DRC: Wanajeshi walinda amani wa Tanzania wajeruhiwa katika mapigano na M23

DRC: Wanajeshi walinda amani wa Tanzania wajeruhiwa katika mapigano na M23

Tatizo lenu mnakuwa too theoretical, hata nikikuiliza utoe ushahidi wa kwanini JWTZ ni bora kuliko RDF najua hauna. Mimi naongelea RDF sababu ya milestones zake, kuanzia campaign za kule Uganda, hadi kuiteka Rwanda mpaka kuivamia DRC mpaka kujipenyeza Angola na Jamhuri ya Afrika ya Kati hizo sio milestone ndogo tena ndani ya mwaka mmoja tu toka watoke kwenye vita ya wenyewe kwa wenyewe. Recently tu wamezima magaidi wa Mozambique!!

Na ambacho hufahamu nchi inayoongoza kuwa na majeshi kwenye foreign land na peacekeeping mission ni Rwanda. Licha ya udogo wa jeshi imeweza kusambaa nchi nyingi sana mpaka Leo so tusidharau sababu hatuna taarifa za kutosha.

Sasa kwa faida ya mjadala na wewe njoo na counter arguments for JWTZ maybe mission za Seychelles, Darfur n.k ila sio kuita wengine wanachekesha huku hauna milestone hata moja ya kushare hapa.
We mkuu kwa Sasa hivi Rwanda haina uwezo Kama ule wa Congo was kupigana na nchi 7 kwa wakati mmoja, coz ile Congo war nyuma alikuwa Ni USA alimpa kila KITU , ushaidi upo mwingi Sana.
 
Mkuu itafaa zaidi kama utasema pia haikua ni ‘full out war’ Rwanda alikua na jeshi lake la askari kama elfu ishirini na vikundi alivyoviunga mkono, Angola walikua na kiwango kidogo sana cha askari na papo hapo walikuwa wakipigana na kikundi kingine cha waasi ukiacha vile vinavyoungwa mkono na Rwanda, Uganda kama Rwanda, Zimbabwe pia askari walikua wachache sana hasa focus yao ikiwa ni kulinda mji mkuu na kumlinda kabila...
Kiufupi it was a very complex issue... ila kuipa credit Rwanda ati ali-face nchi tatu tofauti ni kuipendelea. Kiuhalisia Rwanda wanafanya vizuri kiintelijensia lakini ni karibia haiwezekani kwao kupigana vita on 3 fronts. Honestly speaking.
Yes mkuu,
Rwanda lilikuwa Ni jeshi la kitutsi Tena walikuwa Ni waasi RPA( Rwanda Patriotic Army) wale walikuwa hawalipwi walikuwa wanajitolea kutoka rwanda civil war mpaka Congo war. RPA walikuwa wapo 26,000. Nilisikia kutoka kwa JAMES MUNYANDINDA kagame former bodyguard. Na pia BAADA ya kuchukua nchi kutoka Rwanda alichukua Genocide survivor akawapa mafunzo na wengi wake aliwapeleka congo Sasa hii inamaana waliongeza idadi. Na hata kwenye first Congo hawakuwa pekeao kumbuka kulikuwa na Uganda, Baadhi ya wanajeshi wa kitutsi kutoka Burundi, na Banyamulenge na waasi wa Congo senior kabila. So hawakuwa pekeao.
Tena kwenye second Congo war
Kulikuwa majeshi ya rwanda ya kitutsi na vikundi vya uhasi vya Congo hasa Banyamulenge na Askari wa mabotu seseko,
Nimewahi kumsikiliza Laurent nkunda batwale alisema kuwa alikuwa na vijana zaidi ya 10,000 kwenye second Congo war. Na alikuwa upande wa rwanda, na vikundi vilikuwa Ni vingi na idadi ya Askari wa rwanda Ni kweli walikuwa wengi.
Ila Ni KWAMBA WANAMOYO WA KUPIGANA HASA. Japo walikuwa wengi ila walishidwa kukimaliza kikosi Cha Angola na Zimbabwe ambavyo viliwasumbua Sana.
zitto junior
 
[emoji1][emoji1] Kwamba vifaru ni mzigo sio?nenda kawaulize wale mercenaries Kule Ukraine waliokimbia Vita wanasemaje khs vifaru vya Warussi.Sniper hatari wa kutoka Canada aitwae Wali anakwambia mizinga inapigwa non-stop mwisho wa siku ameishia kupiga risasi 2 tu na kukimbia Vita [emoji1][emoji1][emoji1].
Ngoja niwaraisishie

 
Kwa maoni yangu Afrika tunawasumbua vijana wetu na kuwatia majeraha bure tu. Unafiki Ni mwingi.....tunaanzisha Vita wenyewe kwa uroho wa madaraka halafu tunakimbia Ulaya kutafuta pesa za kutadhili ugaidi then eti vijana wetu wakalinde amani huku tunazunguka nyuma kuwaangamiza. Sipendi
 
Tanzania JWTZ should take note.

Hao M23 ni jeshi la Rwanda, siyo wahuni.

Wahuni wanapata wapi vifaru na mizinga.

Kama mbwai iwe mbwai.
Kwani jeshi la DRC linasemaje mbona Congo ni kubwa kuliko Tanzania pia kiuchumi sio masikini wanajeshi wetu warudi nyumbani sisi ya kwetu yanatushinda kila mtu apambane na hali yake.
 
Acha propaganda, bomu moja tu linasambaratisha Rwanda yoote.
Umewahi kujiuliza Ukraine na Russia ipi Kubwa?
Kwa taarifa yako vita ya Ukraine na Russia inaenda miezi kadhaa sasa.
 
[emoji1][emoji1] Kwamba vifaru ni mzigo sio?nenda kawaulize wale mercenaries Kule Ukraine waliokimbia Vita wanasemaje khs vifaru vya Warussi.Sniper hatari wa kutoka Canada aitwae Wali anakwambia mizinga inapigwa non-stop mwisho wa siku ameishia kupiga risasi 2 tu na kukimbia Vita [emoji1][emoji1][emoji1].

[emoji2][emoji2][emoji2][emoji2][emoji2][emoji2][emoji2][emoji2][emoji2][emoji2][emoji2][emoji2]
 
Kwani jeshi la DRC linasemaje mbona Congo ni kubwa kuliko Tanzania pia kiuchumi sio masikini wanajeshi wetu warudi nyumbani sisi ya kwetu yanatushinda kila mtu apambane na hali yake.
[emoji1][emoji1] labda siku wanajeshi wa Drc wakiwa serious.
FT3XE4qXsAUg6FF.jpg
 
Hiyo ndio maana ya proxy wars hata vita ya Armenia Vs Arzebeijan walioshangilia ni Uturuki ilihali hawakuwa Frontline!! ama vita ya Syria inayosifiwa ni Urusi kwamba imemshinda US licha ya kwamba hakuna Wanajeshi wa marekani huko Syria physically.

All out war siku hizi ni chache sana nyingi ni proxy lakini mwisho wa siku ndio zinaamua Mshindi hata kama umepeleka askari buku pekee.

Hata Tanzania huwa tunajisifia Kuzima mapinduzi Burundi, Seychelles, Comoros n.k ila je zilikua all out war? But we're still proud sababu technically tulishinda vita whether kwa askari 10 au 100.

2. Yes objective ni kumlinda lakini ukisema ni mji mkuu pekee hapana. Majeshi ya wageni yalikuwepo kuanzia Pweto na Kasai huko kusini mpaka Province Equator kaskazini hadi Bas Congo province huko magharibi na huko kote kulikua na engagement dhidi ya Kagame.

3. Kusema Angola ilikua na vita na waasi wa UNITA sio kisingizio hata Rwanda ilikua inapambana na FDLR, Burundi nayo kulikua na waasi, M7 naye alikua na waasi huko kaskazini na kasese n.k in fact Rwanda walitwangana na Uganda wakiwa katikati ya vita na Kinshasa!! Ila nguvu haikupungua na zaidi Uganda alipigwa in both battles.

Kusema haya kwa udogo wao ule bila kuwa na air cover walionyesha ujasiri wa hali ya juu, so hawako overrated ila they earned their status.
Hiyo ndio maana ya proxy wars hata vita ya Armenia Vs Arzebeijan walioshangilia ni Uturuki ilihali hawakuwa Frontline!! ama vita ya Syria inayosifiwa ni Urusi kwamba imemshinda US licha ya kwamba hakuna Wanajeshi wa marekani huko Syria physically.

All out war siku hizi ni chache sana nyingi ni proxy lakini mwisho wa siku ndio zinaamua Mshindi hata kama umepeleka askari buku pekee.

Hata Tanzania huwa tunajisifia Kuzima mapinduzi Burundi, Seychelles, Comoros n.k ila je zilikua all out war? But we're still proud sababu technically tulishinda vita whether kwa askari 10 au 100.

2. Yes objective ni kumlinda lakini ukisema ni mji mkuu pekee hapana. Majeshi ya wageni yalikuwepo kuanzia Pweto na Kasai huko kusini mpaka Province Equator kaskazini hadi Bas Congo province huko magharibi na huko kote kulikua na engagement dhidi ya Kagame.

3. Kusema Angola ilikua na vita na waasi wa UNITA sio kisingizio hata Rwanda ilikua inapambana na FDLR, Burundi nayo kulikua na waasi, M7 naye alikua na waasi huko kaskazini na kasese n.k in fact Rwanda walitwangana na Uganda wakiwa katikati ya vita na Kinshasa!! Ila nguvu haikupungua na zaidi Uganda alipigwa in both battles.

Kusema haya kwa udogo wao ule bila kuwa na air cover walionyesha ujasiri wa hali ya juu, so hawako overrated ila they earned their status.
Mkuu, juhudi za Tanzania ktk kuzima mapinduzi huko Burundi, Comoro na kwingineko ni kukosea kuziita ‘Vita’ tutakuwa tunapoteza maana ya vita mkuu kwa sababu kuu moja, huko tuendako kuzima mapinduzi hatuendi pigana na jeshi zima la nchi hiyo, bali sehemu tu ya askari waloamua kuasi, hivyo si vita. Tanzania vita tulikuwa nayo mwaka 1977 dhidi ya Uganda. Pia mbali na kushinda machungu tuliyaona.

Ukirejea tena nilichoandika awali sikusema ni ‘Mji mkuu pekee’ nilisema focus kubwa ilikua huko, na hiyo haikuwa na maana kuwa walienda Kinshasa tu.

Bado naamini Rwanda wako overrated, Ndiyo walifanikisha kwa nafasi kuwa ktk kuipata Congo hii tuionayo leo. sababu tukiangalia Military objectives zao walizotazamia kuzikamilisha Congo si zote zilitimia pia napata ukakasi kuziita juhudi zao kuwa zilishindwa ila ni ukweli kwa kiasi kikubwa zilishindwa hiki ndicho kinanfanya nichelee kuipa Rwanda hadhi ya kana kwamba ni ‘invincible’ au kuiona kwa hadhi kubwa kama inavyooneshwa na waandishi kadhaa upande wa kijeshi.

Kumfurusha Mobutu walifanikiwa.
Kutwaa ardhi ya Congo hawakufanikiwa japo waliendelea kukwapua maliasili zake.
Kuongeza usalama mpakani mwao na Congo ili kuwaweka mbali interahamwe walifanikiwa.
Kuwa na ushawishi ndani ya Congo hawakufanikiwa kwa kiwango kikubwa.

Mwanzoni tu wakati Rwanda, Uganda na L. Kabila wanafanya oparesheni kumfurusha Mobutu na mpaka walipofanikiwa Rwanda alikua na ushawishi mkubwa ndani ya Congo kiasi hata Millitary chief of staff wa jeshi la L.Kabila alikuwa ni Mnyarwanda James Kabare, askari wa Rwanda pamoja na vikundi vinavyoungwa mkono nao walikuwa wakizunguka Kinshasa... wakati wote huo Rwanda waliweza ingia, toka na kufanya chochote ndani ya Congo mpaka alipotimuliwa bwana Kabare julai 1998.
Mwanzoni Vita vya pili vya Congo vya wenyewe kwa wenyewe Rwanda waliishika karibu Congo yote, si mashariki si Magharibi. Waliweza kuviunganisha vikundi kadha wa kadha kupigana upande wao.

Hayo yote yaliwezekana kabla ya kuingia Angola na askari wao wazoefu, Zimbabwe na jeshi lao la anga takatifu, Sudan, Libya, Chad na Namibia.

Dhahiri kabisa askari wachache wa Angola walivirudisha nyuma vikundi na jeshi la Rwanda kutoka maeneo ya Magharibi mwa Congo, jeshi la Zimbabwe likavirudisha nyuma vikosi vilivyokuwa karibu kuizingira Kinshaza, Zimbabwe pia walifanya kazi nzuri kuvuruga mpangilio wa jeshi la Rwanda na wanamgabo wake kwa mashambulizi ya Anga hasa mashariki mwa Congo.

Mwisho nasistiza kuwa Rwanda walifanya nafasi kubwa, lakini si sawa kuichorea picha kuifanya kuwa ‘invincible’ machoni pa wengi hasa watanzania. Rwanda walinufaika sana na uwepo wa watu wa makabila yao mashariki mwa Congo, wakanufaika na madudu ya Mobutu yaliyowafungulia njia kuingia ndani ya Congo, wakanufaika na ukarimu wa Kabila kuwakaribisha, ikiwa Rwanda wakaingia vitani ktk mazingira tofauti kama ya Kenya au Tanzania ambako hakuna mazingira sawa na Congo basi jeshi la Rwanda litadhalilika sana.
 
Yes mkuu,
Rwanda lilikuwa Ni jeshi la kitutsi Tena walikuwa Ni waasi RPA( Rwanda Patriotic Army) wale walikuwa hawalipwi walikuwa wanajitolea kutoka rwanda civil war mpaka Congo war. RPA walikuwa wapo 26,000. Nilisikia kutoka kwa JAMES MUNYANDINDA kagame former bodyguard. Na pia BAADA ya kuchukua nchi kutoka Rwanda alichukua Genocide survivor akawapa mafunzo na wengi wake aliwapeleka congo Sasa hii inamaana waliongeza idadi. Na hata kwenye first Congo hawakuwa pekeao kumbuka kulikuwa na Uganda, Baadhi ya wanajeshi wa kitutsi kutoka Burundi, na Banyamulenge na waasi wa Congo senior kabila. So hawakuwa pekeao.
Tena kwenye second Congo war
Kulikuwa majeshi ya rwanda ya kitutsi na vikundi vya uhasi vya Congo hasa Banyamulenge na Askari wa mabotu seseko,
Nimewahi kumsikiliza Laurent nkunda batwale alisema kuwa alikuwa na vijana zaidi ya 10,000 kwenye second Congo war. Na alikuwa upande wa rwanda, na vikundi vilikuwa Ni vingi na idadi ya Askari wa rwanda Ni kweli walikuwa wengi.
Ila Ni KWAMBA WANAMOYO WA KUPIGANA HASA. Japo walikuwa wengi ila walishidwa kukimaliza kikosi Cha Angola na Zimbabwe ambavyo viliwasumbua Sana.
zitto junior
Umeeleza uzuri sana mkuu, nami ndiyo ilikuwa hoja yangu.
 
Umewahi kujiuliza Ukraine na Russia ipi Kubwa?
Kwa taarifa yako vita ya Ukraine na Russia inaenda miezi kadhaa sasa.
Niko upande wa Ukraine katika Vita hii, Russia wanaweza kuimaliza vita hii hata ndani yasiku moja, ukweli unaujua.
Kwa nini Vita ya Ukraine haiishi?
1.Ukraine ni Proxy katika vita hii
2.Vita hii inaweza kumalizika kwa mazungumzo, na wa kuimaliza ni Washington D.C
3.Ni vita ya Putin na sio Russia
4.Vita hii ni Opportunity kwa Russia na US.
5.Imeamuliwa na West kuwa hii vita iachwe iwe prolonged ili Putin atumie gharama kubwa kumpunguza nguvu.
 
Kwanza JWTZ huko Congo inatafuta nn? Km kulinda Aman mbna hapa kwetu Panya Road wanasumbua? Ngoro Ngoro je? Km sio unafiki na ufukunyuku n nn? Umbea na ukuda wa kiwango cha juu, tena hao M23 naona bado hawafanyi ipasavyo, wanatakiwa kuwasha motoo had wapoteane.

Nasemaje M23 piga hao JWTZ kipigo cha mbwa mwizi had wapate akili ya kurudi kwao, msieeeew unafiki tyuuh.
 
M 23 imewajeruhi wanajeshi wetu huko Kivu ya Kaskazini.

Ifahamike m23 ni wahuni wanaoungwa mkono na Serikali ya Kigali na ikumbukwe wahuni hao m23 kipindi cha Kikwete tuliwatwanga hali iliyopelekea mgogoro mkubwa wa kidipromasia baina ya Serikali ya Kikwete na Serikali ya Kigali.

Sasa baada ya Serikali ya Samia kuingia madarakani wahuni hao wamerejea kwa nguvu pengine wakiamini Samia hawezi kuwafanya lolote.Tusikubali aslani!

Tuwashughulikie hao wahuni kabla hawajaleta mgogoro mkubwa ndani ya Kanda yetu na Serikali ya Kigali ionywe wazi iache kuwakumbatia hao chawa wao.

Tusimchekee Kagame kwa sababu si mtu mwema hata kidogo.

Mzee Kikwete hakuwa mjinga ku deal naye kibabe huyo mwana- hizaya mpenda vya bure.

=====

Wanajeshi walinda amani wa Tanzania wajeruhiwa katika mapigano na M23 DRC​

Jeshi la Jamuhuri ya Kidemokrasi ya Jamuhuri ya kidemokrasi ya Congo, FARDC, limetangaza kuwa wanajeshi watatu wa Tanzania wanaohudumu katika kikosi cha walinda amani cha Umoja wa Mataifa MONUSCO wamejeruhiwa wakati wapiganaji wa M23 waliposhambulia ngome yao iliyopo Rutshuru.

MONUSCO imethibitisha kuwa wanajeshi wake watatu wamejeruhiwa na kupelekwa kutibiwa katika hospitali ya mjini Goma uliopo mashariki. Katika tangazo hilo jeshi la serikali ya Congo limesema mmoja wa wanajeshi hao amejeruhiwa vibaya.

MONUSCO inasema kuwa wanajeshi hao wamejeruhiwa katika shambulio lililofanyw na wapiganaji wa M23 katika ngome yao iliyopo ivukatika eneo la Shangi -Rutshuru.

Kundi la M23 linasema kuwa majeshi ya FARDC na na MONUSCO ndio waliofanyanya mashambulio kwanza dhidi yao katika ngome yao iliyopo katika eneo la Jomba Jumatatu.

Hii inakuja wakati mapigano yakiendelea kwa siku ya nne mfulurizo kati ya pande hizo yaliyoibuka baada ya mapigano hayo kusitishwa kwa muda wa wiki mmoja- mapigano yanayoendelea katika eneo la Rutshuru katika Kivu ya Kaskazini.

MONUSCO ilitangaza kuwa imo katika mapigano ikisaidia upande wa jeshi la Congo FARDC linalopigana na wapiganaji wa M23.

Tanzania ina wanajeshi zaidi ya 800 katika jeshi la MONUSCO kilichopo Mashariki mwa DRC.

Katika taarifa yake iliyotolewa Jumatano usiku, jeshi la DRC, FARDC linaishutumu Rwanda kutuma kikosi chake maalum cha wanajeshi 500 kuwasaidia wapiganaji wa M23, likisema kuwa walikuja wakiwa wamevalia mavazi yenye rangi ya kijani kibichi na nyeusi.

Serikali ya Rwanda kwa imekuw aikikana mara kwa marakuwa inawasaidia M23, ikisisitiza kuwa tatizo lao liko ndani ya nchi yao wenyewe ya DRC.

Kikundi cha M23 Jumatano pia kilitoa tangazo kikiishutumu serikali kwa ‘’kuchagua njia ya vita’’, kwa vikosi vyake kushirikiana na wanajeshi wa MONUSCO na wapiganaji wa kundi linaloshutumiwa na Rwanda kufanya mauaji ya kimbari ya mwaka 1994 la FDLR kuwashambulia.

Tangazo hil la M23linasema: “Kuchagua vita kwa serikali ya Congo badala ya kuchagua mazungumzo ya amani, ni tatizo katika kurejesha amani katika mashariki mwa DRC”.

Wakati huo huo, jeshi la DRC- FARDC limetangaza kuwa maazimio yakikao cha wakuu wa majeshi kilichofanyika Goma ya kubuni kikosi maalumu cha kupigana na makundi ya wanamgambomashariki mwa Congo.

Yatawasilishwa mbele ya kikao cha wataalamu wa masuala ya kijeshi na wakuu majeshiitakayofanyika kati ya tarehe 15 na 19 mwezi huu mjini Nairobi Kenya, kabla ya kuidhinishwa na maraisi wa Kanda.

Chanzo: BBC

raisi yuko royal tour ngoro ngoro
 
Ndio tatizo letu watanzania, kuendekeza ushabiki wa simba yanga, Chadema na CCM hata kwenye ishu nyeti. Ukubwa wa nchi hauna impact kwenye ubora wa kivita. Israel ni taifa dogo sana, angalia anavyosumbua mataifa makubwa ya kiarabu duniani. Angalia Israel inaingia mara ngapi kwa Iran, angalia population yao na iran.

Vita sio ukubwa wa nchi, vita ni mbinu za kimedani, ubora wa silaha, ari ya wanajeshi na intelejensia imara. Ikiwa jeshi lako, lipo wazi kila mtu anajua una nini, mpo wangapi na wapi, basi kukupiga ni jambo la kawaida tu.

Nasisitiza, sio rahisi kuwapiga Rwanda kwa kukurupuka mnaweza kuunguzwa na moto msioujua umetoka wapi.
Waambie na akili iwakae.
 
Back
Top Bottom