Duru: Hatima ya Muungano na dalili za kuvunjika mapema

Duru: Hatima ya Muungano na dalili za kuvunjika mapema

MTAZAMO WA UPANDE WA PILI WA WAZANZIBAR

Video za awali zimeonyesha kundi moja linalotaka uwepo wa serikali 3.
Hili ni la kamati ya maridhiano
Kwa upande wa pili, lipo kundi la wazanzibar wanaotaka muundo wa sasa wa muungano uendelee

Kundi la pili halina hoja ya wazi kwanini wanaotaka serikali .
Hoja zao zimejificha katika ukweli kuwa Zanzibar inahitaji muungano kuliko ilivyokuwa inadai na watu wa kundi hilo hilo siku za nyuma.


Hoja zao zimesaidia kuelewa madai ya wazanzibar kuhusu kuonewa au kupunjwa katika muungano

Hoja zaio zimesadia pia kuwaeleza Watanganyika, ni wapi na kwanini Zanzibar ni mzigo katika muungano

Tuangalie video hizi za mkutano tukiwanukuu wasemaji bila kuwawekea maneno kama tulivyoangalia upande wa kwanza. https://www.youtube.com/watch?v=YthCo16Bx-0

https://www.youtube.com/watch?v=k6qUyt7dMLA

Video ya kwanza, Muongeaji kwa jina la Najma ni mwanasheria.
Najma anasema iliyokuwa rasimu ya Warioba iliacha suala la Elimu kama suala la muungano.


Najma akasema, uwepo wa Polisi wa nchi shirikishi utatengeneza mvutano.
Kwamba, Rais wa shirikisho atakuwa na nguvu sawa na za washirika na hivyo maamuzi kuwa magumu.
Najma anasema, rasimu ya Warioba ilipendekeza iwapo jambo linaongezwa au kupunguzwa ni lazima iwepo kura ya maoni, na hilo litaongeza gharama

Hoja zetu:
Katika video ya pili, wazungumzaji wafuatao walizungumzia suala la elimu ya juu .


Dakika ya 5, mzungumzaji amesema faida za muungano ni elimu ya juu inayodhaminiwa na Tanganyika.
Kasema bila hivyo wanafunzi 6,000 wa znz hawatapata nafasi.


Hamis Hajidakika ya 12 anasema, mikopo wanapata kupitia muungano.
Hata kozi zisizotolewa znz bado wanapata bara kwa mikopo ya bara.


Dakika ya 22 Machano kaongelea HESLB kama bodi inayotoa mikopo kwa wznz na ni faida kwao

Wazungumzaji wote wameongelea mikopo na elimu ya juu kama suala la muungano.
Na ni wznz waliolalamika mambo ya muungano kuongezwa kinyemela. Elimu halijawahi kuwa suala la muungano.


Pamoja na hao, kwa upande mwingine wznz wanalalamika kuwa muungano umedumaza elimu znz.
Haya kayasema mzee Maulidi katika video hii https://www.youtube.com/watch?v=PCwc-W8mIuA dakika ya 50


Hivyo, wznz wanaposema elimu ya juu ni kero ni makosa. Wznz wanapodai muungano umevuruga elimu ya znz ni makosa.
Elimu si jambo la muungano, na wao wanalitaka liwe la muungano,nyuma ya pazia wanalipiga vita.
Hapa hoja kubwa ya wznz ni nini?


Elimu ya juu ni ufadhili tu wanaoupata kutoka Tanganyika .
Ndiyo msingi wa tume ya Warioba kuliondoa suala hilo katika mambo ya muungano kama walivyodai wznz.
Ni vema kama wangeangalia hoja za tume ya Warioba kwa kuzingatia matakwa yao
bila malalamiko yasiyo na uhahidi

Kwanini tunasema ni ufadhili. Majibu wanayatoa wznz wenyewe katika video hii https://www.youtube.com/watch?v=k6qUyt7dMLA Katika dakika ya 12 Haji Hamis anasema, iwapo kutakuwa na serikali 3, znz itaweza kuchangia nini?

Na akahoji, je wakishindwa si muungano utavunjika.
Hams akasema huko nyuma serikali ya Mkapa ililipa madeni ya SMZ, sasa kukiwa na serikali 3 nani atalipa madeni hayo?



Mchangiaji Machano katika dk ya 22 anasema, znz ikiambiwa ichangie asilimia 25 tu ya muungano, katika bajeti ya Bilioni 600 watachangia nini?

Zuberi katika dk 45 anasema, katika mwezi mzuri wa makusanyo znz inakusanya bilioni 14, anasema hata kama znz itaambiwa ichangie wanajeshi wastaafu tu kuwalipa, haitaweza.

Hayo ni maoni yao, lakini yana maana sana yakitazamwa kwa jicho la pili


  1. Ile hali ya madai kuwa znz inapunjwa, sasa inajijibu yenyewe. Kwamba, wao ndio wafaidika wa huu muungano.
    Hakuna hata mzungumzaji mmoja aliyeonyesha wapi wanapunjwa na kwa njia zipi,
  2. Inatoa fursa kwa Watananyika kuelewa ni kwa jinsi gani huu muungano unavyokuwa mzigo kwao.
    Tunaona wakidai huduma ambazo hawana mchango nazo.

    Katika dakika ya 45 Omar Zuber anasema ''sisi tunaweza kwenda kupata ardhi Tanganyika kwa kutumia Utanzani, lakini wao hawawezi kuja kupata ya znz kwasababu si wznz'' Hoja ya Utanzani wameitumia pia katika suala la elimu.
    Hapa inaeleza kuwa wznz ni Watanzania pale wanapohitaji kukidhi haja zao.
    Wote kwa pamoja ni wznz pale wanapokuwa na masilahi yao wenyewe.


Wazanzibar wanadai huu ni muungano wa nchi mbili na hivyo kunatakiwa usawa. Jambo wanalokubali ni kuwa katika muungano huu hawana mchango kwa mujibu wa wazungumzaji wenyewe, angalia dk 30 Omari Ali Omar anavyosema.

Usawa wa muungano unapatikanaje kama hakuna usawa katika kuhudumia muungano huo?
Lakini muhimu zaidi, ni wznz kutambua kuwa kile wanachokiita kero, si kero ni madai.
Hapa pa la kujiuliza, inawezakanaje uombe halafu udai kama haki?



Itaendelea..
 
MTAZAMO
Inaendelea

Kwa muda mrefu wzn wamelalamika kuhusukuongezwa mambo ya muungano hadi 22 na 47 kwa kunyumbulishwa.
Awali mambo ya mkataba wa muungano yalikuwa 11.
Tume ya Warioba imepunguza hadi 7 ili kutoa nafasi kwa nchi washirika kujitawala.

Kitendo cha wznz kudai elimu ya juu iwe sehemu ya muungano ni kwenda kinyume na madai yao ya ‘unyemela' wa kuongeza mambo ya muungano.
Wanafunzi 1024 wa znzwanaodhaminiwa na bodi ya mikopo HESLB wanachukua nafasi za wanafunzi waTanganyika.
Zanzibar ina bodi yake ZHSEL ambayo Mtanganyika hana nafasi.


Wznz wanadai nafasi hizo kwasababu ni Watanzania. Katika muundo wa S2, Watanganyika hawana nafasi ya kudai Utanganyik awao kwa manufaa yao. Inapotokea watoto 1024 wa Tanganyika wakanyimwa fursa kwasababu zimekwenda Zanzibar, huko ni kuwanyima haki yao.

Tumesema mara nyingi na tunasisitiza tena,kati ya wanafunzi 1024 wanaopata mikopo kutoka znz hakuna anAyerudisha mikopo hiyo HESLB.
Mikopo inakwenda znz kama ufadhili, ili hali walipa kodi waTanganyika si tu wananyimwa nafasi zao bali pia wanapaswa kurudisha mikopohiyo.


Ni mfumio huo usioitambua Tanganyika, ndiou natumika katika mambo mengine. Kwa mfano, wznz hawana bajeti ya ulinzi nausalama.
Msemaji Najma katika video alisema wazi kuwa kutenganisha polis ikutaleta mtafaruku. Hakueleza ukweli kuwa kutaondoa utegemezi wa znz katika hilo.


Waziri muungano Samiya, anasema sualala kodi limepatiwa ufumbuzi. Kwamba znz inapata Bilioni 1.2 za kodi zawafanyakazi wa muungano.
Hapa tujiulize, SMZ inapata kiasi gani kutoka kwawafanyakazi wake 10,000?

Ni wazi kuwa kodi za wafanyakazi wa SMZ hazifiki hatamilioni 200. Sasa iweje wapewe Bilioni 1.2 ambazo ni kodi za wafanyakazi waTanganyika?


Mzungumzaji Najma kasema katika video kuwa,kutenganisha benki na kuwa na bank kuu ya washirika kwa mujibu wa tume yaWaroba, kutapunguza mafao kwa znz. Hapa ana maana znz inapata 4.5%ya pato la Tanganyika kutoka BoT, pesa ambazo, znz inazipata bila maelezo ya kueleweka

Ipo hoja dhaifu sana ya mikopo na misaada kama ndio mchango wa znz. Hoja hii inajibika kwa hali ya leo.
Wahisani wamezuiapesa zao, lakini znz inaendelea kupata 1.2B za watumishi wa muungano na 4.5%ya kodi zinazokusanywa Tanganyika.


Ni kodi za Tanganyika kwasababu waziri wa fedha, Saada Nkuya na waziri wa muungano katika mkuatano wa CCM naShein(angalia video mabandiko yaliyotangulia) wamekiri kodi za znz zinabaki huko huko(TRA).

Na zaidi ya hapo wamekiri kuwa wafanyakazi wa TRA znz wanalipwa na TRA makao makuu.
Hii maana yake, kodi zao zinatumika kwa ajili ya maendeleo yao, kodi za Watanganyika zinatumika kwa ajili ya mishahara yawafanyakazi wanaokusanya kodi za znz kwa ajili ya znz


Haya ni mambo yanayoonekana ni madogo, hata hivyo mbele ya safari yatakuwa na madhara makubwa sana.
Kwa mfano, hakuna mkoa wa Tanganyika unaopata mafao wanayopata wznz kwa mwezi/mwaka.

Na hakuna mkoa unaoweza kulinganishwa kwa mchango wake katika pato la taifa na znz.


Hata mkoa mdogo au wenye uchumi mdogo bado una mchango mkubwa kuliko znz. Hili wanasema wenyewe na takwimu zote ikiwemo za BoT/TRA zinaonyesha, znz haina mchango kwa pato la Tanzania

Watanganyika wajiulize, ni kwa faidagani hasa zinazowasukuma kuwanyima watu wao kwa ajili ya wananchi wa taifa jingine?

Znz ni taifa jingine kwa vile ina kila kitu chake tofauti na sehemu nyingine ya Tanzania.
Na wznz hujanisibu wao si Watanzania, isipokuwa pale tu wanapohitaji jina hilo kwa mafao yao.
Hali hii inajenga chuki isiyo ya lazima

Katiba ya 1977 ambayo imeandikwa upya naChenge/Samwel Sitta haijatoa majibu ya matatizo.Tume ya Warioba kwailikuja na suluhisho la tatizo.

Ndio maana tunasema kujadili katiba ya Chenge ni kushangilia madhara ya muungano. Katiba ya Chenge haipaswi kujadiliwa hata aya moja.


Kwa bahati mbaya ni wznz wanaotaka mamlaka kamili, na wanaolaani muungano ndio wamegeuka kuwa mabingwa wa katiba ya Chenge

Katiba ya Chenge imetengenezwa kwa ajili yakulinda mafisadi, si kuwapa nafasi wznz au kutoa majibu ya ya muungano makubwa kuliko ilivyokuwa.

Challenge kubwa ya muungano haipokwa wznz . Wznz wametambua bila shaka, ndani ya muungano umuhimu wao si kama walivyokuwa wameaminishwa.

Hoja kubwa zipo kwa Watanganyika, ambao kwasasa wameona, ndio wanaoubeba mzigo wa muungano, na ndio wanaohudumia serikaliya nchi jirani ya znz kwa gharama za watu wake.

Na muhimu zaidi, wanajiuliza katika dunia ya leo, umuhimu wa kuwa na znz ni upi hasa ?

Ikifika hapo, hatima ya muungano inaweza kutimia haraka, ni suala la muda
 
Nguruvi3,

Mkuu wangu katika hoja zoote unazoandika humu hili la Uzanzibar na Utanganyika kusema kweli huwa unanishangaza sana kwa sababu unashindwa kuelewa maana isipokuwa unaitazama nafsi yako wewe kama mume katika ndoa dhidi ya mkeo basi...Unatumia uume wako kutafsiri sheria na kamwe hutaelewa!.

Nitakwambia kwa nini, mathlan wewe unafanya kazi ama una biashara inakuwaje sheria inasema mnapoachana na mkeo mgawane mali? yeye achukue nusu ya assets zote ilihali mwenye mali ni wewe? unayefanya kazi na kutafuta mali ni wewe? Sheria hii unaweza kuiona mbaya wa wanaume lakini kama utazingatia kwamba sheria kama hii imetokana na kudhalilishwa kwa wanawake ktk ndoa kwa miaka mingi, hivyo ili kuleta usawa sheria ikatungwa na sii kwa sababu sheria inataka kumfilisi mwanamme bali kulinda haki za wanawake ktk ndoa. Hivyo unaweza bishana na wananwake hadi kiyama na hamtafikia suluhu!

Haya mambo ya Elimu na nafasi za mikopo, haikusaidii wewe lolote zaidi ya kwamba fedha hizo ni za mikopo na wafadhili kupitia mabenki makubwa wanaofaidika na riba itokanayo ni benki na wafadhili wenyew. Mfuko wa fedha za Elimu unatolewa na nchi za nje kwa ajili ya ujenzi wa elimu nchini, hili ni deni la TAIFA na litalipwa kupitia wizara ya muungano kwa riba kubwa kitaifa. Hivyo hata kama mwanao wewe Mtanganyika ndiye kapewa mkopo ilihali mwanangu mimi Mtanganyika hakupata! naweza tumia sababu hizo hizo kwa kutumia kabila lako ama vyovyote ili mradi nijenge hoja dhidi yako. Sii akili hata kidogo bali - Ubinafsi!

Nitakwambia ukweli wa kinachoendelea nchini, Je unajua kati ya watoto walochaguliwa kuendelea na masomo ya juu ni asilimia 20 tu ndio walopewa mikopo wengine wakanyimwa kwa sababu fedha nyingi zimetumika ktk kulipa posho za wabunge wa bunge maalum la katiba? na pengine sababu nyinginezo za misafara ya viongozi kufanya kampeni za mipasho kuhusu serikali 2 au 3! Leo wewe unashindwa kulizungumzia hili unaleta ya Muungano ambao viongozi wote wameapa kuulinda!

CCM waliwajengea hoja ya serikali 2 au 3 makusudi watu kama nyie mjikite akili zenu katika jambo lisilowezekana ili msifikirie kabisa kwamba wananchi waliitaka katiba mpya ili kuuvunja mfumo wa Ufisadi uliopo na kuandika katiba mpya itakayo walazimisha viongozi kuwa Wazalendo, waadilifu, wawajibikaji kwa kuweka miiiko na maadili kuwa msingi wa uwazi na usawa kwa wote. CCM walijua ujinga wetu kwamba tukilishwa sumu basi tutaitafutia mchawi tu na sii kutafuta tiba ya maradhi yetu!

Na tusivyokuwa na akili tukaingia mkenge tukachukua miezi mingi kubishana juu ya serikali 2 au 3, tukasahau mambo muhimu haswa yalotakiwa katika kuandika katiba mpya na CCM kinyemela wakaweza kuandika katiba waloitaka wao wakiwaridhisha kwa machache ya muungano mlokuwa mkiyapigia kelele! Sasa haya yatawafaidisha nini maana unaposema mambo yamepunguzwa bado Wazanzibar watapiga mayowe na Watanganyika wataendelea kupiga miayo!

Msiwe watu wa kusikiliza sana hizi hadithi za siasa ambazo hazisaidii Mtanganyika wala Mzanzibar zaidi ya kuweka chuki za kijinga ambazo athari yake itakuwa kubwa zaidi kwa pande zote mbili. Tumia akili zako mweyewe kama yule mbayuwayu kushindwa ya Gong'ota! Hapa hatuna Mzanzibar wala Mtanganyika tuna WATANZANIA (WATU) haya ya serikali 2 au3 ni mfumo tu wa kuwezesha huduma za serikali ziwafikie wananchi. Unachoweza kudai ni muundo huo unakuletea huduma au unadhoofisha huduma na kwa nini?..Kodi zako hazijengi nchi wala kuleta maendeleo haya ni matumizi ya ndani ya wizara zisizozalisha uchumi, ni matumizi ya kuunda policies dhidi yako wewe mwananchi ambazo pia zinambeba mwekezaji kutoka nje.

Unachotakiwa wewe kupigania ni haki yako wewe kama mzawa upewe fursa na nafasi ya juu katika kulijenga taifa hili kwa sababu TAIFA letu litajengwa na mwananchi sii mgeni mwekezaji. Mzanzibar sii mgeni wala wewe sii mgeni ni mzawa na haki hiyo ndiyo inayokutambulisha wewe kwanza. Mgeni yupo hapa kuchota kama maji kisimani yakiisha wanatuachia mashimo matupu yasokuwa na maji, Iwe Mzanzibar, Mtanganyiika, mimi, wewe, wanetu na kizazi chetu ndio tutaagiza tena maji ya chupa kutoka nje! kaliwa nani?
 
Last edited by a moderator:
Mkandara, kwanza unachojitahidi ni kuonyesha wazanzibar ni Watanzania, kujenga uhalali kutumia Utanzania kunufaika,wakiutukana Utanzania unaowafaidsha. Tunatajaribu kuonyesha muungano haujakidhi haja. Hadi Wazanzibar watakapokubali Utanzania kwa dhati na kuuhudumia, muungano ni tatizo kubwa. Prof Palamagamba kasema, ya Watanganyika yakitoka kifuani itakuwa balaa!

Mzanzibar anapojiita mznz hilo tu linamuondoa Utanzania. Hatujawahi kusikia Mkigoma, Mlindi au Mtanga.
Sisi Watanganyika tupo tumeua Utanganyika, ili hali wao ni wznz.

Unaposema athari za kuvunjika muungano ni kubwa, hapo unajaribu kueleza umuhimu wa kuangalia muungano na ndicho tunachokifanya

Kwa bahati mbaya, hupendi kusikia usichotaka kusikia. Unataka kusikia kile unachokitaka, na ndio sababu ya kusema tuna chuki. Mzee Maulid, katibu wa kwanza wa BLM kawaita Watanganyika washenzi,kuna chuki iliyozidi hiyo! Mbona sijakusikia ukilaani hilo.

Kuhusu katiba, tunachokifanya ndicho unachosema. Kwamba, tunawaonyesha watu wa pande zote katiba ya Chenge na CCM ni ya kulinda mafisadi, haipaswi kupewa nafasi hata ya mjadala.

Kinachotakiwa hapa ni ima turudi katika ubao kuandika upya, au twende na ya Warioba iliyokuwa mwarobainii.

Kuhusu elimu, wznz miaka mingi wamelalamika mambo yameongezwa kinyemeala.

Mzee Maulid katibu wa kwanza wa BLM kasema, muungano umeua elimu.
Hapa tumeonyesha wazi kwa wznz wenyewe kusema elimu ya juu iwe ya muungano.
Ndio msingi wa kuuliza hawa watu wanajua wanasema nini? Leo wanasema si muungano, kesho wanasema iwe muungano

Lakini pia tunaonyesha, Utanzania ni dirisha la wznz kuingia na kuchota bila kuweka.Gavana wa benki kuu akiwa na waziri wa fedha wa znz walitihibitisha Dodoma kuwa katika pato la taifa hili znz haichangii chochote

Waziri wa fedha ambaye ni mznz amesema, kodi za znz zinabaki huko huko kwa kazi za maendeleo ya Zanzibar na si Tanga au Ludewa. Waziri Samia kasema, wafanyakazi wa TRA znz wanalipwa na TRA Tanzania na mapato yanabaki huko.
Hapo hujaongelea gharama nyingine ambazo znz haiichangii kwasababu ya mgongo wa jina Tanzania.

Ukiangalia mikoa yote ya Tanzania, katika takwimu za BoT kila mkoa una mchango kwa pato la taifa.
Znz haionekan,lakini inachukua mapato kuliko mikoa 10 combine kwa mwaka.

Kwa eneo na idadi ya watu, znz inapata 100& ya pato la Tanganyika kwa kuhudumia watu wake

Swali linakuja, kwanini mwananchi wa mkoa masikini kama Tanga au Singida, alipe kodi kwenda kujenga nchi ya Zanzibar?

Kwanini kodi ya mwananchi wa Igalula na Isevya, viwanja sitini na Magoroto itumike kusomesha watoto wa nchi ya znz ambayo haina mchango katika pato la taifa hili? na wakati huo huo watoto wa walipa kodi hizo wakiachwa? Mwaka huu ni 1024

Hapa ndipo tunasema, HESLB ni kwa ajili ya Watanganyika. Lakini, kwavile wznz wanaingia kwa jina la Tanzania wao wametengewa nafasi maalumu. Hakuna mkoa wa Tanganyika unaopewa nafasi za HESLB.

Hakuna mkoa wa Tanganyika unaopewa kodi za watumishi wa muungano(Bilioni 1.2), na hakuna mkoa wa Tanganyika unaopewa 4.5% ya BoT achilia mbali 21% ya ajira

Haitawezekana Watanganyika wakalalamika mikopo kwa makabila kwasababu wao ni Watanganyika.
Malalamiko yanakuja pale Watanganyika wanapotengwa kwa bodi ya ZHSLB.

Na ubaguzi huo upo katika kila nyanja, na ndio maana ya kitambulisho cha Uzanzibar! hakuna kitambulisho cha Ukilimanjaro au Utanga. Kile cha mzanz kimewekwa ili kumbagua Mtanganyika.
Hilo haliwezi kupatiwa ufumbuzi katika hali iliyopo, ni lazima tubadili mfumo.

Kwa mfano, waziri wa mafuta wa znz anasema si muungano.
Waziri wa muungano Samia anataka nafasi za ajira TPDC. Hapa unaweza kuona uchoyo wa wznz katika vyao.

Gesi na mafuta ya Mtwara wanataka yawe yao pia, klile chao kidogo wanataka kibaki chao.

Hakuna mkoa Tanganyika wenye loophole hiyo ya ubaguzi.
Huu ubaguzi ndio unatia Watanganyika hasira. Hatuwezi kuwazuia wznz wasiwe wznz ni haki yao, lakini tusizuiliwe kuwa Watanganyika kwasababu ni haki yetu.

Ni haki yetu hasa katika hali ya sasa ambapo muungano umebaki kuwa Tanganyika, znz ikiwa mzigo mzito sana usiobebeka tena.
Ni mzito kwasababu licha ya kuwa beneficiary wa muungano wao pia ndio chanzo cha migogoro. Wananyimwa haki gani? Na kuna tatizo gani wakiachwa na haki zao. Kuna Mtanganyika gani anafadika na fursa kule znz. Kwanini kelele za muungano zimuumize Mtanganyika yule yule aliyeubeba.

Ni makosa kuumiza watu wa Singida, ili kwenda kujenga nchi jirani.
Ni nchi jirani kwasababu wznz wanajitambua kwa uzanzibar wao na wala si Utanzania.

Tunataka kila sehemu ipewe fursa ya ku deal na mambo yake
Znz wapewe nafasi ya kukopa na misaada bila kumshirikisha Mtanganyika katika dhamana au chochote
Watanganyika wahangaike na mafisadi wao na matatizo mengine bila kuwashirikisha wazanzibar

Hapa tulipo, hakuna namna bali kurudi kwa Warioba ili tuangalie misingi imara ya kukabiliana na ufisadi, mgawanyo wa mamlaka ya nchi wahusika n.k.

Labda utueleze, kuna sababu gani za znz isiyo na mchango wa aina yoyote ile katika taifa hili kupewa mgao mkubwa kuliko mikoa masikini Tanganyika ambayo ni masikini zaidi ya znz tena zaidi ya 10. Hii investment ni ya nini

Kuna sababu gani za wznz kulalamika kuhusu muungano tukijua kuwa hawana mchango wowote zaidi ya kuchota hata kidogo kilichopo. Ni kwanini wznz wasiachwe waijenge znz na uzanzibar wao kwa mikopo yao na misaada yao wenyewe
 
ZHESLB (Bodi ya mikopo ya elimu yajuu Zanzibar)MissionTo have a Zanzibar society with sufficient numberof professionals in all fields of expertise capable of working competently inpublic and private sectors to satisfy manpower demand such that the Islesbecome free from depending on professional experts from neighbouring countries

Kwa tafsiri isiyo rasmi

Kuipa jamii ya Wzaznibar idadi ya kutosha ya wana taaluma mahiri katika Nyanja za umma na za binafsi ili kukikidhi mahitaji ya rasilimali watu ili kwamba visiwa wajiondoe katika utegemezi wa wanataaluma kutoka nchi jirani

My take
Nchi jirani na Zanzibar ni pamoja na Kenya, Tanzania na kwa mbali Somalia.
Kwa kauli hii tu, bodi ya mikopo ya elimu ya juu Zanzibar inaonyesha wazi kuwa Zaznibar si sehemu ya Tanzania, bali ni Zanzibar. Na hiyo Tanzania ni nchi jirani

Tukieleza haya tunaambiwa tuna chuki, je haya hayasemwi na wazanzibar wenyewe?

Wakati huohuo, waziri wa wlimu Shamhuna ameeleza kuwa wanafunzi watakaopatiwa mikopo mwaka huu ni 1000 tu kutokana na ufinyu wa bajeti. Hivyo wanaoendelea na wapya jumla yao itakuwa 2800

Kati ya hao,wanafunzi 1024 wanadhaminiwa na HESLB ya Tanzania.
Ni HESLB hiyo ya Tanzania ambayo Wazanzibar wanaita nchi jirani kwa kauli zao.


Vigezo vya kupata ZHELB havimruhusu Mtanganyika kupewa nafasi hizo.
Hizo ni kwa ajili ya wazanzibar. Wale wanaokosa wana fursa nyingine ya HELSB ya nchi jirani yaTanzania au Tanganyika.


Unaweza kuona kuwa ni hadi pale wznz wanapotafuata mafao ndipo wanakuwa Watanzania,kinyume chake kwa kauli zao, Tanganyika ni nchi jirani

Ni mwendohuo huo ambao waziri wa nishati wa znz kasema mafuta na gesi si za muungano.
Halafu, waziri Samia Suluhu kasema mgawanyo wa nafasi za ajira TPDC yaTanganyika sasa umepatikana.

Hivi wznz wanaondoaje mafuta na gesi, halafu waje kupata ajira TPDC?
Hiyo TPDC haiwahusu, wapi wanapata mtima wa kudai nafasi zaajira?


Ni uzanzibar huo ndio unataka TRA ikusanye mapato na kuyaacha huko kwao.
Halafu wanataka asilimia 21 ya ajira ambazo mishahara na gharama zake zinatoka Tanganyika.

Imefika mahali wafanyakazi wa TRA yao wanalipwa na Tanganyika ili kukusanya mafao ya nchi yao.


Hapa ndipo Watanganyika wanatakiwa wafungue macho, waone wasichokiona
Huu Utanzania ni ufunguo wa bank, baada ya hapo ni uzanzibar tu hakuna muungano
 
ZHESLB (Bodi ya mikopo ya elimu yajuu Zanzibar)MissionTo have a Zanzibar society with sufficient numberof professionals in all fields of expertise capable of working competently inpublic and private sectors to satisfy manpower demand such that the Islesbecome free from depending on professional experts from neighbouring countries

Kwa tafsiri isiyo rasmi

Kuipa jamii ya Wzaznibar idadi ya kutosha ya wana taaluma mahiri katika Nyanja za umma na za binafsi ili kukikidhi mahitaji ya rasilimali watu ili kwamba visiwa wajiondoe katika utegemezi wa wanataaluma kutoka nchi jirani

My take
Nchi jirani na Zanzibar ni pamoja na Kenya, Tanzania na kwa mbali Somalia.
Kwa kauli hii tu, bodi ya mikopo ya elimu ya juu Zanzibar inaonyesha wazi kuwa Zaznibar si sehemu ya Tanzania, bali ni Zanzibar. Na hiyo Tanzania ni nchi jirani.......

Binafsi nilishangaa kuwa FCC wanaohusika na ukamataji wa 'Counterfeit product' zinazoingizwa nchi ama kuzalishwa nchini (Zingatia FCC wanatetea/wanalinda kampuni zilizosajiliwa BRELA) hawafanyi kazi Zanzibar. Na Zanzibar ndiko mahala bidhaa fake/substandard/counterfeit zinakopitia kutokea hasa China na nchi nyingine kutokana na ulegelege wa wafanyakazi walioko Tanzania Visiwani (Zanzibar). Ni Zanzibar ambako unaweza kuuziwa bidhaa ambayo imeandikwa specifications kwa lugha ya Kichina wakati mnunuaji hajui hata neno moja la kichina. Sheria/Kanuni za Viwango nchini (TBS) inazuia kuuza bidhaa ambayo maelezo/specifications zake haziko kwenye lugha inayofahamika kwa mteja(kama nitakuwa nimekumbuka vizuri).Nilipojaribu kuhoji kwa nini suala la kudhibiti uingizaji wa bidhaa fake nchi halihusishi Sehemu ya JMT inaiyoitwa Zanzibar; nilijibiwa kuwa hapo ninaamusha uchokonozi wa masuala ya muungano, kwanza inasemakana Zanzibar iko mbioni kuanzisha ZBS ambayo itafanya kazi sawa na TBS.

Kwa kweli kuendelea na muungano wa namna hii, kunahatarisha usalama wa mlaji (consumer security) wa Tanzania. Na kwa hili nimepata sababu nyingine ya kukataa Katiba Pendekezwa.
 
Binafsi nilishangaa kuwa FCC wanaohusika na ukamataji wa 'Counterfeit product' zinazoingizwa nchi ama kuzalishwa nchini (Zingatia FCC wanatetea/wanalinda kampuni zilizosajiliwa BRELA) hawafanyi kazi Zanzibar. Na Zanzibar ndiko mahala bidhaa fake/substandard/counterfeit zinakopitia kutokea hasa China na nchi nyingine kutokana na ulegelege wa wafanyakazi walioko Tanzania Visiwani (Zanzibar). Ni Zanzibar ambako unaweza kuuziwa bidhaa ambayo imeandikwa specifications kwa lugha ya Kichina wakati mnunuaji hajui hata neno moja la kichina. Sheria/Kanuni za Viwango nchini (TBS) inazuia kuuza bidhaa ambayo maelezo/specifications zake haziko kwenye lugha inayofahamika kwa mteja(kama nitakuwa nimekumbuka vizuri).Nilipojaribu kuhoji kwa nini suala la kudhibiti uingizaji wa bidhaa fake nchi halihusishi Sehemu ya JMT inaiyoitwa Zanzibar; nilijibiwa kuwa hapo ninaamusha uchokonozi wa masuala ya muungano, kwanza inasemakana Zanzibar iko mbioni kuanzisha ZBS ambayo itafanya kazi sawa na TBS.

Kwa kweli kuendelea na muungano wa namna hii, kunahatarisha usalama wa mlaji (consumer security) wa Tanzania. Na kwa hili nimepata sababu nyingine ya kukataa Katiba Pendekezwa.
Hili la TBS linasahangaza sana. Tayari wameanzisha ZBS na sababu iliyopelekea kufanya hivyo ni eti TBS inazuia kuingizwa bidhaa Zanzibar na hivyo wanataka chombo chao. Hilo wakasema ni kero na kukimbilia kuanzisha yao

Utashangaa kuwa bidhaa zinazoruhusiwa na ZBS asilimia 99 zinakuja Tanganyika.
Wanapozuiwa kuingiza sub standards, hoja yao kubwa hilo ni kero.
Kwamba wanaweza kuingiza sumu Tanganyika kwa ruhusa ya ZBS na TBS inapozuia tayari wanadai wao ni sehemu ya Muungano.

TBS inakosa nguvu kwasababu bodi ya wajumbe wapo wazanzibar. Hapa napo kuna kituko, hivi mzanzibar anahusika vipi na bodi ya TBS. Hawa wajumbe kutoka znz wapo kama ajira tu lakini hawana interest yoyote na Tanzania au Tanganyika.

Hivyo wazaznibar wanaitumia TBS kwa njia mbili

  1. Kuingiza bidhaa zao pale wanapogeuka kuwa Watanzania hata kama wana ZBS ya znz
  2. Kutumia TBS kama eneo la ajira. Fahamu kuwa ndani ya TBS lazima kuwe na wazaznibar kwasababu ni chombo cha muungano kwa jina la Tanzania.

Haya ni mambo yasiyoonekana katika huu muungano. Na kwa bahati mbaya sana wasioona ni Watanganyika kwasababu kama Znz wameamua kuwa na ZBS, basi hilo si la muungano tena.

Ukisikia muungano unatajwa na mzanzibar kuna mafao, baada ya hapo to hell na muungano, wao ni wazanzibar.

Suala la kujiuliza, hivi investment inayofanywa kwa watu hawa milioni 1, tena wakiishi kwa utegemezi wa Tanganyika inatarajiwa kuleta dividend gani kwa Mtanganyika?
 
Mkandara, kwanza unachojitahidi ni kuonyesha wazanzibar ni Watanzania, kujenga uhalali kutumia Utanzania kunufaika,wakiutukana Utanzania unaowafaidsha. Tunatajaribu kuonyesha muungano haujakidhi haja. Hadi Wazanzibar watakapokubali Utanzania kwa dhati na kuuhudumia, muungano ni tatizo kubwa. Prof Palamagamba kasema, ya Watanganyika yakitoka kifuani itakuwa balaa!

Mzanzibar anapojiita mznz hilo tu linamuondoa Utanzania. Hatujawahi kusikia Mkigoma, Mlindi au Mtanga.
Sisi Watanganyika tupo tumeua Utanganyika, ili hali wao ni wznz.

Unaposema athari za kuvunjika muungano ni kubwa, hapo unajaribu kueleza umuhimu wa kuangalia muungano na ndicho tunachokifanya

Kwa bahati mbaya, hupendi kusikia usichotaka kusikia. Unataka kusikia kile unachokitaka, na ndio sababu ya kusema tuna chuki. Mzee Maulid, katibu wa kwanza wa BLM kawaita Watanganyika washenzi,kuna chuki iliyozidi hiyo! Mbona sijakusikia ukilaani hilo.

Kuhusu katiba, tunachokifanya ndicho unachosema. Kwamba, tunawaonyesha watu wa pande zote katiba ya Chenge na CCM ni ya kulinda mafisadi, haipaswi kupewa nafasi hata ya mjadala.

Kinachotakiwa hapa ni ima turudi katika ubao kuandika upya, au twende na ya Warioba iliyokuwa mwarobainii.

Kuhusu elimu, wznz miaka mingi wamelalamika mambo yameongezwa kinyemeala.

Mzee Maulid katibu wa kwanza wa BLM kasema, muungano umeua elimu.
Hapa tumeonyesha wazi kwa wznz wenyewe kusema elimu ya juu iwe ya muungano.
Ndio msingi wa kuuliza hawa watu wanajua wanasema nini? Leo wanasema si muungano, kesho wanasema iwe muungano

Lakini pia tunaonyesha, Utanzania ni dirisha la wznz kuingia na kuchota bila kuweka.Gavana wa benki kuu akiwa na waziri wa fedha wa znz walitihibitisha Dodoma kuwa katika pato la taifa hili znz haichangii chochote

Waziri wa fedha ambaye ni mznz amesema, kodi za znz zinabaki huko huko kwa kazi za maendeleo ya Zanzibar na si Tanga au Ludewa. Waziri Samia kasema, wafanyakazi wa TRA znz wanalipwa na TRA Tanzania na mapato yanabaki huko.
Hapo hujaongelea gharama nyingine ambazo znz haiichangii kwasababu ya mgongo wa jina Tanzania.

Ukiangalia mikoa yote ya Tanzania, katika takwimu za BoT kila mkoa una mchango kwa pato la taifa.
Znz haionekan,lakini inachukua mapato kuliko mikoa 10 combine kwa mwaka.

Kwa eneo na idadi ya watu, znz inapata 100& ya pato la Tanganyika kwa kuhudumia watu wake

Swali linakuja, kwanini mwananchi wa mkoa masikini kama Tanga au Singida, alipe kodi kwenda kujenga nchi ya Zanzibar?

Kwanini kodi ya mwananchi wa Igalula na Isevya, viwanja sitini na Magoroto itumike kusomesha watoto wa nchi ya znz ambayo haina mchango katika pato la taifa hili? na wakati huo huo watoto wa walipa kodi hizo wakiachwa? Mwaka huu ni 1024

Hapa ndipo tunasema, HESLB ni kwa ajili ya Watanganyika. Lakini, kwavile wznz wanaingia kwa jina la Tanzania wao wametengewa nafasi maalumu. Hakuna mkoa wa Tanganyika unaopewa nafasi za HESLB.

Hakuna mkoa wa Tanganyika unaopewa kodi za watumishi wa muungano(Bilioni 1.2), na hakuna mkoa wa Tanganyika unaopewa 4.5% ya BoT achilia mbali 21% ya ajira

Haitawezekana Watanganyika wakalalamika mikopo kwa makabila kwasababu wao ni Watanganyika.
Malalamiko yanakuja pale Watanganyika wanapotengwa kwa bodi ya ZHSLB.

Na ubaguzi huo upo katika kila nyanja, na ndio maana ya kitambulisho cha Uzanzibar! hakuna kitambulisho cha Ukilimanjaro au Utanga. Kile cha mzanz kimewekwa ili kumbagua Mtanganyika.
Hilo haliwezi kupatiwa ufumbuzi katika hali iliyopo, ni lazima tubadili mfumo.

Kwa mfano, waziri wa mafuta wa znz anasema si muungano.
Waziri wa muungano Samia anataka nafasi za ajira TPDC. Hapa unaweza kuona uchoyo wa wznz katika vyao.

Gesi na mafuta ya Mtwara wanataka yawe yao pia, klile chao kidogo wanataka kibaki chao.

Hakuna mkoa Tanganyika wenye loophole hiyo ya ubaguzi.
Huu ubaguzi ndio unatia Watanganyika hasira. Hatuwezi kuwazuia wznz wasiwe wznz ni haki yao, lakini tusizuiliwe kuwa Watanganyika kwasababu ni haki yetu.

Ni haki yetu hasa katika hali ya sasa ambapo muungano umebaki kuwa Tanganyika, znz ikiwa mzigo mzito sana usiobebeka tena.
Ni mzito kwasababu licha ya kuwa beneficiary wa muungano wao pia ndio chanzo cha migogoro. Wananyimwa haki gani? Na kuna tatizo gani wakiachwa na haki zao. Kuna Mtanganyika gani anafadika na fursa kule znz. Kwanini kelele za muungano zimuumize Mtanganyika yule yule aliyeubeba.

Ni makosa kuumiza watu wa Singida, ili kwenda kujenga nchi jirani.
Ni nchi jirani kwasababu wznz wanajitambua kwa uzanzibar wao na wala si Utanzania.

Tunataka kila sehemu ipewe fursa ya ku deal na mambo yake
Znz wapewe nafasi ya kukopa na misaada bila kumshirikisha Mtanganyika katika dhamana au chochote
Watanganyika wahangaike na mafisadi wao na matatizo mengine bila kuwashirikisha wazanzibar

Hapa tulipo, hakuna namna bali kurudi kwa Warioba ili tuangalie misingi imara ya kukabiliana na ufisadi, mgawanyo wa mamlaka ya nchi wahusika n.k.

Labda utueleze, kuna sababu gani za znz isiyo na mchango wa aina yoyote ile katika taifa hili kupewa mgao mkubwa kuliko mikoa masikini Tanganyika ambayo ni masikini zaidi ya znz tena zaidi ya 10. Hii investment ni ya nini

Kuna sababu gani za wznz kulalamika kuhusu muungano tukijua kuwa hawana mchango wowote zaidi ya kuchota hata kidogo kilichopo. Ni kwanini wznz wasiachwe waijenge znz na uzanzibar wao kwa mikopo yao na misaada yao wenyewe
Mkuu ndio maana nikasema wewe unaandika vitu kwa jazba na hisia za kiume dhidi ya wanawake, ukinielewa hapo tutakata huu mzizi wa fitna. Tazama basi mbona ktk madai ya haki za wanawake, kila mahala utasikia wanawake hivi wanawake vile na wanaume ndio mahasidi wakubwa! Na wala haijatokea sisi wanaume kujitambulisha kama wao, tukajiita wanaume iwe ktk kujitetea ama kudai haki zetu ama vinginevyo.

Tunachotakiwa sisi ni kuyatazama madai ya haki zao na sii ushindani wa nani na kwa nini wakajiita mwanamke! Ulitaka wajiite nani wanapoweka madai hayo dhidi ya wanaume? Unachokwepa hapa ni swala la msingi ambalo ndio chanzo na chimbuko la madai ya Wazanzibar nayo mgao wa keki ya TAIFA. Madai ya Wazanzibar ni dhidi ya bara na hakuna jina wanaloweza kujitofautisha nasi pasipo kutumia Uzanzibar maana ndio utambulisho wao.

Sasa kama wewe ungekuwa kweli mwenye kuelewa ungetumia madai yao na sii wao kama nani ama kile walichonacho wao maana penye Muungano fungu la Jamhuri ya Muungano mahala popote duniani huzihusu nchi washirika! na sii nani mwenye zaidi ama ana hisa kiasi gani, nani ana nini bali wananchi wa jamhuri hiyo kwa usawa wanafaidika vipi na maliasili na rasilimali zao. Unanishangaza zaidi unapoweza kuyaweka madai ya Utanganyika kwa kujisifia utajiri ilihali wewe mwenyewe unailaani CCM kwa uwekezaji mbovu na kuifanya nchi iwe maskini. Huku unaponda walalamikaji lakini upande wapili unawatetea wadhalilishaji kwa sababu wewe ni baina yao! yale yale ya kuponda Muungano ukiwa ushirika pamoja na kina Jussa lakini upande mwingine Jussa ni mwarabu na adui wa mapinduzi!

Hii ni tabia mbaya sana na imekuwa kama mila na desturi ya Watanzania ambao wako radhi kuhakikisha Mtanzania mwenzake hafanikiwi japo mwizi mkubwa wa maliasili zake ni mgeni kutoka nje. Tazama kesi ya IPTL leo yule Ruge kila mtu kamkalia kooni, Mama Anna Tibaijuka na wengine wakati huyo Ruge alikuwa na asilimia 30 tu ya uwekezaji IPTL, waloamua kuuza ni viongozi wa CCM, yeye kalipwa na kalipa kodi zake lakini yule Mhindi wa Kenya mwenye kucuhukua asilimia 70 tena asijulikane katokea wapi, na hakulipa kodi hakuna mwanaharakati hata mmoja anayeshinikiza huyu Mhindi na IPTL ndiye hasidi na mali zake zitaifishwe.

Tena maajabu imefikia hadi watu wanasema kutaifisha mashirika binafsi yalohujumu uchumi, itatuletea picha mbaya kwa Mataifa wakati hata hiyo Marekani yenyewe hutaifisha kila mwaka mashirika yanayohujumu uchumi wa nchi hiyo, hutaifisha mashirika na hata mali za wahujumu Uchumi na kuwasweka ndani. Muuza unga tu akikamatwa hutaifishwa mali zake zote hadi nyumba, wata freeze account zake na kifungo juu, leo sisi tumekuwa na ujasiri wa kuwatetea wageni wahujumu uchumi na kuwasakama Watanzania kwa kutumia Huu Uzalendo wa Uzanzibar na Utanganyika. Halafu kwa ujinga wote huu wa ufisadi na hali mbaya ya maisha bado watu wanaitaka CCM iendelee kutawala, sasa mnalia nini jamani inapokuwa hali mbaya?

Kama wewe ni Mtanganyika, kwa nini hujiiti Mtanganyika, nani alokushika shati ama kukwambia usijiite Mtanganyika! tembea dunia mkuu wangu uone wapo watu wanajiita Wascotish na anakataa kabisa kuitwa M - British ama muingereza, Wa Irish na kadhalika kutokana na imani kwamba wao wanaonewa na hawataki kuwa kundi moja na mdhalilishaji. Ni Fikra za watu huwezi kuwazuia hisia zao isipokuwa unachoweza kufanya ni kutazama na kupima haki gani hizo wanazolilia na ukazichambua bila kuitana majina!

Wao ZnZ wana hasira na Muungano na wanajulikana haswa wenye kuleta hizi vurugu, wana lao jambo wanalitafuta sii vizuri nasi tuwe kama wao, itakuwa tunamfukuza kichaa tukiwa uchi na ndicho unachokifanya humu JF..
 
Tunachotakiwa sisi ni kuyatazama madai ya haki zao( 1a) na sii ushindani wa nani na kwa nini wakajiita mwanamke! Ulitaka wajiite nani wanapoweka madai hayo dhidi ya wanaume?

Unachokwepa hapa ni swala la msingi ambalo ndio chanzo na chimbuko la madai ya Wazanzibar nayo mgao wa keki ya TAIFA.(1b)

Madai ya Wazanzibar ni dhidi ya bara na hakuna jina wanaloweza kujitofautisha nasi pasipo kutumia Uzanzibar maana ndio utambulisho wao.

Sasa kama wewe ungekuwa kweli mwenye kuelewa ungetumia madai yao na sii wao kama nani ama kile walichonacho wao maana penye Muungano fungu la Jamhuri ya Muungano mahala popote duniani huzihusu nchi washirika! na sii nani mwenye zaidi ama ana hisa kiasi gani, nani ana nini bali wananchi wa jamhuri hiyo kwa usawa wanafaidika vipi na maliasili na rasilimali zao.(2)


Unanishangaza zaidi unapoweza kuyaweka madai ya Utanganyika kwa kujisifia utajiri(3) ilihali wewe mwenyewe unailaani CCM kwa uwekezaji mbovu na kuifanya nchi iwe maskini.

Kama wewe ni Mtanganyika, kwa nini hujiiti Mtanganyika(4), nani alokushika shati ama kukwambia usijiite Mtanganyika!

tembea dunia mkuu wangu uone wapo watu wanajiita Wascotish na anakataa kabisa kuitwa M - British ama muingereza, Wa Irish na kadhalika kutokana na imani kwamba wao wanaonewa na hawataki kuwa kundi moja na mdhalilishaji. Ni Fikra za watu huwezi kuwazuia hisia zao isipokuwa unachoweza kufanya ni kutazama na kupima haki gani hizo wanazolilia (5)na ukazichambua bila kuitana majina!a

Wao ZnZ wana hasira na Muungano na wanajulikana haswa wenye kuleta hizi vurugu, wana lao jambo wanalitafuta sii vizuri nasi tuwe kama wao(6), itakuwa tunamfukuza kichaa tukiwa uchi na ndicho unachokifanya humu JF..
Mkandara
Nijibu hoja zako kama nilivyozianisha kwa namba

(1a) Haki inaambatana na wajibu, hakuna ushahidi wa znz kunyimwa haki.
Upo ushahidi wa znz kutokuwa na wajibu katika muungano. Tutafananua

Tumeyatazama madai ya wazanzibar baada ya kukaa kimya mingi.
Moja ya madai yao ni kunyonywa na Tanganyika. Kodi zao kuja kujenga Tanganyika na mgawanyo usio sawa wa misaada na mikopo ya maendeleo

Jibu: Hakuna mahali wazanzibar wameonyesha kwa ushahidi kunyonywa.
Takwimu zote za uchumi zinaonyesha wazanzibar kutochangia muungano(Gavana wa BoT na waziri wa fedha wa znz Dodoma) kwa takribani miaka 30.

Waziri wa fedha wa znz ameeleza kuhusu mchango wa JMT katika bajeti.
Katika idadi ya mikoa na ZNZ inayochangia muungano, Znz haina mchango wa aina yoyote ile. Mkoa masikini sana Tanganyika unachangia pato la taifa kubwa kuliko znz kwa takwimu halisi. Mchango wa znz ambao ni wajibu wao katika muungano ni sifuri

Misaada na mikopo:
Tumeonyesha kuwa znz inapata misaada na mikopo ya moja kwa moja(direct) na kupitia (indirect)

Direct ni pamoja na kufidiwa bajeti yao. Nakisi ya bajeti ya znz ni Tsh Bilioni 300 na pato lao ni Tsh Bilioni 400 ili kutengeneza bajeti ya znz ya Tsh Bilioni 700.

Bilioni 300 zinatoka katika mfuko unaochangiwa na Tanganyika yenyewe.
Hii maana yake ni kuwa, znz inapata pesa kuliko mikoa zaidi ya 10 ya Tanganyika.

Mkoa wa Dar es Salaam wenye wakazi milioni 5 na chanzo kikuu cha mapato na uchumi wa nchi inapewa bilioni 20 kwa mwaka.

Znz yenye mchango sifuri na watu milioni 1.2 ambao nusu wanaishi Tanganyika inapewa pesa za bajeti bilioni 300 ikiwa ni mara zaidi ya 15 ya mkoa wa Dar es Salaam

Znz inapewa bilioni 1.2 kila mwezi kama kodi ya wafanyakazi wa muungano.

Wafanyakazi wa muungano ni pamoja na wale wanaofanya kazi katika maeneo yasiyo ya muungano. SMZ Ina watumishi takribani 10,000. Kodi zao hazitoi hata milioni 100 kwa

Leo wanapewa 1.2 Bilioni kwa kigezo gani? Idadi ya watu ni ndogo, mchango katika uchumi wa Tanzania ni sifuri na wafanyakazi wa muungano ni msaada kwasababu waajiriwa wa znz huku Tanganyika wengi kuliko SMZ.
Znz walipaswa kulipa kodi kwa JMT kama msaada wa kuwapunguzia ajira na si kulipwa.

Indirect: Znz haina bajeti ya ulinzi na usalama.
Haina wizara ya mambo ya ndani.

Pesa za elimu ya juu kwa wanafunzi 1024 ni msaada. Hilo si suala la muungano.

Kwa minajili ya mjadala huu endapo mwanafunzi anagharamiwa kiasi cha sh milioni 4 kwa mwaka, hiyo ni sawa na Bilioni 4 za kusomesha wazanzibar wenye mchango sifuri, tena wakipoka nafasi za Watanganyika wenye mchango asilimia zote za muungano

Gharama za kuendesha muungano kazibeba Mtanganyika.
Znz isiyo na mchango hailipi chochote kwa watumishi wa muungano zaidi ya kudai nafasi.

Znz inakusanya mapato ya TRA na wafanyakazi wa TRA wanalipiwa na TRA ya JMT.

Hii mana yake mapato yao ni kwa maendeleo yao ya ZNZ.
Mapato ya TRA Kigoma na Singida, Mbeya na Tangan yanagawanywa kwa JMT ikiwemo znz na wala si Tanganyika peke yake.

Taasisi na mashirika ya kimataifa yanalipwa na JMT ambayo znz haina mchango.
Mchango wa znz ni kudai nafasi tu. Hakuna mahali panaonyesha wanahudumiaje balozi, mashirika ya kimataifa ay taasisi nyingine

Wahisani wamegoma kutoa pesa, znz inaendelea kupata 4.5% kutoka BoT na 1.2 za watumishi wa muungano, huku wakiwa hawana habari na wizara ya ulinzi, mambo ya ndani na taasisi nyingine na mashirika ya kimataifa.

Hii inaonyesha kuwa hoja ya mikopo na misaada ni mfu kwasababu hata bila hayo znz inaendelea kuchota kilicho ‘chake' bila huruma kutoka kwa masikini mlipa kodi wa Tanganyika

Ni kwa msingi huo, znz nchi yenye watu wachache kuliko jimbo la Ubungo imeweza kuwa na Rais na makamu wawaili. Hii inatokana na ukweli kuwa, mzigo na gharama za SMZ anazibeba Mtanganyika, hivyo wao kugawana vyeo si jambo la ajabu

Inaendelea Hoja (1B)
 
Inaendele majibu

(1b) Mgao wa keki ya taifa
Hakuna haki isiyo na wajibu.
Mgao wa keki ya taifa lazima uwe na namna ya kuutafuta.
Znz haina mchango wa keki ya taifa. Haki ya kudai keki ya mtu inatoka wapi.


Hakuna mkoa Tanganyika unaodai keki kama separate entity, znz wana haki gani zaidi ya Singida, Mtwara au Lindi kwenye wananchi wanaowajibika kwa serikali yao kodi

Znz haina haki ya keki ya taifa ljingine. Kama wanaomba hiyo si haki. Msaada haugeuki kuwa haki.
Hawana haki ya kudai wasichojua kinapatikana wapi.


(2) Zanzibar wanafaifika vipi na rasilimali mali ya taifa hili.
Nimeonyesha jinsi wanavyopewa zawadi kama sehemu ya kufadika na rasilimali na mali za taifa hili.

Dhabu na ndizi za Muleba zinasomesha watoto wao 1024, wao wamekimbilia kuondoa mafuta na gesi ili Mtanganyika asijenufaika.
Wameweka vikwazo vya kitambulisho n.k. kuzuia Watanganyika katika fursa mfano,
ardhi, yao wameiwekea vikwazo na tena wakijisifu.
Angali video utaona jinsi gani walivyo na kauli za jeuri kudai haki ya ardhi kwaUtanzania


Znz hawahitaji kudaia zaidi wanachokipata. Na kama wanadhani kuna kuonewa, ni vema wakaondoka.

Tupo hapa kuwasaidia wapate taifa lao, uonevu ufike mwisho. Nini kinawakwaza kuishi katika maonezi ya ‘mkoloni' Tanganyika?
Let them go to live in paradise, hakuna anayewazuia.

(3) Ni haki znz kujivunia uzanzibar .Hakuna tatizo kwa hilo.
Tatizo ni pale wanapovua uzanzibar wakati wa kuhemea
Huku kujificha katika koti ndiko tunakulaani na hatukutaki.
Wanaweza kuja kuomba msaada kama wazanzibar, lakini si Watanzania maana huo Utanzania kwao ni haramu.

Sisi wengine tunahitaji Tanganyika ili tuhangaike na umasikini na mafisadi wetu
Hatuwezi kuchukua zaidi ya bilioni 300 za masikini wa Tanganyika kwenda kujenga nchi jirani ya znz(wanasema wao nimekuonyesha).

Ni makosa mkoa masikini kulipia kodi za utitiri wa viongozi wa znz. Huo mzigo waubebe wenyewe.
Hawawezi kutafuta matatizo kasha kutubebesha mzigo. Hawatutambui hawa! Kama wangetutambua wasingekuwa wabaguzi

(3) Tanganyika ni masikini sana nimesema hilo. Hakuna mahali nimesema ni tajiri.

Ni katika umasikini wa Tanganyika ndipo tunajiuliza, kwanini masikini wa Singida alipe kodi ya utitiri wa viongozi wa nchi jirani

(4)Sihitaji kujiita Mtanganyika, ninahitaji uwepo wa Tanganyika.
Ni kero kuwa na znz ambayo haina hawana madai ya maana au namna ya kujenga muungano.

Tumeonyesha, mchango wao ni sifuri, na hata rasilimali zao ndio hivyo tena. Tanganyika inaihitaji znz ?

Labda utuonyesha tunaihitaji znz kwa lipi na kitu gani mwaka 2015? Ulinzi! Upi katika dunia ya leo

(6) Tumevumilia sana tusiwe kama wao. Kinachoudhi ni wao kudhani ni sehemu muhimu sana ya muungano.
Wamefikia mahali wanadai msaada kama haki. Wana haki gani bila wajibu


Wanajitambulisha kama sehemu tofauti na muhimu ya taifa hili inayohitaji priority ya ina fulani.

Hatuwezi kuendelea kuishi na malalamiko yasiyo na msingi
Tuna mambo mengi ya kushugulikia na wala si kuwasikiliza wznz wanataka nini.
Wapewe taifa lao nasi tuwe na letu. Kama wanahitaji msaada, tukutane tunapodhani kuna masilahi iyo wanapodhani wana nufaika.


Tuna umasikini, ufisadi n.k. ambavyo ni muhimu sana kujadili kuliko mjadala wa znz ambao hata wasipokuwepo haina athari kwa Mtanganyika.
 
Mkuu Wao ZnZ wana hasira na Muungano na wanajulikana haswa wenye kuleta hizi vurugu, wana lao jambo wanalitafuta sii vizuri nasi tuwe kama wao, itakuwa tunamfukuza kichaa tukiwa uchi na ndicho unachokifanya humu JF..
Kwa muda mrefu Watanganyika ima hawaelewi kinachoendeleaau zito waliououbea.
Waliaminishwa
uongo, znz ni chanzo cha mapato ya Tanzania na inanyimwa misaada na mikopo


Tunachokifanya ni kuwaeleza Watanganyika uzito wa muungano, kuisadia Tanganyika kuondokana na adha.
Kama tutakuwa uchi, basi
na iwe


Hakuna mznz anayeonyesha kwa data ni wapi wanaonewa.
Siku hizi wanatumia neno kero za muungano. Hakuna kitu kero, kero ni pale wanapotaka kitu au jambo.


Kuna kero iliyotolewa BLW , znz iingize bidhaa Tanganyika bila kodi kwasababu ni Tanzania.
Hapa Tanzania imetumika katika kukidhi haja.

Leo Watanganyika wanafahamu TRA haikusanyi chochote znz na kile kinachokusanywa na Zanzibar kinabaki huko

Hii ina maana kuruhusu bidhaa za znz bila kodi ni kuacha mapato yabaki znz, walipa kodi wa Tanganyika wenye mzigo wa kuhudumia muungano walipe kodi kutoka mifukoni mwao.

Znz ina sifa ya kutokusanya kodi. Hilo likiruhusiwa maana ni kuikosesha Tanganyika mapato kwa huruma za nchi jirani.
Bidhaa zitaingia bure znz na kama zinalipiwa kidogo, kodi hiyo haivuki bahari. Hilo eti kwa wznz ni kero!

Lakini pia, znz wameanzisha ZBS. Maana yake ni kuwa kwavile bidhaa nyingi zinakuja bara, wanachotaka ni kuidhinisha bidhaa hovyo kwa gharama ya afya za Watanganyika. Kulikuwa na haja gani ya kuwa na ZBS kama tuna TBS?

Kero za wznz ni kuhusu ajira za muungano Wanadai, kiongozi akitoka upande mmoja mwingine atoke upande mwingine.

Katika ajira, asilimia 21 wanayopewa ni fadhila. Si haki yao kwasababu SMZ inaajiri nusu ya ajira walizo nazo wznz Tanganyika. SMZ haikusanyi hata milioni 100,inapata bilioni 1.2 za Tanganyika
Ni hesabu gani inayotumika kupata 21%. Hili wanasema ni kero pia


Hoja ya mikopo na misaada imepata jibu ambalo pengine wabishi hawana hoja tena.

Wahisani wamezuia mikopo na misaada. Wznz hawaathiriki na hali hiyo kwasababu wanapata 4.5% ya pato la Tanganyika, 1.2Bilioni ya kodi za wafanyakazi pamoja na gharama za ulinzi na usalama, mambo ya ndani na kuendesha muungano.


Hiyo 4.5% wanayopata wanasema ni kero wanapaswa kupata Zaidi.

Ukiangalia BoT wznz hao hawana hata 0.0001 ya mchango. Kwa maneno mengine, wakati Mtanganyika unavunjika mgongo wa kodi, ongezeko la pato la Tanganyika ni samba mba na ongezeko la 4.5%. Hii formula imepatikanaje?


Hivi unawezaje kudai dividend ikiwa huna shea ?Tena wanadai dividend hiyo kama haki.
Hapa Watanganyika wajiulize, ni kwa faida gani wanafanyahii investment?


Wakati wa mafao ya muungano znz inadai usawa kama nchi iliyoungana na nyingine.
Tena bila haya wanadai usawa wa nusu kwa nusu.


Sikiliza maongezi yao, hakuna hata mmoja anayeongelea ni jinsi gani tunahudumia huu muungano.
Na pale wanapotakiwa, hoja yao ni uchache na udogo wa nchi.

Endapo wanatambua wao ni wachache na wadogo, wanapata wapi haki ya kudai usawa?


Watanganyika wanapaswa kuamka. Wanatakiwa kuzinduka ili kukinusuru kizazi hiki na kijacho.

Huu mzigo ni mzito na wakati wa kuutua ni sasa. Haiwezekani znz ambayo ni ndogo kuliko asilimia 95 ya Wilaya za Tanganyika, na ambayo haina mchango wa aina yoyote kwa uchumi wa Tanzania ipewe mgao mkubwa Zaidi ya halmashauri za miji 54 za Tanganyika


Watanganyika ninyi ni tatizo. Ni tatizo kwasababu hamuoni tatizo.
Kama hamtafungua macho, huu mzigo mtaubeba na kurithisha vizazi vyenu.


Tusemezane
 
Mkandara
Nijibu hoja zako kama nilivyozianisha kwa namba

(1a) Haki inaambatana na wajibu, hakuna ushahidi wa znz kunyimwa haki.
Upo ushahidi wa znz kutokuwa na wajibu katika muungano. Tutafananua

Tumeyatazama madai ya wazanzibar baada ya kukaa kimya mingi.
Moja ya madai yao ni kunyonywa na Tanganyika. Kodi zao kuja kujenga Tanganyika na mgawanyo usio sawa wa misaada na mikopo ya maendeleo

Jibu: Hakuna mahali wazanzibar wameonyesha kwa ushahidi kunyonywa.
Takwimu zote za uchumi zinaonyesha wazanzibar kutochangia muungano(Gavana wa BoT na waziri wa fedha wa znz Dodoma) kwa takribani miaka 30.

Waziri wa fedha wa znz ameeleza kuhusu mchango wa JMT katika bajeti.
Katika idadi ya mikoa na ZNZ inayochangia muungano, Znz haina mchango wa aina yoyote ile. Mkoa masikini sana Tanganyika unachangia pato la taifa kubwa kuliko znz kwa takwimu halisi. Mchango wa znz ambao ni wajibu wao katika muungano ni sifuri

Misaada na mikopo:
Tumeonyesha kuwa znz inapata misaada na mikopo ya moja kwa moja(direct) na kupitia (indirect)

Direct ni pamoja na kufidiwa bajeti yao. Nakisi ya bajeti ya znz ni Tsh Bilioni 300 na pato lao ni Tsh Bilioni 400 ili kutengeneza bajeti ya znz ya Tsh Bilioni 700.

Bilioni 300 zinatoka katika mfuko unaochangiwa na Tanganyika yenyewe.
Hii maana yake ni kuwa, znz inapata pesa kuliko mikoa zaidi ya 10 ya Tanganyika.

Mkoa wa Dar es Salaam wenye wakazi milioni 5 na chanzo kikuu cha mapato na uchumi wa nchi inapewa bilioni 20 kwa mwaka.

Znz yenye mchango sifuri na watu milioni 1.2 ambao nusu wanaishi Tanganyika inapewa pesa za bajeti bilioni 300 ikiwa ni mara zaidi ya 15 ya mkoa wa Dar es Salaam

Znz inapewa bilioni 1.2 kila mwezi kama kodi ya wafanyakazi wa muungano.

Wafanyakazi wa muungano ni pamoja na wale wanaofanya kazi katika maeneo yasiyo ya muungano. SMZ Ina watumishi takribani 10,000. Kodi zao hazitoi hata milioni 100 kwa

Leo wanapewa 1.2 Bilioni kwa kigezo gani? Idadi ya watu ni ndogo, mchango katika uchumi wa Tanzania ni sifuri na wafanyakazi wa muungano ni msaada kwasababu waajiriwa wa znz huku Tanganyika wengi kuliko SMZ.
Znz walipaswa kulipa kodi kwa JMT kama msaada wa kuwapunguzia ajira na si kulipwa.

Indirect: Znz haina bajeti ya ulinzi na usalama.
Haina wizara ya mambo ya ndani.

Pesa za elimu ya juu kwa wanafunzi 1024 ni msaada. Hilo si suala la muungano.

Kwa minajili ya mjadala huu endapo mwanafunzi anagharamiwa kiasi cha sh milioni 4 kwa mwaka, hiyo ni sawa na Bilioni 4 za kusomesha wazanzibar wenye mchango sifuri, tena wakipoka nafasi za Watanganyika wenye mchango asilimia zote za muungano

Gharama za kuendesha muungano kazibeba Mtanganyika.
Znz isiyo na mchango hailipi chochote kwa watumishi wa muungano zaidi ya kudai nafasi.

Znz inakusanya mapato ya TRA na wafanyakazi wa TRA wanalipiwa na TRA ya JMT.

Hii mana yake mapato yao ni kwa maendeleo yao ya ZNZ.
Mapato ya TRA Kigoma na Singida, Mbeya na Tangan yanagawanywa kwa JMT ikiwemo znz na wala si Tanganyika peke yake.

Taasisi na mashirika ya kimataifa yanalipwa na JMT ambayo znz haina mchango.
Mchango wa znz ni kudai nafasi tu. Hakuna mahali panaonyesha wanahudumiaje balozi, mashirika ya kimataifa ay taasisi nyingine

Wahisani wamegoma kutoa pesa, znz inaendelea kupata 4.5% kutoka BoT na 1.2 za watumishi wa muungano, huku wakiwa hawana habari na wizara ya ulinzi, mambo ya ndani na taasisi nyingine na mashirika ya kimataifa.

Hii inaonyesha kuwa hoja ya mikopo na misaada ni mfu kwasababu hata bila hayo znz inaendelea kuchota kilicho ‘chake’ bila huruma kutoka kwa masikini mlipa kodi wa Tanganyika

Ni kwa msingi huo, znz nchi yenye watu wachache kuliko jimbo la Ubungo imeweza kuwa na Rais na makamu wawaili. Hii inatokana na ukweli kuwa, mzigo na gharama za SMZ anazibeba Mtanganyika, hivyo wao kugawana vyeo si jambo la ajabu

Inaendelea Hoja (1B)

Nguruvi3,

Mara nyingi sana napata taabu sana na maneno yako hususan unapojikita katika UCHUMI. Siku zote napata taabu kwani mimi nimekaa na mara kadhaa nimewahi kuwa mkuu wa kitengo cha bajeti katika Wizara ya fedhwa na mipango wa Muungano. (1979 - 1983).

Kuna masuala ya msingi labda uniweke wazi na kwa kuwa nafuatilia kwa karibu sana bajeti za JMTz na ile ya SUK Znz kwa miaka yote labda nijibu masuala haya:
1. Je JMTz wanachangia katika account gani pesa zake za muungano?
2. Je Znz anatakiwa kuchangia kiasi gani katika muungano?
3. Nieleze kwa kutumia bajeti ya 2012/13 au 2013/14 au 2014/15 ni wapi wameeleza michango hiyo ya kila mshiriki katika huo muungano wenu
4. Naomba jina la hiyo account ambayo kila nchi inatakiwa kuchangia humo na kujua nani msimamizi wake.

Haya kwangu ni mas'ala ya msingi sana katika kuweza kudadavua masuala ya uchumi. Kwa kwa watu wa TGK hta katika vikao vya harusi zenu mnakuwa na kamati za harusi na kunakuwa na uongozi kwa maana mwenyekiti, katibu na mweka hazina na wajumbe.

Kila mtu nayechangia katika harusi hiyo pesa hizo anapeleka kwa mwekahazina na kila kunapofanyika kikao basi LAAZIMA TAARIFA YA FEDHWA kwa maana kila mtu amechangia kiasi gani laazima isomwe na hata kukabidhiwa nakala. Na kamti yote kwa jumla ndio inayoridhia na kupitisha matumizi ya kila kitu ikiwemo ukumbi, mc, music,etc.

Huo ni mfumo basic kabisa wa uchumi na hata nchi zikiungana zinapita katika mfumo kama huo lakin unakuwa na uwazi zaidi kutokana na wingi wa mambo lakin mkusanya mapato na kuidhinisha matumizi ni llaazima ajulikane.

Pole sana

 
Inaendele majibu

(1b) Mgao wa keki ya taifa
Hakuna haki isiyo na wajibu.
Mgao wa keki ya taifa lazima uwe na namna ya kuutafuta.
Znz haina mchango wa keki ya taifa. Haki ya kudai keki ya mtu inatoka wapi.


Hakuna mkoa Tanganyika unaodai keki kama separate entity, znz wana haki gani zaidi ya Singida, Mtwara au Lindi kwenye wananchi wanaowajibika kwa serikali yao kodi

Znz haina haki ya keki ya taifa ljingine. Kama wanaomba hiyo si haki. Msaada haugeuki kuwa haki.
Hawana haki ya kudai wasichojua kinapatikana wapi.


(2) Zanzibar wanafaifika vipi na rasilimali mali ya taifa hili.
Nimeonyesha jinsi wanavyopewa zawadi kama sehemu ya kufadika na rasilimali na mali za taifa hili.

Dhabu na ndizi za Muleba zinasomesha watoto wao 1024, wao wamekimbilia kuondoa mafuta na gesi ili Mtanganyika asijenufaika.
Wameweka vikwazo vya kitambulisho n.k. kuzuia Watanganyika katika fursa mfano,
ardhi, yao wameiwekea vikwazo na tena wakijisifu.
Angali video utaona jinsi gani walivyo na kauli za jeuri kudai haki ya ardhi kwaUtanzania


Znz hawahitaji kudaia zaidi wanachokipata. Na kama wanadhani kuna kuonewa, ni vema wakaondoka.

Tupo hapa kuwasaidia wapate taifa lao, uonevu ufike mwisho. Nini kinawakwaza kuishi katika maonezi ya ‘mkoloni' Tanganyika?
Let them go to live in paradise, hakuna anayewazuia.

(3) Ni haki znz kujivunia uzanzibar .Hakuna tatizo kwa hilo.
Tatizo ni pale wanapovua uzanzibar wakati wa kuhemea
Huku kujificha katika koti ndiko tunakulaani na hatukutaki.
Wanaweza kuja kuomba msaada kama wazanzibar, lakini si Watanzania maana huo Utanzania kwao ni haramu.

Sisi wengine tunahitaji Tanganyika ili tuhangaike na umasikini na mafisadi wetu
Hatuwezi kuchukua zaidi ya bilioni 300 za masikini wa Tanganyika kwenda kujenga nchi jirani ya znz(wanasema wao nimekuonyesha).

Ni makosa mkoa masikini kulipia kodi za utitiri wa viongozi wa znz. Huo mzigo waubebe wenyewe.
Hawawezi kutafuta matatizo kasha kutubebesha mzigo. Hawatutambui hawa! Kama wangetutambua wasingekuwa wabaguzi

(3) Tanganyika ni masikini sana nimesema hilo. Hakuna mahali nimesema ni tajiri.

Ni katika umasikini wa Tanganyika ndipo tunajiuliza, kwanini masikini wa Singida alipe kodi ya utitiri wa viongozi wa nchi jirani

(4)Sihitaji kujiita Mtanganyika, ninahitaji uwepo wa Tanganyika.
Ni kero kuwa na znz ambayo haina hawana madai ya maana au namna ya kujenga muungano.

Tumeonyesha, mchango wao ni sifuri, na hata rasilimali zao ndio hivyo tena. Tanganyika inaihitaji znz ?

Labda utuonyesha tunaihitaji znz kwa lipi na kitu gani mwaka 2015? Ulinzi! Upi katika dunia ya leo

(6) Tumevumilia sana tusiwe kama wao. Kinachoudhi ni wao kudhani ni sehemu muhimu sana ya muungano.
Wamefikia mahali wanadai msaada kama haki. Wana haki gani bila wajibu


Wanajitambulisha kama sehemu tofauti na muhimu ya taifa hili inayohitaji priority ya ina fulani.

Hatuwezi kuendelea kuishi na malalamiko yasiyo na msingi
Tuna mambo mengi ya kushugulikia na wala si kuwasikiliza wznz wanataka nini.
Wapewe taifa lao nasi tuwe na letu. Kama wanahitaji msaada, tukutane tunapodhani kuna masilahi iyo wanapodhani wana nufaika.


Tuna umasikini, ufisadi n.k. ambavyo ni muhimu sana kujadili kuliko mjadala wa znz ambao hata wasipokuwepo haina athari kwa Mtanganyika.

Nguruvi3,

mawazo yako yangekuwa kwa wajumbe wote wa kutoka Tgk basi pale katika Bunge la katiba mpya. Na katika kura yake ya kuipitisha rasimu hiyo kuwa katiba pendekezwa basi ingepata taabu sana kupita kwa upande wa TGK.

Labda nikuulize je kwanini katiba pendekezwa ilipata taabu sana kupitishwa kwa upande wa Znz na sio TGK?

Fikiri.

 
Nguruvi3,
umeandika hivi
Znz inakusanya mapato ya TRA na wafanyakazi wa TRA wanalipiwa na TRA ya JMT.

Ebu fafanua hili maana sikukuelewa kabisa unless wewe mwenyewe unaandika vitu pasipo kujua maana ya miundo wa serikali...
 
Nguruvi3,
umeandika hivi

Ebu fafanua hili maana sikukuelewa kabisa unless wewe mwenyewe unaandika vitu pasipo kujua maana ya miundo wa serikali...

Mkandara utapoteza muda tu kwani hana alijualo kata uchumi n hata mfumo wa Serikali wa nchi yake.

Kwa bahti kubwa leo nilibahatika kukutana na Mh Saada na Mh Malima pale SERENA hotel katika GCC INVESTMENT PROMOTION FORUM IN TZ na tumejadil mengi sana ikiwemo fursa za uwekezaji na sijasikia lolote miongoni mwa maneno ya Nguruvi3.

Nguruvi3 nakushauri fika kesho aljumaa SERENA ujifunze mengi kuhusu nchi yako Nitakuwepo.
 
Mkandara utapoteza muda tu kwani hana alijualo kata uchumi n hata mfumo wa Serikali wa nchi yake.

Kwa bahti kubwa leo nilibahatika kukutana na Mh Saada na Mh Malima pale SERENA hotel katika GCC INVESTMENT PROMOTION FORUM IN TZ na tumejadil mengi sana ikiwemo fursa za uwekezaji na sijasikia lolote miongoni mwa maneno ya Nguruvi3.

Nguruvi3 nakushauri fika kesho aljumaa SERENA ujifunze mengi kuhusu nchi yako Nitakuwepo.
Kwanza nikushukuru, kumbe ulipokuwa kwenye mkutano bado ulikuwa unawaza mabandiko ya Nguruvi na pengine kutaraji kimoja kingejitokeza. Hiyo reflection tu kwangu mimi imenitia sana moyo. Ndani ya forum, yapo aliyekuwa ananinfikira

Pili, Unapomwambia swahba Mkandara asipoteze, unamdanganya. Wewe uliyepo hapa ukisoma tena na kufikiria ukiwa serena Hotel sijui kama unapoteza muda. Laiti ungehisi hivyo basi usingeweza hata kuandika lolote. Unapoandika tayari unatumia muda wako kwasababu nzuri. Na muhimu, si lazima wewe au Mkandara msome mabandiko haya! mna hiari kabisa

Tatu, nadhani hoja zinajibiwa kwa hoja. Wewe unayefahamu uchumi na mfumo ulitakiwa uufahamishe umma wapi sahihi na wapi ni makosa. Kinyume chake unakuwa bingwa wa kuporomosha matusi.
Najua siku zote azma yako ni kuvuruga nyuzi na mabandiko ya duru. Ninakuhakikishia tutaendelea kusema tunachoataka kusema si kile unachotaka kusikia.

Nadhani, hatuwatendei haki wasomaji, njia nzuri ya kujibu hoja zisizo na mashiko ni kupuuza, na hilo tunalianza sasa.
 
MWANASHERIA NAJMA WA ZNZ ALIPOPOTOSHA UMMA

https://www.youtube.com/watch?v=YthCo16Bx-0

Video hiyo inaonyesha mwanasheria wa znz akieleza kuhusu tatizo la rasimu ya Warioba katika maeneo tofauti.
Msemaji amedai uwepo wa Polisi katika nchi washirika na wale wa serikali ya shirikisho kutaleta mvugano katika kupokea amri na utekelezaji.

Najma hakufanya utafiti wa kutosha kutoka nchi zenye mifumo hiyo.
Kwa mfano, nchi Marekani kila Jimbo kwa maana ya state ina Polisi, vyombo vya sheria, mahakama n.k. ambavyo ni tofauti kabisa na state nyingine.

Pale inapobidi, sheria za Marekani zimetoa idhini kwa serikali kuu kuingilia kati serikali za majimbo kwa kufuata utaratibu maalumu

Ndio msingi wa kusikia kuna uchunguzi unaohusu FBI n.k.
Hivyo uwepo wa Polisi wa nchi washirika si tatizo kama Najma anavyodai.

Mfano wa Pili, ni nchi kama Canada, na hili Mkandara atalithibitisha kama lina shaka.
Kuna polisi wa majimbo, miji na hata vimiji ndani ya miji.

Pia wapo Polisi wa shirikisho wanaojulikana kama RCMP.
Zipo taratibu zinaongoza maingiliano ya kazi za makundi hayo. Hakuna tatizo lililojiyokeza katika utekelezaji.

Najma amesahau kuwa rasimu ya Warioba ilieleza vema mambo 7 ya msingi ya pamoja, na yale ya washirika.
Hakudurusu kubaini maana nzima ya ulinzi na usalama, hivyo kutoa hoja bila kuwa na utafiti au kuzingatia weledi wa taaluama yake.

Najma alificha ukweli usiotakiwa kuelezwa hasa kwa Watanganyika.

Waziri Mkuya amethibitisha kuwa mapato ya TRA hayavuki bahari.
Hii maana yake kinachoingia hazina kuu Dar es Salaam ni kile cha Watanganyika.

Kuondoa Polisi ina maana ni kuweka jukumu la kuhudumia Polisi wa SMZ. Kwasasa hawana jukumu hilo.

Kazi ya kuhudumia Polisi wa zanzibar kimasilahi, mshahara n.k. ni jukumu la wizara ya mambo ya ndani ya JMT.

Hapa ni kodi za Watanganyika tu zinazofanya kazi na ndio msingi wa Najma kuficha ukweli kwa udanganyifu hoja ya Polisi

Suala la pili alilozungumzia Najma na vyama vya siasa.
Akasema iwapo kutakuwa na vyama vinavyoongoza kutoka nchi washirika tofauti, hilo litaleta mfarakano.

Najma haelewei kuwa serikali ya shirikisho ilikuwa na mambo 7 tu ambayo ndiyo yanabeba sehemu muhimu ya sera za nchi.

Mfano, katika nchi ya Marekani Republican wanaweza kuongoza state fulani, Democ state tofauti na bado halijaleta tatizo lolote.

Ndivyo pia ilivyo katika nchi nyingine kama Canada.
Katika jimbo la Ontario chama kiachoongoza ni Liberal, na jimbo la Alberta ni conservative.

Serikali kuu inaongozwa na conservative. Hakuna tatizo
Yote yanayosemwa na akina Najma, ni kutokana na kupewa majukumu bila kufikiri kiasi gani yanaathiri heshima zao katika jamii

Najma alitakiwa ajiridhidhishe na anachokisema si kuwakosoa manguli Prof Palamagamba, mzee Warioba, Prof Baregu na wenzao

Hapo pia tunajifunza somo kuwa, kuna tatizo visiwani. Na pia somo kwa Watanganyika hasa kwa mzigo wanaobebeshwa bila kujua hatma yake kimasilahi ni ipi.

Tusemezane
 
Kwanza nikushukuru, kumbe ulipokuwa kwenye mkutano bado ulikuwa unawaza mabandiko ya Nguruvi na pengine kutaraji kimoja kingejitokeza. Hiyo reflection tu kwangu mimi imenitia sana moyo. Ndani ya forum, yapo aliyekuwa ananinfikira

Pili, Unapomwambia swahba Mkandara asipoteze, unamdanganya. Wewe uliyepo hapa ukisoma tena na kufikiria ukiwa serena Hotel sijui kama unapoteza muda. Laiti ungehisi hivyo basi usingeweza hata kuandika lolote. Unapoandika tayari unatumia muda wako kwasababu nzuri. Na muhimu, si lazima wewe au Mkandara msome mabandiko haya! mna hiari kabisa

Tatu, nadhani hoja zinajibiwa kwa hoja. Wewe unayefahamu uchumi na mfumo ulitakiwa uufahamishe umma wapi sahihi na wapi ni makosa. Kinyume chake unakuwa bingwa wa kuporomosha matusi.
Najua siku zote azma yako ni kuvuruga nyuzi na mabandiko ya duru. Ninakuhakikishia tutaendelea kusema tunachoataka kusema si kile unachotaka kusikia.

Nadhani, hatuwatendei haki wasomaji, njia nzuri ya kujibu hoja zisizo na mashiko ni kupuuza, na hilo tunalianza sasa.

Nguruvi3,

Napenda kusema katika katika andiko langu lolote lile NIMEPOROMOSHA MATUSI naomba liweke hadhwarani nami nitawajibika kwalo.mara zote ninakusisitiza USOME na kubainisha ILMU ni bora sana katika majadiliano na sio mameno au vijambo vya katika vilabu vya pombe. Hizo ni bayana na sifikirii kama zitaweza kuwa na mbadala.

Kinachokusumbua Nguruvi3 ahali yangu wewe ni CHUKI NA DHWARAU DHIDI YA ZNZ NA WAZNZ na hivyo kukupelekea kuandika ndivyo sivyo na kila baya kulipeleka Znz na kusahau ukweli ambao upo wazi. Ushabiki wako ni mbaya sana katika uandishi wako.

Hakika ni mara nyingi sana nimebainisha solutions ya huu Muungano wenu ili kuondoa malalamiko na manung'uniko kwa kila upande ni KUTIMIZA ILE SHARIA ILIYOPITISHWA NA BUNGE LA MUUNGANO YA UANZISHWAJI WA JOINT FINANCE COMMISSION (JFC)(Tume ya pamoja ya fedhwa na uchumi) ili kila kitu kiwe hadhwarani.

Kwani kwa kutimiza sharia hii ya kuanzishwa JFC kutaweka KILA KITU KITAKUWA HADHWARANI yaani
1. Kila mmoja ataelezwa achangia kiasi gani katika muungano kwa mujibu wa formula watakayotumia.
2. Kila mtu ataonekana amechangia kiasi gani katika muungano.
3. Kutukuwa na usawa wa wafanyakazi kwa mujibu wa formula itakayotumika.
4. kutakuwa ma mgawanyo uliosawia kwa mujibu wa formula kwa misaada na mikopo yote.
5. Uwazi wa masuala yooote ya kiuchumi na kijamii ya muungano na kuondosha malalamiko.

Kukataa kuitumia Sharia hii ya kuanzishwa JFC ndio chanzo kikubwa sana cha manung'uniko na malalamiko katika muungano huo.


Haya nilibainisha siku nyingi sana kwako ila unafumbia macho tu na kuzidi kutoa shutuma dhidi ya Znz na waZnz na kuwazulia mambo ambayo si kweli na hata kimantiki hayana uzito wala nini.

ushauri wangu kwako. UCHUMI NI TAALUMA AMBAYO INASIMAMIWA NA DATA na si bla bla na maneno ya kwenye ma PUB.

Pole sana.

Nguruvi3 unaweza kunipata kwa darsa zaidi kwa siku ya leo kutumia local number 255 777 420 000.

 
MWANASHERIA NAJMA WA ZNZ ALIPOPOTOSHA UMMA

https://www.youtube.com/watch?v=YthCo16Bx-0

Video hiyo inaonyesha mwanasheria wa znz akieleza kuhusu tatizo la rasimu ya Warioba katika maeneo tofauti.
Msemaji amedai uwepo wa Polisi katika nchi washirika na wale wa serikali ya shirikisho kutaleta mvugano katika kupokea amri na utekelezaji.

Najma hakufanya utafiti wa kutosha kutoka nchi zenye mifumo hiyo.
Kwa mfano, nchi Marekani kila Jimbo kwa maana ya state ina Polisi, vyombo vya sheria, mahakama n.k. ambavyo ni tofauti kabisa na state nyingine.

Pale inapobidi, sheria za Marekani zimetoa idhini kwa serikali kuu kuingilia kati serikali za majimbo kwa kufuata utaratibu maalumu

Ndio msingi wa kusikia kuna uchunguzi unaohusu FBI n.k.
Hivyo uwepo wa Polisi wa nchi washirika si tatizo kama Najma anavyodai.

Mfano wa Pili, ni nchi kama Canada, na hili Mkandara atalithibitisha kama lina shaka.
Kuna polisi wa majimbo, miji na hata vimiji ndani ya miji.

Pia wapo Polisi wa shirikisho wanaojulikana kama RCMP.
Zipo taratibu zinaongoza maingiliano ya kazi za makundi hayo. Hakuna tatizo lililojiyokeza katika utekelezaji.

Najma amesahau kuwa rasimu ya Warioba ilieleza vema mambo 7 ya msingi ya pamoja, na yale ya washirika.
Hakudurusu kubaini maana nzima ya ulinzi na usalama, hivyo kutoa hoja bila kuwa na utafiti au kuzingatia weledi wa taaluama yake.

Najma alificha ukweli usiotakiwa kuelezwa hasa kwa Watanganyika.

Waziri Mkuya amethibitisha kuwa mapato ya TRA hayavuki bahari.
Hii maana yake kinachoingia hazina kuu Dar es Salaam ni kile cha Watanganyika.

Kuondoa Polisi ina maana ni kuweka jukumu la kuhudumia Polisi wa SMZ. Kwasasa hawana jukumu hilo.

Kazi ya kuhudumia Polisi wa zanzibar kimasilahi, mshahara n.k. ni jukumu la wizara ya mambo ya ndani ya JMT.

Hapa ni kodi za Watanganyika tu zinazofanya kazi na ndio msingi wa Najma kuficha ukweli kwa udanganyifu hoja ya Polisi

Suala la pili alilozungumzia Najma na vyama vya siasa.
Akasema iwapo kutakuwa na vyama vinavyoongoza kutoka nchi washirika tofauti, hilo litaleta mfarakano.

Najma haelewei kuwa serikali ya shirikisho ilikuwa na mambo 7 tu ambayo ndiyo yanabeba sehemu muhimu ya sera za nchi.

Mfano, katika nchi ya Marekani Republican wanaweza kuongoza state fulani, Democ state tofauti na bado halijaleta tatizo lolote.

Ndivyo pia ilivyo katika nchi nyingine kama Canada.
Katika jimbo la Ontario chama kiachoongoza ni Liberal, na jimbo la Alberta ni conservative.

Serikali kuu inaongozwa na conservative. Hakuna tatizo
Yote yanayosemwa na akina Najma, ni kutokana na kupewa majukumu bila kufikiri kiasi gani yanaathiri heshima zao katika jamii

Najma alitakiwa ajiridhidhishe na anachokisema si kuwakosoa manguli Prof Palamagamba, mzee Warioba, Prof Baregu na wenzao

Hapo pia tunajifunza somo kuwa, kuna tatizo visiwani. Na pia somo kwa Watanganyika hasa kwa mzigo wanaobebeshwa bila kujua hatma yake kimasilahi ni ipi.

Tusemezane

Nguruvi3,

Mimi nazidi kukushauri tena na tena SIKU ZOOOTE LAAZIMA UJIFUNZE KUTENDA HAKI. Kumbuka si vizuri kuchukua video ya mtu na kuanza kuijadili humu wakti mtu mwenyewe hayupo humu ukumbini.. Mimi ningekushauri kama yeye alizungumza hadhwarani au katika kiriri cha siasa au gazeti ni vizuri na wewe utumie njia hiyo hiyo kumjibu. Hapo utakuwa umetenda haki. Kumbuka kwa kumpa nafasi mnaweza kupata mnakasha mzuri sana.

Mimi jana jioni saa mbili usiku nilikuwa Sea Cliff hotel nilibahatika kukaa na mwanasharia na mwanasiasa na kiongozi wa juu wa Serikali ya JMTz ambaye tulisoma wote mlimani. yeye alisimama kidete sana kuipinga rasimu ya Warioba na alinipa reasons zake. Nikijiuliza je ningepata nafasi ya kuonngea na Humprey Pole pole nafikiri ningepata mengine mengi zaidi. LaKIN NIKASEMA NIVURI MTUMIE BUSARA KATIKA KUILIMISHANA kuhusu katiba yenu kwani huo ni mustakabali wa maisha na maendeleo ya nchi yenu.


La kukukumbusha Znz ni nchi na vile nchi hiyo ina watu chini ya 1.5 milion na eneo lisilozidi 2000sq Km. hivyo lina mengi na wengi. kauli ya mtu mmoja sio kauli ya waZnz kwa ujumla wao.

Pole sana

 
Nguruvi3,

Mimi nazidi kukushauri tena na tena SIKU ZOOOTE LAAZIMA UJIFUNZE KUTENDA HAKI. Kumbuka si vizuri kuchukua video ya mtu na kuanza kuijadili humu wakti mtu mwenyewe hayupo humu ukumbini.. Mimi ningekushauri kama yeye alizungumza hadhwarani au katika kiriri cha siasa au gazeti ni vizuri na wewe utumie njia hiyo hiyo kumjibu. Hapo utakuwa umetenda haki. Kumbuka kwa kumpa nafasi mnaweza kupata mnakasha mzuri sana.
.....
....................................................

La kukukumbusha Znz ni nchi na vile nchi hiyo ina watu chini ya 1.5 milion na eneo lisilozidi 2000sq Km. hivyo lina mengi na wengi. kauli ya mtu mmoja sio kauli ya waZnz kwa ujumla wao.

.....


Nyekundu: Hapa haujitendei haki kwa kumkingia kifua chako Waziri wako wa sheria, ili kauli zake zisijadiliwe hapa jukwaani kwa kigezo cha 'si vizuri kutumia video kujadilia'. Na sema haujitendei haki kwa sababu, kwanza kwa taratibu za jukwaa hili hakuna mahala pameelekeza kuzuia hilo. Pia kumbuka Mwanasheria wa Zanzibar ni mtu muhimu huko zanzibar na mahala pengine ambapo kuna wadau wanaoguswa na tasnia ya sheria. Kujadili kauli zake kupitia nukuu za video ni muhimu pia.

Na shangaa hotuba za wabunge, madiwani, kada wa vyama, marais, wahandisi, walimu, nakadhalika kauli zao zinajadiliwa kwa kutumia vyombo mbalimbali tofauti na vyombo ambavyo walivitumia kutoa kauli zao, na wala hakuna malalamiko kama haya ya kwako dhidi ya mwanzisha mada hii...! Mwezi disemba tumejadili hotuba ya Prof. Jakaya aliyoitoa kuhusu escrow... kwa kutumia video, magazeti n.k.(wakati yeye alitoa kauli zake kwa njia ya redio na televisheni, hatujamsikia Salva R. akilalamika); bado tunaendelea kujadili hotuba mbalimbali za Baba wa Taifa la Zanzibar Sheikh A. A. Karume (R.I.P), Baba wa taifa la Tanganyika baadaye Tanzania Mwl. J.K.Nyerere (R.I.P) walizozitoa na kunakiliwa katika video bila kukingiwa vifua...tena hao hatunao kimwili...!!!

Hivi unajua sababu za hao walioweka video hizo Youtube...!? Sababu kubwa, naweza kuhakikishia, ilikuwa watu wote wajue kilichosemwa na mwanasheria na wenzake, na wakijadili. Walijua kabisa akina Nguruvi3 na wenzake akiipata wanaweza kuijadili. Na mijadala inafanyika kwa njia mbalimbali ikiwemo hii ya hapa JF. Nguruvi3 anaanzisha mada hapa jukwaani kwa lengo la kueleimisha, kuhabarisha, na kujieleimisha(3K) kupitia mijadala. Neno alitumialo (Nguruvi3) la Tusemezane kwa kiasi kikubwa linabeba dhana hiyo ya 3K.

Si vyema/vema hata kidogo kijinyima haki ya kujielemisha, kuelimisha, kuhabarisha kwa kuzuia mijadala inayotokea kutokana na kauli wanazozitoa na kunakiliwa katika vyombo mbalimbali vya mawasiliano kisa tu lazima wahusika wahusishwe kwenye mjadala. Wewe ni 'member' humu JF muhabarishe (mwanasheria wako) aje ajiunge jukwaani ili ajibu hoja zinazotolewa juu ya kauli zake alizozitoa na kunakiliwa kwenye video.

Bluu: Ushauri wako si mzuri, kama kweli unataka kujitendea haki pia kumtendea haki mwanasheria wako mshauri ajiunge JF na aanze kujibu hoja zinazomkabili hapa, kama nilivyoelekeza aya ya mwisho ya sehemu ya kwanza.

Kijani: Nafasi iko wazi hapa JF wala hajachelewa.
 
Back
Top Bottom