Eric Mandala akamatwa na kilo 200 za Cocaine

Eric Mandala akamatwa na kilo 200 za Cocaine

Pichani ni Eric Mandala Kizenga, raia wa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Fally Ipupa alitunga wimbo maarufu kumsifia mkewe, Maria Piron Mandala (PM). Wimbo huu ulizua gumzo sana, na kuonyesha namna alivyokuwa akimpenda mkewe.

Hata hivyo, kuanzia juzi, habari kuhusu Eric Mandala zimekuwa tofauti kabisa. Mtu huyu ambaye alikuwa akitajwa kuwa na utajiri mkubwa nchini Kongo sasa amekumbwa na kashfa kubwa. Juzi, akiwa nchini Colombia, Eric Mandala alikamatwa akiwa na kilo 200 za cocaine ndani ya gari lililokuwa limeegeshwa kwenye moja ya malls maarufu nchini humo.

Cocaine hiyo inadaiwa ilitoka Ecuador na ilikuwa inaelekea Morocco kupitia bandari ya Algeciras, Hispania.


Mandala alikamatwa pamoja na mwanamke wa Kikolombia, na walikamatwa wakiwa na kiasi cha dola 50,000 za kimarekani taslimu. Polisi waligundua kuwa Eric Mandala alikuwa akifuatiliwa na maafisa wa kudhibiti dawa za kulevya tangu Agosti mwaka jana, na hatimaye alikamatwa juzi kwenye mtego wao.


Zaidi ya hayo, mwaka 2020, Eric Mandala alijivunia kununua nyumba ya kifahari katika jengo refu zaidi duniani, Burj Khalifa, jijini Dubai, kwa kiasi cha Euro milioni 1.85 cash, jambo ambalo lilishangaza wengi na kuacha vinywa wazi.


Wakati Eric Mandala akisota kwenye mikono ya polisi, maswali yanajitokeza kuhusu kama Adolphe Muteba Tshilamwina ataungana na mzozo huu au ataepuka mtego huu. Hali inavyokuwa ni ngumu kusema, lakini ni wazi kuwa hadithi hii itazidi kutoa makala nyingi.

View attachment 3214542
Si huwa wanasema ukiwa boss wewe unaagiza tu vijana wanabeba, wakikamatwa unawapambania kuwatoa kazi iendelee! Sasa boss Mandala akaingia fronline yeye mwenyewe! Nani atampambania sasa!
 
Erix-Mandala-et-Tshisekedi-2-689x1024.jpeg

Akiwa na Félix Tshisekedi,raisi wa Democratic Republic of the Congo
 
Ile Docuseries iliyofanywa na Aljazeera ina mambo mengi sana kuhusu Africa, ukiingalia kwa upande wa Zimbabwe pekee na nchi zilizotajwa yake utakuwa haitumii akili yako vizuri.

Kiufupi huwezi ukawa unafanya uhuni wakubwa wako wasikujue,hakuna kitu kama hicho. Watu kama hawa unakuta ndiyo wanachangia kampeni au makada.

Si mnaona hata ile chain ya ML inavyounganika kibongobongo. Rudieni ile Docuseries, fananisha na eneo unaloishi
 
Kwa wanaouliza wasanii wa Muziki wanakuwaje Matajiri lakini Utajiri wao haundelei kwa vizazi, njia hii na Kutakatisha fedha ndio huwapa pesa zao, wote unaowaona wanapesa nyingi, how they do it.

Muziki ni kazi ambayo mapato yake hulipwa kwa "Cash money", unga na madawa ya Kulevya huuzwa kwa "Cash Money" lakini ukiwa huna kipato/biashara ya Kueleweka huwezi kuelezea pesa umepata wapi.

So Wafanya biashara wa Madawa ya Kulevya, humfata msanii (Mfano Almasi) na kumwambi kwenye shoo yako umepata viingilio vya 1M TZS mimi nina 100M TZS ndani hivi hela nataka kuziweka Bank, Tunafanyaje? Hapo ndio msanii ataomba kwenye deal apewe 20M wakikamilisha, zile 101M TSZ zinapelekwa bank kama hela zilizopatikana Kwenye show and vijana wetu wanakuwa wameathirika na madawa, pia njia ya kuzitakatisha hivi fedha ni kununua high value properties kama Magari na mikufu ya Thamani na vitu vingine ambavyo huficha footprints za vyanvo vya mapato.

Tanzania tukiwa serious na financial crimes watu wengi wataenda jela, kwanza kabisa Uchunguzi wa kina ungefanya na uanzishwaji wa Vituo vya mafuta ambavyo vitakufa in next 5 years, Nyumba ambazo huuzwa ghali kuliko thamani yake, na hata vyombo vya Radio vinavyoanzishwa na wasanii wa Muziki au watu wenye ukaribu na wanasiasa, wasanii wote wanaoalikwa na CCM

Ni mtu asiye utulivu wa akili ndio anayeweza kuamini Chadema wanazidiwa uwezo/nia ya Kuanzisha chombo cha habari na Wasanii wa muziki(Hivi vyombo vya Habari vya Wasanii siku vifanyiwe uchunguzi wa Kina).
 
Pichani ni Eric Mandala Kizenga, raia wa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Fally Ipupa alitunga wimbo maarufu kumsifia mkewe, Maria Piron Mandala (PM). Wimbo huu ulizua gumzo sana, na kuonyesha namna alivyokuwa akimpenda mkewe.

Hata hivyo, kuanzia juzi, habari kuhusu Eric Mandala zimekuwa tofauti kabisa. Mtu huyu ambaye alikuwa akitajwa kuwa na utajiri mkubwa nchini Kongo sasa amekumbwa na kashfa kubwa. Juzi, akiwa nchini Colombia, Eric Mandala alikamatwa akiwa na kilo 200 za cocaine ndani ya gari lililokuwa limeegeshwa kwenye moja ya malls maarufu nchini humo.

Cocaine hiyo inadaiwa ilitoka Ecuador na ilikuwa inaelekea Morocco kupitia bandari ya Algeciras, Hispania.


Mandala alikamatwa pamoja na mwanamke wa Kikolombia, na walikamatwa wakiwa na kiasi cha dola 50,000 za kimarekani taslimu. Polisi waligundua kuwa Eric Mandala alikuwa akifuatiliwa na maafisa wa kudhibiti dawa za kulevya tangu Agosti mwaka jana, na hatimaye alikamatwa juzi kwenye mtego wao.


Zaidi ya hayo, mwaka 2020, Eric Mandala alijivunia kununua nyumba ya kifahari katika jengo refu zaidi duniani, Burj Khalifa, jijini Dubai, kwa kiasi cha Euro milioni 1.85 cash, jambo ambalo lilishangaza wengi na kuacha vinywa wazi.


Wakati Eric Mandala akisota kwenye mikono ya polisi, maswali yanajitokeza kuhusu kama Adolphe Muteba Tshilamwina ataungana na mzozo huu au ataepuka mtego huu. Hali inavyokuwa ni ngumu kusema, lakini ni wazi kuwa hadithi hii itazidi kutoa makala nyingi.

View attachment 3214542
Mmhhh hatari
 
Back
Top Bottom