Duniani kote usafiri wa reli ndiyo rahisi kuliko wote. SGR tulitegemea kuwa kiama cha usafiri wa mabasi na malori, imeshindikana

Duniani kote usafiri wa reli ndiyo rahisi kuliko wote. SGR tulitegemea kuwa kiama cha usafiri wa mabasi na malori, imeshindikana

~ Hivyo ndivyo ingalikuwa kwa usafirishaji wa abiria. Trip moja ya passenger train yenye urefu wa si chini ya kilomita 3 ingalikuwa sawa na mabasi yasiyopungua 500 na wangalisafirishwa kwa raha kwa spidi ya 170 kph.
Sasa ulijaribu kufikiria economic impact ya kuondoa hayo mabasi 500 barabarani?!

Ni madereva wangapi hao ambao utaondoa ajira zao?

Utakuwa umeondoa ajira za makonda wangapi?

Utakuwa umeondoa ajira za wakata tiketi wangapi?

Itakuwa umeathiri soko la Mama Lishe wangapi?

Turudi kwenye macroeconomic...

Utakuwa umepunguza lita ngapi za mafuta ambazo zingetumika na hayo mabasi 500... mafuta ambayo yangeleta kodi?!

Ungeathiri kodi ya kiasi gani ya uagizaji mabasi kwa siku za baadae?!

Uchumi hauendi hivyo...
 
Mkiu hebu nitonye jina la huyo mmiliki maana amanikwaza natamani niruke nae
Watoa maamuzi wengi ndo wenye makampuni ya usafirishaji. Wapo kuanzia bungeni na kwingineko.

Hivi unategemea mtu kama huyu atasema nini when it comes to kuamua nauli na uebdeshaji wa reli?
 
Hizi treni zetu ni za mwendo wa kawaida kwa ulimwengu wa leo. Hizo za enzi za Hitler tulizokuwa tunatumia, dunia ya sasa walisha achana nazo.

Treni ya maximum speed ya 160 kph (sawa na ya Noa) ndiyo ya kawaida tu. Hizo za maximum speed ya 40 kph kama zile tulizo nazo ni za dunia ya kale, na lengo letu ni kuzi phase out tutakapokamilisha ujenzi wa reli yenye geji inayotakiwa. Hatutakuwa tena na hiyo MGR maeneo ambako SGR imekamilika. MGR ya kwenda Kilimanjaro hadi Arusha ndiyo itakuwa ya mwisho kuwa phased out. Huu ndiyo ukweli na msema kweli ni mpenzi wa Mungu.

Hizo za mwendo wa haraka unazosema zinaitwa bullet trains. Zinakimbia mwendo kasi wa kuanzia 350 kph hadi 650 kph. Yaani ni ndege za chini. Kwa speed hiyo kubwa nyingi zake huelea tu juu ya reli by magneto, hazina magurudumu - no friction energy loss. Zingine zinazungukwa na vacuum, yaani zinapaa ndani ya vacuum, hazipambani na upepo kama zile ndege za angani. Zinavuta mabehewa machache sana, ni za abiria tu na ni kwa safari fupi fupi tu na hasa kama usafiri wa mijini. Sisi hatuna mpango wa kuleta treni za aina hiyo, kwanza hata hii SGR haina uwezo wa kuzipitisha (support). Hata huko ulaya na kwingineko ziko chache sana tu na zingine bado ziko kwenye majaribio/ utafiti - wanataka ziweze kukimbia kwa zaidi ya spidi ya 1,000 kph.
Aliyekudanganya nani hiyo MGR itaondolewa, huoni reli imeboreshwa na kuzidi kuboreshwa kutoka 45,56, 60 pounds hadi 80 pounds huoni zinanunuliwa advanced diesel electric locomotives, huoni yananunuliwa mabehewa mapya ebu acha kupotosha watu.

South Africa wana meter gauge, cape gauge na standard gauge hadi leo hii, ukitazama India wana standard gauge, broad gauge na bado hiyo meter gauge hawajaicha.

Kuna haja gani ya kufanya maboresho makubwa ikiwa wanahitaji kuiacha hiyo reli fuatilia kwanza ndo uandike siyo unakurupuka.
 
Huko hawatumii treni kama hizi za kwetu zenye spidi hii ya kinyonga inayolingana na spidi ya Vitz au Noah. Za kwao ni ndege za chini zinazo fly over the rail in vacuum at a speed of an aeroplane, my dear. Na hazisimami simami njiani. Ni city to city only. Za kwetu ni za kawaida tu za walala hoi. Engine na mabehewa yake yanaweza kuwa adjusted upana na kuweza kutembea kwenye reli ya MGR yakitumia dizeli kama ulivyoyaona yakichapa kazi juu ya MGR baada ya kuwasili nchini hivi karibuni.
Yale mabehewa hayajawa adjusted katika Axle. Yametoka huko South Korea hivyo hivyo na axle yenye 1000mm kwa ajili ya kuhudumu katika reli ya meter gauge. Hao viongozi wenu tu ndiyo wamejichanganya namna ya kuuleza umma wa watanzania.

Manufacturer yeye anapewa specifications anakutengenezea kitu kwendana na hitaji lako yapo ya meter gauge na yapo ya standard gauge vile vile, uliyoyaona yanafanyiwa test juzi kati yale ni ya meter gauge Mzee.
 
Yale mabehewa hayajawa adjusted katika Axle. Yametoka huko South Korea hivyo hivyo na axle yenye 1000mm kwa ajili ya kuhudumu katika reli ya meter gauge. Hao viongozi wenu tu ndiyo wamejichanganya namna ya kuuleza umma wa watanzania.

Manufacturer yeye anapewa specifications anakutengenezea kitu kwendana na hitaji lako yapo ya meter gauge na yapo ya standard gauge vile vile, uliyoyaona yanafanyiwa test juzi kati yale ni ya meter gauge Mzee.
Yamekuja ya SGR na pamoja na ya MGR ila rang za behewa zinafanana na muundo ndo mana watu wanachanganya fatlia page za TRC utaona utofauti
 
Reli ya Uhuru aliyotujengewa mkoloni tumeishidwa itakuwa hii SGR.

Tanzania tunatumia 1% ya uwezo wetu wa kufikiri...hii yaweza kuwa kweli.
Akili hizi ndiyo napenda kuzisikiliza maoni yake, mfano reli ya TAZARA tu ilikamilika ikiwa advanced kuliko ile ya kati ya mkoloni kaitazame leo inasikitisha mno.

Sasa tunajengewa reli ambayo ipo very advanced kuliko ile katika mambo mbali mbali ngoja Korail wamalize muda wa kuisimamia waachiwe wabongo uone shoo yake.
 
Wapi duniani usafiri wa treni ya haraka bei rahisi? Tupe mfano wa nchi 3 tu duniani?

Mtu uko Chato huko hata Dubai tu hujafika unaleta uongo wako hapa.
Hebu usiwe mjinga ww nimepanda Treni kutoka hongkong mpaka china lakin pia nimepanda train za under ground kama dala dala duniani pote trein ndio usafiri rahisi sio kila kitu kupinga Pinga tu na aslimia kubwa hizo treni wanafanya kama huduma kwa jamii sio biashara
 
Yamekuja ya SGR na pamoja na ya MGR ila rang za behewa zinafanana na muundo ndo mana watu wanachanganya fatlia page za TRC utaona utofauti
Yah sijakataa yapo SGR na MGR ila ambayo yameanza test ni ya MGR kwa 400km yani kutoka Dar to Moro (200km) na kurudi.
 
Vya dezo kwa lipi? Kwani hiyo SGR na hizo treni zimegharimiwa na nani?

Kwa taarifa yako huo mradi ni wa wananchi wote wa Tanzania. Wao ndiyo wameugharimikia na wataendelea kuugharimia kupitia kodi zao.

Si mali ya hao wajanja wachache pekee yao. Wananchi ndiyo wenye mamlaka ya kupanga hiyo nauli ya treni yao na siyo hao akina Kadogosa, Mbawala na wafanya biashara za mabasi na malori.

Hilo jina ulilotaja baada ya Kadogosa kuna mzee mmoja rafiki yangu sana msukuma ni contractor mnene sanaaaa halafu huwa havai suruali akiwa home anavaa shuka tu halafu anavaa kandambili kubwaaa, na hua hanywi chai anakunywa uji tu halafu ananywea kwenye sufuria, na mwisho kabisa ana mapengo, hana meno matatu matatu juu na chini ndo hua nae hilo jina analitaja hivyo kama wewe sasa nimejisikia kumkumbuka sana, nashukuru sana kwa kuipendezesha siku yangu.[emoji1317][emoji1317]
 
Watoa maamuzi wengi ndo wenye makampuni ya usafirishaji. Wapo kuanzia bungeni na kwingineko.

Hivi unategemea mtu kama huyu atasema nini when it comes to kuamua nauli na uebdeshaji wa reli?
NImekuelewa mkuu, na sasa naona kuna mzigo mpya wa majenereta umeingia
 
Duniani kote usafiri wa reli ndiyo usafiri wa bei rahisi sana kuliko usafiri mwingine wowote. Malengo makuu ya kuboresha usafiri huu kwa kiwango cha SGR yalikuwa:

~Trip moja ya treni ya mizigo ingaliweza kusafirisha mzigo wa sawa na semi-trailers za malori 500 kwa mara moja, kwa spidi ya 120 kph na kwa bei ya sawa na bure ukilinganisha na malori.

Yaani mzigo wa ukubwa huo wa semi trailer 500 ungeweza kuondolewa kutoka bandari yetu ya Dar es Salaam kila siku na kufikishwa Mwanza au Kigoma ndani ya masaa 10 au 12 tu. Hakungalikuwa tena na mrundikano wa mizigo pale bandari ya Dar es Salaam.

Hata hizo bandari kavu zilizoko mkoa wa Dar es Salaam zingalikosa kazi. Bandari kavu zingalijengwa Mwanza na Kigoma. Uchumi wa nchi ungepaa kwa kasi kubwa na ndani ya muda mfupi tungeifikia Singapore ambayo uchumi wake unategemea bandari tu.

Barabara zetu zingalidumu zaidi kwani usafiri wa malori unalifikia kiama chake. Hata hizo ajali lukuki za barabarani zinazosababishwa na malori haya katika njia hizi kuu zingalifikia tamati. Traffic police wetu wangetafutiwa kazi zingine.

~ Hivyo ndivyo ingalikuwa kwa usafirishaji wa abiria. Trip moja ya passenger train yenye urefu wa si chini ya kilomita 3 ingalikuwa sawa na mabasi yasiyopungua 500 na wangalisafirishwa kwa raha kwa spidi ya 170 kph.

Yaani kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza au Kigoma ni mwendo wa saa 7 tu, kwa bei ya chee ukilinganisha na mabasi ambayo nayo yalikuwa yafikie kiama chake kwa njia hizi kuu za uchumi wa nchi na kuokoa uharibifu wa barabara zetu na ajali lukuki za barabarani. Uchumi wa nchi ungalipaa na wananchi wangalipata furaha.

Bahati mbaya kabisa matarajio hayo ya wananchi yameshindikana kufikiwa. TRC imepanga nauli za train hizo za spidi kubwa kuwa mara tatu ya bei za usafiri wa mabasi. Kwa sasa mtu anasafiri kwa basi kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza kwa nauli ya Sh 55,000 hadi 65,000.

Hii ni nauli ya kupanda kwa mafuta kwa sababu ya Ukraine. Kabla ya hapo ilikuwa Shs 35,000 hadi 45,000 na tunategemea hiyo Ukraine itakapokwisha bei hizi zitarejea. Sasa TRC wamepanga ziwe Sh 150,000 kwani hadi Dodoma tu ni Sh 75,000. Yaani ni karibu sawa na nauli ya ndege. Hawa Waha na Wasukuma wetu kweli watazipanda hizo treni?

Bado TRC hawajatoa nauli za mabehewa ya mizigo. Kwa mantiki hiyo hiyo bei inayotarajiwa ni mara tatu ya bei ya kukodi lori la semi trailer. Hivyo tutegemee mambo kubaki kama kawa. Matajiri wa malori na mabasi wamekataa kufika kiama.

Wameshinda hiyo vita na inasemekana hata hizo treni za SGR zitaendeshwa na wafanya biashara binafsi kwa mtindo wa PPP (private public partnership)! Ni wajanja, wametupokonya SGR yetu tuliyoijenga na tunaendelea kuijenga kwa kodi zetu. Zingine tumekopa lakini tutazirejesha kwa kodi zetu.

Mapendekezo:
1. Nauli ya abiria kutoka Dar had Mwanza isizidi Sh 25,000 kwa economy class. Yaani isizidi nusu ya nauli ya basi. Hayo madaraja mengine mnaweza kuweka mnavyotaka. Hao wanaoishia njiani hususani Dodoma ziende kwa uhusiano huo wa umbali hadi Mwanza.

2. Behewa la mizigo bei yake isizidi theluthi moja ya bei ya kukodi lori.

3. Hakuna mantiki ya kuwa na tofauti ya nauli kati ya MGR inayotumia dizeli na SGR inayotumia umeme. Kwa vyovyote vile uendeshaji (running cost) ya ile ya umeme ni rahisi kuliko ile ya dizeli.

TRC lazima ijue kuwa jukumu lake ni kutoa huduma na si biashara ya kutaka kurejesha kile serikali imewekeza kwenye huo mradi wa SGR. Wanachotakiwa ni kukusanya tu pesa itakayowawezesha kulipa mishahara ya staff wao na mambo mengine ya uendeshaji.
Watu kama wewe, mwendazake aliwapenda sana , maana bila hata kutumia common sense mnaleta suluhisho
Reli ni usafiri nafuu sana , ila inategemea na yo topography ya nchi husika , kuna muda reli inakuwa ni expesiive option .
Kwa nchi kama Tanzania ambapo kuna mazao kusini na soko lipo kanda ya ziwa , bandari mashariki inayohudumia kaskazini kusini na magharibi, makaa ya mawe kusini ambayo yanasafri kwenda pande zote, Reli haiqezi.kuleta suluhisho la kudumu wala unafuu, pendekezo la nauli za sgr zimewastua usingizini, the elites walishajua kuwa sgr haiwezi kuwa reli nafuu
 
Wapi duniani usafiri wa treni ya haraka bei rahisi? Tupe mfano wa nchi 3 tu duniani?

Mtu uko Chato huko hata Dubai tu hujafika unaleta uongo wako hapa.
Hata shuleni tumesomea hivyo,usafiri wa treni na meli ni bei rahisi na rafiki wa mazingira ulilinganisha na barabara,sema wewe unareta uchawa kwenye mambo ya msingi
 
So far so good, SGR popote duniani ni almost 3/4 ya tiketi ya ndege ila sio SGR ya kusimama simama kila mahali .

Pili SGR ya kusimama kila mahali bei ni bei ni ndogo zaidi
Kwan kuna tren ambazo zinaenda bila vituo kama ndege
 
Nchi hili ni la kipumbavu! Wamiliki wa malori na mabasi ni hao hao vingozi wa serikali sasa wanaona kabisa wakiiacha SGR ifanye inavyotaka watakosa wateja ndiyo maana wanafanya kila liwezekanalo kuihujumu! Na hili li maushungi linalaza mimacho tu! Bure kabisa!
 
Hizi treni zetu ni za mwendo wa kawaida kwa ulimwengu wa leo. Hizo za enzi za Hitler tulizokuwa tunatumia, dunia ya sasa walisha achana nazo.

Treni ya maximum speed ya 160 kph (sawa na ya Noa) ndiyo ya kawaida tu. Hizo za maximum speed ya 40 kph kama zile tulizo nazo ni za dunia ya kale, na lengo letu ni kuzi phase out tutakapokamilisha ujenzi wa reli yenye geji inayotakiwa. Hatutakuwa tena na hiyo MGR maeneo ambako SGR imekamilika. MGR ya kwenda Kilimanjaro hadi Arusha ndiyo itakuwa ya mwisho kuwa phased out. Huu ndiyo ukweli na msema kweli ni mpenzi wa Mungu.

Hizo za mwendo wa haraka unazosema zinaitwa bullet trains. Zinakimbia mwendo kasi wa kuanzia 350 kph hadi 650 kph. Yaani ni ndege za chini. Kwa speed hiyo kubwa nyingi zake huelea tu juu ya reli by magneto, hazina magurudumu - no friction energy loss. Zingine zinazungukwa na vacuum, yaani zinapaa ndani ya vacuum, hazipambani na upepo kama zile ndege za angani.

Zinavuta mabehewa machache sana, ni za abiria tu na ni kwa safari fupi fupi tu na hasa kama usafiri wa mijini. Sisi hatuna mpango wa kuleta treni za aina hiyo, kwanza hata hii SGR haina uwezo wa kuzipitisha (support). Hata huko ulaya na kwingineko ziko chache sana tu na zingine bado ziko kwenye majaribio/ utafiti - wanataka ziweze kukimbia kwa zaidi ya spidi ya 1,000 kph.
Dr Akili naona unalitendea haki hilo jina lako. Naona kabisa unawajibu kwa facts hawa wanaokujibu kwa dhihaka. Wakati wenzako wanataka upanic ili muanze kutukanana mpigwe ban hii thread ionekane takataka [emoji23][emoji23][emoji23].. Akili nyingi [emoji848]
 
Hebu usiwe mjinga ww nimepanda Treni kutoka hongkong mpaka china lakin pia nimepanda train za under ground kama dala dala duniani pote trein ndio usafiri rahisi sio kila kitu kupinga Pinga tu na aslimia kubwa hizo treni wanafanya kama huduma kwa jamii sio biashara
Bahasha zinaangamiza Taifa ndugu yangu!
 
Mi naona tunatoka kwenye ujamaa taratibu na tunatakiwa tutoke uko kabisa ili watu wawe serious na Maisha. MTU unakuta anazaa watoto 11 alafu Kwa mke mmoja alafu anawake watatu bhado wa njee alafu ni maskin wa kutupwa sasa hao matoto Yao ndo yanata kilakitu serikali iweke vya burebure lakin hawaangali matrilioni ambayo serikali imetumia zikiaribika utawaona uku jfee wanatukana serikali. Kama MTU unaona ni gali panda basi zako ulizozoea kwan kuna mkoa ambao bhas alifiki, siyo lazma upande Tu kwasababu ni kitu kipya kimekuja panda basi.
 
Back
Top Bottom