LITAIBUKA KUNDI LA KUJENGA HOJA
HUO NDIO UTAKUWA MWANZO WA KUVUNJIKA MUUNGANO
Tunaona jinsi CCM wanavyotumia ulaghai wa vijana na akina mama kama ndilo tatizo kubwa la katiba.
Wanaficha ukweli ikiwemo maadili yanayowahusu na mambo yanayolikabili taifa kwa hoja laini tamu tamu.
Mbinu hii ni kama ‘big G'. Haina muda thamani yake itakwisha.
Mfano, kuna wizara maalumu inayoshughulikia akina mama na watoto
Kwa miaka zaidi ya 10 wizara hii imekuwa sehemu ya ajira tu ikiwaacha akina mama huko vijijini hoi.
Laiti ingekuwa na mashiko, basi hoja ya akina mama isingekuwepo kwasababu chombo kinachoshughulikia tayari kipo.
Pamoja na uwepo wake akina mama bado wanajifungua katika matenga ya baiskeli, vifo vyao wakati wa uzazi ‘maternal death' ni vingi na vifo vya watoto chini ya umri wa miaka 5 ni vingi sana.
Ukiangalia kwa undani vifo hivyo vinazuilika.
Kwanini basi serikali isianzie hapo hadi kuweka usawa wa jinsia kikatiba? Hao wabunge sawa wanasaidiaje akina mama wa vijijini endapo sasa hawawezi kusema wanabaki na misimamo ya CCM ?
Kwani tatizo la akina mama ni haki au ni usawa wa jinsia? Inakuwaje basi akina mama ambao ni wapiga kura wengi hao hao wachague wanaume kuwaongoza endapo mfumo uliopo unawanyima haki kwa kutokuwa na usawa?
Hoja kubwa hapa si uaswa wa jinsia, ni kueleza tu kuwa katiba ni sukari guru wanayopewa.
Baada ya mradi wa Chenge/Sitta kukamilika, sheria zitakazowahusu hazitatiliwa maanani.
Katiba itatamka, hawatetenda kwa sasbabu hawajaweza kutenda leo hii, na mradi wao utakuwa umekamilika
Kuhusu vijana, nako kuna tatizo. Kwasasa tuna mbaraza ya vijana.
Vijana hao hao wanaosemwa katika mradi wa Chenge/Sitta hawjaweza kuwa kitu kimoja.
Tunaona wakitumika kama karatasi za maliwato kama wapiga debe na si watu wanaotazama siku za mbeleni ''shape their future''
Kuwatengenezea baraza ni kutafuta kuungwa mkono. Hakuna kitakachofanyika zaidi kwasababu hata sasa hivi hawana haki ya elimu. Wangapi hawana mikopo au uwezo wa kulipa ada za kumaliza masomo ya sekondari?
Wangapi hawana ajaira na je, baraza tamu waliloahidiwa na Chenge linamaliza vipi matatizo yao?
Hoja kubwa hapa ni kuonyesha jinsi nao watakavyotumika na kutupwa kama walivyotumika viongozi wa dini katika mchakato.
Pamoja na matamko na jitihada za kuunga mkono mradi wa Chenge/Sitta, mwisho wa siku Sitta kawaita wapuuzi.
Mbinu za kutoa peremende kwa wazanzibar na Big G kwa vijana na akina mama ni hafifu sana.
Litatokea kundi lenye weledi litakalohitaji majibu ya maswali ambayo CCM hawana kwa sasa na wala hawatakuwa nayo. Miongoni mwa maswali hayo ni ya kiuchumi na hata kugusa muungano wenyewe.
Mathhalani, vijana watakapohoji nini faida za muungano.
Kwanini hakuna uwiano katika kuubeba muungano. Kwanini wao walipe gharama za muungano ikiwa tuna muungano.
Kwanini upande mmoja wa muungano upewe kipaumbele na ufumbiwe macho katika kuwajibika kitaifa.
Nini maana ya investment kubwa zznz na return yake ni nini
Ikifika hapo itatafutwa hoja ndogo tu ya kuhalalisha madai yao.
Ndivyo ilivyokuwa kwa Jumbe, Nyalali n.k. Kwamba, G55 ilipopata mwanya wa passport na IOC basi Tanganyika ikadaiwa kwa nguvu hasa.
Haikuwa nguvu ya mbavu au wizi wa kura wa Sitta, ilikuwa nguvu ya hoja inayozizima hadi leo.
Na hapo ndipo sababu ndogo tu itahitimisha muungano.
Sijui kama wanaolitakia taifa hili mema wanaona hatari hiyo.
Tusemezane
cc
Alinda gfsonwin