Erdogan asema Uturuki sasa kuingia Israel kuwasaidia Wapalestina

Uturuki ilinunua mtambo wa ulinzi wa anga wa S-400 kutoka Urusi japo waliwekewa mikwara sana na Marekani
 
Umechambua vizuri ila ulipofika Israel kuivamia Iraq nimecheka.
Wingi wa silaha hauleti ushindi kwenye vita.Nguvu kazi watu ni lazima hatimae itumike.Kwanini Ukraine wamekuwa hoi kwa Urusi pamoja na kupewa misaada na nchi za Nato,ni kwamba hakuna tena watu wa kupigana.Kupata watu wa kuingia jeshini imekuwa mshike mshike mpaka watu wanaogopa kwenda harusini na kula mikahawani.
Israel nayo kwa sasa inakimbizana na ultra orthodox kuwaingiza vitani ambao wamegoma wakisingizia matakwa ya dhehebu lao.
Baada ya miezi 10 ya vita huko Gaza sasa Israel imekuwa dhaifu sana kijeshi na kiuchumi .Wamebakiwa na ndege za kivita tu kama silaha yao kuu.Hawawezi kupigana ana kwa ana na hata Hizbullah wachilia mbali kuvuka mipaka kwenda kuivamia Iraq.
Waarabu ni watu wanafiki na waogo sana lakini kwa sasa kama wana miongozo na sababu za kiimani kuipigq Israel ni rahisi mno.Habari za vita vya 1967 hakuna tena hofu hiyo.
 
Wewe ni muongo, Urusi hakupeleka majeshi kwani Azeri na Armenia na marafiki wa Urusi , acha story za kahawa
 
Majenerali wa Iran kuuliwa IRAN ALISHALIPIZA KILA KISASI CHA MAJENERALI WAKE KUULIWA.
Hili mbona nishalisema mkuu!?Hapa unarudia point ile ile,katika kila shambulio la Israel kuua jenerali wa Iran basi huwa linalipwa kwa shambulio la Hizbollah au Syria.
Na mbona ushahidi upo ukitaka unawekewa!?
Hata Iran consulate pale Syria ilivyolipuliwa Iran alilipa kisasi kwa kurusha makombora na drones 300+.
Na sababu za kutokwenda front nilishazitaja ngojea nizirudie tena;
-Iran ina struggle economically kwasababu ya kuwa na economic sanctions,hivyo uchumi huo sio mzuri kwa vita hata kiduchu.
-Iran ina maadui wengi ambao wanasubiri chanzo tu ili wamshambulie.Na kama akithubutu kuivamia Israel basi huwenda ndio mwisho wake maana kila taifa la Ulaya na USA wataweka full force ili kumuangusha,kwasababu tokea 1980 mpaka leo wanajaribu kufanya regime change pale Iran.
-Mwisho nilitaja ni umbali,umbali pia imesababisha moto kutokusambaa.

Usijifiche kichaka cha kuuawa kwa majenerali wa Iran hapo Syria,ilhali Iran Nae analipizaga kisasi kupitia hapo hapo Syria.Kama mtu wa kuingia frontline wa kwanza ni ISRAEL.
Kwasababu zifuatazo;
1)Amani ya Israel ipo mashakani kwa Syria kuwa command center ya vikundi vya kiasi vya Hamas,Hizbollah na Houthi.
2)Iran ndiye mfadhili wa mashambulizi ya Hizbollah dhidi ya Israel.Na hayo mashambulizi yameleta maafa makubwa Israel kwa kuleta vifo na ulemavu wa kudumu wa askari takriban 5000 kaskazini kwa Israel.
Hivyo hizi sababu mbili ni sababu kubwa tosha za Israel kumvamia Iran kuliko Iran kumvamia Israel.
Maana vita zote anazo kumbana nazo Israel mfadhili ni Iran.Je nani ana sababu kubwa ya kumvamia mwenzake!!??

Kuhusu vita ya Iraq na Iran,Iran ilikua ina jeshi dogo ambalo bado halikua stable maana ndio kwanza mwaka uliopita lilitoka kufanya mapinduzi.
Pia hayo mataifa ulotaja yalisaidia silaha tu ilhali Iraq ya Saddam Hussein ilisaidiwa kwa silaha na wanajeshi pia,na kwa kipindi kile inajulikana USA alikua baba wa majeshi na Iraq alikua baba wa majeshi middle east.

-Kuhusu missile power mkuu hivi unadhani nuclear inatumika tu kiwepesi!??
Kama ni hivyo basi Israel angeshapiga bomu pale Syria ambapo panatumika kama command center ya vikundi vyote vya uasi mashariki ya kati ambavyo vinaishambulia Israel kila leo.
Na Iran alishafikia hatua ya urutubishaji silaha na ripoti ilitoka,ndio maana USA na Israel kila leo wanakataa Iran kurutubisha vinu vya Nuke kwasababu wanajua kama akiyapata hakuna cha kumdhibiti tena middle east.

Israel hii unayoisemea wewe ambayo imeshindwa kuhimili vita ya miezi 9 tu.
Na tizama chini madhara iliyopata na hapo imepigana na Hamas tu pekee yake.
Sasa jiulize kama kundi dogo ambalo lina askari elfu 30 limewatia ulemavu je jeshi lenye watu zaidi ya laki 6 kitawafanya je!!??

Mkuu unadanganya sana punguza uongo unadanganya sana punguza uongo bana.
Battle is synonymous to war hiyo ni linguistics.
Israel imekua ikilipua majengo hovyo kimakusudi na ushahidi umekua ukitolewa hapa,wakidai eti Hamas wanajificha humo ndani.
Wameua wanawake na watoto wasio na hatia.Ukitaka ushahidi nakuletea hapa we sema niulete.
Street battles vita za uso kwa uso ISRAEL AMESHINDWA GAZA NA WALEMAVU WENGI WA IDF WALIPATIKANA KATIKA VITA ZA MITAA KWA MITAA HAPO GAZA.
Wengi wakiwa wana matatizo ya saikolojia wengine wakiwa wamevunjwa miguu kwa grenade na risasi.
Ukitaka ushahidi nakuletea.
Watu kuhamishwa kutoka Central Gaza kwenda Khani younis ni kwa usalama wao ni sahihi kuhama,japo huko huko Khani younis imeripotiwa kuwa Israel imekua ikishambulia kimakusudi ilhali hakuna Hamas wala sign of Hamas huko.Ukitaka ushahidi nakuletea pia.
Hao askari wa IDF laki tatu waliletwa kwaajili ya kupambana na HAMAS wala usisingizie waarabu eti kama watajaribu kuungana ndio hilo jeshi litatumika.
Mbona wanajeshi waliisha na sasa hivi Israel imekua ikilazimisha raia kuingia jeshini??
Au hauna habari kaka kama Israel inalazimisha raia kuingia jeshini ili kupunguza uhaba wa askari!?
Hapo pia usisahau kaskazini kwa Israel haikaliki kwa mashambulizi madogo tu ya Hizbollah.

-Kuhusu suala la Iran kushindwa kumuokoa na kumpata rais wake hilo linafahamika kuwa Iran haijajipambanua katika teknolojia ya aerospace.Uturuki ni nchi ambayo imejipambanua sana katika teknolojia ya aerospace,kuna ndege yao inaitwa RAAD niliwahi ifuatilia ilivyo na ufanisi.
Ila kutokua na upembuzi katika teknolojia ya anga Iran haimaanishi haijiwezi kisilaha.Iran ilijikita katika uundaji ADS pamoja na ballistic missiles.Na middle east inafahamika Iran ameendelea katika masuala ya makombora.
Ana makombora ambayo yana uwezo wa kukwepa hata ADS ili yafikie lengo.Kwahiyo mtu kutokua vizuri sehemu ya anga haimaanishi hata sehemu zingine yuko vibaya.
Hii analysis hujaifanya vizuri kaka.

πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚Mkuu tuache utani na masihara.
Hii iron dome unayoisemea tarehe 7 October Hamas walirusha roketi tena ni homemade roketi zilizoundwa na mabomba ya maji Hamas walirusha roketi 5000 katika hayo 5000 roketi 2300 zimepenya.
Tusiende mbali,kambi ya kaskazini kwa Israel Galilee au Galilaya ilipigwa na cruise missiles za Hizbollah ikiwa na iron dome kama tatu iliteketea kambi nzima.
Na katika makombora yote Hizbollah alorusha kaskazini hakuna hata moja Iron dome iloweza kudungua.Sasa huu ufanisi wa iron dome uko wapi!??
Basi tusiende mbali,juzi tukio la drone ya Yemeni kuingia Tel Aviv pasi na kuonekana na kushambulia Tel Aviv Iron dome ikiwa active.
Ufanisi wa Iron dome uko wapi!!??
Ukiniambia nichague kati ya Iron dome Na Bavaar-373 nitaichagua Bavaar-373.Maana walau Bavaar ilionesha ufanisi hapo Iran.
Hiyo S-300 mwaka 2021 iliangusha ndege za Israel kama tatu zilipoingia Syria baada ya kuwa activated.
Hakuna ADS mbovu kama iron dome.
Tafuta namna nyingine ya kuipamba mkuu ila imeonesha udhaifu mkubwa sana katika vita hivi vya Gaza.
Still hapa bro unatereza tena.
Iran ina jeshi kubwa hapo Syria.
Na kila siku silaha na askari wanasafirishwa toka Iran kuja Syria kuingia Lebanon.Je hiyo Israel haioni na ikauzia hilo!?
Maana hizo silaha na askari ndio hao wanaoingia katika proxies na kuishambulia Israel.
Syria ni command centre ya Iran na vikundi vyake.
Israel 2000 walitangaza kutoka Lebanon ila hawakuiachia ardhi yote.
Pia kilichochochea vita zaidi ni Israel kumkamata kiongozi mmoja wapo wa Hizbollah 2006 ndipo Hizbollah ilivuka mpaka ikaua askari wa mpaka 8 na kuteka wanne japo wawili walifariki kwa majeraha.
IDF ndio iliamua kuvamia bint jubeir ili kuiweka iwe buffer zone ku demand askari wao.
Na waligoma kumrudisha kiongozi wa Hizbollah.
Yaliyotokea nadhani unayajua,kama isingekuwa USA kuingilia kati basi Israel ingepoteza hadi shebaah Farms.Maana walikua wanarudishwa nyuma kwa bunduki sio kwa kutaka wao.Israel ina sababu ya kuivamia Lebanon ila mbona hujiulizi hawajaivamia mpaka sasa!?
Ilhali mashambulizi ya Hizbollah yameleta maafa Israel kiasi cha kuleta internal displacement.Pia askari 5000 kati ya wale 70000 waliopata ulemavu wa kudumu wamepatikanika kaskazini kwa Israel as a result ya mashambulizi ya Hizbollah.Raia laki 2 wa Israel wameyakimbia makazi.Ila sijaona Israel ikiivamia Hizbollah.
Nadhani itakua unajua sababu.
Israel is millitary crippled ndio maana hata Biden na Macron walimwambia Netanyahu is unhealthy to go full out war with Hizbollah.Sasa mpaka hao watu wazima wanazungumza hivyo jiulize mkuu.

Cha mwisho Syria hajanunua S-300 bali Russia alizileta kulinda askari wake hapo Syria.
Ndio maana Israel inajua kuwa Russia iko Syria na haijawahi kugusa kambi za Russia.
Unazungumzia vita za zamani sana kipindi cha utafutaji uhuru.
Mimi ninazungumza mapigano ya kugombea Kashmir.
Yalitokea mapigano matano India ilishinda pigano moja tu la mwisho la 2010.Kafuatilie mapigano ya kugombea Kashmir.
Jeshi sio tu bajeti kubwa na uchumi peke yake.Bali pia ni mbinu na ari ya vita.Pakistan wana mbinu na ari ya vita kuliko India.
Taleban ilikua inatumia silaha za Marekani.Kumbuka Taleban hiyo hiyo ndio iliyovunja USSR kwa Ufadhili wa USA.
Hivyo USA kui attack Taleban kwa mara kwanza ni rahisi kwasababu jeuri na cheo hapo Afghanistan Taleban alipewa na USA.
Ila ile Taliban iliyotoka madarakani na kuamua kujipanga ilileta vifo vingi vya askari wa USA.
Ndio maana kama ulimsikiliza Trump aliongea wazi kwa Jeshi la USA itabidi liache kulipa gharama kubwa isiyokuwa na faida ya askari wake na pesa zake huko Afghanistan.
Hivyo Afghanistan ijilinde yenyewe.
Kuna vijana wengi pale Afghanistan wa jeshi la Marekani wamekufa na kuwa walemavu.Ungefuatilia namna riaa walivyokua wanakosoa jeshi la USA kuwepo Afghanistan halafu kila siku wanaletewa vijana wao katika majeneza.
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚Yani kwa shambulio la Iran kulipiza kisasi Israel mataifa manne yaliisaidia Israel kudungua mashambulizi.
USA,UK,JORDAN NA SAUDI ARABIA.
Still makombora 7 yakapenya na kuharibu airbase ya Israel.
Sasa jiulize kama hayo mataifa manne yasingeshiriki kudungua Israel ingefanya je!??

-Bro tuongee vitu kwa ground,hivyo vitu unavyosema kama Israel anavyo kwanini hajazuia makombora kutoka Lebanon ambayo yameua wanajeshi wake na kusababisha wanajeshi 5000 kuwa walemavu!?
Yani sawa utambe una hela halafu unashindia mlo mmoja wa ugali na Kisamvu.
Mkuu Embu kuwa realistic.
Kama Israel ingekua iko vizuri hivyo ulivyosema basi sasa hivi Galilee ingekuwa salama Salmin na ingekuwa raha mustarehe.
Tunaona yanayojiri tuna macho sio vipofu sisi.
Nimalizie kwa maneno machache huku chini.
Unaongea stori nyingi zisizo na uhalisia.
S-300 Syria haijanunua bali imeletwa na Russia kulinda askari wake pale Syria.
Ndio maana huoni Israel ikishambulia kambi ya Russia.
Hamas wana brigade tatu wana AL QASSAM wanavaa gwanda wana Islamic resistance wanavaa gwanda nyeusi na wana Hamas ambao wao wanavaa randomly.
Madai yako ya kusema kuwa Hamas wanajificha nyuma ya raia,wanajificha hospitali yalishafichuliwa kama ni uongo.
Israel aliunda hadi video fake na zikachunguzwa inajulikana ni staged videos.
Hakuna jipya mnaloweza singizia.
ISRAEL IS A WEAK ARMY.

PKK Na Hamas au Hizbollah ni tofauti.
Japo hao PKK wakifanya shambulio Uturuki huwa inawasaka na inawawajibisha kiukweli.
Operation ya mwisho Uturuki ilituma askari hawazidi 100 na ilirudi na rundo la wapuuzi wa PKK na kuwawajibisha.
PKK ni pana sana maana ni kikundi cha kurudi,pia kipo nchi jirani.
Sio kama Hamas ipo ndani ya OCCUPIED territories ambazo Israel anazi monitor na kuingia anavyotaka.
Mbaya zaidi Gaza ukubwa wake wa Kigamboni ila miezi 9 mmeshindwa hata kuokoa mateka.
Na mmepoteza askari na kupata majeruhi wengi.

Israel haina uwezo wa kuhimili vita muda mrefu.Israel sawa yake ni Hizbollah.
Itetee unavyoitetea ila mimi nikija nakuletea madhaifu ya Israel hapa.
Hizbollah wana gwanda na wana kambi zao kusini mwa Lebanon,mbona wameshindwa kutuma ndege vita zao kuchoma kambi za Hizbollah!!??
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚Baada ya kusikia Iran itatuma ADS pale wakifuata wanaishia na drone strikes tu.
 
Wewe ni muongo, Urusi hakupeleka majeshi kwani Azeri na Armenia na marafiki wa Urusi , acha story za kahawa
Mkuu uliza ushahidi usikurupuke.
Humu tunaongea kwa facts sio kwa kuropoka.
Russia iliisaidia ARMENIA KATIKA VITA YA NAGORNO-KARABAKH.
HAYA CNN HAO HAPO WAITE WAONGO.
Na baada ya kushindwa hiyo vita Armenia imeamua kuachana na ushirika wa kijeshi na Russia.
Soma hapo chini.
 
Uturuki ilinunua mtambo wa ulinzi wa anga wa S-400 kutoka Urusi japo waliwekewa mikwara sana na Marekani
Ndio maana nimesema ijapo suala la maslahi basi mmoja wapo kumgeuka mwenziwe ni rahisi.
Hivi una habari kuwa inasemekana kuna drones Uturuki ilimfadhili Ukraine kupitia USA katika hili vita ya sasa!?
 
Nakufuatia kaka.
 
Siku ukileta taarifa ya Uturuki kuingia Israel, naomba uni tag!
 
Uturuki hawezi kufanya hivyo. israel ina mabom mengi ya nukes, wakati uturuki yale yaliyopo ni ya NATO/MAREKANI walioweka base pale. atakachofanya uturuki ni kutoa msaada wa silaha kama drones kwa hamas na hezbollah, jambo litakalofanya israel pia watoe msaada wa silaha nzito na bora kwa WAKURDI ambao uturuki kwa miaka kibao imeshindwa kuwapiga. nchi kubwa vile hadi leo haina uwezo kuwashinda wakurdi. jambo hili litaiangamiza zaidi uturuki kuliko israel kwasababu israel in backup ya mataifa mengi yenye nguvu, na once wakurdi wakipata silaha bora toka kwa yeyote, wanao uwezo mkubwa na ujasiri kuisumbua uturuki hadi itapike nyongo.
 
Hao wote unaowataja ni ndg zako ktk imani. sasa nani aje awasaidie?. Hizo Yemen, Syria, Iraq na Lebanon ni fallen states hivyo hawana cha kupoteza ndo maana wanabweka ingawa hawana meno na wanajua kabisa hawana nguvu.
 
Hao wote unaowataja ni ndg zako ktk imani. sasa nani aje awasaidie?. Hizo Yemen, Syria, Iraq na Lebanon ni fallen states hivyo hawana cha kupoteza ndo maana wanabweka ingawa hawana meno na wanajua kabisa hawana nguvu.

Wanayokumbana nayo ingekuwa wewe unaeogopa hata mende, ungeshaikimbia kwenu. Kama una kwenu.
 
Siandiki sana vitendo umeviona jana Hamas na Hezbollah wako na maombolezo.

Israel imemuua mkuu wa Hamas akiwa Iran, dharau kubwa sana. Tunaomba Iran waende frontline kama wao wanaume.

Upande mwinginez Israel imeshambulia Beirut na kumuua Chief of Staff wa Hezbollah. Tunaomba washirikiane na wajomba zao kuishambulia Israel. Tutarudi hapa kutajiana nani miji yake imegeuzwa magofu, anayetaka kurudi zama za mawe za kale karibuni sababu zote za vita wanazo.
 
Mkuu hizi ni normal confrontations tu ambazo zitalipwa kisasi na maisha kuendelea.
Tegemea majibu makali sana kuliko yale ya makombora 300+.
Hivyo Iran hana sababu ya kuanzisha vita ya moja kwa moja,muacheni jamaa wa watu ajenge uchumi wake uliodumaa.
Hizbollah watalipa kisasi na Hamas.
Maana aliyeuawa ni kiongozi wa Hamas na Hizbollah.
Ila kama wa kuanzisha vita ni Israel kwasababu matatizo ya kushambuliwa na makundi ya wanamgambo chanzo ni Iran.

Ila wacha tusubiri majibu kaka,japo vita sio kitu chepesi cha kukiamua mkuu maana kina gharama zake.
 
Makombora 300+ yalimuua nani, yaliharibu nini, kitu gani hakifanyi kazi baada ya makombora 300+. Mimi nimekuvunja taya kwa ngumi moja, wewe umerusha mawe 300 juu ya bati langu na halijadhurika. Nani mshindi?

Jana kombora moja la Israel limemuua Haniyeh akiwa Tehran, nyumba za serikali, eneo la jeshi, walinzi kibao, radar zipo, majasusi wapo. Na hawajaona hata vumbi. Baadae Iran itafyatua makombora 300 kisha uje udai yamepenya, nikiuliza yamemuua nani utasema si yamepenyaπŸ˜‚.

Aya sasa mara hii unasema Iran hana sababu ya kuanzisha vita, sasa kwani nilisemaje. Ni kwamba Iran hana uwezo kwenda frontline. Kule front hawavai kanzu na jezi za mpira.
 
Hayo makombora ukumbuke mkuu nchi takriban 4 zilihusika kuyadungua,na 7 yakapenya na kuharibu Airbase ya Israel.
Sasa jiulize hayo mataifa yasingehusika Israel ingeweza kudungua hayo makombora peke yake!?
Haniyeh kifo chake cha utatanishi maana haijafahamika kama limetokea nje au ndani.
-Lakini Iran hiyo hiyo ndio inayosababisha vifo vya askari wa Israel Northern Israel kwa kuwasaidia Hizbollah kijeshi na silaha.
Niliposema mwenye sababu kubwa ya kuingia vitani ni Israel kwasababu maafa anayopata sasa hivi ya kushambuliwa chanzo ni kujihusisha kwa Iran kwenye hizo vita.
Hayo Hizbollah ndani kuna wanajeshi wa Iran wanafanya mashambulizi Israel.
Pia aliyeuliwa ni kiongozi wa Hamas sio Iran.
Tegemea kisasi kulipwa na Hizbollah na Hamas.

πŸ˜‚πŸ˜‚STILL unasema Iran hana uwezo wa Frontline wa kupigana na Israel,ilhali kuharibika kwa Northern Israel Galilaya ni kwa usaidizi wake kupitia hIzbollah.Je akiingia yeye kamili Israel itapona!?
Wewe subiri kisasi kitakacholipwa.
 
Uturuki ni strong ally wa marekani na yeye ndio kazuia nato membership ya israel
Na uturuki ndio ana supply umeme kwenye ofisi zote za IDF israel na israel ministry of defence
Ukweli kuwa pamoja na kauli hiyo hawezi kumvamia israel kwa ukaribu wake na marekani, ingawa ameblock biashara nyingi na israel na sasa hivi israel anataabika kutokana nu kumtegemea sana viwanda vya uturuki kumzalishia bidhaa zake muhimu na chakula
 
Hao wote unaowataja ni ndg zako ktk imani. sasa nani aje awasaidie?. Hizo Yemen, Syria, Iraq na Lebanon ni fallen states hivyo hawana cha kupoteza ndo maana wanabweka ingawa hawana meno na wanajua kabisa hawana nguvu.
Na ndio plan ya mazayuni kutengeneza kitu hapo mashariki ya kati kinaitwa "Great Israel "
Political instability zote za middle East hapo zina mkono wa mazayuni ,lengo ni kuharibu hizo nchi kwa vita na uchumi na kuzifanya kuwa mahame ili ndoto za kutengeneza taifa la mazayuni kutokea mediterranean mpaka kingo za Euphrates kwa expansion policies zao hizo ovu .
Plan ilikuwa kudondosha haya mataifa ambayo yalikuwa tishio ,Iraq , Syria ,Lebanon ,Libya ,Egypt , mfano nguvu ya Egypt kijeshi na influence katika mashariki ya kati inajulikana ni kubwa so wakamfanya Egpyt kuwa puppet Kwa kumpa pesa , watu wengi hawajui kwamba Egypt ni moja kati ya receivers wakubwa wa funds za Marekani kama pesa na vifaa vya kijeshi ili kuwasadia hao puppets wanaoongoza hiyo nchi kuwazima Muslims Brotherhood ambao wanachukua sana uzayuni .
Libya ya Gafafi kama kawaida alikuwa anachukia mazayuni na alikuwa anasaidia sana vikundi na harakati za ukombozi wa palestina miaka mingi , wakamuua na kutokomeza uongozi + kuhakikisha wanaharibu kabisa hilo taifa ili kusiwe tishio tena kwa mazayuni na plan zao ovu
Iraq ya Saadam pia ilikuwa tishio kwa mazayuni na hata Saadam alipinga sana uzayuni ,huyu alikuwa tishio ,wakaona wamzime kwa visingio kwamba anafadhili Alqaida na ana silaha za maangamizi kitu ambacho inajulikana mpaka leo ilikuwa ni uongo na propaganda za mazayuni kuiangusha Iraq .
Maana magaidi karibia wote waliohusika kuiteka na kuziendesha zile ndege za abiria kulenga pentagon na world trade centers ni raia wa Saudia (kibaraka wa Marekani na mazayuni)
Syria pia ya Assad ilikuwa tishio na kama Si Russia na Iran kusimamia show ,ilikuwa nchi ile inadondoka , vikundi vya kigaidi vya ISIS na waasi kama Alnusra ambao wanafadhiliwa wazi wazi na mmarekani na inajulikana ni branch ya Alqaida walitumikia kuhujumu Syria na kuharibu nchi kabisa .
Yule mkuu wa ISIS Abubakhar Alzaqawi alikuwa ni mzayuni aliyekuwa kwenye misheni ya kuharibu kabisa hayo mataifa ya Iraq na Syria na kuhakikisha hayasimami tena .
Ukiangalia big picture unaona kabisa hii ni sinema inachezwa , ISIS hawa hawa hawajawahi kuushambulia Israel na inasemekana baada ya mrusi ,Iran na Hezbollah kuingia kule Syria na kutembeza mkong'oto wa hatari ,yale magaidi feki ya kutengenezwa na Mossad na CIA yalianza kukimbilia kwenye hospitali za Telaviv kutibiwa .
Imagine
Leo hii tunaambiwa na propaganda mainstream media kwamba Iran ni mfadhili wa magaidi , na majitu yanameza tu bila kufanya analysis ya mambo
Hawa malaya malaya wengine washatiwa kiganjani na mzayuni na hawana kauli kabisa , Egypt , UAE , Oman ,Saudia , Turkey ,Jordan
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…