Erick Kabendera: Mwendazake aliendesha genge la wahuni na alikusudia kumkamata Rais Mstaafu Kikwete

Erick Kabendera: Mwendazake aliendesha genge la wahuni na alikusudia kumkamata Rais Mstaafu Kikwete

Ni baada ya twit za ndugu mwandishi Kabendera kuandika Kwa kifupi tu kudai kuwa JPM aliendesha Genge la wahuni kutaka kumkamata Mh rais mstaafu JK

Je, ni kosa lipi mpaka mh mstaafu rais JK atake akamatwe na genge ovu la mwendazake?

Nauliza tuu

Kawaida yetu sisi watanzani, tumekuwa na kawaida ya ufuasi wa vyama na ufuasi wa watu ndani ya chama, ila inapotokea kiongozi mmoja wapo analengo baya juu ya kiongozi mwingine tena bila kosa lolote la kueleweka, hatwezi kuendelea kumlea, ni lazima tumlaani Kwa sauti zetu zote na Kwa Mungu pia

Sasa ni vema kama kumekuwepo tuhuma nzito kama hiyo juu ya kiongozi mwingine kutaka kumdhuru kiongozi mwingine

Basi ni vema tukapewa pia sababu isiyotia Mashaka juu ya hilo,

Kwa nini Mstaafu alitaka akamatwe?
 
Bashite, Kabudi, Kalemani, Msukuma, Lukuvi, Sabaya, Gambo, Gwajima Happi, Polepole, Bashiru, Heri James Dotto James, Biswalo, (niendelee kuwataja?)
Kwa hiyo hao uliowataja hawana madaraka?

Mbona wote wako kwenye mrija wa asali?
 
Je, JPM alizikwa na hilo genge la kiharifu analolidai huyu mkimbizi?

Huyo JK ndo kamtuma kusema hiki anachokiandika kwenye mtandao?

Aqnaweza kuthibitisha mahakamani kuhusiana na tuhuma hizi zeney chembe ya chuki, wivu na uzandiki wa kuhongwa na wafanyabiashara wasio waadilifu?

Je, serikali ya Tanzania inasemaje kuhusu madai ya huyu mtu kutoka Uganda ijapokuwa anajitambulisha kama Mtanzania?

Ana uhakika hilo gene kwa sasa halipo na kwa sasa yuko salama hadi kuthubutu kuzusha tuhuma hizi?

Atunze maneno kwa maana tawala hizi za kisiasa zinabadilika asije akajuta baadae
 
Nadhan ulikuwa mtoto ww,vp vile viroba vya maiti baharin?
Vip wale wasiojulikana waliokuwa wakilindwa????
Acha kujitia upofu
viroba vya watu vilionekana na wanasiasa tu? hao watu hawakuwa na ndugu?
 
View attachment 2386088
Legacy inazidi kuzamishwa chini zaidi. Mwendazake alikuwa wa hovyo sana

====
Aliyoandika Kabendera

Wale mliouza mali zenu kupata pesa za kuhonga kusaidia plea bargain zenu zikubaliwe mjitokeze kutoa ushahidi. Wafanyabiashara mliopelekwa ofisi maarufu ya serikali, mkatishwa kwa mitutu ya bunduki wakati Mwendazake akiangalia kupitia CCTV, mkalazimishwa kutoa pesa mjitokeze.

Kuna mfanyabiashara maarufu alipitia mateso makali kwa kipindi cha miaka minne, ikiwemo kubinywa korodani, akilazimishwa aseme uongo kuwa alitoa dola milioni 100 kwa Rais Kikwete. Mwendazake alitaka kutumia ushahidi huo kumkamata Kikwete. Ni lazima atendewe haki.

Tuhuma dhidi ya Mwendazake kuanzisha na kuendesha genge la kihalifu nje ya mfumo wa serikali na kutoa maelekezo kwa genge hili kuwaua viongozi wa vyama vya upinzani, CCM na viongozi wakuu wastaafu ambao wangekuwa kikwazo kwake kutawala milele zichunguzwe pia.

Si mara ya kwanza zoezi kama hili kufanyika; Rais Mwinyi aliunda tume ya kupitia upya kesi zote ya uhujumu uchumi alizoziendesha Sokoine baada ya kuingia madarakani na kuna watu walirudishiwa mali zao.

Binafsi nimeombwa kuwasilisha maelezo ya maandishi kwa mamlaka husika kuhusu vitisho alivyovitoa Ndugu Biswalo dhidi yangu mara kwa mara baada kuachiwa huru na nimefanya hivyo.
Aisee..sawa
 
Huyu jamaa lazima awe na hasira na Hayati raisi John Joseph Pombe Magufuli kwasababu wakati wa sakata lake na polisi mwamba alifungwa na mama yake ghafla alianza kuumwa na mbaya zaidi akafariki akimuhitaji mwanae hadi anafariki alikuwa akimtaja na kumuomba rais amuachie akamuuguze ila alikataliwa maombi yake.

Kimsingi jamaa ana hasira ile ya kisasi na Hayati kiasi kwamba inabidi apambane na jina lake.
 
Huyu Kabendera ana Mental disorder,sasa Magufuli amkamate Kikwete ili amfanyaje wakati kikatiba Rais haruhusiwi kushitakiwa achilia mbali kukamtwa🤣
Mo alitekwa na timu Msoga kumchafua Magufuli na mauaji ya viongozi timu Msoga ndiyo suspect wa matukio.
Kasome tena na tena na hatimae utafahamu kwamba Rais anaweza kukamatwa na kushitakiwa vile vile!!
 
Back
Top Bottom