Emmanuel Tutuba ateuliwa na Rais Samia kuwa Gavana wa Benki Kuu (BoT)

Emmanuel Tutuba ateuliwa na Rais Samia kuwa Gavana wa Benki Kuu (BoT)

Nakumbuka wakati wa mwinyi uchumi uliyumba kiasi ukiwa na debe la.mahindi unaweza uza hata kwa laki 2
Hali ya kisiasa duniani ilipelekea sana uchumi kuyumba, pia Nyerere aliharibu sana uchumu, akamwachia zigo la Misumari mzee wa watu, ndio akapambana kuanzishwa kwa TRA na Mashirika mengine muhimu kabla ya Mkapa kuja kuyajengea uwezo
 
Bora tutuba kuliko luoga.
Kesho utabadilika na kusema vice verse sisi ndiyo watanzania vigeu geu.

Na ukiulizwa kwanini Luhoga si bora, tunajibu basi tu simpendi.
 
Ana uwezo huo?
Huyo Gavana ahakikishe sisi wananchi mifuko yetu inajaa pesa tunaweza hudumia familia zetu.

Sio kusaini tu hela zetu.

Otherwise hicho cheo itakua kwa faida yake na familia yake.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa viongozi kama ifuatavyo:-

1) Amemteua Bw. Emmanuel Mpawe Tutuba, Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango kuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT). Bw. Tutuba anachukua nafasi ya Prof. Florens Luoga ambaye amemaliza kipindi chake.

2) Aidha, amemteua Dkt. Natu El- Maamry Mwamba kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango.
Dkt. Mwamba alikuwa Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Undeshaji wa Kiwanja cha Ndege cha Kilimanjaro (KADCO).

Dkt. Mwamba anachukua nafasi ya Bw. Emmanuel M. Tutuba ambaye ameteuliwa kuwa Gavana wa Benki Kuu.

Teuzi hizi zinaanza mara moja.

View attachment 2472348
Jamaa kaweka rekodi ya kutumia kipindi kimoja tu madarakani. Watanguliz waliaminiwa vipindi viwili
 
Luoga alikuwa pale kimakosa,sidhani kama anajua hata balance sheet ni.nini,
Hata mie nilishangaa uteuzi wa Luoga ambaye ni Mwanasheria kusimamia Benki Kuu. Nategemea msimamizi wa Benki Kuu awe ni mtu aliyebobea katika masuala ya Benki, Uchumi na Fedha.

Kama ni kushauriwa basi ndo apate ushauri wa kisheria kutoka kwa wanasheria. Ila sio awe Mwanasheria ambaye anapata ushauri wa masuala ya kibenki, fedha na uchumi kutoka kwa wenye fani hizo.
 
Ujinga gani huu. Unafikiri BOT wakiachwa bila kudhibitiwa na serikali ndio watasaidia uchumi wa nchi kama yetu?
Sisi sio uingereza bhana. Hata hapo south afrika bank kuu iko huru na hisa ni makaburu ila inasaidia nini kukwamua uchumi kutoka mikononi kwa makaburu?
Awamu ya kwanza hadi ya tatu BOAT walikua kama kisiwa serikali haingilii. Bila shaka kama hamjui ni wizi mtupu ulikua unafanyika. Yule mbunge wa butiama kofia tarabushi mwenye firm ya sheria kapiga kupindukia pale benki kuu. Jpm alivyokuja kumbana akasusa ubunge akakimbilia kuishi miami marekani na wanae kula matunda ya ufisadi.
Mnakumbuka daudi balali awamu ya tatu mkapa alimleta toka marekana ndio tukaona madudu ya kutisha. Kina ande chande yule mhindi ndio wakawa wanapanga mambo benki kuu.
Mlaumuni jk kwa mengine lakini alikataa eti uhuru wa benki kuu kwa nchi kama yetu na kuanza kudhibiti mambo pale.
Nilikuwa sijui aisee.

Marekani wanalalamika suala la benki kuu yao (Federal Reserve Bureau) kuwa na wanahisa ambao wanalipwa faida.

Wanashangaa kwanini FRB iwe na wanahisa wakati hakuna taasisi nyingine yoyote inayoitwa "federal" yenye wanahisa.

Vipi unaongeleaje busara ya Magufuli kumteua Mwanasheria (Prof. Luoga) kuwa gavana wa BOT, badala ya kumteua mtaalam wa masuala ya fedha na benki?
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa viongozi kama ifuatavyo:-

1) Amemteua Bw. Emmanuel Mpawe Tutuba, Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango kuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT). Bw. Tutuba anachukua nafasi ya Prof. Florens Luoga ambaye amemaliza kipindi chake.

2) Aidha, amemteua Dkt. Natu El- Maamry Mwamba kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango.
Dkt. Mwamba alikuwa Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Undeshaji wa Kiwanja cha Ndege cha Kilimanjaro (KADCO).

Dkt. Mwamba anachukua nafasi ya Bw. Emmanuel M. Tutuba ambaye ameteuliwa kuwa Gavana wa Benki Kuu.

Teuzi hizi zinaanza mara moja.

View attachment 2472348
Safiiii
 
Bashe is doing great job, yaani wakimtoa hapo itakuwa kosa kubwa ingawa hatuwezi kumpangia kwa kuwa wao wanaweza kuwa na other motives...
Ila Bashe ni Msomali. Mie sipendi ninavyomuonaona huku kwenye baraza la mawaziri maana akikaakaa huku sana kuna siku anaweza akawa Rais.
 
Mtaje mwanahisa mmoja au wawili tu wa Federal Reserve Bank ya Marekani.
Nilikuwa sijui aisee.

Marekani wanalalamika suala la benki kuu yao (Federal Reserve Bureau) kuwa na wanahisa ambao wanalipwa faida.

Wanashangaa kwanini FRB iwe na wanahisa wakati hakuna taasisi nyingine yoyote inayoitwa "federal" yenye wanahisa.

Vipi unaongeleaje busara ya Magufuli kumteua Mwanasheria (Prof. Luoga) kuwa gavana wa BOT, badala ya kumteua mtaalam wa masuala ya fedha na benki?
 
Back
Top Bottom