Tetesi: Edward Lowassa kuongea na vyombo vya habari kesho kwenye hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam

Status
Not open for further replies.
Wape faraja kesho... Wanakupenda sana. Kumbuka zile kura million 6 na ushee kumbuka matusi kashfa na kejeli na tuhuma lundo ulizotupiwa... Usije ukawa mwepesi kusahau... Utawaumiza na kuwaliza wengi sana... Usijiwazie wewe... Wawazie hawa watu wanaokupenda sana.

Muda unayoyoma watu wamejawa na kihoro kuwa kesho utaongea nini.. Baadhi wanasema maandalizi ya leo kule Pugu hayakuwa ya hasanali bali wewe... Safari yako ya ikulu na matamshi yako yale tayari yameshawasononesha wengi sana... Ni simanzi kila mahali...

Una utashi msimamo na maamuzi binafsi lakini una tafakuri na hekima pia... Kama ukiamua kurudi ccm waweza kwenda.. Hakuna atakayeweza kukuzuia... Lakini utaleta Maumivu kwa mamilioni ya watanzania waliohangaika nawe bega kwa bega usiku na mchana..

Kuna watu si haba wameumizwa kuteswa na kudhulumiwa maisha na mali zao kwa sababu tu ya kukuunga mkono wewe... Usije kuwasahau hawa... Wengine bado wako mahabusu na wengine wanatumikia vifungo usiwasahau pia.

Watanzania wanapitia kipindi kigumu sana.. Wana sononeko na majonzi hawahitaji kuumizwa zaidi.. Wape faraja wafurahi..

Ikishindikana kabisa waweza kwenda.. Watakaobaki wataukomboa wakati!
 

Umepokea we we umekua liongo abubakar,acha ujinga
 


Kwani hao Watanzania si watamfwata huko aendako?
 
Mshingae katangaza kurejea CCM, wanasiasa watu hatari Sana. OK Ngoja tusubiri.
 
Duh, stori za lissu zote zimezikwa leo, hamna anaeongea ya kamanda lissu for presidence wala sijui kaenda Brussels.
[emoji23] [emoji23] [emoji23] ndio Tanzania “Average mind discuss event” ko usijali sana kaka
 
Mh Lowassa kama atarudi CCM, atakuwa amerudi na mafanikio makubwa kisiasa, kwake kibinafsi:-

1) Hatakuwa tena fisadi (CCM wala Chadema)

2) Atakuwa amejipatia utulivu ambao mwanzoni hakuwa nayo kutokana na kuandamwa andamwa.

3) Atakuwa amepanua wigo mpana wa mashabiki wake (maana sasa anao kotekote).

4) Atakuwa kama siki kwenye meno ya Mh Mbowe na baadhi ya viongozi wa Upinzani.

Na la mwisho, nadhani ndio la muhimu;

5) Mh Lowassa atakuwa funzo moja kubwa na la mwisho (huenda) kwa Chadema na Upinzani kwa ujumla wake; watajifunza namna ya kudili na watu watokao CCM sasa hivi na katika siku sijazo.
 
Kuamua mrengo wa kufuata ni haki na utashi wa mtu ila huyu mzee kama kesho atatangaza kurudi CCM..

Atatia aibu heshima na misimamo aliyojijengea saana. Wanasiasa wamekuwa kama manungayembe yanayoolewa na kuachika na kutafuta mabwana wapya kila uchwayo.
 
Wala sitaki hata kumsikia huyu mtu kuanzia leo. Kaniharibia siku hakuna kunacholika wala kunyweka mpaka muda huu. Heri nikapumzike kambi za alshababu!!
Muhim kujifunza siasa za kistaarab na si za kinafiki,kuweka akiba ya maneno ni muhim zaidi,kuwa mpinzani haimaanishi upinge kila jambo,mambo yanavyochange ndo hali huwa ivo,kajilazimishe kula kamanda.
 
Lema alivyotoa povu Leo hatari.Siasa mchezo wa ujanja ujanja naona ufipa akukaliki kabisa Sasa.
 
Mbona mnalia kiasi hiki??
Kesho ataongea kuwa kumsapoti JPM bila kuhama inawezekana. Tulieni.
 



Akirudi then a new opposition part is going to be born
 
Ni maoni yangu :MZEE atasfu siasa kesho
 
Huyu Lowassa naye akamuunge Mkono magu tubaki na Chadema yetu
 
Unidipu hiyo kesho akiongea
 
Nje ya muda wa wanga una maneno ya kugusa mkuu
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…