Enjoy this! Dhana asili ya kuchoma UDI na kuvukiza mavumba

Enjoy this! Dhana asili ya kuchoma UDI na kuvukiza mavumba

Kuna wale wa sigara kubwa (bangi) wanatumia udi vibaya kwani siku hizi huvutia hzo sigara bwege ndani mageton na huchoma udi kila kona.
 
Mama mweny nyumba kila siku anapoenda kulala lazima nisikie harufu ya UDI vyumba vyetu vimepakana hii ina maana gani kwake kaka mshana...!
 
Niwatakie weekend njema! Najua hizi ndio zile tarehe pendwa... Tarehe za kuitwa majina yote matamu[emoji3] [emoji3] [emoji3]
Nina hakika wengi wetu tumeshawahi kuchoma udi ama kuvukiza mavumba... Wakati mwingine ni taratibu za kiimani kimila ama hata masharti ya mganga
Nimevutika kuandika mada hii kutokana na reply ya mdau Ray 4 real kwenye moja ya mada zangu...
Nitaandika kwa mtazamo wa kijamii zaidi kuliko kiimani kwa maana ya dini
565ea205e3f32a51668f1dac799c3ed4.jpg

Kwanza ni lazima utambue kuwa kuchoma UDI na kuvukiza mavumba kunajumuisha mambo mane makuu

1. Moshi wake ni alama ya hewa na pumzi yaani uhai.. Ukiashiria nguvu zisizoonekana kwa kusambaa na kutoweka milele
2. Moshi husika unatokana na moto, moto ni alama ya jua yaani mwanga
3. Kinachotoa moshi kinatokana na ardhi, ardhi ni msingi, ni mhimili wa dunia... Miti hupandwa ardhini
4. Moshi wake ni zao la maji, bila maji wala unyevu mti hauwezi kumea na kukua ukastawi na kutoa mazao yanayotumika kutengeneza udi
Hivi vinne vinakamilisha uumbaji katika misingi yake.
1b2841365f236761cd38bdb2d48c829b.jpg

Sasa matumizi makubwa ya UDI na kuvukiza mavumba ni yapi?
-kutoa gesi asili ambayo
:italeta harufu anuwai zitakazotumika kwenye mambo ya kiroho, manuizi, matambiko na maagano
:kualika mizimu na mapepo na majini kwa nia ya kutengeneza ama kuharibu
:kuvuta ama kufukuza ukitakacho ama usichokitaka... Maranyingi hapa ni ishu za mahusiano na mapenzi
Lakini kumbuka kwamba si kila mti unaweza kutoa malighafi ifaayo kwa kutengeneza UDI na mavumba.. Miti ama malighafi zifaazo ni kama hizi

(A)Miti ya ubani, yaani miti itoayo malighafi ya ubani... Hii hutumika kutakasa, shughuli za kiroho na kiimani... Maana ya ubani kiroho ni jua na jua ni mwanga ambao unatafsiriwa kama NGUVU ya kiroho

(B) Mti utoao manemane... Mane mane kiroho ni alama ya uponyaji, ulinzi mvuto, na tunu.... Inahusishwa na mwezi ambao kiroho ni nguvu ya mwanamke

(C) Msandali/sandalwood, hutumika kwenye shughuli za kiroho na utakaso

(D) Msandarusi, hutumika kutakasa na mambo ya kiroho pia zana zake kuu ni rangi nyeupe nyeusi na dhahabu... Utakaso wake si wa kiroho tu bali hata kwenye vitu vinavyoonekana.. Huu ndio hutengeneza vanish ya kung'arisha fenicha

(E)Mwerezi/[emoji268] pine tree kutakasa na kinga dhidi ya nguvu hasi zote

(F) Joka mti damu. Hii hutumika kuimarisha mahusiano, kuleta uthubutu na kujiamini lakini mbaya zaidi ikitumika kinyume kwa kunuia husababisha uhanithi wa jinsia zote mbili

Kwahiyo ndugu zangu tunapoenda kutafuta tiba mbadala jihadharini sana na kupewa mavumba na nyudi... Kwakuwa sometimes mganga hukupa malighafi isiyo sahihi na yenye madhara makubwa
667acc3eee2e573fb3f0027ef4d90423.jpg

Alamsiki

Jr[emoji769]
Ushirikina mtupu, total vanity.
 
Mi nikisikia harufu ya udi najihisi vibaya. Mpaka nikamuuliza halafu kajibu labda ni mafuta niliyojipaka. Naomba ushauri kama hii inaweza kuwa na madhara.
Mwambie asiwashe tena udi... Kuna watu naturally hawapatani na udi
 
Au na mi ninao? Maana nilimpa mwanamke mmoja lift akiwa ameombewa na mtu ninayemheshimu. Tulitembea takribani km 33. Kwanza nililazimika kuzima AC na kufungua vioo lakini bado harufu ilinisumbua sana na baadae kumuomba mama ashuke. Maana tayari kichwa kilikuwa kinauma. Ma kawaida kweli sipendi harufu ya udi ila ubani unaowashwa kwa ajili ya kusoma dua haunisumbui. Je, ninaweza kuwa na matatizo ninayohitaji kushughulikiwa? Ushauri tafadhali. Ndo maana nikasema nilikuta harufu ya udi ndani ya ofisi na mtu alikuwa ameingia ni secretary. Sijawa na amani kwamba labda either hakuwa na nia nzuri kwangu au alikuwa na manuizo yake anayoyajua.
Mmh kwa maelezo yako pale juu na haya hapa most likely unao hawa wapangaji na hawapendi harufu ya udi
Halafu nilichogundua kwenye hii mada anayependa ubani hapendi udi na anayependa udi hapendi ubani
 
Mama mweny nyumba kila siku anapoenda kulala lazima nisikie harufu ya UDI vyumba vyetu vimepakana hii ina maana gani kwake kaka mshana...!
Kama si urembo basi ni mambo yetu yale
 
Wengine huwa tunachoma udi duka linukie kama la kanjibai.Wala hatujui hayo.Na ni wengi tunafanya vile bila kujua.
 
Mmh kwa maelezo yako pale juu na haya hapa most likely unao hawa wapangaji na hawapendi harufu ya udi
Halafu nilichogundua kwenye hii mada anayependa ubani hapendi udi na anayependa udi hapendi ubani
Tatizo ni kwamba hata niliokuwa naomkwenye gari walisema harufu ilikuwa inawatesa.
 
Mshana nimekua nikiona UDI ukitumiwa na wavuta bangi hii imekaaje? Na pia Mimi hua napenda harufu yake sana na nikifukiza siku yangu hua inaenda vizuri sana na hua nanunua hizi za dukani kwa ajili ya sala japo ni mkristo hunifanya nijiskie amani ya roho vipi kuna lolote nisilolitambua hapa?
😀😀😀😀😀.

Wala isikutishe.

Ni katika kupotezea MNUKO wa MMEA.

Kwahiyo MOSHI wa MMEA ukichanganyika na MOSHI wa UDI, inakuwa umekata/umepunguza MAKALI.

Sikutegemea kabisa kukutana na BANDIKO kama hili la kwako.

Kwa kweli Umezama sana.

Baab kubwa
 
UDI una raha yake.

Na umkute MLIMBWENDE ambae anaeujulia.

Nilikuwa na MPENZI wangu mmoja huyo, akienda Kuoga utafurahi.

Maana akitoka BAFUNI, BAFU lote linanukia UDI halafu UDI wake unakaa sana.

Na ukija hapo Mwilini, nakuambia ni noma.

MTOTO ananukia huyo
 
Back
Top Bottom