

hayo ndo majipu alisema kuyatumbua inabidi utumie akiri ya ziada.Subiri evidence nyingi ambazo zitapelekea hiyo kitu kutokea
 
Atakua kilaza wa mwisho akifanya hivyo.....mambo yameshakua mabaya msiba wa wengi hunoga kuliko kufa peke yako
Mkuu hii si mara ya kwanza kwa inshu nzito kama hii kutokea nchini. Sio rahisi kama unavyofikiria. Akubali akatae, Dr. Dau na wengine wachache wa NSSF ndio watakuwa kafara kwa ajili ya maslai ya genge kubwa lililo nyuma ya hili sakata.
 
Mkuu hii si mara ya kwanza kwa inshu nzito kama kutokea nchini. Sio rahisi kama unavyofikiria. Akubali akatae, Dr. Dau ndio na wengine wachache wa NSSF ndio watakuwa kafara kwa ajili ya maslai ya genge kubwa lililo nyuma ya hili sakata.
mkuu tulia utaona hata kitilya kuna wazito wataungana nae kwenye ile case ndio walichukua mpunga mrefu na wanajulikana.....mara y kwanza walikataa kuwataja ila tetesi zinasema tayari list imetajwa
 
Achomwe tu shindano ya sumu.Dhambi ya kutafuna mafao ya walala hoi imtafune milele
 
SSRA nao wakatumbuliwe tu haiwezekani waliyaona haya wakaona ni OK. hapana kwa kweli.
 
Kweeeeeeeeeeli siamini hiki ninachokiona kwa dau! Hivi ukiwa mwizi kwanini ujifanye mfia Dini????? Haya tuoneshe aya sasa inayokuruhusu kukwapua hela za watz kama ulivyohodari wa kuquote!!!! Katika hili unaweza sema majambazi wana nafuuuu! Hivi pesa zote hizo zingeokoa maisha ya watz wangapi mahospitalini! Shaaaame on you! Nchi yetu inatia huruma jmn! Daaaa! Na bahati mbaya wadanganyika tumeumbiwa kuchukulia issue poa tu! Nimekasirika sana!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom