Tangu lini yule Bwana angetoka madarakani?Hivi magufuli kama asingekufa na akaendelea na madudu yake haya,halafu akaja kustaafu kama marais wengine,hizi tuhuma zingekuja ibuliwa?na kama zingeibuliwa muhusika angejisikiaje?
Eric Kabendera ni investigative Journalist mwenye kiwango cha juu katika kufuatilia na kuchambua.Pole mkuu watu waliumizwa wengi hadi unajiona huna thamani tena kisa armi ya mtu
Magufuli alikuwa shetani haswaaView attachment 2383359
Serikali imeanza uchunguzi wa ukwapuaji wa mabilioni ya shilingi uliofanywa na Serikali ya Rais John Magufuli, kupitia alichoita, “Sheria ya Plea Bargain," Raia Mwema imeelezwa. Taarifa kutoka serikalini na baadhi ya watu walioswekwa magerezani na kutolewa kwa utaratibu huo, zinaeleza kuwa uchunguzi dhidi ya "mradi huo," unafanywa na Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).
Baadhi ya waathirika ambao hawakupenda kutajwa majina yao gazetini, walithibitisha kuitwa na kufika mbele ya jopo la uchunguzi, katika mikoa mbalimbali nchini. Waathirika hao wanadai kwamba dhana nzima ya plea bargain, iligubikwa na ubabe na kuendeshwa kwa kuangalia kipato cha mtu, badala ya kosa analodaiwa mhusika kulitenda.
Mmoja wa washukiwa waliofanya plea bargain na ambaye alifika mbele ya kamati, alitolea mfano wa kesi yao, iliyokuwa na washitakiwa watatu, kwamba kila mmoja alitoa kiwango cha fedha tofauti na mwenzake.
Alisema: "Mmoja aliambiwa alipe Tsh. milioni 5, mwingine akaambiwa alipe Tsh. milioni 700, lakini mwingine akatozwa Tsh. bilioni moja. Hakukuwa na fomula ya malipo. "Uamuzi ulitegemea wamekuta kiasi gani kwenye akaunti na uwezo ulionao. Yaani si sheria, kiasi utakacholipa kitatokana na utashi wa wenye mamlaka," alisema.
Aliongeza: "Namshukuru sana Rais Samia kwa kuliona hili na kulifanyia kazi. Kuna watu wameugua kwa kupoteza mali zao kwenye jambo hili. Wengine wamekufa na wengine kuhama nchi, kutokana na madhila waliyopata."
Hatua ya serikali ya Rais Samia, kuagiza kufanyika uchunguzi wa uhalali wa jambo hilo na jinsi lilivyoendeshwa, ilitokana na malalamiko kadhaa kutoka kwa wananchi, wakiituhumu Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), kuchukua mali zao kinyume na sheria.
Haijaweza kufahamika mara moja, ni kiasi gani cha fedha kilichokusanywa wakati wa utawala wa Magufuli, ngapi ziliingia kwenye Mfuko Mkuu wa Hazina na kiasi gani kililiwa. Hata hivyo, madai kuwa mamilioni ya shilingi yaliyotolewa yaliishia mikononi mwa wajanja wachache na hata baadhi ya nyumba hazijafikishwa serikalini huku nyingine zikimilikishwa kwa watu binafsi "ndilo gumzo la mjini."
Mchakato wote wa plea bargain, unadaiwa kusimamiwa na kuratibiwa na aliyekuwa DPP, Biswalo Mganga Alisema: "Mfumo mzima ulikuwa hivyo, maelekezo yalitoka juu na kwamba masharti yalikuwa lazima uonekane una makosa. "Tunashukuru Mama (Samia) alipoingia, aliekeza watu wote walioshitakiwa kwa makosa haya na hakukuwa na ushahidi, waachwe huru.
Hakukuwa tena na plea bargain ya aina ile."
Mtoa taarifa hakutaja kwa rnajina waliohama nchi, baada ya kubambikizwa kesi za uhujumu uchumi. Lakini gazeti hili, linaweza kumtaja mfanyabiashara maarufu, Yusuf Manji, aliyekimbilia Marekani na mwandishi wa habari, Erick Kabendera aliye Uingereza. Manji aliyekuwa akilimiki kampuni mbalimbali, alifikishwa mahakamani Februari 2017, alituhumiwa kwa makosa mbalimbali, ikiwamo kutumia dawa za kulevya aina ya heroine na uhujumu uchumi.
Kabendera alituhumiwa kwa makosa matatu ya uhujumu uchumi ikiwamo kujihusisha na genge la uhalifu, kukwepa kodi na utakasishaji fedha alilazimika kuingia 'makubaliano na DPP, kukiri kosa na kumwomba msamaha Rais Magufuli, ili "kupata uhuru wake."
Makosa yote matatu aliyokuwa akituhumiwa nayo, hayana dhamana kwa sheria za Tanzania. Kabendera alikamatwa na Polisi na Uhamiaji, Julai 29, 2019, akidaiwa kuchunguzwa kuhusu uraia wake. Baadaye mawakili wake walitoa taarifa, wakisema Kabendera atashitakiwa kwa kuhusika na ripoti iliyochapishwa katika jarida la The Economist la Uingereza, lakini mahakamani kibao kikageuka na kuwa kesi ya uhujumu uchumi.
Septemba 2019, Bunge lilipitisha muswada wa maboresho ya sheria mbalimbali, ikiwemo ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ambapo mapatano baina ya watuhumiwa na rnwendesha mashitaka yalipitishwa na kusainiwa na Magufuli.
Plea bargain inasimamiwa na vifungu vya 194A hadi 194H vya Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA) ya mwaka 1985, Sura ya 20 na makubaliano yaliyofikiwa yatawekwa katika Kumbukumbu za Mahakama. Kanuni za sheria ya plea bargain, zilisainiwa na Jaji Mkuu Februari 5, 2022. Lakini mamia ya raia wa Tanzania na wa kigeni, walielekezwa kupitia utaratibu huo na DPP tangu mwaka 2019.
Sheria inaeleza katika makubaliano hayo, mshukiwa anaweza kukiri tuhuma au sehemu ya tuhuma dhidi yake, lli kupata afueni fulani ikiwamo kuondolewa baadhi ya mashitaka, ama kupunguziwa muda au aina ya dhabu. Aidha, mshukiwa atatakiwa kula kiapo cha kukubaliana na makubaliano hayo, atapoteza haki ya kukata rufaa, isipokuwa kuhusu urefu au uhalali wa hukumu atakayopewa.
Hata hivyo, wakati utaratibu huo unatumiwa na DPP, Peter Madeleka mmoja wa mawakili mashuhuri nchini, alisema wakati hayo yakifanywa kanuni za plea bargain, zilikuwa hazijaanza kutumika.
"Plea bargain, inasimamiwa na sheria. Wakati Mganga anatekeleza yote haya, kanuni za plea bargain zilikuwa hazijatungwa. Watu "Walianza kukamatwa mwaka 2017 na kutozwa mamilioni ya fedha mwaka 2019, kanun1 zikitungwa mwaka 2021 alisisitiza.
Aliongeza: "Kwa hiyo, vitu vyote vilivyofanyika kabla ya kanuni kutungwa, ni batili. Hili nimekuwa nikilisema siku zote, kwamba haya yaliyofanywa ni haramu tupu." Kuhusu fedha kupelekwa akaunti ya DDP, Madeleka arnbaye aliwekwa gerezani kwa tuhuma za uhujumu uchumi, alieleza kuwa fedha zinapaswa kuhifadhiwa kwenye akaunti ya Msajili wa Hazina.
"Mwenye mamlaka ya kukusanya na kushikilia mali ya Serikali, ni Msajili wa Haz-ina. Sheria ya plea bargain, haimtaji kokote DDP. Kwa hiyo, hilo la kukusanya fedha za watu na kuweka kwenye akaunti yake iliyko. BoT, nalo ni haramu, alieleza.
RAIA MWEMA
BalaaaaaView attachment 2383359
Serikali imeanza uchunguzi wa ukwapuaji wa mabilioni ya shilingi uliofanywa na Serikali ya Rais John Magufuli, kupitia alichoita, “Sheria ya Plea Bargain," Raia Mwema imeelezwa. Taarifa kutoka serikalini na baadhi ya watu walioswekwa magerezani na kutolewa kwa utaratibu huo, zinaeleza kuwa uchunguzi dhidi ya "mradi huo," unafanywa na Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).
Baadhi ya waathirika ambao hawakupenda kutajwa majina yao gazetini, walithibitisha kuitwa na kufika mbele ya jopo la uchunguzi, katika mikoa mbalimbali nchini. Waathirika hao wanadai kwamba dhana nzima ya plea bargain, iligubikwa na ubabe na kuendeshwa kwa kuangalia kipato cha mtu, badala ya kosa analodaiwa mhusika kulitenda.
Mmoja wa washukiwa waliofanya plea bargain na ambaye alifika mbele ya kamati, alitolea mfano wa kesi yao, iliyokuwa na washitakiwa watatu, kwamba kila mmoja alitoa kiwango cha fedha tofauti na mwenzake.
Alisema: "Mmoja aliambiwa alipe Tsh. milioni 5, mwingine akaambiwa alipe Tsh. milioni 700, lakini mwingine akatozwa Tsh. bilioni moja. Hakukuwa na fomula ya malipo. "Uamuzi ulitegemea wamekuta kiasi gani kwenye akaunti na uwezo ulionao. Yaani si sheria, kiasi utakacholipa kitatokana na utashi wa wenye mamlaka," alisema.
Aliongeza: "Namshukuru sana Rais Samia kwa kuliona hili na kulifanyia kazi. Kuna watu wameugua kwa kupoteza mali zao kwenye jambo hili. Wengine wamekufa na wengine kuhama nchi, kutokana na madhila waliyopata."
Hatua ya serikali ya Rais Samia, kuagiza kufanyika uchunguzi wa uhalali wa jambo hilo na jinsi lilivyoendeshwa, ilitokana na malalamiko kadhaa kutoka kwa wananchi, wakiituhumu Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), kuchukua mali zao kinyume na sheria.
Haijaweza kufahamika mara moja, ni kiasi gani cha fedha kilichokusanywa wakati wa utawala wa Magufuli, ngapi ziliingia kwenye Mfuko Mkuu wa Hazina na kiasi gani kililiwa. Hata hivyo, madai kuwa mamilioni ya shilingi yaliyotolewa yaliishia mikononi mwa wajanja wachache na hata baadhi ya nyumba hazijafikishwa serikalini huku nyingine zikimilikishwa kwa watu binafsi "ndilo gumzo la mjini."
Mchakato wote wa plea bargain, unadaiwa kusimamiwa na kuratibiwa na aliyekuwa DPP, Biswalo Mganga Alisema: "Mfumo mzima ulikuwa hivyo, maelekezo yalitoka juu na kwamba masharti yalikuwa lazima uonekane una makosa. "Tunashukuru Mama (Samia) alipoingia, aliekeza watu wote walioshitakiwa kwa makosa haya na hakukuwa na ushahidi, waachwe huru.
Hakukuwa tena na plea bargain ya aina ile."
Mtoa taarifa hakutaja kwa rnajina waliohama nchi, baada ya kubambikizwa kesi za uhujumu uchumi. Lakini gazeti hili, linaweza kumtaja mfanyabiashara maarufu, Yusuf Manji, aliyekimbilia Marekani na mwandishi wa habari, Erick Kabendera aliye Uingereza. Manji aliyekuwa akilimiki kampuni mbalimbali, alifikishwa mahakamani Februari 2017, alituhumiwa kwa makosa mbalimbali, ikiwamo kutumia dawa za kulevya aina ya heroine na uhujumu uchumi.
Kabendera alituhumiwa kwa makosa matatu ya uhujumu uchumi ikiwamo kujihusisha na genge la uhalifu, kukwepa kodi na utakasishaji fedha alilazimika kuingia 'makubaliano na DPP, kukiri kosa na kumwomba msamaha Rais Magufuli, ili "kupata uhuru wake."
Makosa yote matatu aliyokuwa akituhumiwa nayo, hayana dhamana kwa sheria za Tanzania. Kabendera alikamatwa na Polisi na Uhamiaji, Julai 29, 2019, akidaiwa kuchunguzwa kuhusu uraia wake. Baadaye mawakili wake walitoa taarifa, wakisema Kabendera atashitakiwa kwa kuhusika na ripoti iliyochapishwa katika jarida la The Economist la Uingereza, lakini mahakamani kibao kikageuka na kuwa kesi ya uhujumu uchumi.
Septemba 2019, Bunge lilipitisha muswada wa maboresho ya sheria mbalimbali, ikiwemo ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ambapo mapatano baina ya watuhumiwa na rnwendesha mashitaka yalipitishwa na kusainiwa na Magufuli.
Plea bargain inasimamiwa na vifungu vya 194A hadi 194H vya Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA) ya mwaka 1985, Sura ya 20 na makubaliano yaliyofikiwa yatawekwa katika Kumbukumbu za Mahakama. Kanuni za sheria ya plea bargain, zilisainiwa na Jaji Mkuu Februari 5, 2022. Lakini mamia ya raia wa Tanzania na wa kigeni, walielekezwa kupitia utaratibu huo na DPP tangu mwaka 2019.
Sheria inaeleza katika makubaliano hayo, mshukiwa anaweza kukiri tuhuma au sehemu ya tuhuma dhidi yake, lli kupata afueni fulani ikiwamo kuondolewa baadhi ya mashitaka, ama kupunguziwa muda au aina ya dhabu. Aidha, mshukiwa atatakiwa kula kiapo cha kukubaliana na makubaliano hayo, atapoteza haki ya kukata rufaa, isipokuwa kuhusu urefu au uhalali wa hukumu atakayopewa.
Hata hivyo, wakati utaratibu huo unatumiwa na DPP, Peter Madeleka mmoja wa mawakili mashuhuri nchini, alisema wakati hayo yakifanywa kanuni za plea bargain, zilikuwa hazijaanza kutumika.
"Plea bargain, inasimamiwa na sheria. Wakati Mganga anatekeleza yote haya, kanuni za plea bargain zilikuwa hazijatungwa. Watu "Walianza kukamatwa mwaka 2017 na kutozwa mamilioni ya fedha mwaka 2019, kanun1 zikitungwa mwaka 2021 alisisitiza.
Aliongeza: "Kwa hiyo, vitu vyote vilivyofanyika kabla ya kanuni kutungwa, ni batili. Hili nimekuwa nikilisema siku zote, kwamba haya yaliyofanywa ni haramu tupu." Kuhusu fedha kupelekwa akaunti ya DDP, Madeleka arnbaye aliwekwa gerezani kwa tuhuma za uhujumu uchumi, alieleza kuwa fedha zinapaswa kuhifadhiwa kwenye akaunti ya Msajili wa Hazina.
"Mwenye mamlaka ya kukusanya na kushikilia mali ya Serikali, ni Msajili wa Haz-ina. Sheria ya plea bargain, haimtaji kokote DDP. Kwa hiyo, hilo la kukusanya fedha za watu na kuweka kwenye akaunti yake iliyko. BoT, nalo ni haramu, alieleza.
RAIA MWEMA
Hakuna watu wapuuzi kama watanganyika,nyie enzi za Kikwete mlikuwa mnapiga kelele kuwa nchi imevamiwa na mafisadi, mpaka Wapinzani wakafanya maandamano, mpaka Bunge likataka kulipuka Lissu na Zitto wakitoa tuuma za wizi wa IPTL na akina AgeCCo na Richmond,tume kibao ziliundwa watu wakawajibika,hata enzi za Kikwete kuna watu walisamehewa, lakini kwa shariti la kurudisha ela walizozichukua, mpaka Kikwete akaitwa mwizi na dhaifu.Alivyo ingia Magufuli kawashulikia wale waliokuwa wanatumiwa kwa kuwakamata,leo hii eti Magufuli anaonekana mbaya kisa alishughulikia waliokuwa wakipigiwa kelele kuwa wameshindikana,kweli nchi kupata maendeleo ya kweli lazima kizazi hiki cha wanafiki kitoweke,kije kizazi kingine.Udhaifu wa sheria zetu hizi, yaani mtu mmoja anaifanya taasisi ya Rais kama mali ya mama yake na anaangaliwa tu
Kama Bunge lingekuwa na meno na sheria zinafuatwa angetolewa kwa kutokuwa na Imani nae na shtaka juu
Ila kwa nchi masikini na viongozi masikini wa akili na mali na busara basi hakuna namna kila anaekuja anaamua kufanya anavyoamka nayo na hakuna wa kumzuia akisema kesho wote tunakimbia Tutakimbia tu
Kwenye hili unajitoa ufaham kbs 🤣🤣🤣Sheria inasemaje?
Kama watashtakiwa sijui, lakini nilicho ja uhakika ile pesa yote waliyoporwa wale waliotajwa eti ni wahujumu uchumi, marehemu aliichukua kama yake binafsi.Wewe unaamini kabisa hii habari? [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] nakupa muda uje useme hapa nini kinaendelea
Uongozi wa marehemu ulikuwa wa ulaghai mkubwa.Eric Kabendera ni investigative Journalist mwenye kiwango cha juu katika kufuatilia na kuchambua.
Kama angekuwa na kosa la kuchafua nchi, basi tungeona Serikali ikimfungulia mashtaka yanayoendana na Sheria ya Huduma ya Habari au Sheria Cyber crime ya Mwaka 2015.
Kitendo cha kumfungulia mashtaka kwa Sheria ya Kuhujumu Uchumi na kutakatisha fedha ni dhahiri kuwa Eric Kabendera alikuwa ameandika habari za ukweli ambazo Serikali haina majibu. Eric Kabendera ambaye Dikteta alimuweka rumande kwa sababu alikuwa anamkosoa.
Mama wa Eric alikuwa anaishi kwa madawa ya Bei ghali. Yule Bibi alimuomba DIKTETA amuachie mwanaye kwa vile hawezi kuishi bila dawa.
Magufuli hakusikia, na hakumruhusu Eric hata kwenda chini ya ulinzi kumuaga mama yake ambaye alifariki kwa kukosa dawa. Ni nani kwa Watanzania tuliobaki anaweza kutenda kama alivyotenda Magufuli kwa Eric Kabendera na Mama yake? Hakuna, ni hilo dubwasha tu SHETANI la Chato
Hivi kukiwa na kibaka wa kuku, mkampigia kelele, akaondoka. Baadaye akaja wa kuzuia wizi wa kuku, lakini yeye akawa anaiba ng'ombe na kuua wamiliki wa wale ng'ombe, mtatakiwa kunyamaza kwa sababu amezuia wizi wa kuku, na yeye anaiba ng'ombe?Hakuna watu wapuuzi kama watanganyika,nyie enzi za Kikwete mlikuwa mnapiga kelele kuwa nchi imevamiwa na mafisadi, mpaka Wapinzani wakafanya maandamano, mpaka Bunge likataka kulipuka Lissu na Zitto wakitoa tuuma za wizi wa IPTL na akina AgeCCo na Richmond,tume kibao ziliundwa watu wakawajibika,hata enzi za Kikwete kuna watu walisamehewa, lakini kwa shariti la kurudisha ela walizozichukua, mpaka Kikwete akaitwa mwizi na dhaifu.Alivyo ingia Magufuli kawashulikia wale waliokuwa wanatumiwa kwa kuwakamata,leo hii eti Magufuli anaonekana mbaya kisa alishughulikia waliokuwa wakipigiwa kelele kuwa wameshindikana,kweli nchi kupata maendeleo ya kweli lazima kizazi hiki cha wanafiki kitoweke,kije kizazi kingine.
Walioiba Wakati wa Magufuli mwambie Samia hawakamate kama Magufuli alivyokamata wezi wakati wa Kikwete,acheni propaganda wakina Lissu na Silaa na Myika Zitto co,ndio waliotuamanisha wizi ktk Serikali ya Kikwete tena kwa nyaraka na ushaidi, nyinyi naona mnaongea bumba akuna ushaidi wa kuonyesha wizi wa Magufuli labda chuki ndizo zinazowaongoza.Hivi kukiwa na kibaka wa kuku, mkampigia kelele, akaondoka. Baadaye akaja wa kuzuia wizi wa kuku, lakini yeye akawa anaiba ng'ombe na kuua wamiliki wa wale ng'ombe, mtatakiwa kunyamaza kwa sababu amezuia wizi wa kuku, na yeye anaiba ng'ombe?
Hakuna uthibitisho kuwa Kikwete binafsi aliwahi kuiba pesa ya umma, lakini huyi kwa uhakika wa 100% alipora hrla yote waliyoambiwa wahujumu uchumi walipe.
Kuna watu waliiba wakati wa uongozi wa Kikwete kwa sababu ya uungwana wake, lakini walioiba wakati wa Magufuli walifanya hivyo kwa sababu walijua kuwa amewaruhusu.
Alipanga kufia madarakaniHivi magufuli kama asingekufa na akaendelea na madudu yake haya,halafu akaja kustaafu kama marais wengine,hizi tuhuma zingekuja ibuliwa?na kama zingeibuliwa muhusika angejisikiaje?
Kwaiyo singa singa wa IPTL na yeye atarudishiwa pesa za umma?Nilimsoma mahali Samia akisema zitarudishwa sijui process yake itakuwaje.
Koro, trust me hakunaga rais mzuri, hata huyu akitoka watachuguza yakeMama Rais afuatilie na ile miti iliyokatwa Selous pesa ilipelekwa wapi? madudu ni mengi muda ni mchache.
Nchi inaendeshwa kwa utashiMmh ! Nchi yetu inapitia mengi sana asee. Katiba mpya inaweza kuleta ahueni kwa baadhi ya mambo.
Yote kwa yote, Mzee Mwendazake alikuwa na madhaifu yake ila kwenye kuupiga mwingi aliupiga sana. Sasa hivi porojo zimekua nyingi sana kwa mawaziri, Mgao wa Umeme na Changamoto zingine kwa Mzee Magu zilisahaulika. Pumzika kwa Amani Comrade, Mtoto halisi wa Bara la Africa. Kuna mengi maovu yatatajwa na mazuri yako kufunikwa. Mwamba alipambana sana.
Udhaifu wa sheria zetu hizi, yaani mtu mmoja anaifanya taasisi ya Rais kama mali ya mama yake na anaangaliwa tu
Kama Bunge lingekuwa na meno na sheria zinafuatwa angetolewa kwa kutokuwa na Imani nae na shtaka juu
Ila kwa nchi masikini na viongozi masikini wa akili na mali na busara basi hakuna namna kila anaekuja anaamua kufanya anavyoamka nayo na hakuna wa kumzuia akisema kesho wote tunakimbia Tutakimbia tu
Kama ni HAKI yake, YES! utawala wa zuluma umeshapitwa.Kwaiyo singa singa wa IPTL na yeye atarudishiwa pesa za umma?
Badala ya kujibu hoja. Una bwabaja Halafu unaajifanya Ni baba au mama.Watoto wanaweza kukukana kwa sababu hawawezi kurithi IQue ndogo Kama yako.Mungu alikuonea huruma ya kukuwekea kiyenyeoHakuna watu wapuuzi kama watanganyika,nyie enzi za Kikwete mlikuwa mnapiga kelele kuwa nchi imevamiwa na mafisadi, mpaka Wapinzani wakafanya maandamano, mpaka Bunge likataka kulipuka Lissu na Zitto wakitoa tuuma za wizi wa IPTL na akina AgeCCo na Richmond,tume kibao ziliundwa watu wakawajibika,hata enzi za Kikwete kuna watu walisamehewa, lakini kwa shariti la kurudisha ela walizozichukua, mpaka Kikwete akaitwa mwizi na dhaifu.Alivyo ingia Magufuli kawashulikia wale waliokuwa wanatumiwa kwa kuwakamata,leo hii eti Magufuli anaonekana mbaya kisa alishughulikia waliokuwa wakipigiwa kelele kuwa wameshindikana,kweli nchi kupata maendeleo ya kweli lazima kizazi hiki cha wanafiki kitoweke,kije kizazi kingine.
Ni kweli mkuu.Nchi inaendeshwa kwa utashi