Erdogan anaongoza kwa kuwa Rais Ndumilakuwili duniani

Erdogan anaongoza kwa kuwa Rais Ndumilakuwili duniani

Akili zahovyo kutoka kwakijana wahovyo kabisa[emoji2309]
Yaani lijinga hili.NATO na EU wapi na wapi?Kwenye NATO kuna US,Canada ambao hata hawapo bara la Ulaya. Mzee hajui NATO kwa nini ilianzishwa,na nini?Hivi atajua USSR kweli?Halafu ana udini jamaa.
 
Nikweli mwaka 2050 Ulaya yote itakuwa ni Waislam watupu patakapo bakia ni Vatican City kwa Papa lakini sehemu yote ya Ulaya itakuwa na Waislam watupu hiyo ahadi ipo ndani ya Kurani kuwa itakapofika nusura ya Mwenyeezi Mungu na kushinda na utawaona watu wanaingia katika dini ya Kiislam makundi makundi. Hivi sasa nchini Uingereza Waislam wananunuwa baadhi ya Makanisa ya zamani wanayavunja na kutengeneza misikiti Sehemu nyingi jijini London nchini Uingereza kuna misikiti mingi tu .
That will never happen, tatizo waislamu ni ngumu kuassimilate Ulaya. Wazungu wamelijua hilo.Sasa mlengo wa kulia wanaongoza/wataongoza nchi na uislamu hauna nafasi kwa nchi zenye mlengo wa kulia .
 
Kashindikana...lakini sijui kama ana succession plan nzuri ..
Erdogan hana haja ya kuwa na succession plan, Uturuki ni nchi mojawapo yenye demokrasia ya wastani ila utaratibu mzuri sana wa kupata Rais.
 
Mturuki ndie mzalishaji mkubwa wa nguo,vifaa vya ujenzi n.k,walianzia soko lao east europe na kwa sasa soko lao limeenea hadi ulaya yote,wao ndio ufunguo wa kutoka na kuingia black hawataki kuegemea upande wowote kwa maslahi ya nchi yao
 
Naifahamu vizuri sana Geoengineering, ninachojiuliza ni kama inatumika kutengeneza matetemeko ya ardhi
Uturuki ipo kwenye ukanda wa tetemeko na huwa inayapata mara kadhaa, hata Iran ndio iko eneo hatari zaidi kwenye weak joints za earth's crust. Na Japan nayo iko eneo hatari la tectonic plates za baharini. Hivyo Uturuki na Iran kupata matetemeko sio suala la ajabu wala Japan kupata tsunami halitafutiwi mchawi.

Hayo matukio yana mamilioni ya miaka yanatokea. Marekani yenyewe inakumbwa na dhoruba na tufani mara nyingi tu. Mambo ya kusingizia HAARP kwa matukio ya kijiografia ni conspiracy theories, no evidence at all.
 
Alafu mbona hizo ndio sera za Uturuki kutokuwa na upande. Tangu vita ya kwanza ya dunia walivyojichanganya kwenye alliance yao na kusababisha kuvunjika rasmi kwa Ottoman empire wakagundua kuingia kwenye migogoro ya mataifa mengine kwa kiherehere hailipi, wakaanza kutanguliza maslahi yao kwanza.

Hata Mustafa Kemal alivyoona udini haulipi akauondoa na kuifanya nchi iwe secular, wakaondokana na tamaduni za Kiarabu na kuchanganya na za kizungu. Uturuki kwanza haiwapendi Waarabu kama ambavyo hawaipendi, ndio maana ina mchango mkubwa sana kwenye Uislamu duniani ila haipewi credit sababu wenye dini yao hawataki Uturuki ipewe sifa.

Erdogan ni kigeugeu kweli anafanya maamuzi kwa kutazama maslahi. Hata hivyo ni vigumu kuunga mkono uvamizi wa Putin kwa Ukraine, ingekuwa rahisi hata China ingekubali. Sababu za msingi za Urusi kuingia Ukraine hata hazipo, wanataja hizi kesho wanataja zile. Ila hapo kwa kutorosha mateka atafanya Uturuki isiaminiwe tena kwenye kusuluhisha migogoro.
 
Uturuki ipo kwenye ukanda wa tetemeko na huwa inayapata mara kadhaa, hata Iran ndio iko eneo hatari zaidi kwenye weak joints za earth's crust. Na Japan nayo iko eneo hatari la tectonic plates za baharini. Hivyo Uturuki na Iran kupata matetemeko sio suala la ajabu wala Japan kupata tsunami halitafutiwi mchawi.

Hayo matukio yana mamilioni ya miaka yanatokea. Marekani yenyewe inakumbwa na dhoruba na tufani mara nyingi tu. Mambo ya kusingizia HAARP kwa matukio ya kijiografia ni conspiracy theories, no evidence at all.
Well said. Haya majanga yamekuwepo wayback, na kuna maeneo ni hatarishi kiasi huwa yanakua discouraged kuwa na population kubwa sababu even if tukio litakuja kutokea miaka 50 hadi 100 ijayo bado jamii ya sasa inakua na wajibu wa kuilinda jamii inayokuja kwa kuwa na protective plans.
Bahati mbaya wengi hupuuzia. Leo hii kama suyo sababu za utalii, basi watu wangeshavamia na kujenga around Mt. Oldonyo Lengai pamoja na kuambiwa volcano yako ipo active and it erupts
 
Uturuki ipo kwenye ukanda wa tetemeko na huwa inayapata mara kadhaa, hata Iran ndio iko eneo hatari zaidi kwenye weak joints za earth's crust. Na Japan nayo iko eneo hatari la tectonic plates za baharini. Hivyo Uturuki na Iran kupata matetemeko sio suala la ajabu wala Japan kupata tsunami halitafutiwi mchawi.

Hayo matukio yana mamilioni ya miaka yanatokea. Marekani yenyewe inakumbwa na dhoruba na tufani mara nyingi tu. Mambo ya kusingizia HAARP kwa matukio ya kijiografia ni conspiracy theories, no evidence at all.
Kama ni hivyo kwanini wanang'ang'ania kuishi huko na hofu tele.Waje huku kwetu tuishi pamoja nao.
 
Mimi naiheshimu sana nchi ya Uturuki ambako nimekaa kidogo na kuwa ni taifa lenye historia muhimu kwetu waislamu.Zaidi ya hivyo ni nchi yenye kujali sana kuwaendeleza watu wake.Hata ukisikia uchumi umeyumba usidhani ni kama kuyumba kwa uchumi wa nchi zetu za kiafrika. Ukisikia hivyo basi ukiwa Uturuki unaweza ukala na kushiba bure kila siku ikabaki kuoga na kulala tu.

Pamoja na hayo kuingia kwa raisi wa chama cha mrengo wa kiislamu Erdogan kumebadili sana sera zilizokuwa na uhasama mkubwa na imani halisi ya kihistoria ya watu wake ambayo ni uislamu,Lakini raisi huyu amekuwa ni mtu asiyetabirika kabisa hasa katika mahusiano yake na nchi za nje.

Wakati alipouliwa Jamal Kashogi aliyekuwa mchumba wa raia wake wa kituruki na Uturuki kuwa na video za mauwaaji hayo tulidhani Uturuki isingerudisha uhusiano na Saudi Arabia mpaka hukumu ya tukio hiyo itolewe.
Yako mengi lakini kubwa kwa sasa ni huu uhusiano na Urusi na Ukraine. Mara nyingi inaonekana kama kwamba Uturuki ipo karibu zaidi na Urusi katika vita vinavyoendelea baina yake na Ukraine.Wakati vita vinaendelea mara nyingi Erdogan amekuwa akimualika raisi Putin kwa mazungumzo.

Wakati akifanya hivyo Uturuki ndiyo nchi iliyoiuzia Ukraine droni hatari za Bayaktar na ndizo zilizochangia kuitia hasara kubwa urusi katika msafara wa vifaru vilivyokuwa vikielekea Kyiv mwanzoni huko kwa vita.

Mara ikatiliana saini na Urusi kujenga kitujo kikubwa cha kuuza mafuta ya Urusi ili kuisaidia kukwepa vikwazo vya nchi za magharibi katika biashara hiyo na baadae ikafuatia mkataba wa kuuza ngano za Ukraine ili kuisaidia kiuchumi baada ya bandari zake zote kushikiliwa na Urusi.

Baada ya jeshi la Ukraine kushindwa kwenye mapambano ya Azovstal kule Mariupol na vikosi vyoke kuzingirwa na jeshi la Urusi nchi ya Ukraine ilisalimu amri lakini kwa kutaka kuwaokoa makamanda wake na wanajeshi waliobaki hai wakiwa wamekondeana kwa njaa. Uturuki ilikubali kuwachukua makamanda wake kwa makubaliano na Urusi kwamba watabaki huko milele.

Inashangaza juzi raisi Zelensky amekwenda Uturuki ghafla kuonana na riaisi Erdogana.Tangazo la kigeugeuj lililotolewa wazi katika mkutano huo ni Uturuki kuiunga mkono Ukraine kujiunga na NATO juu ya kwamba hilo ni chanzo kikuu cha vita vinavyoendelea.Kumbe hilo lilikuwa ni dogo.

Kubwa ni kuwa kumbe raisi Zelensky amerudi na makamanda wote waliobaki hai na kupelekwa nchini humo kwa mkataba maalum na Urusi. Hilo limetangazwa wakati Zelensky akiwa amerudi Kyiv na makamanda hao wakiwa wamenenepa na huenda tayari kuongoza tena mapambano na Urusi.


Una elimu ndogo kuhuau global diplomacy, uturuki ina approach za china, yaani just because wana ukaribu na urusi haimaanishi eti ndio wasifanye business na ukraine nope.
Nchi zina vipaombele vyake
 
Una elimu ndogo kuhuau global diplomacy, uturuki ina approach za china, yaani just because wana ukaribu na urusi haimaanishi eti ndio wasifanye business na ukraine nope.
Nchi zina vipaombele vyake
Kwa elimu yako wewe.Sisi na Uturuki tunafanana kwa lipi na kipi cha kujifunza kutoka kwao.
 
Nato ni kijeshi tu.Ila EU kumbuka kuna free mouvement of people and goods kati ya wananchi wa nchi member wa EU.Yaani Uturuki wakiruhusiwa EU maana yake waturuki wanaweza kwenda kuishi Ujerumani, France,Italia,Grèce nk.
Ulokole ukizidi saaana ni tatizo pia
 
Umekasirika kweli... wachezaji Saba Tu wamekuuma...hebu nenda katoe pongezi kule Kwa Kardinali mpya...ukimaliza uanzishe thread ya kumtukana Samia 🤣
Utapata nafuu I am sure
Walokole na kadinali na vitu viwili tofauti. Kanda ya ziwa wengi ni walokole na wasabato
 
Kama ni hivyo kwanini wanang'ang'ania kuishi huko na hofu tele.Waje huku kwetu tuishi pamoja nao.
Nchi zote zisizo na changamoto nyingi za asili huwa za kipuuzi na zinaishi kwa tabu.
Nchi ambayo hata usipolima unaweza kula matunda pori basi ina watu wadumavu, akili ya mtu anayeishi sehemu inakuwa na winter vyakula vinakosa na mifugo inakufa njaa haiwezi kuwa sawa na akili ya mtu mwaka mzima jiografia yake inampa chakula bure.

Human development index inakuwa kubwa kwa nchi zenye shida. Kuna mzungu aliamua kutengeneza njia za kuhifadhi maziwa, mwingine akatengeneza njia ya kuhifadhi nyasi za malisho ya winter, mwingine akagundua sufi inazuia baridi na baadae wakagundua kuna bara la watu wanaishi dezo ukilima pamba kule watu watapata nguo. Ukishalima hizo pamba utazibeba mgongoni? Wakatakiwa kuwa na meli na treni. Watu wakafia viwandani kwa mazingira mabovu sheria za kazi zikatungwa, maslahi, mazingira rafiki yakaboreshwa, huduma za afya kama upasuaji na kuunga mifupa.
Waligundua nyumba inakuwa na baridi sana winter na watoto wanakufa kwa pneumonia wakajenga za mbao na kuweka heating system. Mambo mengi sana wameendelea sababu ya necessity.

Hao Iran wanatajwa ni mojawapo ya nchi zenye ufahamu mzuri kuhusu cement. Grades zao za cement ni kubwa sana sababu wanaishi kwenye tetemeko na ukitaka cement kali duniani katika options zako tatu ihusishe Iran hasa wale IRGC wanayotumia kujengea underground military facilities. Sasa unakuja kwa nchi kama Tanzania imepata tetemeko Bukoba limeua watu hata 20 hawafiki vilio nchi nzima na visingizio kibao hadi michango serikali ilikula.
Wakati Uturuki watu zaidi ya 50,000 wamekufa mwaka huu na maisha yanaendelea kama hamna kilichotokea, na uchaguzi wamefanya alafu shangwe mtaani kama kawaida na Erdogan ile Ijumaa ya mwisho kabla ya uchaguzi kakusanya watu zaidi ya milioni mbili uwanjani kutoa hotuba ya mwisho. Muda huohuo bado kuna miili ilikuwa haijapatikana.
 
Nikweli mwaka 2050 Ulaya yote itakuwa ni Waislam watupu patakapo bakia ni Vatican City kwa Papa lakini sehemu yote ya Ulaya itakuwa na Waislam watupu hiyo ahadi ipo ndani ya Kurani kuwa itakapofika nusura ya Mwenyeezi Mungu na kushinda na utawaona watu wanaingia katika dini ya Kiislam makundi makundi. Hivi sasa nchini Uingereza Waislam wananunuwa baadhi ya Makanisa ya zamani wanayavunja na kutengeneza misikiti Sehemu nyingi jijini London nchini Uingereza kuna misikiti mingi tu .

ACHA UONGO WEWE ALAAA!

ULAYA NZIMA UISLAM HAUZIDI 25% SASA HIYO 2050 HAO 75% AMBAO SIYO WAISLAM ITAWAWEKA WAPI??

HALAFU UNAJIITA DR??

HOVYOOOOOO
 
Back
Top Bottom