Duka la "Plea Bargain" lafungwa, Waliochukuliwa fedha zao waitwa kuhojiwa, uchunguzi waanza

Hivi magufuli kama asingekufa na akaendelea na madudu yake haya,halafu akaja kustaafu kama marais wengine,hizi tuhuma zingekuja ibuliwa?na kama zingeibuliwa muhusika angejisikiaje?
Tangu lini yule Bwana angetoka madarakani?
 
Pole mkuu watu waliumizwa wengi hadi unajiona huna thamani tena kisa armi ya mtu
Eric Kabendera ni investigative Journalist mwenye kiwango cha juu katika kufuatilia na kuchambua.

Kama angekuwa na kosa la kuchafua nchi, basi tungeona Serikali ikimfungulia mashtaka yanayoendana na Sheria ya Huduma ya Habari au Sheria Cyber crime ya Mwaka 2015.

Kitendo cha kumfungulia mashtaka kwa Sheria ya Kuhujumu Uchumi na kutakatisha fedha ni dhahiri kuwa Eric Kabendera alikuwa ameandika habari za ukweli ambazo Serikali haina majibu. Eric Kabendera ambaye Dikteta alimuweka rumande kwa sababu alikuwa anamkosoa.

Mama wa Eric alikuwa anaishi kwa madawa ya Bei ghali. Yule Bibi alimuomba DIKTETA amuachie mwanaye kwa vile hawezi kuishi bila dawa.

Magufuli hakusikia, na hakumruhusu Eric hata kwenda chini ya ulinzi kumuaga mama yake ambaye alifariki kwa kukosa dawa. Ni nani kwa Watanzania tuliobaki anaweza kutenda kama alivyotenda Magufuli kwa Eric Kabendera na Mama yake? Hakuna, ni hilo dubwasha tu SHETANI la Chato
 
Magufuli alikuwa shetani haswaa
 
Balaaaaa
 
Hakuna watu wapuuzi kama watanganyika,nyie enzi za Kikwete mlikuwa mnapiga kelele kuwa nchi imevamiwa na mafisadi, mpaka Wapinzani wakafanya maandamano, mpaka Bunge likataka kulipuka Lissu na Zitto wakitoa tuuma za wizi wa IPTL na akina AgeCCo na Richmond,tume kibao ziliundwa watu wakawajibika,hata enzi za Kikwete kuna watu walisamehewa, lakini kwa shariti la kurudisha ela walizozichukua, mpaka Kikwete akaitwa mwizi na dhaifu.Alivyo ingia Magufuli kawashulikia wale waliokuwa wanatumiwa kwa kuwakamata,leo hii eti Magufuli anaonekana mbaya kisa alishughulikia waliokuwa wakipigiwa kelele kuwa wameshindikana,kweli nchi kupata maendeleo ya kweli lazima kizazi hiki cha wanafiki kitoweke,kije kizazi kingine.
 
Wewe unaamini kabisa hii habari? [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] nakupa muda uje useme hapa nini kinaendelea
Kama watashtakiwa sijui, lakini nilicho ja uhakika ile pesa yote waliyoporwa wale waliotajwa eti ni wahujumu uchumi, marehemu aliichukua kama yake binafsi.

Na hilo nililifahamu wakati marehemu akiwa hai.

Lakini pia aliyemwamini, alimpiga marehemu kwa kupeleka pesa pungufu maana wapo waliokuwa wanatajiwa kiwango cha juu cha kulipa, wakisema hawana, anawapunguzia, wanalipa, lakini karatasi za kusaini zikawa zinaonesha kiwango pungufu zaidi ya kile walichokilipa.

Pesa yote, hakuna hata milioni 1 iloypingia kwenye akaunti ya Serikali, benki kuu au mahakama. Na ilikuwa marufuku kulipa kwa cheque au bank transfer, unapeleka pesa cash.
 
Uongozi wa marehemu ulikuwa wa ulaghai mkubwa.

Kuna watu aliokuwa amewaruhusu waibe (akina Bashite, Sambaya, Mgamga, n.k.). Na kuna watu ambao hata wasipofanya kosa lolote aliwatafutia makosa kuhakikisha wanajuta.
 
Hivi kukiwa na kibaka wa kuku, mkampigia kelele, akaondoka. Baadaye akaja wa kuzuia wizi wa kuku, lakini yeye akawa anaiba ng'ombe na kuua wamiliki wa wale ng'ombe, mtatakiwa kunyamaza kwa sababu amezuia wizi wa kuku, na yeye anaiba ng'ombe?

Hakuna uthibitisho kuwa Kikwete binafsi aliwahi kuiba pesa ya umma, lakini huyi kwa uhakika wa 100% alipora hrla yote waliyoambiwa wahujumu uchumi walipe.

Kuna watu waliiba wakati wa uongozi wa Kikwete kwa sababu ya uungwana wake, lakini walioiba wakati wa Magufuli walifanya hivyo kwa sababu walijua kuwa amewaruhusu.
 
Walioiba Wakati wa Magufuli mwambie Samia hawakamate kama Magufuli alivyokamata wezi wakati wa Kikwete,acheni propaganda wakina Lissu na Silaa na Myika Zitto co,ndio waliotuamanisha wizi ktk Serikali ya Kikwete tena kwa nyaraka na ushaidi, nyinyi naona mnaongea bumba akuna ushaidi wa kuonyesha wizi wa Magufuli labda chuki ndizo zinazowaongoza.
 
Mmh ! Nchi yetu inapitia mengi sana asee. Katiba mpya inaweza kuleta ahueni kwa baadhi ya mambo.
Yote kwa yote, Mzee Mwendazake alikuwa na madhaifu yake ila kwenye kuupiga mwingi aliupiga sana. Sasa hivi porojo zimekua nyingi sana kwa mawaziri, Mgao wa Umeme na Changamoto zingine kwa Mzee Magu zilisahaulika. Pumzika kwa Amani Comrade, Mtoto halisi wa Bara la Africa. Kuna mengi maovu yatatajwa na mazuri yako kufunikwa. Mwamba alipambana sana.
 
Nchi inaendeshwa kwa utashi
 

Hivi kumbe haya yalifanywa chini ya sheria!!?
 
Badala ya kujibu hoja. Una bwabaja Halafu unaajifanya Ni baba au mama.Watoto wanaweza kukukana kwa sababu hawawezi kurithi IQue ndogo Kama yako.Mungu alikuonea huruma ya kukuwekea kiyenyeo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…