Erdogan asema Uturuki sasa kuingia Israel kuwasaidia Wapalestina

Erdogan asema Uturuki sasa kuingia Israel kuwasaidia Wapalestina

Hawa wanaichukulia Turkiye taifa poa sana.
Tena asili ya Uturuki wakisema tunaenda vitani basi hawatoki mpaka wahakikishe nini kinapiganiwa.
Reference nzuri ni hii vita ya mwaka jana kati ya Azer na Armenia ya kugombania jimbo la Nagorno.
Armenia ilikua na mkataba wa ushirikiano wa kijeshi na Russia miaka mingi tu,nilidhani Azer atashindwa ile vita baada ya Russia kupeleka jeshi Armenia,ila kilichotokea baad ya Uturuki kupeleka jeshi Azer,ni vifo vya wanajeshi wengi wa Urusi kiasi hadi kikosi kilichobaki kikarudi Moscow.
Wana ndege zao za kivita wanaziita RAAD kazifuatilie mkuu.
Yani kitendo cha Uturuki kuwa NATO ndio kimewafunga kitanzi.
Urusi sio jeshi la kutumainia kwenye mambo yako magumu. Azerbaijan ingeweza kushinda vita dhidi ya Armenia hata kama Uturuki isingekuwa upande wa Azeri. Israel yenyewe ilikuwa na Azerbaijan na hata Azeri wangekosa kununua silaha Uturuki wangenunua Israel.

Azerbaijan wameanza training muda, wamenunua silaha, wamefundishwa mbinu na Uturuki na Israel ili kupambana na silaha za Urusi (Uturuki alikutana nazo Kaskazini mwa Syria na Israel always huwa anakutana nazo na war games anajiandaa dhidi yake). Azeri wana uchumi mkubwa baada ya kugundua mafuta na wanapigania haki yao. Sasa Armenia washinde tu kisa wana vikosi vya Urusi. Silaha zao za Urusi kina Pantsir zilipigwa.
 
Raisi wa Uturuki ndugu Tayeb Erdogan amesema nchi yake inakusudia kuingia ndani ya Israel kuwasaidia wapalestina wanaouliwa na Israel.
Hayo aliyasema kwenye mji aliozaliwa wa Rize wakari akizungumza na wanachama wa chama chake cha AK chenye kufuata mrengo wa dini ya kiislamu.
Akifafanua kusudio hilo,Erdogan amesema hilo ni jambo jepesi kwa nchi yake yenye teknolojia kubwa za kivita kama ambavyo wamewahi kufanya huko Nagoro Karabakh na Libya ambapo matokeo yalionekana.
Serikali ya umoja wa kitaifa inayoongoza sasa nchini Libya na kutambuliwa na umoja wa mataifa imedumu madarakani baada ya Uturuki kuingilia kati na kuiunga mkono kwa kuilinda dhidi ya wapinzani wake.
Hatua hiyo ya Uturuki japo itakuja katika muda wa kuchelewa lakini ni yenye kuhitajika sana kutokana na dhulma kwa wapalestina na tishio dhidi ya msikiti wa Alaqsa.Kwa upande mwengine Uturuki ina uwezo huo japo mara nyengine huwa inakuwa na kigeugeu kisichokuwa na sababu kwenye maamuzi yake.

Erdogan says Turkey might enter Israel to help Palestinians

Watu tumechoshwa na maneno matupu ya Erdogan
 
Erdogan anatania, anajaribu kulinganisha Israel yenye nyuklia na yenye back up ya USA na Libya? Endapo nchi za kiarabu zitaingia vitani dhidi ya Israel, eneo la Goza litaondoka na msikiti wa Al-Aksa itatolewa kwa sababu ya vita hivyo, Israel atarusha kombola halafu atasema ni adui ambaye amepiga kombola eneo hilo. Wakianzisha vita kitakachofuata ni Ordogan kuondoka madarakani kwa sababu Turkey itapata hasira kubwa na itashindwa vita hiyo. Ndege zake nyingi zimetengenezwa na hao hao waisraeli wanaoishi USA.
Msikiti wa aqsa na ule ukuta wao mtakatifu vipo sehemu moja
 
Urusi sio jeshi la kutumainia kwenye mambo yako magumu. Azerbaijan ingeweza kushinda vita dhidi ya Armenia hata kama Uturuki isingekuwa upande wa Azeri. Israel yenyewe ilikuwa na Azerbaijan na hata Azeri wangekosa kununua silaha Uturuki wangenunua Israel.

Azerbaijan wameanza training muda, wamenunua silaha, wamefundishwa mbinu na Uturuki na Israel ili kupambana na silaha za Urusi (Uturuki alikutana nazo Kaskazini mwa Syria na Israel always huwa anakutana nazo na war games anajiandaa dhidi yake). Azeri wana uchumi mkubwa baada ya kugundua mafuta na wanapigania haki yao. Sasa Armenia washinde tu kisa wana vikosi vya Urusi. Silaha zao za Urusi kina Pantsir zilipigwa.
Ni kweli ila Azerbaijan imekua na uhusiano wa kijeshi na Turkiye kwa muda mrefu kuliko hiyo Israel.
Sio tu kijeshi hata kidiplomasia kama biashara Azer ina uhusiano muda refu na Turkiye,nadhani ndio maana ilipotokea mzozo wa Nagorno Karabakh Azerbaijan iliomba msaada directly from Turkiye.
Ila kwa mimi Turkiye ina ubavu wa kijeshi kuliko Israel.
Sijajua mkuu hili unalionaje.
 
NATO inamfunga vipi wakati Israel si mwanachama wa NATO.
Pamoja na hivyo Erdogan amefanya mambo mengi sana ya kuwapiga chenga wenzake na hakuna walichomfanya.
Amempiga chenga mpaka mrusi aliyeonekana ni mshirika wake mkubwa.
Israel sio mwanachama wa NATO ila ni mshirika mkubwa wa USA na EU yote.
Unadhani USA baba wa NATO atakubali mwanachama(mtoto) Uturuki amshambulie Israel ambaye anamlea pale middle east!?
Hayo mambo ya kuwapiga chenga ni yapi hayo alofanya Turkiye dhidi ya NATO ili tupimie uzito!?
Uhusiano wa Russia na Turkiye sio wa kihivyo,inapotokea mmoja anatizama faida yake basi kumgeuka mwenziwe dakika mbili.
 
Israel ishukuru imepakana na waarabu.
Maana waarabu wana kiwango fulani na ustahimilivu na uoga.
Ila angepakana na Iran,Pakistan,Afghanistan,Azerbaijan ama hiyo Turkiye yenyewe.
Leo hii tungekua tunasoma tu katika makala kuwa kulikua na taifa linaitwa Israel.
Hao Iran unaosema majenerali wake wanauwawa na Israel na bado Iran haiendi frontline. Iran bado sana kwenda wenyewe.
Pakistan wenyewe walishindwa kuizuia Bangladesh ndio waje kuifuta nchi ambayo ni very stable kwa ndani. Afghanistan hao kihistoria hawana muda na mambo ya nje yao.

Nchi ya kuitisha Israel hapo ni Uturuki, ambayo nayo sio nchi ya mlengo wa Kiislamu bali baadhi ya vyama. Katiba ya Uturuki haiutaji Uislamu popote, na Wapalestina sio asili ya Waturuki kama ambavyo baadhi ya Azerbaijans walivyo ilipoenda kuwatetea. Na inahitaji resources nyingi kupigana na Israel a formidable foe. Na silaha muhimu za Uturuki ambazo ni Western hazina clearance ya kuishambulia Israel. Erdogan anawahadaa religious fanatics, ni mnafiki.

Israel angekuwa mnyonge angepigwa, maadui nia wanayo ila tatizo uwezo.
 
Ni kweli ila Azerbaijan imekua na uhusiano wa kijeshi na Turkiye kwa muda mrefu kuliko hiyo Israel.
Sio tu kijeshi hata kidiplomasia kama biashara Azer ina uhusiano muda refu na Turkiye,nadhani ndio maana ilipotokea mzozo wa Nagorno Karabakh Azerbaijan iliomba msaada directly from Turkiye.
Ila kwa mimi Turkiye ina ubavu wa kijeshi kuliko Israel.
Sijajua mkuu hili unalionaje.
Azeri wana undugu wa damu na Turkiye kama ambavyo Armenia wana undugu wa damu na Iran. Alafu Azerbaijan ndio nchi pekee inayosaidiwa na Uturuki bila any added interest, msaada pure, mweupe. Uko kwingine Libya na wapi Uturuki haiendi bure kutoa msaada.

Hivyo kiasili Iran aliisaidia Armenia na Uturuki aliisaidia Azerbaijan, Urusi hakuwa serious na Armenia sababu haijiwezi kwa sasa ni mzigo. Armenia zamani aliionea Azerbaijan ikatulia ikatunza uchungu ikajipanga na ikategeshea kipindi gani kile sijui ilikuwa ni uchaguzi wa Marekani ikaja kwa kasi kuchukua jimbo lake.
 
Hao Iran unaosema majenerali wake wanauwawa na Israel na bado Iran haiendi frontline. Iran bado sana kwenda wenyewe.
Pakistan wenyewe walishindwa kuizuia Bangladesh ndio waje kuifuta nchi ambayo ni very stable kwa ndani. Afghanistan hao kihistoria hawana muda na mambo ya nje yao.

Nchi ya kuitisha Israel hapo ni Uturuki, ambayo nayo sio nchi ya mlengo wa Kiislamu bali baadhi ya vyama. Katiba ya Uturuki haiutaji Uislamu popote, na Wapalestina sio asili ya Waturuki kama ambavyo baadhi ya Azerbaijans walivyo ilipoenda kuwatetea. Na inahitaji resources nyingi kupigana na Israel a formidable foe. Na silaha muhimu za Uturuki ambazo ni Western hazina clearance ya kuishambulia Israel. Erdogan anawahadaa religious fanatics, ni mnafiki.

Israel angekuwa mnyonge angepigwa, maadui nia wanayo ila tatizo uwezo.
Iran kutokwenda frontline sio kwamba haina uwezo wa kuishambulia Israel mkuu.Pia kuuliwa kwa makamanda wa IRGC Iran huwa inalipiza kisasi kama sio yenyewe basi kupitia Hizbollah ama Syria,kuna sababu ambazo naweza zisema kama zifuatazo;
1)Economic sanctions zilizokumba Iran kiasi wanapambana kushikilia uchumi.
2)Rundo la maadui pale mashariki ya kati na wa kimataifa hususan USA,UK na Germany.
Kwasababu Iran ikijaribu kuishambulia directly Israel basi kuna mataifa hata respond perpendicularly kwa haraka sana.
Tuchukulie mfano wa kile kisasi cha kulipuliwa balozi ya Iran Syria,Iran alirusha makombora pamoja na drone 300 kwenda Israel ila USA,UK,Jordan walihusika kudungua hayo makombora.
Hata vita ikitokea basi ushiriki itakua hivyo hivyo.
3)Umbali kutoka Iran mpaka Israel,Iran na Israel hawachangii mipaka hii nayo ni sababu zingine.Umbali kidogo unapooza makali.
Iran hii kama 2006 iliweza kusaidia kundi la Hizbollah kwa kupenyeza askari wake na silaha kupigana dhidi ya IDF basi haishindwi kuipiga Israel mkuu.
Tena Iran ina silaha ambazo ni home made kabisa.
-Pakistan kuhusu kuishindwa Bangladesh sijui nitafuatilia,ila Pakistan sio taifa linalokubali kuonewa mkuu hata kidocho,ndio maana unaona inapapatuana na India kuhusu Kashmir na katika 5 border clash India imeshinda moja tu ya 2010 kama sijakosea.
-Afghanistan mkuu ni yaleyale ni taifa lisilokubali uonevu pia,kama Israel ingepakana nayo na ingekuwa inaingilia sovereignty kama inavyoingilia Syria basi kingewaka kaka.

Uturuki inaunda silaha zake yenyewe pia kaka hai import silaha 100%.
Ila katika taifa la kwanza la kumuweza Israel ni Iran.
Kama makundi tu yanayofadhiliwa na Iran kama Hizibollah Israel anayashindwa basi Israel hawezi ku stand full out war na Iran ambayo ina historia ya kuhimili vita vya muda mrefu.
 
Azeri wana undugu wa damu na Turkiye kama ambavyo Armenia wana undugu wa damu na Iran. Alafu Azerbaijan ndio nchi pekee inayosaidiwa na Uturuki bila any added interest, msaada pure, mweupe. Uko kwingine Libya na wapi Uturuki haiendi bure kutoa msaada.

Hivyo kiasili Iran aliisaidia Armenia na Uturuki aliisaidia Azerbaijan, Urusi hakuwa serious na Armenia sababu haijiwezi kwa sasa ni mzigo. Armenia zamani aliionea Azerbaijan ikatulia ikatunza uchungu ikajipanga na ikategeshea kipindi gani kile sijui ilikuwa ni uchaguzi wa Marekani ikaja kwa kasi kuchukua jimbo lake.
Armenia wanasaidiwa na Iran kivipi mkuu!?
Kidiplomasia ama kijeshi!?
Embu nipe HISTORIA ama mlolongo wake kidogo.
 
Iran kutokwenda frontline sio kwamba haina uwezo wa kuishambulia Israel mkuu.Pia kuuliwa kwa makamanda wa IRGC Iran huwa inalipiza kisasi kama sio yenyewe basi kupitia Hizbollah ama Syria,kuna sababu ambazo naweza zisema kama zifuatazo;
1)Economic sanctions zilizokumba Iran kiasi wanapambana kushikilia uchumi.
2)Rundo la maadui pale mashariki ya kati na wa kimataifa hususan USA,UK na Germany.
Kwasababu Iran ikijaribu kuishambulia directly Israel basi kuna mataifa hata respond perpendicularly kwa haraka sana.
Tuchukulie mfano wa kile kisasi cha kulipuliwa balozi ya Iran Syria,Iran alirusha makombora pamoja na drone 300 kwenda Israel ila USA,UK,Jordan walihusika kudungua hayo makombora.
Hata vita ikitokea basi ushiriki itakua hivyo hivyo.
3)Umbali kutoka Iran mpaka Israel,Iran na Israel hawachangii mipaka hii nayo ni sababu zingine.Umbali kidogo unapooza makali.
Iran hii kama 2006 iliweza kusaidia kundi la Hizbollah kwa kupenyeza askari wake na silaha kupigana dhidi ya IDF basi haishindwi kuipiga Israel mkuu.
Tena Iran ina silaha ambazo ni home made kabisa.
Iran bado sana level za kwenda frontline na Israel. Achana na proxy, kama lingekuwa suala la proxy unadhani Israel inashindwa kumtoa Assad pale Syria? Ni kwamba Israel haina huo muda. Iran anazo sababu nyingi za kumzuia kwenda fronltine na Israel.

Tatizo mnaichukulia Iran kwamba inapenda sana vita. Hebu tazama arsenal yake imejaa defensive weapons zaidi ya offensive ukiachana na missiles arsenal. Wakati Israel ina offensive zaidi ya defensive. Iran sio mpenda vita, ni mpenda fujo tu na mtuma viherehere. Hamas wamepigwa amekaa zake kimya, Hezbollah wakitaka watapigana asiende front.
-Pakistan kuhusu kuishindwa Bangladesh sijui nitafuatilia,ila Pakistan sio taifa linalokubali kuonewa mkuu hata kidocho,ndio maana unaona inapapatuana na India kuhusu Kashmir na katika 5 border clash India imeshinda moja tu ya 2010 kama sijakosea.
Kwenye border crash ni small scale na sijui unatumia vigezo gani kusema wanashinda, kwenye vita mbili Pakistan imepigwa na India.
-Afghanistan mkuu ni yaleyale ni taifa lisilokubali uonevu pia,kama Israel ingepakana nayo na ingekuwa inaingilia sovereignty kama inavyoingilia Syria basi kingewaka kaka.
Afghanistan wanapigana kama insurgents, sio troops. Kwenye vita ya state vs state wanapigwa vibaya hao.
Uturuki inaunda silaha zake yenyewe pia kaka hai import silaha 100%.
Ila katika taifa la kwanza la kumuweza Israel ni Iran.
Uturuki air defense alitaka Patriot akanyimwa, akasaini S-400. Angeweza angeunda zake ila hawezi. Kwenye ndege alitaka F-35 akatolewa na hela alishatoa, ndio kwanza ana prototype ya TF Kaan ambayo anabembeleza apewe injini na Marekani Sasa kwenye vita utaenda na prototype?
Kwenye vifaru, Altay inatumia injini ya South Korea ya Black Panther ambayo nayo ni developed from German Leopard MBT.
Main fighter ya Uturuki ni F-16, IFVs bado anazo American made. Airlifters, helicopters hata ATAK aliyounda ina mkono wa Augusta Mangusta. Sasa unasemaje 100% Uturuki inajitegemea silaha. Hizo silaha zote zina some restrictions.
Kama makundi tu yanayofadhiliwa na Iran kama Hizibollah Israel anayashindwa basi Israel hawezi ku stand full out war na Iran ambayo ina historia ya kuhimili vita vya muda mrefu.
Kwenye full out war ya Iran vs Israel ambao hawapakani ikiwa kila mmoja ataachwa bila msaada. Iran itafyatua maelfu ya makombora yake kufanya saturation attack na Israel itatumia some few hundreds missile strikes kufungua njia kwa SEAD missions ili kufanya precision airstrikes na fighters. Iran haina uwezo wa air strikes Israel.
Kikwazo katikati ni Iraq, sasa Iraq imzuie nani kati ya Israel au Iran kupitisha air assets angani kwake. Wakati ni vigumu Iran kupitisha majeshi ardhini yakaivamie Israel, ikitokea hivyo Israel itawahi kuiteka Iraq kuweka buffer zone na Waarabu wataingia na Westerns wataingia.

Wewe unatazama proxy kama vita ya kufa na kupona, yani kisa Uturuki hawaishindi PKK basi unaamini PKK ina jeshi la kuipiga hata Syria iliyochoka hapo Mashariki ya Kati.
 
Lina nguvu na hilo linajulikana au unataka nikupe ushahidi!??
1)Tokea ikiitwa Ottoman Empire 1917 haikuvunjwa Na taifa moja hata Western powers waliungana wengi pamoja na nchi za kiarabu kuvunja himaya ya Ottoman.
2)Vurugu za sasa za vikundi vya kikurdi Turkiye hutumia nguvu ndogo sana kuyakabili kwa idadi ndogo ya askari sio kama Israel anatumia maelfu ya askari na ndege vita kibao kudhibiti Hamas.
3)Vita ya Armenia na Azerbaijan pale Nagorno-Karabakh Armenia ilipewa usaidizi na Russia kwa kupewa 300+ soldiers na vifaa na Turkiye iliisaidia Azerbaijan kwa vifaa na wanajeshi 150+.
Matokeo yake wanajeshi wa Russia zaidi ya 200 walifariki na Armenia ikashindwa vita ya Nagorno Karabakh .
Fuatila matukio sisi hatuongei kwa kuropoka tu bali kwa ithibati.
Huyo ottoman empire iliishia wapi?
 
Iran bado sana level za kwenda frontline na Israel. Achana na proxy, kama lingekuwa suala la proxy unadhani Israel inashindwa kumtoa Assad pale Syria? Ni kwamba Israel haina huo muda. Iran anazo sababu nyingi za kumzuia kwenda fronltine na Israel.
Iran level za kwenda front na Israel anazo kwasababu mbili ama tatu;
-Ana medani nzuri kivita,kuhimili vita ya miaka nane na kushinda dhidi ya jeshi la Saddam Hussein linalosaidiwa Na USA sio jambo dogo.
-Iran ana missile power kubwa kushinda hata Israel.
Israel hana uwezo wa kumuondoa Assad pale hata akitaka hana uwezo.
Kama Hizbollah amemshindwa atamuweza Iran!?
Israel imekua ikipigwa katika street battles na Hamas video zimekua zikisambaa mkuu IDF wanakimbia street battle na Hamas.
Tatizo mnaichukulia Iran kwamba inapenda sana vita. Hebu tazama arsenal yake imejaa defensive weapons zaidi ya offensive ukiachana na missiles arsenal. Wakati Israel ina offensive zaidi ya ndadefensive. Iran sio mpenda vita, ni mpenda fujo tu na mtuma viherehere. Hamas wamepigwa amekaa zake kimya, Hezbollah wakitaka watapigana asiende front.
Hapa katika silaha mkuu hapa patizame vizuri,umeteleza.
Silaha za Iran ziko more offensive,hivi unajua ile Drone ilopenya Tel Aviv pasi na kugunduliwa ni Iranian made!?
Silaha za Iran zimeonesha ubora sehemu nyingi hususan Lebanon,Yemeni na Syria na Russia pia.Iran ina silaha offensive kuliko Israel.Mbaya zaidi Israel airdefense system zake za iron dome zimeonesha udhaifu mkubwa sana mkuu.
Hakuna nchi inayopenda vita ila kama ukiigusa Iran huwezi ukasalimika lazima italipiza kisasi.
Israel unayojaribu kuizungumzia hapa mkuu uvamizi wa Hamas imetumia wanajeshi laki tatu na silaha nyingi kiasi cha kuomba misaada ya silaha USA na wote tunajua na ushahidi tunao kuwa USA ilituma meli vita ikiwa na askari 2000 na silaha za kutosha kwenda Israel.
Sasa tujiulize kama Israel imetumia nguvu hiyo kupigana na Hamas wenye wapiganaji elfu 30 je itatumia nguvu kiasi gani kupigana na jeshi lenye wanajeshi zaidi ya laki 6 kama Iran!?
2006 turejee vita ya Hizbollah na IDF,IDF ilitumia silaha nyingi na makamanda wengi ila wakashindwa kuipoteza bint jubeir mbele ya kundi dogo la Hizbollah.
Kwenye border crash ni small scale na sijui unatumia vigezo gani kusema wanashinda, kwenye vita mbili Pakistan imepigwa na India.

Afghanistan wanapigana kama insurgents, sio troops. Kwenye vita ya state vs state wanapigwa vibaya hao.

Uturuki air defense alitaka Patriot akanyimwa, akasaini S-400. Angeweza angeunda zake ila hawezi. Kwenye ndege alitaka F-35 akatolewa na hela alishatoa, ndio kwanza ana prototype ya TF Kaan ambayo anabembeleza apewe injini na Marekani Sasa kwenye vita utaenda na prototype?
Kwenye vifaru, Altay inatumia injini ya South Korea ya Black Panther ambayo nayo ni developed from German Leopard MBT.
Main fighter ya Uturuki ni F-16, IFVs bado anazo American made. Airlifters, helicopters hata ATAK aliyounda ina mkono wa Augusta Mangusta. Sasa unasemaje 100% Uturuki inajitegemea silaha. Hizo silaha zote zina some restrictions.
-Border clash mkuu usizidharau,maana ile haikuwa vita ya mipakani tu bali ni vita ya kugombania eneo zima la KASHMIR mkuu.Ni sawa na vita ya Nagorno-Karabakh,vita ya kugombania eneo sio sawa na kugombania kilometa za mpaka.
-Afghanistan inaongozwa na Taliban mkuu,Taliban ndilo kundi lililovunja USSR mkuu,tena ni kundi ambalo ukilipia silaha lina ari kubwa ya vita kuliko idhaniavyo,mbaya zaidi huwezi kumaliza vita kwa fighter jets peke yake au missiles peke yake,askari wa ardhini lazima wahusike,katika hilo nadhani mkuu ushahidi upo kuwa Israel ground battle ni weupe.
Kwenye full out war ya Iran vs Israel ambao hawapakani ikiwa kila mmoja ataachwa bila msaada. Iran itafyatua maelfu ya makombora yake kufanya saturation attack na Israel itatumia some few hundreds missile strikes kufungua njia kwa SEAD missions ili kufanya precision airstrikes na fighters. Iran haina uwezo wa air strikes Israel.
Kikwazo katikati ni Iraq, sasa Iraq imzuie nani kati ya Israel au Iran kupitisha air assets angani kwake. Wakati ni vigumu Iran kupitisha majeshi ardhini yakaivamie Israel, ikitokea hivyo Israel itawahi kuiteka Iraq kuweka buffer zone na Waarabu wataingia na Westerns wataingia.

Wewe unatazama proxy kama vita ya kufa na kupona, yani kisa Uturuki hawaishindi PKK basi unaamini PKK ina jeshi la kuipiga hata Syria iliyochoka hapo Mashariki ya Kati.
Uliona lile shambulio la Iran dhidi ya Israel la kulipiza kisasi mkuu?
Iran alirusha kwanza drones zilizoihadaa air defense system ya Israel kesha akarusha ballistic missiles na yapo yaliyopenya licha ya kuwa USA na UK Walishiriki kuyadungua.
Sasa tujiulize kama wafadhili wakikaa pembeni hivi Israel atakuwa na uwezo wa kudungua missile power ya Iran!?
Iraq kuna vikundi vingi vya mujahiddin Israel hawezi kuteka eneo hata punje la Iraq.
Hata akiamua kuteka na kupenyeza askari kuja Iran kupigana vita ya ardhini Israel hana medani hiyo ya vita mbele ya Iran ambayo imehimili vita ya miaka nane ikichangiwa na Iraq na USA.
Israel bado sana kupimana ubavu na Iran mkuu.
Iran hii ambayo iliipa mafunzo Houthi kundi dogo lililosumbua Saudi Arabia na USA ndio Iran hii hii iliyoisaidia Hizbollah 2006 kumfukuza Israel pale bint jubeir kwa mapigano sio kwa mkataba au makubaliano.
Na vita ya makombora ni hatari zaidi ya vita vya ndege,na hata vyombo vya usalama vya kimataifa vimethibitisha kuwa silaha za Iran zina uwezo na athari kubwa maana zimetumika sehemu mbali mbali na zimeonesha matokeo chanya.

Kuhusu silaha za UTURUKI sina ujuzi sana kaka,labda niende nikachunguze ndio nitarudi hapa kuelezea.Ila PKK kila leo wanapigwa na kukamatwa hawaisumbui Uturuki kihivyo.
 
Zee jinga sana hilo,kwanza wanamsitiri sana kwa kukalia hicho kiti akibebwa na NATO.
Pale ndio mlango mkuu wa magaidi yote kuingia Europe kufanya ujinga wao.
Na hata wakitafutwa kukamatwa,wanakimbilia huko na anawalinda.
Zake nae zinahesabika
 
Iran bado sana level za kwenda frontline na Israel. Achana na proxy, kama lingekuwa suala la proxy unadhani Israel inashindwa kumtoa Assad pale Syria? Ni kwamba Israel haina huo muda. Iran anazo sababu nyingi za kumzuia kwenda fronltine na Israel.

Tatizo mnaichukulia Iran kwamba inapenda sana vita. Hebu tazama arsenal yake imejaa defensive weapons zaidi ya offensive ukiachana na missiles arsenal. Wakati Israel ina offensive zaidi ya defensive. Iran sio mpenda vita, ni mpenda fujo tu na mtuma viherehere. Hamas wamepigwa amekaa zake kimya, Hezbollah wakitaka watapigana asiende front.

Kwenye border crash ni small scale na sijui unatumia vigezo gani kusema wanashinda, kwenye vita mbili Pakistan imepigwa na India.

Afghanistan wanapigana kama insurgents, sio troops. Kwenye vita ya state vs state wanapigwa vibaya hao.

Uturuki air defense alitaka Patriot akanyimwa, akasaini S-400. Angeweza angeunda zake ila hawezi. Kwenye ndege alitaka F-35 akatolewa na hela alishatoa, ndio kwanza ana prototype ya TF Kaan ambayo anabembeleza apewe injini na Marekani Sasa kwenye vita utaenda na prototype?
Kwenye vifaru, Altay inatumia injini ya South Korea ya Black Panther ambayo nayo ni developed from German Leopard MBT.
Main fighter ya Uturuki ni F-16, IFVs bado anazo American made. Airlifters, helicopters hata ATAK aliyounda ina mkono wa Augusta Mangusta. Sasa unasemaje 100% Uturuki inajitegemea silaha. Hizo silaha zote zina some restrictions.

Kwenye full out war ya Iran vs Israel ambao hawapakani ikiwa kila mmoja ataachwa bila msaada. Iran itafyatua maelfu ya makombora yake kufanya saturation attack na Israel itatumia some few hundreds missile strikes kufungua njia kwa SEAD missions ili kufanya precision airstrikes na fighters. Iran haina uwezo wa air strikes Israel.
Kikwazo katikati ni Iraq, sasa Iraq imzuie nani kati ya Israel au Iran kupitisha air assets angani kwake. Wakati ni vigumu Iran kupitisha majeshi ardhini yakaivamie Israel, ikitokea hivyo Israel itawahi kuiteka Iraq kuweka buffer zone na Waarabu wataingia na Westerns wataingia.

Wewe unatazama proxy kama vita ya kufa na kupona, yani kisa Uturuki hawaishindi PKK basi unaamini PKK ina jeshi la kuipiga hata Syria iliyochoka hapo Mashariki ya Kati.
Umeongea mno porojo kama unasumulia gazeti la riwaya
 
Iran level za kwenda front na Israel anazo kwasababu mbili ama tatu;
-Ana medani nzuri kivita,kuhimili vita ya miaka nane na kushinda dhidi ya jeshi la Saddam Hussein linalosaidiwa Na USA sio jambo dogo.
-Iran ana missile power kubwa kushinda hata Israel.
Iran majenerali wake wanauwawa na Israel. Mbona haendi frontline? Kama uwezo anao ataenda lini sasa.
Kuhimili miaka 8 hata Iraq iliweza. Hapo Iran ilitumia US made weapons kama F-14 Tomcats na F-5 Phantom ingawa ilinyimwa spare parts ila ilifanya kuhamisha spares.

Suala la kusaidiwa ni silaha gani ya Marekani ilienda Iraq kama msaada? Haipo.
Wakati Iran wao walikuwa na nchi kama Chinaz Yugoslavia, Bulgaria, North Korea (ambako ndio walitoa missile technology) na wengine. Hata Iraq naye alikuwa na nchi za kumuunga mkono, mbona unaandika as if Iran ilikuwa peke yake.

Alafu kama ni suala la missile power mbona Israel ina nukes. Sasa maelfu ya makombora ya Iran yanamtisha nani wakati ukijifanya kuyatumia unajibiwa na nuclear strike moja utulie.
Israel hana uwezo wa kumuondoa Assad pale hata akitaka hana uwezo.
Kama Hizbollah amemshindwa atamuweza Iran!?
Israel imekua ikipigwa katika street battles na Hamas video zimekua zikisambaa mkuu IDF wanakimbia street battle na Hamas.
Kwahiyo Iran itapigana street battles na Israel alafu ishinde? Israel inashinda wars, sio battles. Hapo Gaza nani kamkimbia mwenzie. Nani amevuruga mji wa mwenzie na vita inapiganiwa wapi. Yani Israel wameamuru watu zaidi ya milioni wa Gaza wahame na wametii, wamelipua makazi, wameua zaidi ya watu 39,000 na hapo ni bila kukusudia kama ambavyo Hamas wanadhamiria kabisa kuua. Alafu unasema street battles Israel inakimbia. Kama ingekuwa inakimbia hizo streets zingekuwa hivi?
Hapa katika silaha mkuu hapa patizame vizuri,umeteleza.
Silaha za Iran ziko more offensive,hivi unajua ile Drone ilopenya Tel Aviv pasi na kugunduliwa ni Iranian made!?
Unajua drone iliyoiona helicopter ya Raisi iliyodondoka milimani ni ya wapi na ilitumia muda gani. Baada ya Iran kutumia masaa mengi siku nzima bila mafanikio wakaomba msaada Uturuki, ikaja Akinci drone ikatumia 2 and ½ hours ikatumia sensors zake ikaona kwenye ukungu na gizani. Wairan wana drones hazina hata NV likiingia giza au ukungu hamna kitu.

Iran anaonekana sababu analazimisha aonekane, kwamba kisa hujawahi ona silaha za South Korea zinatumika basi hazina uwezo. Uturuki ina silaha bora maradufu kuliko za Iran ila tu haina fujo.

Tofautisha kuwa na fujo na kuwa na nguvu.
Silaha za Iran zimeonesha ubora sehemu nyingi hususan Lebanon,Yemeni na Syria na Russia pia.Iran ina silaha offensive kuliko Israel.Mbaya zaidi Israel airdefense system zake za iron dome zimeonesha udhaifu mkubwa sana mkuu.
Nitajie air defense system yeyete duniani yenye effectiveness percentage kubwa kuliko Iron Dome. Itaje na useme success rate yake niko nasubiri.

Sijaona hata iwe Patriot, S-400, S-300 wala nani. Kama unaijua ilete nami nilete numbers za Iron Dome.
Hakuna nchi inayopenda vita ila kama ukiigusa Iran huwezi ukasalimika lazima italipiza kisasi.
Israel unayojaribu kuizungumzia hapa mkuu uvamizi wa Hamas imetumia wanajeshi laki tatu na silaha nyingi kiasi cha kuomba misaada ya silaha USA na wote tunajua na ushahidi tunao kuwa USA ilituma meli vita ikiwa na askari 2000 na silaha za kutosha kwenda Israel.
Askari 2,000 ni kitu gani kwenye vita ya taifa. Hiyo si ni infantry brigade moja ya Israel.
Hamas hupokea silaha vilevile, Israel silaha imenunua.

Hao wanajeshi laki tatu walikuwa mobilized in case Waarabu watajiunga iwe total war. Yalikuwa maandalizi maana Iran ilijifanya inataka kuwapanda kichwani. Brigades zinazotumika Gaza hata 10 hazifiki, hao wanajeshi 300,000 walikuwa vitani wapi.
Sasa tujiulize kama Israel imetumia nguvu hiyo kupigana na Hamas wenye wapiganaji elfu 30 je itatumia nguvu kiasi gani kupigana na jeshi lenye wanajeshi zaidi ya laki 6 kama Iran!?
Jinsi ambavyo Israel ilipigana na jeshi la Egypt na Syria yaliyokuwa na wanajeshi mara 2 zaidi ya Israel. Ndivyo ambavyo Iran itakuwa. Wanajeshi 600,000 wa Iran hawapakani na Israel, je:

Watakuja kwa ungo vitani?

Wataenda kwa airlifters, zipi? Kwanza wana paratroopers wangapi Iran na mazoezi hufanyia wapi maana zana hizo hawana.

Wataenda kwa magari, Israel ina air dominance si itawachoma moto kabla hata hawajakanyaga ardhi yake?

Watavuka ardhi wapitie Iraq, itawaruhusu? Ikiwarusu si inakuwa mshirika wa vita na ina haki ya kupigwa. Iraq ikubali kuua nchi yake kisa Iran.
2006 turejee vita ya Hizbollah na IDF,IDF ilitumia silaha nyingi na makamanda wengi ila wakashindwa kuipoteza bint jubeir mbele ya kundi dogo la Hizbollah.
Israel iliteka maeneo ya Lebanon tangu miaka ya 1980s mpaka mwaka 2000 baada ya Barak kushinda uchaguzi na aliahidi kuiondoa Israel Lebanon. Sijajua hiyo occupation ya 2006 ilikuwaje, hata hivyo kama Hezbollah wanajiweza uwanja upo wazi wajaribu. Maana kupigana kwao ni ushujaa na sifa.
-Border clash mkuu usizidharau,maana ile haikuwa vita ya mipakani tu bali ni vita ya kugombania eneo zima la KASHMIR mkuu.Ni sawa na vita ya Nagorno-Karabakh,vita ya kugombania eneo sio sawa na kugombania kilometa za mpaka.
India iliipiga Pakistan ikaitenga Bangladesh. Hakuna vita ambayo Pakistan iliishinda India, alafu mkuu hivi kwa akili yako kabisa unaiona India hii ni ya kushindwa na Pakistan???

Yaani ukitazama uchumi, ubora na idadi ya silaha, jeshi, population, budget, teknolojia, landmass. Unaona ni kipi Pakistan inaizidi India?
-Afghanistan inaongozwa na Taliban mkuu,Taliban ndilo kundi lililovunja USSR mkuu,tena ni kundi ambalo ukilipia silaha lina ari kubwa ya vita kuliko idhaniavyo,mbaya zaidi huwezi kumaliza vita kwa fighter jets peke yake au missiles peke yake,askari wa ardhini lazima wahusike,katika hilo nadhani mkuu ushahidi upo kuwa Israel ground battle ni weupe.
Taleban walikaliwa na Marekani kwa miaka 20 mpaka pale Trump alipoamua kuondosha majeshi yake. Taliban ilipigwa na coalition iliyokuwa na wanajeshi 5,000 wa Marekani.
Yaani Marekani ilitumia Brigade moja kuipiga Taleban kwa miezi miwili, sasa jeshi linalopigwa na brigade moja ya Marekani ni kitu gani mbele ya Israel?

Tangu mwaka 2001 Marekani wamekaa wee hapo Afghanistan mpaka wakasahau kwanini walienda, siasa zao zikaamua waondoke mwaka 2021.
Uliona lile shambulio la Iran dhidi ya Israel la kulipiza kisasi mkuu?
Madhara gani yalitokea, silaha zipi ziliharibiwa, vifo vingapi mkuu. Israel iliua majenerali watatu, aya sasa Iran ili-achieve nini.
Iran alirusha kwanza drones zilizoihadaa air defense system ya Israel kesha akarusha ballistic missiles na yapo yaliyopenya licha ya kuwa USA na UK Walishiriki kuyadungua.
Sasa tujiulize kama wafadhili wakikaa pembeni hivi Israel atakuwa na uwezo wa kudungua missile power ya Iran!?
Yaliyopenya yalifanya nini. Hivi unajua F-35 Adir za Israel zina command link inayoweza elekeza SAM site ya ardhini ifanye lock-on kwenye aerial target na kufanya interception? Hiyo ni ndoto kwa Iran.

Israel inaweza shoot ballistic missile kwa kutumia AH-64 Apache na fighter jets. Iran inaweza?

Then baada ya hapo unajua Israel ilifyatua air launched ballistic missile na likapenya anga la Iran, na likaacha missile booster Iraq. Iran inaweza?
Makombora ya Iran yana uzito wa makumi ya tani na yanabebwa na launchers nzito kama semi trucks, sasa Israel ina kombora ambalo hata tani halifiki ila linarushwa na fighter jet linapita Iraq linaingia Iran. Na liko very resistant na jamming, ni dogo na precise. Huogopi?
Iraq kuna vikundi vingi vya mujahiddin Israel hawezi kuteka eneo hata punje la Iraq.
Hata akiamua kuteka na kupenyeza askari kuja Iran kupigana vita ya ardhini Israel hana medani hiyo ya vita mbele ya Iran ambayo imehimili vita ya miaka nane ikichangiwa na Iraq na USA.
Iraq kuna Washia na Wasuni almost nusu kwa nusu. Wasuni hawaitaki Iran na wakipata nafasi wataipinga.
Iran ina majimbo yanataka kujitenga, ni kuwapa silaha waanzishe proxy muda huohuo Iran iko busy na Israel.

Israel hawezi pigana miaka vita ya kufa na kupona, ni miezi kadhaa ikizidi. Achana na operation ya Gaza.
Israel bado sana kupimana ubavu na Iran mkuu.
Iran hii ambayo iliipa mafunzo Houthi kundi dogo lililosumbua Saudi Arabia na USA ndio Iran hii hii iliyoisaidia Hizbollah 2006 kumfukuza Israel pale bint jubeir kwa mapigano sio kwa mkataba au makubaliano.
Unaisema Israel ambayo inafanya airstrikes nyingi Syria na wana air defense systems wamenunua Russia ila kila muda huwa hawajui nini kimetokea angani kwao. Wairan wenyewe wahanga huwa wanapigwa sana Syria wakiwa wanapeleka shehena ya silaha kwa makundi.
Na vita ya makombora ni hatari zaidi ya vita vya ndege,na hata vyombo vya usalama vya kimataifa vimethibitisha kuwa silaha za Iran zina uwezo na athari kubwa maana zimetumika sehemu mbali mbali na zimeonesha matokeo chanya.
Kwani mkuu Israel haina makombora? Jericho I, Jericho II, Jericho III zote hizo ni ICBM. Nitajie ICBM hata moja ya Iran nasubiri hapa.

Israel ina nuclear warheads, ina submarines na zinaweza kufyatua makombora. Iran haina vyote hivyo.

Iran ina ballistic missiles nyingi ambazo ikifyatua kama mvua inajibiwa na nuke strike. Mjanja nani hapo.
Kuhusu silaha za UTURUKI sina ujuzi sana kaka,labda niende nikachunguze ndio nitarudi hapa kuelezea.Ila PKK kila leo wanapigwa na kukamatwa hawaisumbui Uturuki kihivyo.
Haphapo kwa Uturuki, kwa kuwa PKK haijaisha basi Uturuki ina jeshi bovu si ndio unamaanisha ambavyo Hamas haijaisha basi Israel mbovu?

Sasa Wakurdi wako Syria, walimsaidia Assad kupigana na ISIS. Alipowalipa fadhira akawafuga na PKK wakaishambulia Uturuki. Basi Uturuki ikaja Kaskazini mwa Syria ikampiga vibaya na silaha zake za Urusi na Wakurdi wake. Si ndipo Urusi ikafanya mkataba na Uturuki kufanya ukaguzi wa pamoja na mapigano yakaisha. Bila hivyo Syria ingepigwa vibaya.
Sasa huoni PKK wakiwa Uturuki wanavaa kiraia, wakija Syria bwana wao anapigwa sembuse wao.

Chukua Hamas wavalishe sare, wape kambi za jeshi watoke kwenye makazi na mahospitalini. Wape mwezi uone kama watakaa frontline. We unadhani kwanini siku zote hudai Israel inauwa wanawake na watoto. Wao Hamas huwa wanakuwa wapi.

Iran ikipigana na Israel hakuna kukaa mafichoni, hakuna kuvaa kanzu ukaficha grenade mfukoni ukategeshea troops wa Israel wakitazama nyuma wakidhani wewe ni raia mwema ndio uwalipue. Unavaa gwanda uonekane ni IRGC au regular forces utuambie jinsi Israel ilivyo mbovu.
 
Back
Top Bottom