Embassy Hotel na Motel Agip: Nini hasa kilitokea?

Embassy Hotel na Motel Agip: Nini hasa kilitokea?

Hoteli ya Embassy ambayo ipo posta jijini Dar imeshazungushiwa uzio kama dalili ya mabadiliko fulani. Hoteli hii ilikuwa sokoni kitambo tu. Mwenye habari atujuze kinachoendelea kuhusu mmiliki na je watavunja na kuweka SKY Mark au ndiyo yale mabox yanapigwa rangi tena?

Two years ago kulikuwa na huu mjadala Nini haswa tatizo la iliyokuwa Embassy Hotel??
 
Duh, Kwakweli nimesikitika sana. Nilkua naiwinda sana hii hoteli niinunue. Lakini walificha sana kuhusu mauzo yake. I hope that alieipata ataifanyia kazi pasavyo. Namtakia mema na Mungu amsaidie
 
ndio nimepita juzi hapa nikaona, bongo kumebadilika saaana...nilikimbia tangu mwaka 1999 nimerudi sasa hizi nimekua kama mgeni anaejua sehemu kwa ramani tu.:nerd:
 
Wakikusikia "vijana" wa mjini unaliuzia hilo jengo wataku-mind kinoma, embassy siku hizi imegeuka gesti poa, unakamta mlupo wako unaongea na mlinzi mambo shwari, kwa kawaida wenyewe wanasema huwa wanawapoza walinzi kwa buku tano, ingawa vitanda mwanzoni vilikuwa na vumbi "(kwasababu ya kutotumika) sasa hivi mambo shwari kwani walinzi wanasafisha ili "biashara" yao iende sawa. Hiyo ndio bongo bwana kila mbuzi anakula kwa urefu wa kamba yake, wengine wana-access ya EPA basi acha na walinzi wa embassy nao wajipatie ka-EPA kao kadogodogo.

Na mavumbi yale kaka ukiingia si unatoka na mafua mabaya sana!???
 
Aiseeee babaangu nashauri kama alina kazi viwekwe vyumba liwe hostel kwa jili ya wanafunzi wa ifm na vyio jirani
 
Aiseeee babaangu nashauri kama alina kazi viwekwe vyumba liwe hostel kwa jili ya wanafunzi wa ifm na vyio jirani

Mkuu jana nimepita pale nikakuta Embassy imezungushiwa mabati. Hii ina maana kwamba aidha inafanyiwa karabati mkubwa ama inapigwa chini kinasimamishwa kitu kipya cha nguvu. Afadhali manake Embassy ambayo ilikuwa miongoni mwa Hotel murua hapa mjini iligeuka kuwa guest house ya machangu!
 
Wadau siku ya Tatu sasa napita eneo hili naona mafundi wakichomelea bodi ya gari(Lori).

Ina maana ssasa ni karakana rasmi kwa kazi hiyo!?

Tujuzane jamani!
 
zamani ilikuwa ni danguro ulikuwa unaongea na mlinzi unaingia kule kuna kitanda safi unamkunja demu wako unaondoka mwepesi
 
NAOMBA KUULIZA NI NANI MMILIKI WAKE?
KAMA NI YA SEREKALI KWA NINI WASIBINASFISHE!/
NA KUMBUKA ENZI HIZO DA, PALIKUWA NI ENEO TULIVU SANA HAPO NA AGIP HOTEL SIJUI IPO?AU ISHAJIFIA.
 
NAOMBA KUULIZA NI NANI MMILIKI WAKE?
KAMA NI YA SEREKALI KWA NINI WASIBINASFISHE!/
NA KUMBUKA ENZI HIZO DA, PALIKUWA NI ENEO TULIVU SANA HAPO NA AGIP HOTEL SIJUI IPO?AU ISHAJIFIA.
Kuna wakati nilisikia wamebinafsishiwa akina Mwinyi rais mstaafu.
 
NAOMBA KUULIZA NI NANI MMILIKI WAKE?
KAMA NI YA SEREKALI KWA NINI WASIBINASFISHE!/
NA KUMBUKA ENZI HIZO DA, PALIKUWA NI ENEO TULIVU SANA HAPO NA AGIP HOTEL SIJUI IPO?AU ISHAJIFIA.
Agip Hotel mkuu huwezi amini ukipita pale nje pamekuwa sehemu ya kuuzia vitabu na zile chuma kule juu zote zimekwisha kwa kuoza na pembeni kwenye zile ngazi kwasasa kuna garage na mafundi ndio hukaa hapo.
 
Wewe piga maji ya uhai kama Ray achana na mambo hiyo. Ukiwaza ya watu utachelewa yakwako
 
Nipo dsm. Haya wewe mtaalamu wa dar niambie peguot house iko wapi?
Na club maisha iko wapi?
Mkuu kwa nia njema tu peguot house iko pale mataa ya bibi titi na ohio pale juu kuna ofisi za bank ya Barclays,Maisha club kabla hujafika kilima nyege kuelekea barabara ya chole ukitokea mataa ya oysterbay shule,na Embassy hotel mkuu iko hapa opp na Imalaseko supermarket kabla hujafika PPF tower.
 
Mkuu kwa nia njema tu peguot house iko pale mataa ya bibi titi na ohio pale juu kuna ofisi za bank ya Barclays,Maisha club kabla hujafika kilima nyege kuelekea barabara ya chole ukitokea mataa ya oysterbay shule,na Embassy hotel mkuu iko hapa opp na Imalaseko supermarket kabla hujafika PPF tower.
Umeuwa
 
Back
Top Bottom