Edward Lowassa arejea CCM, apokelewa na Uongozi wa juu wa chama

Edward Lowassa arejea CCM, apokelewa na Uongozi wa juu wa chama

Huu uzi umeanzishwa saa kumi na moja jioni sasa hivi una repplies zaidi ya 850.kesho full day watu wengi wapo sijui utafika wapi.
Maskini Ruge katupwa kapuni.
 
Hapo kwenye kampuni hewa ya korosho 'kutoka Kenya' nazidi kukazia. Bongo lala Bongo nyoso.
Kagoda, Richmond nyingine inanukia ooh nimesahau kampuni ya korosho toka kenya
 
jiwe anamwisho mmbaya sana mbinu anazotumia.

mambo anayofanya hayana tija kwa taifa.

uchumi unakufa yeye anahangaika na hama hama.
 
Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa Amerejea Rasmi CCM Leo.

Amepokelewa Lumumba Makao Makuu Madogo Ya Chama Cha Mapinduzi Na Katibu Mkuu Dr Bashiru Ally.

Aidha, katika mapokezi hayo walikuwepo Rais Magufuli, Rostam Aziz, Mzee Phillip Mangula, Waziri Mkuu Majaliwa Kassim, Humphrey Polepole n.k



View attachment 1035375
View attachment 1035459
View attachment 1035448

Unaweza soma pia:

Edward Lowassa na Frederick Sumaye mbioni kurejea CCM - JamiiForums

Edward Lowassa: Wanaodhani nitarudi CCM wanapiga porojo na kuota ndoto - JamiiForums

Lowassa hana namna zaidi ya kuipigia magoti CCM, Mkwewe Sioi Sumari mpaka sasa yupo lockup - JamiiForums



Mimi binafsi sitadiriki kumlaumu Mzee Lowassa kwa uamuzi aliochukua. Kufanya siasa katika mazingira ya awamu hii iliyojaa "Hostility" na kwa umri wake ni ngumu sana.

Wapenzi na wanachama wa Chadema wanatakiwa wamshukuru Mzee Lowassa kwa kukiwezesha chama chao kupata madiwani wengi na wabunge ijapokuwa baadaye wale waliomfuata walirudi walikotoka.

Jambo lingine ambalo namsifu mzee Lowassa ni hekima na busara iliyotukuka ya kuvumilia kejeli na masimango ya CCM. Mwenyezi Mungu amemlipia hapa hapa duniani kwa kuwaabisha wabaya wake waliokuwa wanamwita fisadi; leo wamempokea kwa nderemo na vifijo akiwemo kubwa la maadui!

Ombi langu kwa vijana wa Chadema tuendelee kumpa heshima mzee wetu. Tusitoe maneno ya kejeli wala kashfa kwa kuwa Mwenyezi Mungu ameamua kutufungua macho kuwa kwa mwanasiasa kuitwa fisadi au msaliti au kibaraka wa mabeberu ni msemo wa kupita na unaweza ukabadilika muda wowote.
 
Wimbo ulianza kwa chadema, hakuna kupinga. Kila pembe ilikuwa ni "Lowassa fisadi, Lowassa fisadi" alipokosa kuteuliwa kuwania urais wa tiketi CCM akajitoa CCM na kuhamia chadema, akapewa nafasi ya kugombea urais kwa tiketi ya chadema, ghafla chorus ya "Lowassa fisadi, Lowassa fisadi" ikawa inaimbwa na wana CCM.

Sasa karudi CCM nani ataiimba chorus hiyo?

Siasa ni mchezo mbaya sana.
Achunguzwe tuhuma za Richmond
 
Hii ni faida zaidi kwa upinzani kama wataamua kutulia nakujipanga vizuri.Kwasababu hali ya kisiasa ya huyo mzee lilikua robo tatu ccm na robo upinzani kwaiyo kuondoka kwake kutaifanya chadema kupumua zaidi nakujipanga na uko ccm mzee kaenda kuungana ile robo tatu yake aliyokua kaiacha nakwavile ile robo tatu yake iliyobaki ccm ilikua imepooza itafufuka sasa.Kwaiyo tutegemee ccm kua naushindani mkubwa sana wa ndani kwa ndani kwasababu kundi hili sioni kama ni kundi lakukaa kimya nakusubiri mwenyekiti apange nakuamua.ile robo aliyokua nayo mzee cdm ilishindwa kufurukuta kwasababu walikua ugenini kwaiyo kurudi kwa mzee ccm kunawapa nguvu zaidi yakufufuka.Ngoja tuone maana muda ni mwalim mzuri.Mim binafsi credit naitupa Upinzani.
Watajipangaje na wakati wako jela,itabidi wawe majasiri kama late mzee Mandela.yaan upinzani unakufa,na uchaguzi serikali za mitaa hampati hata kiti kimoja,kwenye ubunge 2020 mkivusha wabunge watatu tu, mshukuru sana.
 
Wimbo ulianza kwa chadema, hakuna kupinga. Kila pembe ilikuwa ni "Lowassa fisadi, Lowassa fisadi" alipokosa kuteuliwa kuwania urais wa tiketi CCM akajitoa CCM na kuhamia chadema, akapewa nafasi ya kugombea urais kwa tiketi ya chadema, ghafla chorus ya "Lowassa fisadi, Lowassa fisadi" ikawa inaimbwa na wana CCM.

Sasa karudi CCM nani ataiimba chorus hiyo?

Siasa ni mchezo mbaya sana.
WANASIASA WOTE WATASEMA LOWASA SI FISADI NA MWANASIASA BORA WA KARNE
 
Back
Top Bottom