Ewura: Bei ya gesi ya kupikia imepanda kwa kati ya Tsh 2000 hadi 5000 kutokana na kupanda kwenye soko la dunia

Natamani ningekua naishi nje ya mji nifuge mang'ombe nipate biogas. Huku umeme tabu mara gas inapaa. Mkaa nao shida wacha niendelee kupikia kuni
 
Hata nyama ikipanda bei tatizo soko la dunia.
 
Soko la dunia linahusika vipi na Gas inayochimbwa Tanzania?
Baadae utawasikia, kufikia mwaka 2025 tutapiga marufuku matumizi ya mkaa na kuni ili kulinda mazingira. Huyo ni bwana J.Makamba.
Unapigaje marufuku ya matumizi ya hizo nishati wakati hujajenga mazingira rafiki watu wa kipato cha chini kutumia nishati mbadara?
Mkazo ungewekwa kitengenezwe kiwanda cha kuchakata gesi ya mtwara kwa ajili ya matumizi ya ndani.

Lakini nchi hii hatujui tushike wapi tunashika kila kitu hadi hakuna kinachifanikiwa hata kwa asilima 60.
Yani we are jack of many trades, master of none.

Ajabu yani toka kipindi hicho mpaka sasa hakuna kwianda cha kuprocess gesi ya mtwara ili itumike kwa matumizi ya kupikia ndani. Bado tuan import gas.

Hivi bado tunawaza kuwa hii nchi itakuja kulingana na nchi kama Singapore hata baada ya miaka 100 au tutaendelea laumu wakoloni?
 
Hiyo gas wanaitoa nchi gani mpaka kukapelekea mlipuko wa bei kwenye soko la dunia??

Jamaa wanatuonaga mbumbumbu sana!!
 
Hii ndo kazi wanayoiweza hawana cha kufanya intervation
 
Kwa mawazo yako gesi iki chimbwa ina wekwa tu kwenye mitungi.

Kwani badala ya kuwekeza kuweka gesi ya kwetu mitungini walikuwa bado wako busy kununua madege kwa cash money?
 
Hii nchi Ina baadhi ya Viongozi ni wa Ovyo sana
 
huku choma cha nkola tuna-i teketeza misitu kwa kwenda mbele adi, habari ya bei ya gas ni huko huko mjini........
 
Unapandisha bei ya bidhaa muhimu kwa zaidi ya miaka 5 mfulilizo lkn mishahara na masla mengine hayarekebishwi huo si ungwana hata kidogo.
 
Mpaka Sasa serikali 0% hakuna kitu apo
 
Hata mafuta ya kula tuliambiwa ivyo.

Sasa sijajua na mawese ya kigoma, alizeti ya singida, na ufuta wa iringa na makambako navyo yalipanda Bei kwenye soko la duniani?
Hao hawuni tu, yaani imekuwa kama soko la dunia ndio chaka lao la kujifichia madhaifu yao!!mfano leo hii mfuko wa mbolea umefikia 120, 000 , wakati mbolea hiyo hiyo zambia/malawi mbolea hiyo hiyo inauzwa 60, 000!!!na zote zinatoka huko huko nje?!!wenzao wanatoa ruzuku ili kumpunguzia mwananchi mzigo, hapa lawama zote anapewa SOKO LA DUNIA.
Hii nchi Ina baadhi ya Viongozi ni wa Ovyo sana
Pamoja na sisi wananchi!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…